Showing posts with label Catherine Russell. Show all posts
Showing posts with label Catherine Russell. Show all posts

Chanjo huzuia Vifo million 3.5 ila Zaidi ya watoto milioni 14 hawakuchanjwa 2024Afyaclass Forum •

Chanjo huzuia Vifo million 3.5 ila Zaidi ya watoto milioni 14 hawakuchanjwa 2024



Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya watoto milioni 14 hawakupata chanjo kabisa mwaka 2024.

Kulingana na makadirio ya Umoja wa Mataifa, chanjo huzuia vifo milioni 3.5 hadi 5 kwa mwaka.

Taarifa ya pamoja ya Shirika la Afya Duniani, WHO, na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto, UNICEF, iliyotolewa Jumanne, imeeleza kuwa barani Ulaya na Asia ya Kati, viwango vya wastani vya chanjo ya watoto vilishuka kwa asilimia 1.

Maafisa wameonya kwamba kuenea kwa habari potofu na kupunguzwa kwa misaada ya kimataifa kunaongeza pengo la chanjo na kuwaweka malioni ya watoto hatarini.

Nchi tisa ndiyo zimechangia zaidi ya nusu ya watoto wasiokuwa na chanjo duniani.

Nchi hizo ni pamoja na Nigeria, India, Sudan, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Ethiopia, Indonesia, Yemen, Afghanistan, na Angola.

Mkurugenzi Mkuu wa UNICEF, Catherine Russell, amesema mamilioni ya watoto bado hawajapata chanzo za kuwaepusha na magonjwa yanayoweza kuzuilika, na kwamba jambo hilo linatia wasiwasi.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD