Afyaclass Bongo Social Mtoto aliyeokolewa kutoka tumboni mwa mamake afariki

Mtoto aliyeokolewa kutoka tumboni mwa mamake aliyeuawa Gaza Afariki.

Mtoto aliyeokolewa kutoka tumboni mwa mamake aliyekuwa mahututi baada ya shambulizi la anga la Israel kusini mwa Gaza amefariki, BBC imebaini.

Mtoto Sabreen al-Sakani alizaliwa kupitia upasuaji katika hospitali ya Rafah muda mfupi baada ya saa sita usiku Jumapili.

Hata hivyo alifariki siku ya Alhamisi na amezikwa karibu na mama yake.

Mtoto Sabreen alikuwa miongoni mwa watoto 16 waliouawa katika mashambulizi mawili ya anga huko Rafah wikendi iliyopita.

Wote waliuawa katika shambulio la bomu lililolenga nyumba walimokuwa wakiishi.

You, Mehreen and others
Hashtag:

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD