Bajeti ya wizara ya vijana,mambo yaliyowasilishwaAfyaclass Forum •

Bajeti ya wizara ya vijana

Bajeti ya Wizara ya Maendeleo na Vijana ikisomwa kwa mara ya kwanza

Bajeti ya Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana imesomwa kwa mara ya kwanza Bungeni Dodoma leo Aprili 20, 2026 tangu kuanzishwa rasmi kwa wizara hiyo na Rais Samia Suluhu Novemba 17 mwaka jana.

Akiwasilisha bajeti hiyo Aprili 20, 2026 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Joel Nanauka ameliomba Bunge liidhinishe Sh35.9 bilioni kwa mwaka wa fedha 2026/27 ili kutekeleza shughuli mbalimbali za wizara hiyo.

Awali masuala ya vijana yalikuwa yakishuguhulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu chini ya Waziri Ridhiwani Kikwete

Kwa mujibu wa Rais Samia lengo la kuanzisha wizara hiyo ni kuhakikisha vijana wanapata jukwaa la kusikika na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Pamoja na kuanzishwa kwa wizara hiyo Rais Samia aliahidi  kuanzisha kitengo cha washauri wa vijana ndani ya ofisi ya Rais.

Akizungumza leo Aprili 20, 2026 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Joel Nanauka, ameeleza kuwa kati ya bajeti hiyo inayosubiri kuidhinishwa na Bunge Sh30.1 bilioni zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Katika kiasi hicho cha matumizi hayo ya kawaida, Sh1.22 bilioni ni kwa ajili ya mishahara, huku Sh28.8 bilioni zikiwa kwa matumizi mengineyo (OC). 

Kwa upande mwingine Sh5.85 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambapo Sh5 bilioni ni fedha za ndani na Sh853.03 milioni ni fedha za nje.

Aidha, Nanauka amesisitiza ukubwa na umuhimu wa kundi la vijana nchini, akibainisha kuwa zaidi ya vijana milioni 20, sawa na asilimia 34.4 ya Watanzania, wanachangia zaidi ya asilimia 55 ya nguvu kazi ya taifa.

0 Comment

Howard Tucker,daktari mzee zaidi kuwahi kufanya kazi dunianiAfyaclass Forum •

Howard Tucker,daktari mzee zaidi kuwahi kufanya kazi duniani

Daktari wa Marekani, Howard Tucker, ametunukiwa rasmi rekodi ya Dunia ya Guinness (Guinness World Records) kama daktari mzee zaidi kuwahi kufanya kazi duniani, baada ya kuendelea na taaluma yake hadi akiwa na umri wa miaka 103.

Tucker, ambaye amekua mtaalamu wa magonjwa ya neva (neurologist), aliendelea kuwahudumia Wagonjwa wake kwa bidii hadi miezi miwili tu kabla ya kufariki dunia tarehe 22 Desemba 2025, uvumilivu wake kazini umevutia watu wengi duniani, ukionyesha kuwa umri si kikwazo kwa kujituma na kujitoa.

Kwa mujibu wa taarifa, maisha yake yalijikita katika taaluma ya tiba kwa zaidi ya miongo kadhaa, akihudumia jamii na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Sekta ya Afya.

Hadithi ya maisha yake sasa inaelezwa zaidi kupitia Mjukii wake, ikilenga kuhamasisha vizazi vijavyo kuhusu umuhimu wa kujituma, kujifunza na kufanya kazi kwa moyo wote hadi uzeeni.

0 Comment

Cristiano Ronaldo kucheza na mwanawe Cristiano Ronaldo Jr katika timu ya Al Nassr msimuAfyaclass Forum •

Cristiano Ronaldo kucheza na mwanawe Cristiano Ronaldo Jr katika timu ya Al Nassr msimu

Nyota wa soka duniani Cristiano Ronaldo (40) anaweza kuandika historia nyingine kubwa ya michezo iwapo atafanikiwa kucheza pamoja na mwanawe Cristiano Ronaldo Jr katika timu ya Al Nassr msimu ujao.

Ripoti kutoka vyombo vya habari vya Kiarabu zinasema kuwa klabu hiyo ya Saudi Arabia inaangalia uwezekano wa kumuinua kijana huyo mwenye umri wa miaka 15 kutoka timu za vijana na kumjumuisha kwenye kikosi cha wakubwa kutokana na maendeleo yake makubwa.

Cristiano Ronaldo Jr, ambaye tayari amewahi kucheza kwenye akademi za Real Madrid, Juventus na Manchester United, kwa sasa yupo kwenye mfumo wa vijana wa Al Nassr na ameonyesha uwezo mkubwa wa kufunga mabao kwa wingi.

Cristiano Ronaldo Jr

Inadaiwa kuwa amefunga zaidi ya mabao 50 katika misimu tofauti akiwa kwenye timu za vijana, jambo lililovutia macho ya makocha na viongozi wa klabu hiyo.

Iwapo mpango huo utakamilika, Cristiano Ronaldo angeweza kuungana na mwanawe uwanjani hali ambayo ingekuwa nadra sana katika historia ya soka la kiwango cha juu duniani.

Tukio hilo lingemfanya Ronaldo kuiga mfano wa wanamichezo wachache duniani waliowahi kucheza pamoja na watoto wao katika ngazi ya juu ya ushindani.

Kwa sasa, Al Nassr inaendelea kufanya vizuri katika ligi ya Saudi Arabia na inaongoza msimamo, huku Ronaldo akiwa bado miongoni mwa wafungaji bora wa timu hiyo akiwa na mabao kadhaa msimu huu.

Hata hivyo, uamuzi wa mwisho kuhusu kupandishwa kwa Cristiano Ronaldo Jr utategemea tathmini ya maendeleo yake mwishoni mwa msimu.

0 Comment

Mwanamke mmoja wa Nigeria ameshiriki tukio lililomfanya avunje ndoa yakeAfyaclass Forum •

Mwanamke mmoja wa Nigeria ameshiriki tukio lililomfanya avunje ndoa yake.

Judith Yop Pam-Tok, mtaalamu wa maendeleo ya jamii, alivunja ndoa yake mwaka 2009 - miaka 17 iliyopita.

Katika chapisho la Facebook Jumanne, alisimulia jinsi mumewe alivyoitikia bila kujali alipokuwa na changamoto ya kutokwa na damu nyingi baada ya Kubeba Mimba hali iliyopelekea kuamua kuvunja kabsa ndoa yake.

Alieleza kwamba alikuwa na mtoto wa miezi 8 ambaye alikuwa akimnyonyesha na tayari alikuwa na mimba ya miezi 2. Alisema alipoanza kutokwa na damu nyingi, mumewe alimpuuza na ilikuwa binti yake mkubwa, mwenye umri wa miaka 8, ambaye ilibidi aingie katika nafasi ya utu uzima ili kumsaidia.

Aliandika

“So this is how the events that finally broke the camel’s back unfolded.

People often say, “it ended suddenly.” But for many of us, it never does. It is a quiet accumulation of moments, each one chipping away at something sacred, until one day, clarity arrives. 

"This was mine. 

"It started with a new pregnancy, while I still had a baby barely six months old. My body had not even healed, yet life was already asking more of it. 

"By about two months into the pregnancy, I began to bleed. Perhaps it was my rhesus negative status, perhaps something else. 

"But one thing was certain, I needed medical attention. 

"A doctor at the Catholic hospital in Kubwa, (Daughters of Charity) had already scheduled me for an evacuation. Necessary. Urgent. Non-negotiable. 

"Yet, the man I was married to, the one who should have been concerned about my wellbeing, refused to take responsibility for the medical bills, not because he didn't have but because he just didn't care. 

"I was meant to return to the hospital. I thought I could hold on till Monday.

But that night, at about 9:00pm, while feeding my 8-month-old baby, everything changed. 

"A sudden, heavy “boom.” then Blood. I stood up immediately. What I saw on the floor… was beyond anything I had imagined. The blood. 

"I was scared. Confused. I walked to the corridor and stood, bleeding… and bleeding… until I found myself standing in a pool of my own blood. It was terrifying. 

"And yet, in that moment, instinct took over. I needed help. I asked my first daughter, to get me my phone. Even now, that detail stays with me, the role reversal, a child stepping into a moment no child should witness. But my 8yrs old child was more useful to me than a full grown adult. 

"All the while, he sat there. Watching. Silent.

No urgency. No alarm. No movement. Just… watching. 

"I called my brother, Dr. Ibrahim Ango, a gynaecologist. His response was immediate, “Judith, you need to get to the hospital now. If not, you could bleed to death.” 

"It was only then that the man I married spoke, I don't know if he heard what was being said, He just muted a “If you want me to take you to the hospital, let’s go.” (If I want!!!?) 

"I didn’t have the luxury of processing that statement. I went into the bathroom, had a wash, got dressed, and went to my neighbour to ask her niece to please watch my babies while we rushed out. 

"But even leaving for the hospital came with another moment I would never forget.

We lived in an official compound with eight flats, each with designated parking. My car was parked behind his. 

"So I moved my car, waiting for him to move his, But he refused. He did not want his car used. He did not want it stained with blood. So we used mine. 

"And then, he did something I still struggle to fully comprehend. He walked to the passenger seat,  and sat down. And I, the patient, bleeding, weak, and in distress, drove myself to the hospital. 

"Yes I drove the car with this man sitting on the passenger's seat beside me. Sometimes when I remember that moment, I feel a surge of anger,  because I was confronted with something deeply unsettling, the absence of basic humanity where I expected care. It was not just neglect. It was the coldness of it. The detachment. The willingness to remain untouched by someone else’s pain, someone you were meant  to take care of." 

She went on to narrate how she also got next to no support from her husband when they got to the hospital and how he left the hospital as soon as the doctor began attending to her. 

0 Comment

TANZIA:Muuguzi auwawa na mpenzi aliyemsomesha kisa wivu wa mapenziAfyaclass Forum •

TANZIA:Muuguzi auwawa na mpenzi aliyemsomesha kisa wivu wa mapenzi

Ofisa Muuguzi wa Hospitali ya Mji Same mkoani Kilimanjaro, Asha Bakari (25), anadaiwa kuuawa kwa kukatwa shingo na mpenzi wake, huku chanzo cha tukio hilo kikihusishwa na wivu wa mapenzi.

Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Aprili 21, 2026, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Mgeni amesema tukio limetokea jana Jumatatu, Aprili 20, 2026, katika Kata ya Kisima, karibu na hospitali hiyo.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, amesema mauaji hayo yalitokea saa tatu usiku.

Amesema Asha alikuwa akifanya kazi kwa kujitolea hospitalini hapo na alishambuliwa akiwa nyumbani kwake.

“Mtumishi wa Hospitali ya Mji Same aliuawa kwa kuchomwa kisu na mpenzi wake katika eneo la makazi karibu na hospitali aliyokuwa akifanya kazi,” amesema Mgeni.

Ameongeza kuwa kabla ya kutokea kwa mauaji hayo, alipigiwa simu na mtuhumiwa akimtaka wakutane, ndipo alipofika nyumbani kwake na kutekeleza mauaji hayo.

Kwa mujibu wa taarifa ya mkuu huyo, marehemu alikuwa na uhusiano na wanaume wawili, lakini mmoja wao na ndiye aliyemsaidia kumsomesha hadi kufikia hatua ya kupata ajira.

“Inadaiwa kuwa baada ya kuanza kazi alianza uhusiano mwingine na mtumishi wa hospitali hiyo, jambo lililomkera mtuhumiwa na kusababisha kutokea kwa tukio hili la kikatili,” amedai mkuu huyo wa wilaya akirejea taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi wilayani Same.

Mgeni amesema baada ya kutekeleza mauaji hayo, mtuhumiwa ambaye ni dereva wa bodaboda alitoroka na kutokomea kusikojulikana, huku juhudi za kumsaka zikiendelea.

“Tayari tumemtambua kwa jina na kazi yake. Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka, akipatikana atafikishwa kwenye vyombo vya sheria,” amesema.

Amesema muuguzi huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kushambuliwa kwa kuchomwa kisu shingoni.

Akizungumzia tukio hilo, Diwani wa Kisima, Kei Mbwambo amesema ni tukio la kinyama na kifo hicho ni pigo kwa wakazi wa eneo hilo kwa sababu ndiyo kwanza alikuwa ameanza kazi ya kuwahudumia.

“Hili ni tukio la kusikitisha na la kikatili. Haikubaliki kwa mtu kuchukua uhai wa mwingine kwa namna hii, hata kama kulikuwa na tofauti zozote za kimahusiano,” amesema Mbwambo.

Via:Mwananchi

1 Comment

Mawe kwenye mfuko wa nyongo (Gallstones) hutibiwa vipi?Afyaclass Forum •

 Mawe kwenye mfuko wa nyongo (Gallstones) hutibiwa vipi?

Mawe kwenye mfuko wa nyongo (Gallstones) hutibiwa kulingana na dalili Zake, ukubwa wake, na hali ya mgonjwa.

1. Kama hayana dalili

  • Mara nyingi hayatibiwi moja kwa moja
  • Unashauriwa:
    • Kula chakula chenye mafuta kidogo
    • Epuka uzito kupita kiasi
    • Fuata uchunguzi wa mara kwa mara

2. Kama yana dalili (maumivu, kichefuchefu, kutapika)

Hapa ndipo matibabu yanahitajika:

(a) Dawa

  • Dawa za maumivu
  • Dawa za kusaidia kuyeyusha mawe madogo
  • Na wakati mwingine huweza Kutumika kwa muda mrefu
  • Sio kwa kila mtu, na mawe yanaweza kurudi

(b) Upasuaji (Njia kuu na bora zaidi)

  • Kuondoa mfuko wa nyongo
  • Hufanyika kwa njia ya tundu dogo (laparoscopy)
  • Ni salama na wagonjwa wengi hupona haraka

3. Dalili za hatari (nenda hospitali haraka)

  • Maumivu makali upande wa juu kulia wa tumbo
  • Homa
  • Ngozi au macho kuwa ya njano
  • Kutapika sana

4. Vyakula vya kusaidia

  • Epuka: vyakula vya mafuta mengi (chips, nyama yenye mafuta)
  • Kula: mboga, matunda, nafaka zisizokobolewa
  • Kunywa maji mengi
Je,Una Changamoto hii na hujapata Suluhu? Kwa Ushauri Zaidi,Elimu na Tiba Tuwasiliane kwa namba +255758286584.
0 Comment

Cheti cha kuzaliwa cha mtoto,Maombi ya CHETI cha KuzaliwaAfyaclass Forum •

Cheti cha kuzaliwa cha mtoto,Maombi ya CHETI cha Kuzaliwa

Maelezo ya RITA juu ya Cheti cha Kuzaliwa na Upatikanaji wake.

Maombi ya Cheti cha Kuzaliwa

Usajili wa kuzaliwa unaweza kufanywa katika:

i.Katika kituo cha tiba au ngazi ya kitongoji kwa watoto wachanga (ndani ya siku 90)

ii.Katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya (usajili wa kuchelewa)

iii.Kwa mtandao (usajili wa kuchelewa, kubadilisha cheti cha zamani kuwa kipya)

Mtoto anasajiliwa mara tu baada ya kuzaliwa katika kituo cha tiba ambapo tukio la kizazi limetokea au katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata kwa vizazi vya nyumbani. Ikiwa kwa sababu fulani mtu anakosa kusajili mahali hapo, mtoto anaweza kusajiliwa wakati wa chanjo ndani ya siku 90. Aidha, tukio la kuzaliwa linaweza kusajiliwa kama usajili wa kuchelewa katika Ofisi ya Katibu wa Wilaya kwa kupitia mtandao.

Mahitaji ya jumla kwa maombi ya cheti cha kuzaliwa:

Mwombaji lazima aambatishe baadhi ya hati mbili kati ya zifuatazo:

  • Kadi ya Kliniki ya Mama
  • Kadi ya Kliniki ya Mtoto
  • Tangazo la kuzaliwa
  • Cheti cha Ubatizo cha Mtoto (kwa wale walio batizwa wakiwa na umri mdogo)
  • Cheti cha Kumaliza elimu (Shule za Msingi au Sekondari - O Level)
  • Pasi ya kusafiria
  • Kadi ya mpiga kura
  • Cheti cha ubatizo

Pamoja na mojawapo ya haya:

  • Kitambulisho cha Kitaifa cha mzazi/mlezi
  • Hati ya kusafiria ya mzazi
  • Utambulisho kutoka Mtendaji wa Kata

N.B: Uhitaji wa kuweka vitambulisho vya wazazi vitatumika ikiwa wazazi wapo hai.

USAJILI UNAVYOFANYIKA KWA WATOTO WACHANGA
Mwombaji (Mzazi/mlezi) atasajili tukio hili kwenye dawati la Usajili katika Kituo cha tiba kizazi kilipotokea wakati mtoto anapozaliwa au wakati wa kupata chanjo. Pia Usajili unaweza kufanyika katika ofisi ya kata kwa vizazi vya nyumbani.

Soma Zaidi kwenye Ukurasa Wao: https://www.rita.go.tz/page.php?p=9

0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD