Showing posts with label Balozi Thabit Kombo. Show all posts
Showing posts with label Balozi Thabit Kombo. Show all posts

Waziri Mahmoud Thabit Kombo akutana na Mabalozi wa nchi mbali mbaliAfyaclass Forum •

Waziri Mahmoud Thabit Kombo akutana na Mabalozi wa nchi mbali mbali

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo leo katika kikao na Waandishi wa Habari, ameeleza kuwa amekutana na Wanadiplomasia wanaowakilisha Mataifa yao na Taasisi za kimataifa hapa Nchini wakiwemo Mabalozi wa Nchi mbalimbali na kuwaeleza kuhusu hali ya Tanzania kwa sasa.

Mazungumzo hayo yamefanyika hii leo Novemba 28, 2025 ambapo katika taarifa yake, Balozi Kombo amewahakikishia Mabalozi hao kuhusu dhamira ya Tanzania ya kuendeleza ushirikiano na Nchi pamoja na Taasisi wanazowakilisha.

Waziri Kombo amesisitiza kuwa Tanzania imepitia kipindi kigumu ambacho hakijawahi kutokea katika historia yake ambapo kwa sasa Taifa linaingia katika hatua ya kujenga upya, kuimarisha umoja, udugu na mshikamano wa kitaifa na kwamba Serikali ya Tanzania itahakikisha inafanya tathmini ya kina na kuchukua hatua muhimu zikiwemo majadiliano, uwajibikaji na kuimarisha Taasisi ili kuzuia kilichotokea kisitokee tena.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD