Howard Tucker,daktari mzee zaidi kuwahi kufanya kazi duniani
Daktari wa Marekani, Howard Tucker, ametunukiwa rasmi rekodi ya Dunia ya Guinness (Guinness World Records) kama daktari mzee zaidi kuwahi kufanya kazi duniani, baada ya kuendelea na taaluma yake hadi akiwa na umri wa miaka 103.
Tucker, ambaye amekua mtaalamu wa magonjwa ya neva (neurologist), aliendelea kuwahudumia Wagonjwa wake kwa bidii hadi miezi miwili tu kabla ya kufariki dunia tarehe 22 Desemba 2025, uvumilivu wake kazini umevutia watu wengi duniani, ukionyesha kuwa umri si kikwazo kwa kujituma na kujitoa.
Kwa mujibu wa taarifa, maisha yake yalijikita katika taaluma ya tiba kwa zaidi ya miongo kadhaa, akihudumia jamii na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Sekta ya Afya.
Hadithi ya maisha yake sasa inaelezwa zaidi kupitia Mjukii wake, ikilenga kuhamasisha vizazi vijavyo kuhusu umuhimu wa kujituma, kujifunza na kufanya kazi kwa moyo wote hadi uzeeni.
You, Mehreen and others


