Mapacha tisa wa Mali watimiza miaka 4 kwa Sasa

Mapacha tisa wa Mali watimiza miaka 4 kwa Sasa

#1

Mnamo mwaka 2021, dunia ilishuhudia muujiza wa kipekee: mama Halima Cissé kutoka Mali alijifungua watoto tisa kwa mpigo — wavulana wanne na wasichana watano — tukio ambalo halijawahi kutokea tena kwa mafanikio duniani!



Serikali ya Mali iliwasafirisha yeye na mume wake, Abdelkader Arby, hadi Morocco kwa matibabu ya hali ya juu baada ya kugundua alikuwa na ujauzito wa mapacha 7. Lakini walipofika Morocco, walipokea mshangao mkubwa — walikuwa ni mapacha tisa!

Kutokana na tukio hilo la kipekee, Halima Cissé aliandikishwa rasmi katika Kitabu cha Rekodi za Dunia cha Guinness (Guinness World Records) kama mwanamke wa kwanza kuwahi kujifungua watoto tisa kwa mpigo na wote wakaishi, jambo lililovutia dunia nzima.

Sasa mapacha hao wametimiza miaka minne, wakiwa na afya njema na furaha kubwa. Wazazi wao hivi karibuni walisherehekea siku hiyo ya kipekee kwa kushiriki picha na kumbukumbu kupitia Instagram, wakikumbuka safari yao ya ajabu ya uzazi.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code