Showing posts with label Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Show all posts
Showing posts with label Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Show all posts

Hali ya Joto Kali nchini TMA yatoa TaarifaAfyaclass Forum •

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu kuongezeka kwa viwango vya joto katika maeneo mbalimbali nchini, hususan katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Ongezeko hilo limetokana na kusogea kwa Jua la Utosi pamoja na upungufu wa mvua katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni.

Kwa mujibu wa TMA, vipindi vya Jua la Utosi hufikia kilele mwishoni mwa Novemba wakati jua likielekea kusini kwenye Tropiki ya Kaprikoni, na hurudi tena mwezi Februari likielekea kaskazini kwenye Tropiki ya Kansa. Kipindi hicho Jua la Utosi huambatana na hali ya ongezeko la Joto kwa sababu uso wa Dunia katika eneo tajwa huwa karibu zaidi na Jua kuliko maeneo mengine.

Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha ongezeko kubwa la joto katika baadhi ya vituo vya hali ya hewa nchini, ambapo hadi kufikia tarehe 27 Novemba, 2025 kituo cha hali ya hewa cha Moshi (Kilimanjaro) kiliripoti kiwango cha juu zaidi cha nyuzi joto 35.7°C mnamo tarehe 21 Novemba, 2025 ikiwa ni ongezeko la nyuzi joto 4.2°C ukilinganisha na wastani wa muda mrefu kwa mwezi Novemba katika kituo hicho. Kituo cha hali ya hewa cha Ilonga (Morogoro) kiliripoti nyuzi joto 35.5°C mnamo tarehe 20 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.7°C). 

Kituo cha hali ya hewa Morogoro kiliripoti nyuzi joto 34.5°C mnamo tarehe 26 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.3°C). Kituo cha Ibadakuli (Shinyanga) kiliripoti nyuzi joto 33.6°C mnamo tarehe 14 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 2.2°C), na Dar es salaam nyuzi joto 33.2 °C mnamo tarehe 19 na 21 Novemba (ongezeko la nyuzi joto 1.6°C).

Hata hivyo, mamlaka hiyo imesema kuwa katika kipindi cha mwezi Desemba, 2025 vipindi vya mvua vinatarajiwa kujitokeza katika maeneo mengi nchini. Hali hii inatarajiwa kusababisha kupungua kwa

Joto katika baadhi ya maeneo hususan yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

TMA imewahimiza wananchi kufuatilia taarifa rasmi za utabiri wa hali ya hewa na kuchukua tahadhari ili kukabiliana na athari za vipindi vya joto kali.




0 Comment

Kimbunga Hidaya na kinachoendelea kwa sasaAfyaclass Forum •

Kimbunga Hidaya na kinachoendelea kwa sasa

Pwani ya Afrika Mashariki hususan Tanzania inatazamiwa kukumbwa na Kimbunga Hidaya ambacho kitasababisha mvua kubwa.

Mapema wiki hii Mamlaka ya hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitangaza kuwepo kwa mgandamizo mdogo wa hewa ambao ulitarajiwa kutawala na kusababisha mvua kubwa na upepo mkali katika mikoa mitano nchini ikiwa ni pamoja na Mtwara, Dar es Salaam, Lindi, maeneo ya Tanga, Morogoro, visiwa vya Pemba na Unguja pamoja na maeneo jirani.

Kimbunga Hidaya kilianza kujitengeza siku ya Jumatano kusini mwa Bahari ya Hindi kuelekea mashariki mwa Tanzania na kaskazini-mashariki mwa visiwa vya Komoro.

Kwa mujibu wa TMA, kufikia sasa mienendo ya mifumo ya hali ya hewa baharini bado inaonesha uwezekano mkubwa wa Kimbunga Hidaya kuendelea kusogea karibu na pwani ya Tanzania na kuendelea kuwepo hadi Jumatatu, Mei 6 2024.

Kulingana na mamlaka hiyo, kimbunga hicho kinaendelea kuimarika na kwamba hadi kufikia usiku wa kuamkia leo kasi yake ilikuwa imeimarika na kufikia kilomita 110 kwa saa.

Taarifa ya mamlaka hiyo aidha ilisema kwamba kimbunga hicho kitaendelea kuimarika na kuwa kikubwa zaidi katika saa 24 zijazo.

Tahadhari zilizotolewa na TMA?

Serikali imewashauri wananchi kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya hewa ili kupata ushauri na mwongozo wa wataalamu katika sekta husika kwa lengo la kujikinga na athari zinazoweza kuibuka.

TMA imesema kwamba ongezeko la mvua na upepo mkali utakaoambatana na mawimbi makubwa baharini vinatarajiwa kusambaa katika maeneo mengi ya ukanda wa pwani kuelekea tarehe 4 hadi 6 mwezi Mei 2024.

Kutokana na hilo, TMA imetoa tahadhari kwa wananchi katika maeneo husika na wote wanaojihusisha na shuguli mbalimbali baharini .

Vilevile Mamlaka hiyo imewataka Watanzania kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya Hewa.

Kenya imesema nini?

Serikali ya Kenya siku ya Alhamisi tarehe 2, Mei ilionya kwamba eneo la Pwani huenda likakumbwa na kimbunga Hidaya ndani ya siku chache zijazo kutokana na mvua kubwa inayoshuhudiwa kwa sasa kote nchini humo.

Onyo hilo lilitolewa baada ya kikao maalum cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Alhamisi kujadili hatua za ziada za kukabiliana na athari mbaya zinazoendelea za mafuriko, maporomoko ya udongo na maporomoko ya ardhi.

Baraza la Mawaziri lilifahamishwa kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa muda wa miezi mitatu ijayo, ambao ulionyesha kuwa mvua za wastani hadi juu ya wastani zitaendelea kunyesha katika maeneo yote ya nchi.

Kimbunga ni nini?

Kulingana na Shirika la Hali ya Hewa Ulimwenguni, kimbunga cha kitropiki – ni dhoruba inayozunguka kwa kasi ambayo huanza juu ya bahari ya kitropiki.

Kimbunga cha Kitropiki katika Bahari ya Hindi kina nguvu zaidi kuliko dhoruba ya kitropiki.

Ilipewa jina la ‘Hidaya’ na Meteo France La Reunion, huku mifano ya utabiri ikiifuatilia magharibi-kaskazini-magharibi kati ya Mei 2-4, 2024.

Kimbunga cha mwisho kuikumba Tanzania ilikuwa mwaka 1952 (wakati huo koloni la Tanganyika) na kilitua mkoani Lindi katika pwani ya kusini ya Tanzania.

Kimbunga cha mwisho kuikumba Zanzibar kilikuwa mwaka 1872 na athari zake zilifika mpaka upande wab ara katika eneo la Bagamoyo, kaskazini mwa Dar Es Salaam.

Ikiwa Kimbunga Hidaya kitatua kwa kasi, itakuwa ni mara ya kwanza katika historia kwa Dar Es Salaam kukumbwa na kimbunga.

Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania pia ilikuwa katika ya kupigwa na vimbunga vingine viwili, mwaka 2019 Kimbunga Kenneth kilitabiriwa kupiga mkoa wa Mtwara lakini hata hivyo kilibadili mwelekeo na kutua nchini Msumbiji.

Mwaka 2021 ilitolewa tahadhari ya Kimbunga Jobo lakini hata hivyo kilipunguza makali na hakikusababisha maafa yeyote makubwa.

Kimbunga Hidaya na kinachoendelea kwa sasa
0 Comment

TMA: Tahadhari juu ya Upepo mkali kutokea Leo,uwepo wa mgandamizo mdogo wa hewaAfyaclass Forum •

TMA: Tahadhari juu ya Upepo mkali kutokea Leo,uwepo wa mgandamizo mdogo wa hewa

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa mgandamizo mdogo wa hewa katika Bahari ya Hindi mashariki mwa Pwani ya Mtwara ambapo mifumo ya hali ya hewa iliyopo kwa sasa inaonesha kuwa mgandamizo huo mdogo wa hewa unatarajiwa kuimarika na kufikia hadhi ya kimbunga kamili Leo May 2, 2024.

TMA imesema wakati mgandamizo huo mdogo wa hewa ukiendelea kuimarika, unatarajiwa pia kusogea kuelekea baadhi ya maeneo ya Pwani ya Tanzania kuanzia usiku wa kuamkia siku ya Ijumaa May 3, 2024 na kuendelea kuwepo katika maeneo ya ukanda huo hadi May 6,2024 kisha utapungua nguvu baada ya May 6, 2024.

“Uwepo wa mgandamizo huo mdogo wa hewa unatarajiwa kutawala na kuathiri mifumo ya hali ya hewa hapa Nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha vipindi vya mvua kubwa na upepo mkali katika baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Morogoro, Dar es salaam na maeneo ya jirani hivyo Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya Wataalamu katika Sekta husika ili kujikinga na athari zinazoweza kujitokeza.

“Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa mgandamizo huo mdogo wa hewa na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa chini na itaendelea kutoa taarifa mara kwa mara kila inapobidi” – imeeleza taarifa ya TMA

TMA: Tahadhari juu ya Upepo mkali kutokea Leo,uwepo wa mgandamizo mdogo
wa hewa
0 Comment

MVUA kubwa kwenye Mikoa 16 Tanzania bara,chukua tahadhariAfyaclass Forum •

MVUA kubwa kwenye Mikoa 16 Tanzania bara,chukua tahadhari.

Mikoa hiyo ni Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga, Simivu. Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema baadhi ya maeneo katika mikoa 16 ya Tanzania bara na visiwa na Unguja na Pemba zitashuhudia mvua kubwa leo Ijumaa, Aprili 26, 2024.

Mikoa hiyo ni Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga, Simivu, Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa na visiwa vya Unguja na Pemba.

Taarifa hiyo imetolewa leo Aprili 26, 2024 na TMA huku ikiweka angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili.

Upepo huo ni kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya  Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara na visiwa vya Unguja na Pemba).

“Athari zinazoweza kujitokeza, baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini,” imeelezwa na TMA.

Kwa siku zilizobaki kuanzia Aprili 27 hadi Aprili 30, TMA imetoa tahadhari ya ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mita mbili.

Upepo huo ni kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba) na ukanda wa ziwa Nyasa (Mikoa ya Songwe, Njombe na Ruvuma).

Aprili 28, 2024, TMA imesema kutakuwa na upepo mkali unaoziDi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili.

“Tahadhari hiyo ni kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya bahari ya Hindi (mikon ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba) na ukanda wa ziwa Nyasa (Mikoa ya Songwe, Njombe na Ruvuma,” imeandikwa.

Aprili 29, TMA imesema upepo mkali wa kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayouzidi mita mbili itakumba baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Aprili 30, Upepo mkali wa kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili pia itashuhudiwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba).

MVUA kubwa kwenye Mikoa 16 Tanzania bara,chukua tahadhari
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD