Showing posts with label Dawa za VVU. Show all posts
Showing posts with label Dawa za VVU. Show all posts

Mwaka 2023:Watu 8,145,576 walipima Virusi vya UKIMWI (VVU)Afyaclass Forum •

Mwaka 2023:Watu 8,145,576 walipima Virusi vya UKIMWI (VVU)

Wizara ya Afya imesema kati ya Watu waliopima mwaka 2023, Watu 163,131 walingundulika kuwa na maambukizi ya VVU ukilinganisha na Watu 182,095 mwaka 2022 na Watu 198,042 mwaka 2021 (DHIS2 2023) ambapo waliokuwa wanatumia dawa za kufubaza virusi vya VVU walikuwa 1,663,651 hadi kufkia December 2023 ukilinganisha na Watu 1,612,512 December 2022 na Watu 1,520,589 mwaka 2021.

Taarifa iliyotolewa na Wizara imeeleza yafuatayo ———> “Serikali imeendelea kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI ambapo katika mwaka 2023 jumla ya Watu 8,145,576 walipima Virusi vya UKIMWI (VVU) ukilinganisha na Watu 6,930,758 mwaka 2022 na Watu 6,493,583 mwaka 2021 (Taarifa kutoka mfumo wa DHIS2 2023)”

Katika kuhakikisha kuwa huduma kwa WAVIU zinasogezwa karibu zaidi na jamii, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo imekuwa ikifanya jitihada za makusudi kabisa za kuhakikisha kila kituo cha afya Nchini kinakuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa Waathirika wa UKIMWI.

“Hadi kufikia Desemba 2023 Idadi ya vituo vinavyotoa huduma ya tiba na matunzo vimefikia vituo 7,396 kutoka vituo 7,072 mwaka 2021 na kati ya hivyo CTC kamili ni 3,572 na vituo vya huduma ya Mama na Mtoto (RCHS) vinavyotoa huduma ya kutoa dawa ya kufubaza Virusi vya UKIMWI vipo 3,824” ——— imeeleza Wizara ya Afya.

Mwaka 2023:Watu 8,145,576 walipima Virusi vya UKIMWI (VVU)
0 Comment

Mwanaume wa Marekani anakaribia kutangazwa kuwa ameponywa VVU na saratani ya damuAfyaclass Forum •

Mwanaume wa Marekani anakaribia kutangazwa kuwa ameponywa VVU na saratani ya damu.

Paul Edmonds, mwenye umri wa miaka 68, kutoka California ambaye alitrend kwenye vichwa vya habari vya kimataifa mnamo 2023 alipotoa hadithi yake, bado hana athari za hali zote mbili miaka mitano baada ya kupandikizwa seli ambazo ziliondoa magonjwa yote mawili mwilini.

Katika makala mpya ya timu ya madaktari waliomtibu, madaktari walisema alipona rasmi saratani na miaka miwili kabla ya kutangazwa kuwa amepona VVU.

Safari ya matibabu ya Edmonds ilianza alipogundulika kuwa na UKIMWI mwaka 1988, wakati ambapo virusi hivyo viliua wanaume wengi wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Licha ya kuwatazama marafiki zake wengi wakifa kutokana na maambukizo hayo, hakufa, na aliishi hadi utambuzi mbaya wa leukemia mnamo 2018 nusura ukatize matumaini yake ya kuishi maisha marefu.

Alitibiwa saratani hiyo kwa tiba ya seli shina, ambayo inahusisha kuchukua nafasi ya seli zilizoharibiwa na chemotherapy na zile zenye afya kutoka kwa wafadhili, wakati madaktari waliona fursa ya kipekee: kupata wafadhili na mabadiliko ya jeni yanayokinzana na VVU.

Madaktari walitaka kujua kama wanaweza kuiga mafanikio ya wagonjwa wa awali ambao walikuwa wameripotiwa kuponywa VVU na saratani kwa njia hii.

Kulingana na kliniki ya City of Hope huko California, Edmonds ni mmoja wa watano walioshinda magonjwa yote mawili na mtu mzee zaidi kufanya hivyo.

‘Ninashukuru sana… siwezi kuwashukuru vya kutosha,’ Bw Edmonds alisema kuhusu madaktari wake katika kliniki ya City of Hope huko California.

Kupandikiza seli shina ni sehemu ya mwisho ya matibabu ya saratani ya damu kama vile leukemia na lymphoma.

Inatolewa wakati seli za shina zinazounda damu kwenye uboho wa mgonjwa zimeuawa na mionzi au chemotherapy.

Mnamo Novemba 2018, Bw Edmonds alianza matibabu,Alihitaji raundi tatu ili kufikia hatua nzuri, ambapo katikati ya Januari 2019 alifanikiwa.

Mwezi uliofuata alipokea seli kutoka kwa wafadhili wake.

Seli shina alizopewa zilikuwa na nakala mbili za mabadiliko ya nadra ya kijeni inayoitwa CCR5 delta-3, ambayo huwafanya watu kuwa sugu kwa VVU. Asilimia moja hadi mbili tu ya watu wana mabadiliko haya.

VVU hutumia kipokezi CCR5 kuingia na kushambulia mfumo wa kinga, lakini mabadiliko ya CCR5 huzuia virusi kuingia kwa njia hii.

Inakadiriwa kuwa watu milioni 36.3 wamekufa kutokana na magonjwa yanayohusiana na UKIMWI tangu kuanza kwa janga hilo mnamo 1981.

Mwanaume wa Marekani anakaribia kutangazwa kuwa ameponywa VVU na
saratani ya damu
0 Comment

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)Afyaclass Forum •

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

ARVs ni kifupi cha neno antiretroviral drugs, ikiwa na maana ya dawa kwa ajili kupunguza makali ya Virusi vya Ukimwi,

Hivo basi ARV sio dawa moja bali ni kundi au mjumuisho wa dawa zote ambazo hutumika kwa Mgonjwa mwenye virusi vya Ukimwi(VVU) na mfano wa dawa hizo ni kama vile;

  •  Zidovudine
  • Tenofovir
  • Abacavir
  • Lamivudine
  • Didanosine
  • Emtricitabine n.k

Dawa za VVU zinaweza kusaidia kupunguza wingi wa virusi, kupambana na maambukizi, na kuboresha maisha yako. Zinaweza kupunguza uwezekano wa kusambaza VVU pia, lakini kama ukizitumia vibaya, bado unaweza kuwapa wengine VVU,

Kumbuka pia; Dawa hizi za ARVs Sio tiba ya kuondoa kabsa VVU.

>>Malengo ya dawa hizi ni:

  • Kudhibiti ukuaji wa virusi vya Ukimwi(VVU)
  • Kuboresha mfumo wako wa kinga ya mwili Kufanya kazi vizuri
  • Kupunguza Dalili au kuzuia kabsa dalili za Ukimwi kujitokeza
  • Kuzuia maambukizi ya VVU kwa wengine.n.k

Imeidhinishwa matumizi ya zaidi ya dazeni mbili za dawa za kurefusha maisha kwa ajili ya maambukizi ya VVU. Mara nyingi dawa hizi(ARVs) hugawanywa katika makundi sita kwa sababu hufanya kazi kwa njia tofauti. Madaktari wanapendekeza kuchukua mchanganyiko au “cocktail” ya angalau dawa kwenye makundi mawili. Hii inaitwa tiba ya kurefusha maisha, au antiretroviral therapy(ART).

Daktari wako atakujulisha hasa jinsi unapaswa kutumia dawa zako kwa usahihi. Unahitaji kufuata maagizo haswa, na haupaswi kukosa hata dozi moja. Ukikosa dozi, unaweza kupata aina za VVU zinazokinzana na dawa, na dawa zako zinaweza kuacha kufanya kazi.

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)

Haya ni baadhi ya makundi ambapo dawa za ARVs zimegawanywa;

1. Nucleoside/Nucleotide Reverse Transcriptase Inhibitors (NRTIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Abacavir, or ABC (Ziagen)
  • Emtricitabine, or FTC (Emtriva)
  • Lamivudine, or 3TC (Epivir)
  • Tenofovir alafenamide, or TAF (Vemlidy)
  • Tenofovir disoproxil fumarate, or TDF (Viread)
  • Zidovudine or ZDV (Retrovir)

2.Non-nucleoside Reverse Transcriptase Inhibitors (NNRTIs)

Hapa kuna dawa kama vile;

  • Doravirine, or DOR (Pifeltro)
  • Efavirenz or EFV (Sustiva)
  • Etravirine or ETR (Intelence)
  • Nevirapine or NVP (Viramune)
  • Rilpivirine or RPV (Edurant)

3.Protease Inhibitors (PIs)

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Atazanavir or ATV (Reyataz)
  • Darunavir or DRV (Prezista)
  • Lopinavir + ritonavir, or LPV/r (Kaletra)
  • Ritonavir or RTV (Norvir)

4. Integrase Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Bictegravir or BIC (combined with other drugs as Biktarvy)
  • Cabotegravir and rilpivirine (Cabenuva)
  • Dolutegravir or DTG (Tivicay)
  • Elvitegravir or EVG (Vitekta)
  • Raltegravir or RAL (Isentress)

5.Fusion Inhibitors

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  • Enfuvirtide, or ENF or T-20 (Fuzeon)

6.Capsid Inhibitor

Kwenye kundi hili kuna dawa kama vile;

  •  Lenacapavir(Sunlenca) n.k

Kumbuka; Dawa hizi hutumii moja peke yake zinakuwa kwenye mchanganyiko wa zaidi ya dawa moja(combination) Mfano;

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Elvitegravir + TDF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)
Elvitegravir + TAF + FTC + cobicistat, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)

Bictegravir + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or BIC/TAF/FTC (Biktarvy)
Dolutegravir + abacavir + lamivudine, or DTG/ABC/3TC (Triumeq)
Dolutegravir + rilpivirine, or DTG/RPV (Juluca)
Dolutegravir  + lamivudine, or DTG/3TC (Dovato)
Elvitegravir + cobicistat +  tenofovir alafenamide + emtricitabine, or EVG/c/TAF/FTC (Genvoya)
Elvitegravir + cobicistat + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EVG/c/TDF/FTC (Stribild)

Atazanavir + cobicistat, or ATV/c (Evotaz)
Darunavir + cobicistat, or DRV/c (Prezcobix)
Darunavir + cobicistat + tenofovir alafenamide + emtricitabine, or DRV/c/TAF/FTC) (Symtuza)
Non-nucleoside reverse transcriptase inhibitor (NNRTI)-based:

Doravirine + tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or DOR/TDF/3TC (Delstrigo)
Efavirenz + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or EFV/TDF/FTC (Atripla)
Rilpivirine + tenofovir alafenamide + emtricitabine , or RPV/TAF/FTC (Odefsey)
Rilpivirine + tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or RPV/TDF/FTC (Complera)

Abacavir + lamivudine, or ABC/3TC (Epzicom)
Abacavir + lamivudine + zidovudine, or ABC/3TC/ZDV (Trizivir)
Tenofovir alafenamide + emtricitabine, or TAF/FTC (Descovy)
Tenofovir disoproxil fumarate + emtricitabine, or TDF/FTC (Truvada)
Tenofovir disoproxil fumarate + lamivudine, or TDF/3TC (Cimduo)
Zidovudine + Lamivudine or ZDV/3TC (Combivir) N.K

>> Soma pia hapa kuhusu Muda sahihi wa Kutumia dawa za ARVs

>> Tofauti ya ARVs na PEP

Kuna PEP,PrEP,ARVS

Dawa za Kurefusha maisha(ARVs);

Dawa hizi sio za kutibu au kuponyesha kabsa Ukimwi bali hufanya kazi ya kupunguza Virusi vya ukimwi (Viral Load) hali ambayo huupa nafasi Mfumo wa kinga ya mwili kupambana vizuri na maambukizi haya.

Ili dawa hizi zilete matokeo mazuri unashauriwa kutokuacha kutumia dawa kutokana na maelekezo uliyopewa, kwani ni hatari na unaweza kutengeneza hali ya virusi kutokusikia dawa yaani Drug resistance.

Je ni Muda gani wa kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una HIV?

Zipo Dhana mbali mbali kwenye jamii kuhusu Muda wa Kuanza dawa za ARVs baada ya kugundulika una Virusi vya UKIMWI,

Huku baadhi ya watu wakisema,hutakiwi kuanza dawa za ARVs mpaka uanze kuumwa, je ni kweli?

Soma zaidi hapa chini…!!!

Tiba ya VVU inahusisha unywaji wa dawa zenye ufanisi mkubwa yaani antiretroviral therapy (ART) ambazo hufanya kazi kudhibiti virusi.

ART inapendekezwa kwa kila mtu mwenye VVU.

Watu walio na VVU wanapaswa kuanza ART haraka iwezekanavyo baada ya utambuzi (hata siku hiyo hiyo).

Nimatumaini yangu kwamba umepata majibu kuhusu Muda wa kuanza dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi maarufu kama ARVs.

Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi(ARVs)
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD