Mtoto kujisaidia choo cha kijani Chanzo na tibaAfyaclass Bongo Social •

Mtoto kujisaidia choo cha kijani Chanzo na tiba

kujisaidia choo cha rangi ya kijani ni hali inayowakumba watoto wadogo mara kwa mara, hasa katika kipindi cha awali cha maisha yao. Hali hii inaweza kusababisha wasiwasi kwa wazazi, lakini si kila mara inaashiria tatizo kubwa kiafya.

Je, hali hii inamaanisha nini? Na chanzo chake ni kipi? Je, kuna hatari yoyote kubwa kwa mtoto?

Chanzo Cha kujisaidia choo cha kijani kwa WATOTO

Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula, au digestive system, una jukumu muhimu katika kubadilisha chakula kuwa nishati na kutoa uchafu kama kinyesi. Baada ya chakula kumeng’enywa kwenye tumbo, kinyesi hupita kwenye sehemu mbalimbali za mfumo wa mmeng’enyo. Awali, kinyesi kinapofika kwenye utumbo mdogo, hubadilika rangi kuwa kijani kutokana na kuchanganyika na bile (nyongo) ambayo inasaidia kumeng’enya mafuta.

Kwa kawaida, kinyesi kinapoendelea kuingia kwenye utumbo mkubwa, mchakato wa kubadilisha rangi huendelea, na kinyesi huanza kubadilika kuwa rangi ya kahawia iliyokolea (dark brown) ambayo ni rangi ya kawaida ya kinyesi cha mtu mwenye afya.

Sababu kuu ya kujisaidia choo cha kijani ni mchakato wa haraka wa kupitisha kinyesi kwenye utumbo mkubwa, ambao haufikii hatua ya kubadilisha rangi kuwa kahawia. Hivyo, mtoto anapojisaidia kinyesi cha kijani, inamaanisha kuwa mfumo wake wa mmeng’enyo haujatoa muda wa kutosha kufanya mabadiliko ya rangi ya kinyesi kutokana na mwendo wa haraka wa uchafu kupitia kwenye mfumo huo.

JE,KUNA SABABU YOYOTE YA KUWA NA WASIWASI?

Kwa watoto wadogo, hii ni hali ya kawaida na isiyo na madhara makubwa. Mara nyingi kinyesi kitabadilika rangi na kuwa cha kawaida, Hata hivyo, ni muhimu kufahamu chanzo chake na sababu zinazosababisha hali hii ili kuepuka wasiwasi usio wa lazima, na kupata Msaada na Maelekezo  kutoka kwa Wataalam wa afya hasa ikiwa hali hii inadumu kwa Muda Mrefu.

VISABABISHI VYA KUJISAIDIA CHOO CHA KIJANI KWA WATOTO

1. Uharaka wa mmeng'enyo:

 Kama ilivyoelezwa hapo awali, moja ya sababu kuu ni pale kinyesi kinapopita haraka kwenye utumbo mkubwa, ambapo mchakato wa kubadilisha rangi ya kinyesi haukamiliki.

2. Ulaji wa vyakula vyenye rangi ya kijani: 

Watoto wanaonyonya, au wanaokula vyakula vya rangi ya kijani kama vile mboga za majani, wanaweza pia kuwa na hali hii ya kujisaidia kinyesi cha kijani. Rangi ya chakula huathiri rangi ya kinyesi.

3. Matumizi ya baadhi ya dawa: 

Baadhi ya dawa kama vile vitamini au virutubisho vya madini ya chuma vinaweza kubadilisha rangi ya kinyesi na kukifanya kuwa kijani.

4. Maambukizi ya bakteria au virusi:

 Ingawa hali hii ni nadra, maambukizi fulani ya mfumo wa mmeng'enyo yanaweza kusababisha kinyesi chenye rangi ya kijani. Ikiwa kinyesi cha kijani kinaambatana na dalili nyingine kama homa, kutapika, au kupoteza hamu ya kula, ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

JE, NI LAZIMA KUWA NA WASIWASI?

kujisaidia choo cha kijani si dalili ya ugonjwa hatari kwa watoto wachanga. Mara nyingi tatizo hili huisha kadri mtoto anavyoendelea kukua na mfumo wake wa mmeng’enyo unavyokomaa. Hata hivyo, ikiwa kuna dalili za ziada kama vile kuongezeka kwa joto la mwili, kukosa hamu ya kula, au mtoto kuwa mchovu zaidi ya kawaida, ni vyema kumwona mtaalamu wa afya kwa ushauri na uchunguzi zaidi. Au tuwasiliane ndani ya afyaclass kupitia namba +255758286584.

Kumbuka, hali hii ya kinyesi cha kijani mara nyingi hutokea katika hatua za mwanzo za ukuaji wa mtoto, na siyo dalili ya tatizo kubwa. Kwa hiyo, wazazi wanashauriwa kuwa watulivu na kufuatilia mabadiliko ya afya ya mtoto kwa umakini bila kuwa na hofu isiyo ya lazima.

USHAURI NA TIBA

Ikiwa unakutana na hali hii mara kwa mara na una wasiwasi, ni vizuri kushauriana na daktari au mtaalamu wa afya kuhusu hali hiyo. Wazazi wengi wanahitaji tu faraja na ufahamu zaidi juu ya jinsi mfumo wa mmeng'enyo wa mtoto unavyofanya kazi. Pia, ni muhimu kwa wazazi kuelewa kwamba chakula na hali ya afya ya mtoto inaweza kuathiri rangi ya kinyesi, lakini hii haina maana kwamba kuna ugonjwa mkubwa unaomsumbua Mtoto wako.

Hivo basi kwa kuhitimisha,kujisaidia choo cha kijani ni ya kawaida kwa watoto wachanga na haina madhara makubwa. Mfumo wa mmeng'enyo wa mtoto bado unakua, na mabadiliko haya ya rangi mara nyingi huonyesha kasi ya mchakato wa kumeng'enya chakula. Hivyo, wazazi wanapaswa kuwa na uvumilivu na kuepuka wasiwasi mwingi, lakini wakati huo huo, kufuatilia kwa karibu hali ya afya ya mtoto na kutafuta ushauri wa daktari inapobidi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

Ajali Mbaya Dodoma Yaua Watatu Baada ya Malori KugonganaAfyaclass Bongo Social •

Ajali Mbaya Dodoma Yaua Watatu Baada ya Malori Kugongana na Kuwaka Moto

Watu watatu wamefariki dunia kufuatia ajali mbaya iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Mataa, kwenye barabara inayoelekea kwa Dodoma, baada ya magari mawili makubwa kugongana uso kwa uso na kisha kuwaka moto.

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Dodoma, Rehema Menda, tukio hilo limetokea majira ya saa 12 asubuhi na kusababisha taharuki kubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo.

Imeelezwa kuwa ajali hiyo ilihusisha lori lenye namba za usajili T179 EQF lililokuwa limebeba mchanga, ambalo lilikuwa likiendeshwa na mtu aliyetambulika kwa jina moja la Lucas. Lori hilo liligongana uso kwa uso na gari jingine lenye namba T764 EPW pamoja na tela namba T238 EPW, lililokuwa limebeba saruji likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma.

Baada ya kugongana, magari hayo yaliteketea kwa moto uliodaiwa kusababishwa na msuguano mkali uliotokea wakati wa ajali. Askari wa zimamoto waliofika eneo la tukio walifanya juhudi za kuuzima moto na kuokoa miili ya watu watatu waliopoteza maisha.

Hadi sasa, mtu aliyethibitishwa kutambulika ni dereva wa lori la mchanga, Lucas, huku utambuzi wa wengine ukiendelea kufanywa na vyombo husika.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Emanuel, amesema watu waliokuwa kwenye gari lililobeba saruji walifanikiwa kutoka salama mara baada ya ajali. Hata hivyo, waliokuwa ndani ya lori la mchanga walikwama baada ya mlango kugoma kufunguka hadi askari wa uokozi walipofika na kuuvunja.

Ajali hiyo imeibua maswali mapya kuhusu usalama wa vyombo vikubwa barabarani, hasa katika maeneo yenye msongamano wa magari makubwa yanayosafirisha mizigo kati ya Dar es Salaam na Dodoma.

Mamlaka husika zinaendelea kuchunguza chanzo halisi cha ajali hiyo.

0 Comment

Kifo cha Padre Andrew Ifele Chasikitisha Waumini Ndani na Nje ya MarekaniAfyaclass Bongo Social •

Kifo cha Padre Andrew Ifele Chasikitisha Waumini Ndani na Nje ya Marekani

Ni Habari za kusikitisha kufuatia kifo cha Padre Mkatoliki kutoka Nigeria, Padre Andrew Ifele, aliyefariki dunia akiwa nchini Marekani. Taarifa hizo zimethibitishwa rasmi na mamlaka za Kanisa Katoliki, zikieleza kuwa kiongozi huyo wa dini alifariki akiwa usingizini siku ya Jumatatu, tarehe 27 Aprili 2026.

Alikokuwa Anahudumu Kabla ya Kifo Chake

Kabla ya umauti wake, Padre Ifele alikuwa akihudumu kama msimamizi wa parokia ya La Santisima Trinidad iliyopo Arroyo Seco, ndani ya Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Santa Fe nchini Marekani. Nafasi hiyo ilimfanya kuwa kiongozi muhimu wa kiroho kwa waumini wengi katika eneo hilo.

Mbali na jukumu hilo, Padre Ifele alikuwa pia akihudumu katika Kanisa la St. Anthony’s Catholic Church lililopo Questa, pamoja na makanisa yake ya misheni. Makanisa hayo ni pamoja na:

  • Nuestra Señora de Guadalupe (Cerro)
  • Sagrado Corazón (Costilla)
  • Santo Niño (Amalia)
  • St. Edwin’s (Red River)

Alihudumu katika maeneo hayo tangu mwaka 2011, akijitolea kwa bidii kuwahudumia waumini na jamii kwa ujumla.

Uthibitisho wa Kifo na Taarifa Rasmi

Kifo chake kimethibitishwa na Jimbo Katoliki la Awka nchini Nigeria kupitia taarifa rasmi iliyotolewa siku ya Jumanne. Taarifa hiyo ilisainiwa na kansela wa jimbo hilo, Padre Charles Ndubisi, ambaye alieleza kuwa mipango ya mazishi itatangazwa baadaye.

Maisha ya Huduma na Urithi Wake

Padre Andrew Ifele anakumbukwa kama mtumishi wa Mungu aliyejitolea kwa dhati, aliyegusa maisha ya watu wengi kupitia huduma yake ya kiroho. Uwepo wake katika makanisa mbalimbali nchini Marekani uliimarisha mshikamano wa waumini na kusaidia kukuza imani katika jamii.

Kifo chake kimeacha pengo kubwa si tu kwa familia yake na marafiki, bali pia kwa Kanisa Katoliki kwa ujumla, hasa wale waliopata fursa ya kuhudumiwa naye kwa miaka mingi.

Wakati dunia ikiendelea kuomboleza msiba huu, waumini wengi wanakumbuka mchango mkubwa wa Padre Ifele katika kueneza Injili na kuwahudumia watu kwa moyo wa upendo na unyenyekevu. Taarifa zaidi kuhusu mazishi na heshima za mwisho zinatarajiwa kutolewa hivi karibuni.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

0 Comment

Sababu za Period Kujirudia Mara kwa MaraAfyaclass Bongo Social •

Sababu za Period Kujirudia Mara kwa Mara: Fahamu Chanzo na Suluhisho

Wanawake wengi hupitia mzunguko wa hedhi kila mwezi, lakini wakati mwingine period inaweza kujirudia mapema kuliko kawaida. Hali hii inaweza kusababisha wasiwasi, hasa kama inatokea mara kwa mara. Kwa kawaida, mzunguko wa hedhi huwa kati ya siku 21 hadi 35, lakini ukianza kuona damu mara mbili ndani ya mwezi mmoja au period kurudi mapema sana, ni muhimu kuelewa sababu zinazoweza kusababisha hali hiyo.

Period Kujirudia Ina Maana Gani?

Period kujirudia ni pale hedhi inapokuja tena ndani ya muda mfupi kuliko kawaida, mfano baada ya wiki mbili au tatu tangu hedhi iliyopita. Wakati mwingine inaweza kuwa hedhi halisi au damu inayotokana na sababu nyingine za kiafya.

Sababu Kuu za Period Kujirudia

1. Mabadiliko ya Homoni

Homoni zina jukumu kubwa katika kudhibiti mzunguko wa hedhi. Ikiwa homoni kama estrogen au progesterone zimevurugika, period inaweza kuja mapema au kuchelewa.

Kwa hiyo mabadiliko ya homoni au tatizo la hormone Imbalance huweza kuwa chanzo

2. Msongo wa Mawazo (Stress)

Stress kubwa inaweza kuathiri sehemu ya ubongo inayodhibiti hedhi, hivyo kusababisha mzunguko kubadilika na period kujirudia.

Stress husababisha zaidi kutolewa kwa cortisol, ambapo huvuruga vichocheo(hormones);hasa hasa estrogen na progesterone—ambazo huhusika na kurekebisha mzunguko wa hedhi,matokeo yake ni kupata hedhi mapema kabla ya muda au premature menstruation. 

3. Kutumia Njia za Uzazi wa Mpango

Vidonge vya uzazi wa mpango, sindano au vifaa vingine vya homoni vinaweza kusababisha hali ya Damu ya Vitone tone mara kwa mara au spotting au damu kurudia mara kwa mara hasa mwanzoni mwa matumizi.

4. Ugonjwa wa PCOS

Polycystic Ovary Syndrome unaweza kusababisha hedhi zisizoeleweka, kuchelewa au kujirudia mara kwa mara kutokana na matatizo ya ovulation.

5. Tatizo la Uvimbe au Fibroids au Polyps Kwenye Uterasi

Uvimbe usiyo wa saratani kwenye mfuko wa uzazi unaweza kusababisha damu nyingi au period kurudia kabla ya muda.

6. Matatizo ya Tezi (Thyroid)

Tezi ikiwa inafanya kazi kupita kiasi au chini ya kawaida inaweza kuvuruga homoni na kuathiri period.

7. Maambukizi ya Mfumo wa Uzazi

Baadhi ya maambukizi yanaweza kusababisha damu kutoka katikati ya mzunguko, ambayo wengine hudhani ni period nyingine.

8. Ujauzito wa Mapema au Kuharibika kwa Mimba

Wakati mwingine damu ya ujauzito wa mapema au miscarriage inaweza kufanana na period iliyojirudia.

Lini Umuone Daktari?

Ni muhimu kumuona daktari ikiwa:

  • Period inajirudia mara kwa mara kila mwezi
  • Damu ni nyingi sana kuliko kawaida
  • Una maumivu makali ya tumbo
  • Unahisi kizunguzungu au udhaifu
  • Hedhi imebadilika ghafla bila sababu inayojulikana
  • Unashuku ujauzito

Jinsi ya Kupunguza Tatizo

  • Punguza stress na pata usingizi wa kutosha
  • Kula lishe bora yenye madini ya chuma
  • Fuatilia kalenda ya hedhi yako
  • Tumia dawa au uzazi wa mpango kwa ushauri wa daktari
  • Fanya uchunguzi wa afya ukiwa na dalili zinazoendelea

Kwa kuhitimisha tu,Period kujirudia inaweza kusababishwa na mambo madogo kama stress au mabadiliko ya homoni, lakini pia inaweza kuwa ishara ya tatizo la kiafya linalohitaji matibabu. Ukiwa na hali hii mara kwa mara, usiipuuzie. Kufanya uchunguzi mapema kunaweza kusaidia kupata tiba sahihi.

Kwa Ushauri,Elimu na Tiba tuwasiliane +255758286584.

vyanzo: Healthline, WebMD, Mayo Clinic

0 Comment

Historia ya Hashim Kambi: Nyota wa Uigizaji nchini TanzaniaAfyaclass Bongo Social •

Historia ya Hashim Kambi: Nyota wa Uigizaji nchini Tanzania

Tasnia ya filamu Tanzania imewahi kubarikiwa na vipaji vingi vilivyoacha alama kwa mashabiki na kizazi kipya cha wasanii. Miongoni mwa majina yaliyoheshimika sana ni Hashim Kambi, mwigizaji aliyefahamika kwa uwezo wake mkubwa wa kuigiza na mchango wake wa muda mrefu katika filamu za Kiswahili.

Hashim Kambi alizaliwa tar. 21 Oktoba 1956 na kufariki 27 Aprili 2026,alikua mwigizaji nguli wa filamu kutoka nchini Tanzania. Amepata kucheza katika filamu mbalimbali nchini Tanzania. Awali alikuwa mchezaji mpira kupitia klabu ya Yanga.

Mwanzo wa Safari Yake

Hashim Kambi alikuwa mmoja wa waigizaji waliotokea katika kipindi ambacho filamu za Tanzania zilikuwa zikianza kukua kwa kasi. Kupitia juhudi, nidhamu na kipaji chake, alifanikiwa kujijengea jina na kuwa miongoni mwa sura zilizoaminika katika filamu nyingi za nyumbani. Alijulikana pia kwa jina la “Mzee Kambi,” jina lililoonyesha heshima kubwa aliyokuwa nayo ndani ya tasnia.

Umahiri Katika Uigizaji

Kilichomtofautisha Hashim Kambi ni uwezo wake wa kucheza nafasi mbalimbali kwa uhalisia mkubwa. Mara nyingi alionekana kama baba wa familia, mzee mwenye busara, au mtu mwenye msimamo mkali katika hadithi. Mashabiki wengi walivutiwa na namna alivyoweza kuifanya kila nafasi ionekane ya kweli na yenye kugusa hisia.

Alishiriki katika kazi mbalimbali za filamu zikiwemo Handsome wa Kijiji (2011), Twisted (2013), Homecoming (2016), Mr. Kiongozi (2018),

Filamu Zingine;

1 Simu ya Kifo

2 Kipusa

3 The Lost Twins

4 Kipuri

5 Zuadiswa

6 Honey Moon

7 Surprise

8 Ripple of Tears

9 Miss Call

10 Romance

11 20% Furaha Iko Wapi

12 The Passion

13 Damu ya Mjomba

14 Bwagamoyo

15 Binti Nusa

16 Sanda Nyeusi

17 Babu Seya

18 Nguvu ya Mapenzi

19 Penzi la Baba

20 Olopong

21 Silent Killer

22 Huba

23 My Fiancee Born Again

24 Pretty Girl

25 Dangerous Deal

Pamoja na nyingine nyingi zilizomfanya aendelee kukumbukwa na watazamaji.

Mchango Kwa Filamu za Bongo Movie

Katika mahojiano mbalimbali, Hashim Kambi aliwahi kusisitiza umuhimu wa ubora, umakini na elimu katika kazi ya uigizaji. Aliamini kuwa filamu za Tanzania zinaweza kufika mbali zaidi endapo waigizaji na watayarishaji watawekeza katika maandalizi bora na taaluma. Hii inaonyesha kuwa hakuwa msanii wa kuigiza pekee, bali pia alikuwa mlezi wa maendeleo ya tasnia.

Urithi Wake

Kwa miaka mingi, Hashim Kambi aliendelea kuwa mfano wa kujituma na uvumilivu. Kazi zake zimeendelea kutazamwa na kupendwa hata baada ya kupita kwa muda, jambo linalothibitisha ukubwa wa mchango wake.

Jina lake litaendelea kubaki katika historia ya Bongo Movie kama mmoja wa waigizaji waliobeba tasnia hiyo katika nyakati muhimu za ukuaji wake.

Kifo chake

Tasnia ya filamu nchini Tanzania imepata pigo baada ya taarifa kuthibitisha kifo cha msanii mkongwe Hashim Kambi aliyefariki dunia leo tarehe 27 Aprili 2026.

Taarifa hizo zimethibitishwa na msemaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Coletha Raymond, kupitia mahojiano yake na vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa Coletha, marehemu alikuwa ametokea mkoani Tabora kwa shughuli za kikazi, na baada ya kurejea aliendelea moja kwa moja kwenye kazi nyingine eneo la Pilipili. Akiwa huko, alidaiwa kuanza kujisikia vibaya kabla ya kukimbizwa hospitalini, ambapo baadaye alifariki dunia.

Historia ya Hashim Kambi ni simulizi ya juhudi, kipaji na mchango mkubwa kwa filamu za Tanzania. Alikuwa zaidi ya mwigizaji — alikuwa sehemu ya msingi ya historia ya burudani nchini. Kizazi cha sasa na kijacho kitaendelea kujifunza kupitia kazi alizoziacha. 

0 Comment

Msanii Mkongwe wa Filamu Tanzania Hashim Kambi Afariki DuniaAfyaclass Bongo Social •

Msanii Mkongwe wa Filamu Tanzania Hashim Kambi Afariki Dunia

Tasnia ya filamu nchini Tanzania imepata pigo baada ya taarifa kuthibitisha kifo cha msanii mkongwe Hashim Kambi aliyefariki dunia leo tarehe 27 Aprili 2026.

Taarifa hizo zimethibitishwa na msemaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Coletha Raymond, kupitia mahojiano yake na vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa Coletha, marehemu alikuwa ametokea mkoani Tabora kwa shughuli za kikazi, na baada ya kurejea aliendelea moja kwa moja kwenye kazi nyingine eneo la Pilipili. Akiwa huko, alidaiwa kuanza kujisikia vibaya kabla ya kukimbizwa hospitalini, ambapo baadaye alifariki dunia.

Imeelezwa kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya presha pamoja na kisukari kwa kipindi fulani.

Shirikisho la Filamu Tanzania limeeleza kuwa linaendelea na vikao vya ndani ili kupanga taratibu zote zinazohusu mazishi pamoja na kutoa taarifa rasmi zaidi kwa umma.

Kifo cha Hashim Kambi ni pigo kubwa kwa wadau wa sanaa na mashabiki wa filamu nchini, kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza tasnia hiyo kwa miaka mingi.

Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na wadau wote wa sanaa nchini.

0 Comment

Tukio la Ufyatuaji Risasi Karibu na Chuo Kikuu cha Indiana Lawajeruhi 9Afyaclass Bongo Social •

Tukio la Ufyatuaji Risasi Karibu na Chuo Kikuu cha Indiana Lawajeruhi 9

Takriban watu tisa wameripotiwa kujeruhiwa kufuatia tukio la ufyatuaji risasi lililotokea karibu na kampasi ya Indiana University katika mji wa Bloomington mapema Jumapili usiku, Aprili 26.

Tukio hilo lilitokea muda mfupi katika eneo la Kirkwood Avenue, ambapo umati wa watu ulikuwa ukiendelea kusherehekea mbio maarufu za baiskeli za vyuo vikuu zinazojulikana kama “Little 500”.

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, milio ya risasi ilianza kusikika katika eneo la mtaa wa 400 East Kirkwood, umbali mfupi kutoka chuo hicho, na maafisa walipofika walikuta watu kadhaa wakiwa wamejeruhiwa.

Watu tisa walikimbizwa hospitalini, baadhi wakisafirishwa kwa magari ya wagonjwa. Hata hivyo, mamlaka hazijatoa taarifa rasmi kuhusu hali zao wala aina ya majeraha waliyoapata.

Mashuhuda wamesema chanzo cha tukio hilo kilianza kama ugomvi kati ya wanawake wawili, kabla ya mmoja wao kudaiwa kutoa silaha na kuanza kufyatua risasi ovyo.

Mmoja wa mashuhuda alieleza kuwa alidhani ni ugomvi wa kawaida hadi alipoona mtu akitoa silaha na kuanza kurusha risasi, hali iliyosababisha watu kukimbia kuokoa maisha yao.

Hadi sasa hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa, huku polisi wakiomba yeyote aliye na taarifa au video ya tukio hilo kujitokeza kusaidia uchunguzi.

Viongozi wa chuo wamesema hakuna ushahidi unaoonyesha wanafunzi wa Indiana University kuhusika moja kwa moja na tukio hilo.

Msemaji wa chuo hicho amesema tukio hilo limeharibu furaha ya wikendi ambayo ilipaswa kuwa ya sherehe, na amelaani vikali vurugu hizo huku akiwashukuru maafisa wa usalama waliokabiliana na hali hiyo.

Uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini chanzo kamili cha tukio hilo na kuwabaini waliohusika.

0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD