Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria, Pauline Gekul kuanzia Novemba 25, 2023.

Gekul anatolewa katika nafasi hiyo, ikiwa ni kipindi kifupi tangu kuibuka tuhuma za ukatili wa haki za binadamu katika mitandao ya kijamii zikimuandama Mbunge huyo wa jimbo la Babati Mjini kuhusika na udhalilishaji.

Taarifa za kutenguliwa kwa Naibu Waziri huyo, zimetolewa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus kupitia mitandao ya kijamii ya Ikulu.

...See more

Related Discussions...

WEKA COMMENT HAPA(Reply)

Karibu Afyaclass Bongo Social,Share mawazo yako hapa au chochote kuhusiana na Makala husika,Karibu Sana Mdau Wetu Muhimu.