Connect with us

magonjwa ya watoto

Tatizo la KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,Damu

Doctor Ombeni

Published

on

349 Views
0 Comments

KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,Damu,Sababu ni nini?

Zipo dalili mbali mbali huweza kujitokeza kwenye Kitovu cha Mtoto wako,Ukiona Dalili hizi,hakikisha Mtoto anapata Msaada, Dalili hizi ni hatarishi sio nzuri wake:

  • Kitovu kinatoa usaha wenye harufu mbaya
  • Damu inatoka mara kwa mara
  • Ngozi kuzunguka kitovu kuwa nyekundu au kuvimba
  • Mtoto ana homa au analia sana
  • Kitovu hakikauki hata baada ya siku 7–14

Sababu zinazoweza kusababisha

1.Maambukizi ya bakteria (kutokana na uchafu au utunzaji mbaya)

2.Kitovu kubaki na unyevunyevu muda mrefu

3.Kitovu Kuguswa na vitu vichafu (mfano majivu, mafuta, dawa za asili zisizo salama) n.k

Nini cha kufanya

Hii ni hali ya muhimu—usichelewe:

Mpeleke mtoto hospitali au kituo cha afya mara moja Au Ongea na Mtaalam wa Afya au Kwa Ushauri Zaidi na Tiba tuwasiliane hapa hapa afyaclass,kupitia namba +255758286584(Call,Sms,Whatsapp).

-Usitumie dawa za kienyeji au kubonyeza kitovu bila Ushauri Sahihi.

-Acha kitovu kiwe kikavu (dry cord care) usiweke maji au Vitu vitakavyoongeza unyevu unyevu

-Epuka kukifunika kwa diaper

-Usikigusie mara kwa mara

Kwa mtoto mchanga, maambukizi ya kitovu yanaweza kuenea haraka mwilini, hivyo ni muhimu kuchukua hatua mapema.

YAPO BAADHI YA MAMBO MUHIMU SANA YA KUZINGATIA KUHUSU KITOVU CHA MTOTO

1-Mama hakikisha kitovu cha mtoto hakivuji damu baada ya kukatwa na kufungwa na mtaalam wa afya.

2-Kitovu hudondoka chenyewe,ambapo kwa asilimia kubwa kwa watoto wengi ndani ya wiki moja,kitovu huwa tayari kimeshadondoka.

3-Hakikisha kitovu cha mtoto hakitoi usaha,au kubalika rangi hasa ya manjano na kutoa harufu mbaya,hii sio dalili nzuri.

4-Usiweke kitu chochote kwenye kitovu cha mtoto mpka kidondoke chenyewe.

5-Epuka imani potofu kama zile za kuweka mavi ya Ng’ombe n.k,kwenye kitovu cha mtoto.

KWA USHAURI,ELIMU AU MSAADA WA KIAFYA MAWASILIANO NI +255758286584.

349 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Guest Avatar

LATEST POSTS

Utafiti3 hours ago

Vifo Vinavyotokana na Mimba kutunga Nje ya Kizazi

Mimba kutunga nje ya kizazi (ectopic pregnancy) ni hali ambayo mimba inajipandikiza nje ya sehemu ya kawaida ya kizazi,Mara nyingi...

Utafiti6 hours ago

Ucheleweshaji wa huduma Ndani ya Hospitali Wawa Tishio Kubwa kwa Maisha ya Mama na Mtoto

Ucheleweshaji wa huduma ndani ya vituo vya afya umeonekana kuwa moja ya sababu kubwa zinazochangia vifo vya wajawazito na watoto...

Afya News16 hours ago

Jinsi Dawa za Kulevya Zinavyoharibu Afya ya Kinywa na Meno

Matumizi ya dawa za kulevya yanaweza kuathiri sehemu mbalimbali za mwili, ikiwemo ubongo, moyo, ini na mfumo wa fahamu. Hata...

magonjwa2 days ago

Ugonjwa wa Selimundu,dalili,chanzo na Tiba

Katika Makala hii tunachambua Zaidi kuhusu Dalili za ugonjwa wa seli mundu,chanzo cha ugonjwa wa Seli mundu pamoja na Matibabu...

Afya News2 days ago

Wataalam wa maabara wahimizwa kuboresha huduma za afya kwa Wananchi

WATAALAM WA MAABARA WAHIMIZWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI Na Zakayo Mosha- WAF Morogoro Wataalam wa Maabara wamehimizwa kutumia...

Ebola2 days ago

DRC yahitaji wahudumu na vitanda zaidi kupambana na Ebola

Mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeendelea kuleta changamoto kubwa kwa mfumo wa afya, huku Shirika...

magonjwa1 year ago

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba Genital warts ni ugonjwa gani,Soma Zaidi hapa kufahamu Genital warts ni moja ya aina...

magonjwa2 years ago

Vipele Sehemu Ya Siri,Vipele Ukeni, Vipele Kwenye Uume

VIPELE SEHEMU YA SIRI,VIPELE UKENI, VIPELE KWENYE UUME Vipele kwenye Uume: Vipele Kwenye Uume: Chanzo, Dalili na Matibabu Tatizo la...

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips3 days ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

350
0