Showing posts with label Breaking News. Show all posts
Showing posts with label Breaking News. Show all posts

Muuguzi apotea baada ya kuondoka Lagos kwenda jimbo la Ogun kumhudumia mgonjwa binafsiAfyaclass Forum •

Muuguzi apotea baada ya kuondoka Lagos kwenda jimbo la Ogun kumhudumia mgonjwa binafsi

Muuguzi wa Nigeria, Ovansa Khadijat, ametangazwa kutoweka baada ya kuondoka nyumbani kwake kumhudumia mgonjwa katika eneo la Aiyetoro katika jimbo la Ogun nchini Nigeria.

Dada yake, Joy, ambaye alithibitisha hali hiyo kwa LIB, alisema Khadijat aliondoka nyumbani kwao katika jimbo la Kogi yapata miezi miwili iliyopita kutafuta kazi bora huko Lagos. Alisema Khadijat alisema ilibidi aache kazi yake ya kwanza kwa sababu bosi wake alimlazimisha kufanya kazi kwa siku nyingi bila mapumziko.

Alisema Khadijat kisha akapata ofa siku chache zilizopita, ya kwenda Aiyetoro kumhudumia mgonjwa wa saratani. Kulingana na Joy, Khadijat alipanda teksi kutoka eneo la Mile 2 la Lagos hadi Aiyetoro katika jimbo la Ogun, lakini hajasikika au kuonekana tangu wakati huo.

Alisema suala hilo limeripotiwa kwa polisi tangu wakati huo.

Yeyote mwenye taarifa muhimu anapaswa kuwasiliana na kituo cha polisi kilicho karibu. 

0 Comment

Mtanzania wa Kwanza Agundulika na Maambukizi ya Homa ya Nyani (Mpox)Afyaclass Forum •

Mtanzania wa Kwanza Agundulika na Maambukizi ya Homa ya Nyani (Mpox)

WIZARA ya Afya imethibitisha kisa cha kwanza cha Mtanzania, kubainika amepata maambukizi ya homa ya nyani (Mpox). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Aidha, imesema Tanzania iko salama na hakuna mgonjwa wa Mpox aliyebainika hapa nchini hadi sasa.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Roida Andusamile, amesema Mtanzania huyo anayekadiriwa kuwa na miaka 32, alibainika kuwa na ugonjwa huo akiwa nchini Zambia.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa umma leo tarehe 11 Oktoba 2024, amesema taarifa ya kisa hicho waliipata jana kutoka mamlaka za serikali ya Zambia.

“Mtanzania huyu alivuka mpaka kutoka Tanzania kwenda Zambia mnamo tarehe 02 Septemba, 2024 kupitia mpaka wa Tunduma (Tanzania) na Nakonde (Zambia), akiwa hana dalili zozote za ugonjwa wa Mpox,” amesema Roida.

Amesema mwezi mmoja baadaye yaani tarehe 02 Oktoba 2024, akiwa nchini humo, alikwenda katika kliniki mojawapo ambapo alipata matibabu ya awali na kuchukuliwa vipimo tarehe 04 Oktoba 2024, ambavyo vilithibitisha kuwa na maambukizi hayo.

“Tarehe 08 Oktoba 2024, vipimo vya maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii ya Zambia vilithibitisha kuwa ni ugonjwa wa Mpox. Mgonjwa huyu bado anapata matibabu nchini Zambia…dalili za ugonjwa wa Mpox huweza kuonekana kati ya siku 3 hadi 21 tangu kuambukizwa. Hivyo, kwa kuwa Mtanzania huyu alianza kuonesha dalili mwezi mmoja baada ya kutoka nchini, ni dhahiri kuwa hakutoka nchini akiwa na maambukizi,” amefafanua.

Ameipongeza serikali ya Zambia kwa kubaini ugonjwa huo mapema, kumhudumia mgonjwa na kutoa taarifa kwa wakati.

Amesema Tanzania inaendelea kushirikiana na Zambia kufuatilia hali ya mgonjwa na kuhakikisha anapona na kurejea nchini, akiwa na afya njema.

“Wizara inapenda kuwahakikishia kuwa, bado Tanzania iko salama na hakuna mgonjwa wa Mpox aliyebainika hapa nchini hadi sasa. Wizara inaendelea kufuatilia kwa karibu kuhusu mwenendo wa ugonjwa huu na itaendelea kutoa taarifa kwa umma.

“Wizara inatoa wito kwa jamii kuendelea kuzingatia kanuni za usafi, kutopeana mikono na kutoa taarifa kwa kutumia namba 199 ili kwa pamoja tuhakikishe ugonjwa huu hauingii nchini,” amesema Roida.

0 Comment

Mtoto Joel aliyepotea karibu mwezi apatikana akiwa haiAfyaclass Forum •

Hatimaye Mtoto Joel aliyepotea karibu mwezi apatikana akiwa hai

Hatimaye mtoto Joel Johannes Mariki (15) mwanafunzi wa shule ya sekondari Bagara iliyopo mjini Babati aliyepotea karibu mwezi mmoja uliopita amepatikana akiwa hai.

Joel alipotea Jumamosi ya tarehe 14 September 2024 katika msitu wa Mlima Kwaraa uliopo Babati alipokua katika ziara ya masomo (study tour).

Joel aliongozana na wanafunzi wenzake pamoja na walimu, lakini wakati ziara ikiendelea msituni huko alipotea ghafla na alipotafutwa hakuonekana. Taarifa ilitolea kituo cha Polsi Babati ambao jitihada za kumtafuta zilifanyika kwa kushiririkisha jeshi la zimamoto na uokoaji, ambapo ilifanyika "patrol" msituni humo bila mafanikio.

Lakini leo majira ya saa 5 asubuhi Familia imepigiwa simu kuwa kuna mtoto anafanana na Joel ameokotwa eneo la Galapu nje kidogo ya mji wa Babati, na kutakiwa kwenda kumtambua kama ni yeye. Familia ilifika eneo hilo na kukuta tayari amekimbizwa hosptali ya mkoa Manyara.

Walienda hospitalini na kumkuta Joel akiwa amedhoofu sana, mwenye majeraha miguuni na michubuko mikononi hali iliyoonyesha kuwa alikua porini kwa siku zote hizo. Kwa sasa anaendelea na matibabu hospitalini hapo ili aweze kurejea katika afya yake. Familia inawashukuru wote waliosaidia kupaza sauti za kumtafuta mtoto wao.!

0 Comment

Watu Sita wafariki dunia Rwanda kwa mlipuko wa MarburgAfyaclass Forum •

Watu Sita wafariki dunia Rwanda kwa mlipuko wa Marburg

Watu sita wameripotiwa kufariki dunia nchini Rwanda kufuatia mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Marburg (MVD) nchini Rwanda.

Kupitia mtandao wa kijamii wa X, waziri wa afya nchini humo Sabin Nsanzimana, amesema jumla ya watu  26 wamethibitishwa kuambukizwa ugonjwa huo wa ambao awali ulijulikana kama homa ya Marburg (MHF) .

Nsanzimana amesema hadi kufikia sasa, watu 20 wamethibitishwa kupata maambukizi ya ugonjwa huo huku wengine sita wakifariki dunia.

Kwasasa, wagonjwa 20 wanaotibiwa ,  zaidi ni wahudumu wa afya  na wametengwa huku uchunguzi kuhusu chanzo cha mripuko huo ukiendelea.

Hatua za kinga pia zimeimarishwa katika vituo vyote vya afya.

Dalili za ugonjwa wa homa ya Marburg MVD ni pamoja na kuumwa na tumbo, kutapika damu na kuharisha. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni takriban asilimia 88 ya wale walioambukizwa ugonjwa huo, hufariki dunia.

Afisa wa afya wa Taasisi ya Kitaifa ya Afya ya Umma akivalia mavazi ya kinga dhidi ya virusi vya Ebola akinyunyiza dawa katika kituo cha afya huko CocodyPicha: Sia Kambou/AFP/Getty Images

Virusi vya ugonjwa huo vimepewa jina hilo la mji wa Ujerumani Marburg kwasababu msaadizi mmoja wa maabara mjini humo, aliambukizwa ugonjwa huo ambao bado ulikuwa haujajulikana mnamo mwaka 1967 alipokuwa akimshughulikia tumbili aliyekuwa ameambukizwa.

Nchi jirani ya Tanzania ilikuwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo mnamo mwaka 2023 huku Uganda ikipata maambukizi kama hayo mwaka 2017.

Huku kukiwa na asilimia 88 ya vifo vinavyotokana na ugonjwa huo, virusi vya Marburg, vinafananishwa na vile vya ugonjwa wa Ebola, na kuambukizwa watu kutoka kwa popo.

Baadaye huenea kwa binadamu kupitia maji maji ya mwili ya watu walioambukizwa.

#SOMA ZAIDI Ugonjwa huu wa Marburg hapa

0 Comment

Afariki akifanyiwa Upasuaji wa Kuongeza MakalioAfyaclass Forum •

Afariki akifanyiwa Upasuaji wa Kuongeza Makalio

Mama wa Watoto watano aitwae Alice Delsie Preete Webb (33), amefariki dunia baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio Nchini Uingereza ikielezwa kuwa alifanyiwa upasuaji huo na Mtu asiyekuwa na mafunzo rasmi ya kitiba.

Maafisa wa Polisi wameanzisha uchunguzi juu ya kifo chake na tayari Watu wawili wamekamatwa na kuachiliwa kwa dhamana wakikabiliwa na tuhuma za mauaji ya Alice ambapo imeandika kuwa huduma hiyo hugharimu pound 2,500 ( zaidi ya milioni 9 Tsh. ) na hufanyika ndani ya dakika 60 tu.

Alice ambaye anatajwa kuwa Muingereza wa kwanza kufariki kutokana na upasuaji wa aina hiyo, ameacha Mume na Watoto wao watano ambao ni Delsie (15), Preete (13), Gracie (12), Nylie (10) na Clarie (7).

0 Comment

TANZIA;kifo cha Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Maji Mzee Eng. Mbogo FutakambaAfyaclass Forum •

TANZIA;kifo cha Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Maji Mzee Eng. Mbogo Futakamba

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametoa taarifa ya msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa BODI YA MAJI YA TAIFA na Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Maji Mzee Eng. Mbogo Futakamba asubuhi ya leo.
Ni msiba mkubwa na pigo zito kwa familia ya sekta ya Maji.

“Tutamkumbuka kama mdau muhimu sana ambae ameendelea kuitumia sekta yetu hata baada ya kustaafu kwake.
Nitoe pole kwa wana Sekta ya Maji, Familia, Ndugu, Jamaa, Marafiki na wote walioguswa na msiba huu” amesema Jumaa Aweso

Via:Global Publishers

0 Comment

Wanafunzi 17 wamefariki dunia na 14 kujeruhiwa katika ajali ya moto KenyaAfyaclass Forum •

Wanafunzi 17 wamefariki dunia na 14 kujeruhiwa katika ajali ya moto Kenya

Wanafunzi 17 wamefariki dunia na 14 kujeruhiwa katika ajali ya moto iliyotokea katika Shule ya Msingi ya Hillside Endarasha iliyopo nchini Kenya.

Kwa mujibu wa tovuti ya Daily Nation, tukio hilo limetokea usiku wa Alhamisi Septemba 5, 2024 na kuteketeza baadhi ya mabweni ya shule hiyo.

Msemaji wa polisi nchini humo, Dk Resila Onyango, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyokatisha uhai wa wanafunzi hao na kuwa chanzo chake hakijajulikana.

Dk Onyango amesema wanafunzi 16 wamefariki hapohapo katika eneo la tukio na mmoja alipoteza uhai wakati akipatiwa matibabu.

“Miili ya wanafunzi 16 waliofariki katika eneo la ajali imeteketea kiasi cha kutotambulika,” amesema Dk Onyango wakati akizungumza na Nation FM.

Kuna hofu kwamba idadi ya waliokufa katika ajali hiyo inaweza kuongezeka kadiri shughuli ya uchunguzi na uokozi inavyoendelea.

Tayari timu ya uchunguzi imeshafika katika eneo hilo ili kutafuta chanzo cha tukio hilo ili hatua zingine ziweze kufuatawa.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD