Showing posts with label ARVs. Show all posts
Showing posts with label ARVs. Show all posts

Dawa za ARV,Matumizi Sahihi ya dawa za ARVAfyaclass Forum •

Dawa za ARV,Matumizi Sahihi ya dawa za ARV



Moja kati ya vitu vya msingi vya kuzingatia ukiwa muathirika wa ugonjwa wa VVU/UKIMWI ni matumizi sahihi ya dawa.Watu wengi wamepotoshwa na taarifa za uongo kuwa  dawa hizi hupunguza nguvu za kiume hivyo wagonjwa wengi wa UKIMWI hawatumii dawa  hizi na badala yake hutumia mitishamba au kutokutumia dawa kabisa.

Tafiti nyingi zimefanyika na kuonyesha kwamba dawa hizi zina uwezo mkubwa wa kuzuia magonjwa yatokanayo na UKIMWI na kuzuia vifo. Aidha dawa  hizi zimeonyosha uwezo mkubwa wa kupunguza maambukizi ya mama kwa mtoto.Matumizi ya dawa  za kufubaza makali ya virusi vya VVU/UKIMWI kwa waathirika wa ugonjwa huu yanahusishwa na  kupungua kwa hatari ya kueneza maambukizi ya virusi vya VVU/UKIMWI wakati wa kushiriki tendo la ndo  kwa sababu ya uwezo wake wa kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI.

KUKMBUKA dawa hizi sio tiba ya virusi vya VVU/UKIMWI.

Utaratibu wa Kuanza Dawa

Kulingana na miongozo ya matibabu ya VVU/UKIMWI anashauriwa kuanza dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI mara tu anapogundulika kuwa ni muathirika wa virusi vya VVU/UKIMWI na kupewa ushauri nasaha. Hii husaidia sana kupunguza makali ya virusi hivi.

Utaratibu wa kuanza dawa huambatana na kujisajili kwenye za kliniki za CTC ambazo zipo kwenye takribani vituo vyote vya afya nchini. Ukishajisajili utapewa namba pamoja na kadi ambayo itakuwa na taarifa zako zote muhimu kama muda au tarehe ya kumuona dakatri, aina na kiwango cha dawa  unachotumia , wingi wa virusi vya VVU kwenye damu (viral load) na kiwango cha CD4.

Endapo uligundulika na virusi vya VVU/UKIMWI na umeshaanza kupata magonjwa nyemelezi, basi utaanza matibabu ya magonjwa hayo na kuanzishiwa dawa za kufubaza virusi vya ukimwi ndani ya wiki mbili.

Kuna baadhi ya magonjwa ikiwemo kifua kikuu (PTB)   pamoja na ugonjwa wa kukakamaa shingo (Cryptococcoal Meningitis) huwa kuanza kutumia dawa haraka sio vizuri kwani inaongeza hatari ya kupata mchafuko wa kinga ya mwili (Immune Reconstitution Inflammatory Syndrome- IRIS) ambayo huzidisha dalili za magonjwa nyemelezi.

Hali hii hutokea kwa sababu madawa ya kufubaza virusi vya UKIMWI husaidia kuongeza kinga ya mwili na hivyo mwili huanza vita na magonjwa nyemelezi ambayo mwanzo mwili ulikuwa hauna uwezo wa kuyadhiti hii huleta mchafuko wa kinga ya mwili na kuzidisha  dalili zilizopo au kusababisha dalili mpya za magonjwa nyemelezi.

Matumizi Sahihi ya Dawa za Kufubaza Makali ya Virusi vya VVU/UKIMWI (ARV)

Matumizi sahihi ya dawa za kufubaza makali ya virusi vya VVU/UKIMWI ni muhimu sana kwani usipofanya hivyo unaweza kupata madhara makubwa zaidi ikiwemo ugonjwa wa UKIMWI kuja kwa kasi zaidi, hali hii huchangia sana mgonjwa kupoteza maisha. Hivyo hakikisha unapata maelekezo yote kuhusu utumiaji wa dawa kutoka kwa daktari wako.

Dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI zipo kwenye makundi mbalimbali. Tafiti tofauti pamoja na miongozo ya matibabu ya VVU/UKIMWI zimependekeza matumizi ya dawa zifuatazo; Tenofovir disoproxil fumarate(TDF), Lamuvidine(3TC), Dultegravir(DTG) kama dawa za kwanza dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI (first line treatment).

Yapo makundi mbalimbali ya mchanganyiko wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya VVU/UKIMWI ambayo  yanaweza kutumika kulingana na kundi analotoka mgonjwa  mfano watoto wadogo, mama mjamzito au kulingana na jinsi ambavyo dawa hizi  hufanya kazi kwa mtu binafsi n.k

Dawa hizi za mchanganyiko hupatikana kama dawa moja  ambayo humezwa kila siku. Dawa hii ya mchanganyiko wa madawa mbalimbali ina nguvu sana hivyo unashauriwa kula lishe bora wakati wote ili kupunguza maudhi madogo madogo yanayotokana na dawa hizi.

Hata hivyo,imeripotiwa kuwa baadhi ya waathirika hupata madhara kutokana na matumizi ya dawa hizi zilizochanganywa  kwa pamoja, endapo mgonjwa atapata madhara ya dawa hizi, basi anashauriwa kumuona daktari haraka iwezekanavyo kwa ajili ya uchunguzi wa kina ili kugundua  ni aina gani  ya dawa inayomsababishia mgonjwa madhara.

Pindi unapougua epuka kununua madawa na kutumia bila kumuona daktari wako. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya dawa huingiliana na dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI katika utendaji kazi hivyo hupelekea kupungua kwa nguvu ya dawa au dawa kubaki mwilini kwa muda mrefu sana (toxicity). Mambo yote hayo tajwa yana madhara kwa mtumiaji.

Pia unashauriwa kupunguza na kuacha unywaji wa pombe.

Muhimu: Hakikisha unameza dawa kwa kufuata maelekezo ya daktari na epuka kuruka ruka kumeza dawa au utoro wa kuhurudhia kliniki ili kuepuka  madhara  zaidi. Credits:TanzMed.

0 Comment

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)Afyaclass Forum •

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

ARVs ni kifupi cha neno antiretroviral drugs, ikiwa na maana ya dawa kwa ajili kupunguza makali ya Virusi vya Ukimwi,

Hivo basi ARV sio dawa moja bali ni kundi au mjumuisho wa dawa zote ambazo hutumika kwa Mgonjwa mwenye virusi vya Ukimwi(VVU) na mfano wa dawa hizo ni kama vile;

  •  Zidovudine
  • Tenofovir
  • Abacavir
  • Lamivudine
  • Didanosine
  • Emtricitabine n.k

Dawa za VVU zinaweza kusaidia kupunguza wingi wa virusi, kupambana na maambukizi, na kuboresha maisha yako. Zinaweza kupunguza uwezekano wa kusambaza VVU pia, lakini kama ukizitumia vibaya, bado unaweza kuwapa wengine VVU,

Kumbuka pia; Dawa hizi za ARVs Sio tiba ya kuondoa kabsa VVU.

>>Malengo ya dawa hizi ni:

  • Kudhibiti ukuaji wa virusi vya Ukimwi(VVU)
  • Kuboresha mfumo wako wa kinga ya mwili Kufanya kazi vizuri
  • Kupunguza Dalili au kuzuia kabsa dalili za Ukimwi kujitokeza
  • Kuzuia maambukizi ya VVU kwa wengine.n.k

Imeidhinishwa matumizi ya zaidi ya dazeni mbili za dawa za kurefusha maisha kwa ajili ya maambukizi ya VVU. Mara nyingi dawa hizi(ARVs) hugawanywa katika makundi sita kwa sababu hufanya kazi kwa njia tofauti. Madaktari wanapendekeza kuchukua mchanganyiko au “cocktail” ya angalau dawa kwenye makundi mawili. Hii inaitwa tiba ya kurefusha maisha, au antiretroviral therapy(ART).

Daktari wako atakujulisha hasa jinsi unapaswa kutumia dawa zako kwa usahihi. Unahitaji kufuata maagizo haswa, na haupaswi kukosa hata dozi moja. Ukikosa dozi, unaweza kupata aina za VVU zinazokinzana na dawa, na dawa zako zinaweza kuacha kufanya kazi.

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

Haya ni baadhi ya makundi ambapo dawa za ARVs zimegawanywa;

1. Nucleoside/Nucleotide Reverse Transcriptase Inhibitors (NRTIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Abacavir, or ABC (Ziagen)
  • Emtricitabine, or FTC (Emtriva)
  • Lamivudine, or 3TC (Epivir)
  • Tenofovir alafenamide, or TAF (Vemlidy)
  • Tenofovir disoproxil fumarate, or TDF (Viread)
  • Zidovudine or ZDV (Retrovir)

2.Non-nucleoside Reverse Transcriptase Inhibitors (NNRTIs)

Hapa kuna dawa kama vile;

  • Doravirine, or DOR (Pifeltro)
  • Efavirenz or EFV (Sustiva)
  • Etravirine or ETR (Intelence)
  • Nevirapine or NVP (Viramune)
  • Rilpivirine or RPV (Edurant)

3.Protease Inhibitors (PIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Atazanavir or ATV (Reyataz)
  • Darunavir or DRV (Prezista)
  • Lopinavir + ritonavir, or LPV/r (Kaletra)
  • Ritonavir or RTV (Norvir)

4. Integrase Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Bictegravir or BIC (combined with other drugs as Biktarvy)
  • Cabotegravir and rilpivirine (Cabenuva)
  • Dolutegravir or DTG (Tivicay)
  • Elvitegravir or EVG (Vitekta)
  • Raltegravir or RAL (Isentress)

5.Fusion Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Enfuvirtide, or ENF or T-20 (Fuzeon)

6.Capsid Inhibitor

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  •  Lenacapavir(Sunlenca) n.k

Kumbuka; Dawa hizi hutumii moja peke yake zinakuwa kwenye mchanganyiko wa zaidi ya dawa moja(combination) Mfano;

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Elvitegravir + TDF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)
Elvitegravir + TAF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)

Bictegravir + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or BIC/TAF/FTC (Biktarvy)
Dolutegravir + abacavir + lamivudine, or DTG/ABC/3TC (Triumeq)
Dolutegravir + rilpivirine, or DTG/RPV (Juluca)
Dolutegravir  + lamivudine, or DTG/3TC (Dovato)
Elvitegravir + cobicistat +  tenofovir alafenamide + emtricitabine, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)
Elvitegravir + cobicistat + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Darunavir + cobicistat + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or DRV/c/TAF/FTC) (Symtuza)
Non-nucleoside reverse transcriptase inhibitor (NNRTI)-based:

Doravirine + tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or DOR/TDF/3TC (Delstrigo)
Efavirenz + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EFV/TDF/FTC (Atripla)
Rilpivirine + tenofovir alafenamide + emtricitabine , or RPV/TAF/FTC (Odefsey)
Rilpivirine + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or RPV/TDF/FTC (Complera)

Abacavir + lamivudine, or ABC/3TC (Epzicom)
Abacavir + lamivudine + zidovudine, or ABC/3TC/ZDV (Trizivir)
Tenofovir alafenamide + emtricitabine, or TAF/FTC (Descovy)
Tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or TDF/FTC (Truvada)
Tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or TDF/3TC (Cimduo)
Zidovudine + Lamivudine or ZDV/3TC (Combivir) N.K

>> Soma pia hapa kuhusu Muda sahihi wa Kutumia dawa za ARVs

>> Tofauti ya ARVs na PEP

Kuna PEP,PrEP,ARVS

Dawa za Kurefusha maisha(ARVs);

Dawa hizi sio za kutibu au kuponyesha kabsa Ukimwi bali hufanya kazi ya kupunguza Virusi vya ukimwi (Viral Load) hali ambayo huupa nafasi Mfumo wa kinga ya mwili kupambana vizuri na maambukizi haya.

Ili dawa hizi zilete matokeo mazuri unashauriwa kutokuacha kutumia dawa kutokana na maelekezo uliyopewa, kwani ni hatari na unaweza kutengeneza hali ya virusi kutokusikia dawa yaani Drug resistance.

Je ni Muda gani wa kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una HIV?

Zipo Dhana mbali mbali kwenye jamii kuhusu Muda wa Kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una Virusi vya UKIMWI,

Huku baadhi ya watu wakisema,hutakiwi kuanza dawa za ARVs mpaka uanze kuumwa, je ni kweli?

Soma zaidi hapa chini…!!!

Tiba ya VVU inahusisha unywaji wa dawa zenye ufanisi mkubwa yaani antiretroviral therapy (ART) ambazo hufanya kazi kudhibiti virusi.

ART inapendekezwa kwa kila mtu mwenye VVU.

Watu walio na VVU wanapaswa kuanza ART haraka iwezekanavyo baada ya utambuzi (hata siku hiyo hiyo).

Nimatumaini yangu kwamba umepata majibu kuhusu Muda wa kuanza dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi maarufu kama ARVs.

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD