Showing posts with label Dawa ya ugonjwa wa macho mekundu. Show all posts
Showing posts with label Dawa ya ugonjwa wa macho mekundu. Show all posts

Dawa zisizo rasmi za macho mekundu(Red Eyes) zitawapa UpofuAfyaclass Forum •

Dawa zisizo rasmi  za macho mekundu(Red Eyes) zitawapa Upofu

Serikali kupitia Wizara ya Afya imewaasa Wananchi kuacha tabia ya kutumia dawa zisizo rasmi za macho kwa lengo la kutibu ugonjwa wa macho mekundu (Red Eyes),

kwakuwa matumizi hayo yanaweza kupelekea upofu usiotibika kama ambavyo itakuwa kwa wengi wa Wagonjwa waliokwisha kupata madhara kwenye kioo cha jicho kwa kutumia vitu hivyo.

Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Wizara ya Afya Prof. Paschal Ruggajo amesema hayo leo Jijini Dar es salaam ambapo amesema ugonjwa wa ‘Red Eyes’ hauleti upofu lakini matumizi ya dawa zisizo rasmi na zinazonunuliwa kiholela yanaweza kupelekea upofu usiotibika kama ambavyo inaweza kuwapata baadhi ya Wagonjwa waliopata vidonda kwenye kioo cha jicho baada ya kutumia dawa hizo zisizo rasmi.

Amesema baadhi ya vitu vinavyotumika ni pamoja na dawa zenye vichocheo vya ‘steroids’ ambazo Wananchi wanakwenda kununua wenyewe kwenye maduka ya dawa, tangawizi, chai ya rangi illiyokolea majani, mafuta tete yaliyokuwa yakitumika wakati wa janga la Covid – 19, maji ya chumvi na maziwa ya Mama, ambavyo vitu vyote hivyo sio salama na havijaelekezwa na Wataalamu.

Wizara imeendeleza kusisitiza Jamii kuzuia kuenea kwa maambukizi haya kwa kuzingatia usafi binafsi na kanuni za afya ikiwa ni pamoja na usafi wa mikono na uso, kuzuia kugusa macho , kunawa mikono na maji tiririka na sabuni au kutumia vipukusi mara kwa mara, kuzingatia kutokushikana mikono maeneo ya sehemu za ibada, kutumia taulo au leso za karatasi kufuta tongotongo au machozi na kufika kwenye kituo cha kutolea huduma pale Mtu apatapo dalili za Red Eyes.

Soma Zaidi; Ugonjwa wa macho mekundu(Red eyes)

Dawa zisizo rasmi za macho mekundu(Red Eyes) zitawapa Upofu
0 Comment

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na MatibabuAfyaclass Forum •

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu

Ugonjwa wa macho mekundu ni ugonjwa ambao hujulikana kama Red Eyes,

Ugonjwa wa red eyes ni ugonjwa ambao huhusisha macho kuwa mekundu kama dalili kubwa.

Katika Makala hii tumechambua chanzo cha Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes), dalili Zake kuu, jinsi ya kuzuia usipate Pamoja na Matibabu yake.

CHANZO CHA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

Ugonjwa wa Macho mekundu(Red Eyes) hutokana na mashambulizi ya vimelea vya magonjwa kama vile Virusi ambavyo husababisha vishipa vidogo ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

Maambukizi ya kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalam “Viral Keratoconjunctivitis” ni Maambukizi yanayosambaa kwa kasi kubwa .Hakuna tiba maalum kwa ugonjwa huu na hata bila tiba, dalili huisha zenyewe ndani ya wiki mbili . Usafi ni jambo muhimu katika kuzuia maambukizi haya kusambaa kwa wengine.

Mlipuko huu husababishwa na Kirusi kijulikanacho kwa jina la “Adenovirus”kwa zaidi ya asilimia 80%.

Dalili za Ugonjwa wa Macho Mekundu

DALILI ZA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NI PAMOJA NA;

• Macho kubadilika rangi na kuwa mekundu,

hii ni ishara ya Vishipa vidogo vya damu ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

• Kuwashwa na macho

• Kuhisi kitu kama mchanga ndani ya jicho lako

• Kuvimba macho yako

• Kuhisi hali ya kuungua ndani ya macho,

Hii ni ishara ya kutengeneza hali ya vidonda ndani ya jicho(Conjunctivitis Sore),

• Macho kuwasha au kutoa maji/nachozi yenyewe n.k

Ni nini cha Kufanya Kama Una Ugonjwa wa Macho Mekundu(Red Eyes)?

Ikiwa jicho lako haliumi na kuona kwako hakujaathiriwa, labda sio jambo kubwa. Ugonjwa huu wa macho mekundu(Red Eyes) unaweza kupona wenyewe ndani ya siku chache.

Mpaka Unapona Unashauriwa;

  • Kutokugusa au kusugua macho yako
  • Usivae miwani inayogusa macho, na kama kuna ulazima wa kuvaa,Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa
  • Zingatia Usafi

JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

– Watoto wadogo Wagonjwa wanaoenda shule wanashauriwa wakae nyumbani hadi dalili zinapoisha kwa kuwa ni ngumu kuzuia maambukizi yasisambae kwenye mazingira ya shule.

– Watu wazima wanaweza kwenda kazini ila wanapaswa kuzingatia kanuni za kuzuia kutokuambukizwa au kuambukiza wengine kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

– Watumishi wa Afya wazingatie kutopeleka Maambukizi hayo nyumbani kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

Zingatia Zaidi Mambo Haya Muhimu;

1. Usisugue au kupikicha macho yako,

Uchafu pamoja na Viini vya magonjwa(germs) kwenye mikono yako pamoja na Vidole vinaweza kusababisha hali Zaidi ya Wekundu na Muwasho ndani ya macho.

2. Kama unavaa miwani, Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa

3. Zingatia Usafi kwa Ujumla, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mikono yako unanawa kwa maji safi tiririka na Sabuni

4. Kwa Wale wanaopaka MakeUp, Hakikisha unaondoa MakeUp yako Vizuri na kuacha macho yako yakiwa Safi(Remove your eye makeup properly, and keep your eyes clean).

5. Pata Mapumziko ya mara kwa mara, ikiwa unafanya kazi zinazohusisha kuangalia computer screen kwa Muda Mrefu.

6. Epuka vitu ambavyo huweza kuleta usumbufu(irritation) wowote machoni kama vile; vumbi,moshi n.k

7. Hakikisha unaenda kuchunguzwa macho au kufanya Vipimo vya macho(Eye exam) ikiwa una shida ya macho kuwa mekundu mara kwa mara au Ikiwa hali ya macho kuwa mekundu haiishi.

MATIBABU YA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU(RED EYES)

– Ugonjwa huu wa Macho mekundu(red eyes) hupona wenyewe ndani ya siku 3 mpaka 5, ndani ya wiki 2 n.k kulingana na uwezo au uimara wa kinga yako ya mwili Wala huhitaji matumizi ya dawa yoyote ile.

Japo lazima kwanza kuchuguzwa na wataalam wa afya baada ya kujihakikishia kuwa ni shida ya red eyes watakupa maelekezo kwa kina ikiwa ni pamoja na jinsi ya kutunza jicho lako.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD