Afyaclass Bongo Social TANZIA: Ngugi wa Thiong’o afariki dunia,Mwandishi gwiji wa Fasihi

TANZIA: Ngugi wa Thiong’o afariki dunia,Mwandishi gwiji wa Fasihi



Ngugi wa Thiong’o Mwandishi gwiji wa fasihi kutoka Kenya, ameripotiwa kufariki dunia leo Mei 28, 2025, akiwa na umri wa miaka 87 ambapo taarifa rasmi zinaeleza kuwa Mwandishi huyo mashuhuri amefariki akiwa Marekani ambako amekuwa akiishi na kufundisha kwa miaka mingi.

Ngugi alitambulika kwa kazi zake mashuhuri kama Weep Not, Child, The River Between, na Petals of Blood, pamoja na maandiko ya kiitikadi kama Decolonising the Mind vilevile alikuwa mtetezi thabiti wa matumizi ya lugha za Kiafrika katika elimu na fasihi na alihamasisha uhuru wa kiakili kupitia maandiko yake yenye nguvu ya kisiasa na kijamii.

Mbali na kuwa mwandishi, Ngugi pia alikuwa Mwalimu na Mwanafikra ambaye alitoa mchango mkubwa katika vyuo vikuu mbalimbali, hasa Chuo Kikuu cha California, Irvine.

You, Mehreen and others
Hashtag:

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD