Showing posts with label Elimu&Ushauri. Show all posts
Showing posts with label Elimu&Ushauri. Show all posts

Uhusiano wa Usugu wa dawa na magonjwa ya figo,Prof. Jeremiah aelezaAfyaclass Forum •

Uhusiano wa Usugu wa dawa na magonjwa ya figo,Prof. Jeremiah aeleza

#Picha:Prof. Jeremiah Seni, Profesa Mshiriki wa Vimelea vya Magonjwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya Bugando, Mwanza Tanzania.

Viongozi wa Umoja wa Mataifa wakutana jijini New York, Marekani kujadili hatua za kudhibiti hatari itokanayo na usugu wa vimelea dhidi ya dawa, UVIDA au kwa kiingereza AMR, nchini Tanzania mtaalamu wa suala hilo amedadavua uhusiano kati ya usugu wa dawa na magonjwa kama vile figo na maambukizi katika njia ya mkojo, UTI.

Katika mahojiano na Jeremiah Seni, Profesa Mshiriki wa Vimelea vya Magonjwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sayansi za Afya Bugando, Bosco Cosmas wa Idhaa ya  Umoja wa Mataifa alimuuliza hasa chanzo na madhara ya usugu wa dawa hizo.

Usugu dhidi ya vimelea vya magonjwa ni hali ambayo vimelea wanaosababisha magonjwa mbalimbali, wanafanya mabadiliko na hivyo kukinzana na dawa ambazo awali zilikuwa zinatumika kuwatibu, na vimelea hawa tunawagawa katika makundi Matano ambayo tuna bakteria, virusi, fangasi, minyoo na jamii zingine za parasaiti kama wale wanaosababisha malaria.

UTI isipotibika inaposababisha magonjwa ya figo

Ingawa watu wengi wameishi na tatizo hili la usugu bila kufahamu, lakini athari zake ziko wazi kwa afya ya umma, nikamuuliza Prof. Seni kuwa usugu unawezaje kuathiri afya ya umma? Profesa Seni akachambua zaidi akisema, “tukiachana na haya magonjwa ambayo serikali yamejiwekea mpango mkakati wa kupambana nayo kama UKIMWI, kifua kikuu na malaria mgonjwa anapopata maambukizi maana yake ule ugonjwa utakaa muda mrefu zaidi kwa hiyo inawezekana mtu alikuja na maambukizi tu kwenye njia ya mkojo (UTI) ni kawaida lakini kama ana usugu maana yake anaweza akachelewa kupona na pia kusababisha mgonjwa kupoteza maisha na kuongezeka kwa gharama za matibabu.”

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, UVIDA husababisha vifo vya watu 700,000 kwa mwaka, lakini wanatabiri kuwa hadi ifikapo mwaka 2030, linaweza kusababisha vifo vya takribani watu milioni 10. Nikamuuliza nini kifanyike tatizo hili lisiwe na madhara zaidi kwa watu ulimwenguni?

Ukiangalia takwimu ni kweli kabisa mwaka 2014 utafiti mkubwa kabisa uliosimamiwa na Shirika la Afya Ulimwenguni ambao uliangalia zaidi vifo vinavyotokana na UVIDA na walifanya makisio ya wale watu takribani 700,000 wamepoteza maisha kutokana na UVIDA na mbaya zaidi robo tatu ya vifo hivyo ni kutoka bara la Afrika na Kusini mashariki mwa bara la Asia kwahia vifo hivyo ni kutoka bara la Afrika na Kusini mashariki mwa bara la Asia kwahiyo ni vyema  kwa serikali kuona ukubwa wa tatizo hili na kuwekea mkazo katika mapambano kama walivyoweka kwa magonjwa mengine makubwa.”

Wafamasia wanachukua hatua gani kudhibiti UVIDA?

Moja kati ya sehemu muhimu ambayo inaweza kusaidia kupunguza ama kumaliza tatizo hili ni katika maduka ya dawa ambapo mara nyingi wagonjwa huwa wanaenda kununua dawa bila kufuata taratibu za vipimo. Clinius Amani Caroly, Mteknolojia dawa katika hospitali ya Mwananchi iliyopo mkoani Mwanza, anaeleza hatua wanazochukua katika utoaji wad awa kwa mgonjwa.

Sasa kwa utoaji wa dawa kwa mgonjwa ambaye hana karatasi ya daktari, kuna makundi mawili, kwanza kwa kitaalamu kuna kitu kinaitwa over the counter medicine, ambazo ni dawa zinazoweza kutolewa kwa mgonjwa bila karatasi ya daktari lakini pia kuna prescription medicine ambazo mgonjwa akija bila karatasi ya daktari hatuwezi kumpatia. Mgonjwa anapokuja bila karatasi ya daktari kwanza tunajiridhisha kama kweli dawa anayotaka inaendana na ugonjwa wake na tunawapa ushauri wa Kwenda kumuone daktari.

Muathirika wa UVIDA na hatua alizochukua sasa

Je, wahanga wana uelewa kuhusu namna sahihi ya kukabiliana na usugu? Neema Gervas, muhanga wa tatizo hili anaeleza nini anafanya anapogundua amepata usugu.

“Kwa upande wangu suala la usugu wa dawa limenitesa kwa muda mrefu sana kwasababu hapo awali  nilikuwa natumia hizi dawa za kutuliza maumivu hasa ninapohisi maumivu ya kichwa lakini kwa sasa nikitumia haisaidii kupata unafuu. Nilienda phamasi nikawaambia dawa ambazo huwa ninatumia hazinisaidii kwahiyo wananishauri kubadilisha daw ana nikawa napata nafuu.” Via;UN

0 Comment

Matumizi yasiosahihi ya Dawa chanzo cha Usugu wa Vimelea vya magonjwaAfyaclass Forum •

FUATENI MAELEKEZO SAHIHI YA WATAALAMU WA DAWA ILI KUEPUKA USUGU WA VIMELEA DHIDI YA DAWA. 

Na WAF- DSM. 

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Afya Bw. ismail Rumatila ametoa wito kwa wananchi kufuata maelekezo sahihi ya Wataalamu wa dawa ili kuepuka changamoto ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa inayoendelea kukua kwa kasi Tanzania na Duniani kwa ujumla. 

Bw. Rumatila amesema hayo leo Septemba 21, 2024 katika matembezi km 5 na km10 yenye ujumbe wa mapambano ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa (UVIDA) yaliyoandaliwa na Wafamasia katika viwanja vya chuo cha Muhimbili Jijini Dar es Salaam. 

"Tunajenga mwamko mpya kwenye jamii yetu, tukisisitiza umuhimu wa kufuata maelekezo sahihi ya wataalamu wa dawa, kuepuka matumizi ya dawa kiholela," amesema Bw. Rumatila. 

Ameendelea kusema, ni muhimu kufuata ushauri na maelekezo ya Wataalamu wa dawa kwa kuhakikisha kuwa tunamaliza dozi zote tunazopewa na watoa huduma za afya hivyo itasaidia kulinda afya ya mwili. 

Sambamba na hilo, amebainisha kuwa, tatizo la usugu wa vimelea dhidi ya dawa limazidi kuwa tishio Tanzania na Duniani kwa ujumla, huku akieleza kuwa kulingana na WHO inakadiria kuwa ifikapo mwaka 2050, watu milioni 10 watakuwa wanapoteza maisha kila mwaka kutokana na maambukizi yanayotokana na vimelea sugu.

Kwa upande wake Rais wa chama cha wafamasia Tanzania (PST) Bw. Fadhili Hezekia amesema kuwa, suala la dawa na afya sio biashara, hivyo kutoa wito kwa wafanyabiashara wa dawa kufuata miongozo na taratibu za utoaji huduma za dawa ili kusaidia katika mapambano dhidi ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa.

0 Comment

Dawa ya kung'atwa na nyuki,Soma hapa kufahamuAfyaclass Forum •

Dawa ya kung'atwa na nyuki,Soma hapa kufahamu

BAADA ya kukithiri kwa matukio ya wananchi kushambuliwa na makundi ya nyuki katika maeneo mbalimbali nchini, wadau wa maendeleo wameanza kutoa elimu kwa wananchi namna ya kuepuka madhara ya wadudu hao.

Shirika la Maendeleo Vijijini (RDO), ndilo limejitosa kutoa elimu kwa wananchi ambapo limewataka wananchi kujikinga kwa kuziba midomo, masikio na macho, pale wanapokutana na kundi la nyuki.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Mafinga mkoani Iringa, Ofisa Nyuki RDO, Teddy Pagi alisema binadamu aking’atwa na nyuki kwenye maeneo hayo ya wazi huwa ni rahisi kupoteza maisha.

Alisema nyuki huwa wanachagua sehemu hizo muhimu kwa binadamu kuuma na kwamba sehemu hizo zikivimba ni rahisi binadamu kupoteza maisha kwa maelezo kuwa zikivimba inamuwia vigumu binadamu kupumua.

Kutokana na hilo alisema watu wanapaswa kuwa makini na siyo kukimbia peke yake bila kuwa na tahadhari yoyote ile kwenye viungo vya mwili wake.

Mbali na madhara ya nyuki pia alizitaja baadhi ya faida zitokanazo na mazao ya nyuki ikiwamo asali na maziwa ambavyo vinatumika kama chakula na dawa pamoja na sumu ambayo hutumika kama malighafi.

Alisema asali inatumika kama tiba katika matatizo mbalimbali ambazo binadamu anakutana nazo ikiwamo kuungua moto katika baadhi ya sehemu za mwili.

Alisema sumu ya nyuki inatumika kama kinga ya kuimarisha viungo vya mwanadamu yeyote yule isipokuwa sehemu ya ulimi, pua macho na masikio.

Hivyo, aliishauri jamii kufuga nyuki  kwa wingi ili wavune mazao yake ambayo yatawapa faida wao na familia zao.

Pia alitoa ushauri kwa wafugaji wa nyuki kuhahakikisha wanatumia mizinga mizuri ambayo nyuki watatengeneza asali itakayowapa manufaa.

Alisema lengo lao ni kuona jamii inafaidika na mazao ya nyuki na siyo kuwakimbia badala yake wafuge ili wapate faida kupitia mazao yanayotolewa na nyuki.

Fahamu Zaidi kuhusu Kung'atwa na Nyuki kutoka @afyaclass|SOMA hapa Chini kupata Elimu Zaidi;

DAWA YA KUNG'ATWA NA NYUKI(huduma ya kwanza)

Kung'atwa na nyuki kunaweza kutoa athari tofauti, kuanzia maumivu ya muda na usumbufu hadi athari kali ya mzio.  Kuwa na aina moja ya majibu haimaanishi kuwa utakuwa na majibu sawa kila wakati unapong'atwa au kwamba itikio linalofuata litakuwa kali zaidi.

Dalili za Kung'atwa na Nyuki

Mwitikio mdogo(Mild reaction);

Mara nyingi, dalili za kung'atwa na nyuki ikiwa mwitio wa mwili ni mdogo ni pamoja na:

  •  Kupata maumivu makali ya kuungua kwenye tovuti ya kuumwa
  •  Rangi Nyekundu kwenye eneo ulilong'atwa
  •  Kuvimba kidogo kuzunguka eneo ulilong'atwa
  •  Kwa watu wengi, uvimbe na maumivu hupotea ndani ya masaa machache.

 Mwitikio wa wastani(Moderate reaction);

Baadhi ya watu wanaong'atwa na nyuki au wadudu wengine huwa na majibu yenye nguvu zaidi, yenye ishara na dalili kama vile:

  •  Uwekundu uliokithiri kwenye eneo husika ulipong'atwa
  •  Kuvimba kwenye eneo husika ulipong'atwa ambapo Uvimbe huongezeka polepole kwa siku inayofuata au mbili

Muitikio wa wastani huelekea kuisha kwa siku tano hadi 10.  

Mwitikio mkubwa wa mzio;

Athari kali ya mzio (anaphylaxis) kwa kung'atwa na nyuki huweza kutishia maisha na hali hii inahitaji matibabu ya dharura.  Asilimia ndogo ya watu wanaoumwa na nyuki au wadudu wengine hupata Athari kali ya mzio haraka.  Dalili na ishara za Athari kali ya mzio ni pamoja na:

- Athari za ngozi, ikiwa ni pamoja na kupata Muwasho mkali kwenye ngozi

 - Kupata shida sana ya kupumua

- Kuvimba kwa koo na ulimi

 - Mapigo ya moyo kuwa chini au moyo kwenda haraka

 - Kupata Kichefuchefu, kutapika au kuharisha

 - Kupata Kizunguzungu au kuzirai

 - Kupoteza fahamu n.k

Watu ambao wana athari kali ya mzio kwa kung'atwa na nyuki wana uwezekano wa 25% hadi 65% wa kupata tena tatizo la anaphylaxis wakati ujao watakapong'atwa tena na nyuki au wadudu wengine. 

 Zungumza na daktari wako au mtaalamu wa afya kuhusu hatua za kuzuia hali hii kama vile tiba ya kinga mwilini ili kuepuka majibu kama hayo iwapo utaumwa tena.

Kung'atwa na nyuki wengi:

Kwa ujumla, wadudu kama vile nyuki na nyigu sio wakali na huuma tu katika kujilinda.  Katika hali nyingi, hii husababisha kung'atwa mara moja au labda chache zaidi.  Katika baadhi ya matukio mtu atavuruga mzinga wa nyuki au kundi la nyuki na kung'atwa mara nyingi.  Baadhi ya aina ya nyuki - kama vile nyuki wa Kiafrika - wana uwezekano mkubwa zaidi kuliko nyuki wengine katika kuruka, wakiuma katika Makundi.

Ukiumwa zaidi ya mara kumi na mbili, mkusanyiko wa sumu unaweza kusababisha athari ya sumu na kukufanya uhisi mgonjwa sana.  Dalili na ishara ni pamoja na:

  •  Kupata Kichefuchefu, kutapika au kuharisha
  •  Kupata Maumivu ya kichwa
  •  Hisia ya kitu kinazunguka (vertigo)
  •  Degedege
  •  Kupata Homa
  •  Kupata Kizunguzungu au kuzirai

Kuumwa mara nyingi kunaweza kuwa hali ya dharura ambayo huhitaji matibabu ya haraka kwa watoto, watu wazima wazee, na watu ambao wana shida ya moyo au kupumua.

Sababu zinazoongeza hatari ya kung'atwa na Nyuki;

Uko kwenye hatari kubwa ya kuumwa au kung'atwa na nyuki ikiwa:

 • Unaishi katika eneo ambalo nyuki wanazunguka sana au karibu na mizinga ya nyuki

• Kazi yako au mambo unayopenda yanahitaji kutumia muda mwingi ukiwa nje, kwenye misitu,vichaka n.k

 Kuna uwezekano mkubwa wa kuwa na athari ya mzio kwa kuumwa na nyuki ikiwa umekuwa na athari ya mzio kwa kuumwa na nyuki hapo awali, hata kama ilikuwa ndogo.

 Watu wazima huwa na athari kali zaidi kuliko watoto na wana uwezekano mkubwa wa kufa kwa anaphylaxis kuliko watoto.

Jinsi ya Kuzuia janga hili:

 Vidokezo vifuatavyo vinaweza kusaidia kupunguza hatari ya kung'atwa na nyuki:

 ✓ Jihadharini wakati wa kunywa vinywaji vitamu nje.  Vikombe vilivyo wazi vinaweza kuwa chaguo bora kwa sababu unaweza kuona ikiwa nyuki yuko ndani yake.  Kagua makopo na majani kabla ya kunywa vitu vitamu.

 ✓ Funika vyombo vya chakula na makopo ya takataka.

 ✓ Ondoa takataka, matunda yaliyoanguka, na kinyesi cha mbwa au wanyama wengine (nzi wanaweza kuvutia nyigu).

 ✓ Vaa viatu vilivyofungwa unapotembea nje.

 ✓ Usivae vitu vyenye rangi ya kung'aa sana au vya maua ukiwa kwenye mazingira yenye nyuki, Hii inaweza kuvutia nyuki.

✓ Usivae nguo za kubana sana, ambazo zinaweza kunasa nyuki kati ya nguo na ngozi yako.

 ✓ Unapoendesha gari, funga madirisha yako

✓ Usipake mafuta au parfumes za kunukia sana ukiwa kwenye mazingira yenye nyuki

 ✓ Kuwa mwangalifu wakati wa kukata nyasi au kupunguza mimea, shughuli ambazo zinaweza kuamsha wadudu kwenye mzinga wa nyuki au kiota cha nyigu.

 ✓ Ondoa mizinga na viota karibu na nyumba yako.

 Jua nini cha kufanya unapoathiriwa na nyuki:

 Ikiwa nyuki wachache wanaruka karibu nawe, tulia na uondoke polepole kutoka eneo hilo.  Kumuua mdudu kunaweza kusababisha kuumwa.

 Ikiwa nyuki au nyigu atakuuma, au wadudu wengi wanaanza kuruka karibu, funika mdomo na pua yako na uondoke haraka eneo hilo.  Nyuki anapouma, hutoa kemikali inayowavutia nyuki wengine.  Ikiwezekana, ingia kwenye jengo au gari lililofungwa.

DAWA YA KUNG'ATWA NA NYUKI(huduma ya kwanza)

Fahamu kuhusu huduma ya kwanza pamoja na matibabu kwa mtu ambaye ameng'atwa na nyuki,

Kwanza hakikisha wewe unayeenda kumsaidia mtu aliyeng'atwa na nyuki unajilinda kwanza, kwa kuvaa nguo ambazo zinafunika mwili wako wote,

Kisha angalia hali ya mtu aliyeng'atwa na nyuki, kama bado nyuki wapo wengi na wanaendelea kumng'ata fanya haya;

- Unaweza kumfunika mwili wake wote kwa blanket nzito

- Kumwagia maji mwilini ili kuondoa harufu ya nyuki mwilini 

- Tumia kitu chembamba sana kuondoa ile miiba ya nyuki sehemu ambapo kang'atwa, usitoe kwa kutumia kucha zako,ni rahisi sumu ile kuendelea kupenya kwenye ngozi na kuingia mwilini

- Muweke aling'atwa na nyuki sehemu ambapo kuna hewa ya kutosha

- Wengine hutumia mafuta ya kupaka kama Calamine n.k

- Tumia dawa mbali mbali za kuzuia maumivu 

- Baada ya muda tumia maji safi na sabuni kuosha sehemu ambazo kang'atwa na nyuki

- Endapo hali ya mgonjwa ni mbaya zaidi,mpeleke kwenye hospital iliyokaribu na wewe ili apate matibabu zaidi

MADHARA YA KUNG'ATWA NA NYUKI

NYUKI huweza kusababisha;

- Hali ya kuvimba sana mwilini

- Mtu kupoteza kabsa fahamu

- Mwili kuwasha sana

- Maumivu makali sana

- Mtu kupoteza maisha

- Maumivu makali ya kichwa

- Kizunguzungu kikali

- Mapigo ya moyo kubadilika na kwenda mbio sana kuliko kawaida

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.


0 Comment

Dalili za kung'atwa na nyoka,Soma hapa kufahamuAfyaclass Forum •

Dalili za kung'atwa na nyoka,Soma hapa kufahamu

Takwimu:

Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema kuwa mtu mmoja hufa kutokana na kuumwa na nyoka kila baada ya dakika nne hadi sita, na zaidi ya theluthi moja ya waathiriwa wote wana umri wa chini ya miaka 20.

Visa milioni 1.8-2.7 vya kuumwa na nyoka hutokea kila mwaka, na hivyo kusababisha vifo kati ya 81,000-138,000.

Wengi wa kuumwa na nyoka hutokea Asia, Afrika, Marekani Kusini, Williams alisema, wakati inakadiriwa watu milioni 1.2 walikufa kutokana na kuumwa na nyoka nchini India pekee mwaka 2000-2019 – wastani wa 58,000 kila mwaka.


Dalili za kung'atwa na nyoka

Zipo dalili mbali mbali za kung atwa na nyoka kulingana na aina ya nyoka aliyekung ata, ila kwa ujumla dalili hizo ni pamoja na;

1. Kuvimba eneo ulilong'atwa

2. Rangi kubadilika kabsa; mabadiliko ya rangi kwenye ngozi yako (ngozi kuwa nyekundu au rangi nyeusi kuliko ngozi yako ya asili).

3. Kuvuja damu eneo ulilong'atwa na nyoka

4. Majeraha ya kutobolewa kutoka kwa alama ya kuumwa kwenye ngozi yako.

5. Kupata Maumivu kama ya kuchomwa, kuungua n.k, kwenye sehemu ya kuumwa au katika kiungo chako au eneo la mwili wako ambalo lina alama ya kung'atwa. Ingawa  Sio kila kuumwa na nyoka wenye sumu husababisha maumivu.

6. Mabadiliko ya rangi kwenye ngozi yako.

7. Kutokwa na jasho na/au kukojoa.

 8. Kupata Kichefuchefu na kutapika.

9. Kupata Maumivu ya kichwa, kizunguzungu na kutoona vizuri.

 10. Kuhisi Ladha ya metali kinywani mwake.

Dalili kali za kuumwa na nyoka wenye sumu ni pamoja na:

- Kutokwa na damu mfululizo au (kuganda kwa damu isiyo ya kawaida).

- Shinikizo la chini la damu, mapigo ya moyo kwenda haraka

- Kupata Ugumu wa kupumua

- Udhaifu kwenye misuli au kutetemeka na kufa ganzi katika uso wako na/au miguu na mikono.

 - Kuvimba Sana

 Kuumwa na nyoka mwenye sumu ni tukio la dharura lenye kuhitaji matibabu ya haraka.


Dalili za kuwa na mzio dhidi ya kuumwa na nyoka

Ikiwa una athari ya mzio kwa kuumwa na nyoka, unaweza kupata mshtuko ambao hujulikana kama anaphylactic shock.  Dalili nyingi za mzio dhidi ya kuumwa na nyoka ni sawa na dalili za kung'atwa na nyoka yenye sumu.  Mbali na dalili za kuumwa na nyoka mwenye sumu, dalili maalum za kuwa na mzio ni pamoja na:

  •  Koo kubana, 
  • Ulimi kuvimba na ugumu wa kuzungumza.
  •  Rangi ya ngozi kubadilika sana.
  •  Kukohoa mara kwa mara n.k

 Je, nyoka anaweza kukung' ata zaidi ya mara moja?

Ndiyo, ikiwa nyoka anajaribu kujilinda, anaweza kukuuma zaidi ya mara moja.  Ikiwa nyoka mwenye sumu atakuuma zaidi ya mara moja, unaweza kupata dozi nyingi za sumu ya nyoka ndani ya mwili wako kwa kila anapokuuma.  Hali Hii inaweza kuongeza ukali wa dalili zako na kupunguza muda wa kupata matibabu ili kuzuia dalili kali zisikuathiri.

KUMBUKA; Sumu ya nyoka inaweza kudhuru mwili wako na kusababisha kifo katika baadhi ya visa.  Ukali wa kuumwa hutofautiana kulingana na aina ya nyoka aliyekuuma.

 Je, ni sababu gani zinazoongeza hatari za kung'atwa na nyoka?

Unaweza kuwa katika hatari zaidi ya kuumwa na nyoka ikiwa:

  •  Unafanya Kazi au kucheza nje.
  •  Kuishi katika hali ya hewa ya joto, ya jangwa au ya kitropiki.
  •  Kushughulikia nyoka.
  •  Kuishi katika eneo la vijijini.
  • Kuwa kwenye maeneo ya vichaka,pori,misitu n.k

 Je, ni matatizo gani unaweza kupata baada ya Kung'atwa na nyoka?

 Shida za kuumwa na nyoka zinaweza kujumuisha:

 - Jeraha kuvimba, kusababisha maumivu, kubadilika rangi na kuvuja usaha au majimaji (maambukizi).

 - Ngozi kuonekana nyeusi,kuoza au kufa karibu na jeraha (necrosis).

- Mfumo wako wa kinga kuathiriwa vibaya na maambukizi kwenye damu (sepsis).

 - Kupata Maambukizi ambayo husababisha shinikizo la chini sana la damu na kushindwa kwa mtu(septic shock).

 - Kupata ugumu wa kupumua na/au uvimbe mkali (majibu ya mzio).

 - Kifo au kupoteza maisha

 Fahamu; Matatizo yanajitokeza zaidi katika maeneo ya dunia ambako kuna ufikiaji mdogo wa huduma za afya na matibabu.

 Maumivu na uvimbe ni madhara ya kawaida ya muda mrefu katika eneo la mwili ambapo kung'atwa kumetokea.

Jinsi ya kutambua baada ya kung'atwa na Nyoka(Diagnosis&Tests)

Mhudumu wa afya atagundua kung'atwa na nyoka baada ya kukagua dalili zako.  Majeraha ya kung'atwa kwenye ngozi yako kutokana na meno ya nyoka huwa ni dalili ya kwanza ya kuumwa na nyoka kwa mhudumu wa afya.  Vipimo vya damu vinaweza pia kumsaidia mtoa huduma wako wa afya kubaini kama kuna sumu mwilini mwako, ambayo inaweza kuwasaidia kutambua matibabu.

Ikiwa uliona nyoka akikuuma na ukaweza kutambua rangi au alama maalum, mjulishe mtoa huduma wako wa afya.

Matibabu na Huduma kwa Mtu aliyeng'atwa na Nyoka

Je, kung'atwa na nyoka asiye na sumu hutibiwaje?

Matibabu ya kuumwa na nyoka asiye na sumu ni utunzaji sahihi wa jeraha.  Hii ni pamoja na:

  •  Kusafisha eneo ulilong'atwa kwa sabuni na maji.
  •  Kulifunika kwa bandage.
  •  Kufuatilia eneo na kumjulisha mtoa huduma wako wa afya kama una dalili za maambukizi kama vile uvimbe, usaha au maumivu.

 Je, kung'atwa na nyoka mwenye sumu hutibiwaje?

Matibabu ya kuumwa na nyoka mwenye sumu ni antivenin (antivenin).  Antivenom ni aina ya tiba ya kingamwili ambayo hupunguza athari za sumu mwilini mwako.  Unaweza kupokea antivenino kama sindano au kwa njia ya IV (kupitia sindano kwenye mkono wako) ili iweze kuchukua hatua haraka iwezekanavyo.

 Kujua ukubwa, rangi na umbo la nyoka kunaweza kumsaidia daktari wako kuamua ni antivenin ipi inayofaa zaidi kwa hali yako.  Kuna antivenomu ambazo hutibu kuumwa kutoka kwa aina maalum ya nyoka (antivenoms monospecific) na zile zinazotibu kuumwa na idadi ya nyoka wanaopatikana katika eneo fulani la kijiografia (polyspecific antivenin).

 Iwapo kung'atwa na Nyoka kulisababisha upotevu mkubwa wa Damu kuliko kawaida, utasaidiwa kupewa damu(blood transfusion).                                                    Ikiwa shinikizo lako la damu litashuka chini ya kiwango fulani, unaweza kuhitaji viowevu vya IV au drip za maji(kupitia sindano kwenye mkono).

 Kwa kuwa antivenin ina madhara yanayoweza kutokea, utahitaji pia kufuatiliwa hospitalini.

Msaada wa kwanza wa kung'atwa na nyoka

Unapaswa kutibu kung'atwa na nyoka kama swala la dharura na la haraka, kwani nyoka wengine wana sumu na kuuma kwao kunaweza kutishia maisha yako.  Piga Simu haraka ya Msaada kwa mtu wako wa karibu au huduma za dharura mara moja. 

 Kujiendesha mwenyewe kwenye chombo chochote cha Usafiri kwenda kwenye chumba cha dharura kunaweza kuwa hatari kwa sababu dalili zako zinaweza kuathiri uwezo wako wa kuendesha gari kwa usalama.

 Baada ya kupiga simu kwa usaidizi, chukua hatua zifuatazo:

  1.  Tulia na uwajulishe watu walio karibu kuwa kuna nyoka na amekuuma.
  2.  Keti au lala chini katika eneo salama mbali na nyoka.
  3.  Ondoa vito au vifaa vyovyote unavyovaa.
  4.  Tumia sabuni na maji kuosha kwa upole eneo la kuumwa.
  5.  Funika jeraha la kuumwa na bandeji safi na kavu.
  6.  Kumbuka uvimbe au mabadiliko yoyote kwenye ngozi yako yanayozunguka kuumwa pamoja na wakati ambapo mabadiliko yalitokea.
  7.  Huduma za dharura zinapowasili, zitatoa dawa ya kuzuia virusi haraka ili kupunguza madhara ya sumu ya nyoka.

 Je,Unapaswa kuepuka kufanya nini wakati wa kutibu kung'atwa na nyoka?

Wakati mwingine, kuumwa na nyoka kunaweza kusababisha watu kuogopa.  Hata hivyo, kuna mambo fulani unapaswa kuepuka kufanya mara baada ya kuumwa au kung'atwa na nyoka, ikiwa ni pamoja na:

 - Usisubiri dalili zionekane kabla ya kuomba msaada.

 - Usimfuate nyoka, Hii inakuweka katika hatari zaidi ya kuumwa tena.  Hata kama nyoka amekufa, bado anaweza kutoa sumu, Jaribu kukaa mbali naye.

 - Usitumie tourniquet, ambayo ni kifaa cha kuzuia mtiririko wa damu kwenye sehemu ya mwili.

- Usikate kwenye jeraha lako. 

- Usijaribu kunyonya sumu.

 - Usipake barafu au kutumia maji kuzamisha jeraha lako.

- Usinywe pombe.

 - Usinywe vinywaji vyenye kafeini.

 - Usinywe dawa zozote za kutuliza maumivu, kama vile ibuprofen au aspirini.

 Je, kuna madhara ya matibabu?

 Madhara ya antivenin ni ugonjwa wa serum.  Hii inaweza kutokea siku nne hadi 10 baada ya kupokea antivenin.  Iwapo utapata mojawapo ya dalili zifuatazo, wasiliana na mtoa huduma wako wa afya:

  •  Vipele.
  •  Mwili Kuwasha
  •  Maumivu ya viungo.
  •  Homa.
  •  Node za lymph kuvimba.

Ni muda Gani baada ya matibabu nitajisikia vizuri?

Muda ambao inachukua kupona kabisa inategemea aina ya kuumwa na nyoka.  Kwa wastani, inaweza kuchukua wiki chache hadi miezi michache kabla ya kujisikia vizuri.  Watu wengine wanaweza kuhitaji muda mrefu kupona kuliko wengine. 

Mara nyingi, utakaa hospitalini kwa angalau saa 24, ili madaktari waweze kufuatilia shinikizo la damu na afya yako kwa ujumla, kisha unaweza kurudi nyumbani ili kukamilisha uponyaji wako.

Je, kung'atwa na nyoka kunaweza kuzuiwa?

Inaweza kuwa vigumu kuepuka kuumwa au kung'atwa na nyoka ikiwa unaishi, unafanya kazi au upo likizo katika eneo ambalo nyoka ni kawaida kuwepo.  Unaweza kuchukua hatua za kuzuia kuumwa na nyoka kwa:

 ✓ Kuwa mwangalifu unapoweka mikono na miguu yako.  Usiingize miguu au mikono kwenye mashimo yasiyojulikana, au chini ya vitu bila kwanza kuhakikisha kuwa nyoka hajajificha hapo.

 ✓ Kuwa na ufahamu wa mazingira yako.  Usilale au kukaa chini katika maeneo ambayo kunaweza kuwa na nyoka.

✓ Kuvaa buti za juu na suruali ndefu wakati wa kutembea au kufanya kazi katika maeneo yenye misitu minene.

 ✓ Usijaribu kukamata, kushughulikia au kuweka nyoka karibu na wewe.

 ✓ Ukikutana na nyoka, rudi nyuma polepole kutoka kwake na uepuke kumgusa.

Hitimisho:

Inaweza kuwa vigumu sana kukaa tu na kutulia baada ya kukutana na nyoka, hasa nyoka anayeuma, Kukiwa na aina 3,000 za nyoka, ni asilimia 15% tu kati yao ulimwenguni kote wana sumu.  Kwa kuwa nyoka ni wepesi wakati wa kuuma, huwezi kumtazama vizuri nyoka ili kutambua ikiwa ana sumu au hana sumu. 

Wakati mapigo ya moyo wako yanaenda kasi, pumua kwa kina na upige simu kwa mtu wa karibu au wahudumu wa dharura baada ya kung'atwa na nyoka.  Hii ni tahadhari ya usalama.  Hofu yako inaweza kuficha maumivu yanayotokana na kung'atwa na nyoka ambapo inaweza kufanya kuumwa kuonekana kuwa hatari kuliko ilivyo kweli.  Kupata matibabu haraka huzuia matatizo ya kutishia maisha.

0 Comment

Ni kwanini Wanaume hawawezi kupata Ugonjwa wa PID kama Wanawake?Afyaclass Forum •

Ni kwanini Wanaume hawawezi kupata Ugonjwa wa PID kama Wanawake?

Hapana, Mwanaume hawezi kuwa na Ugonjwa wa PID(Pelvic inflammatory disease),

Hii ni kwa Sababu PID ni ugonjwa ambayo huhusisha maambukizi ya vimelea vya magonjwa kama vile bacteria kwenye Via vya Uzazi vya Mwanamke.

Kwa Ujumla,Ugonjwa huu wa PID hushambulia mfumo wa Uzazi kwa mwanamke, ikiwa ni Pamoja na;

(1) Kizazi(Uterus)

(2) Mirija ya uzazi(fallopian tubes)

(3) au Vifuko vya Mayai(Ovaries)

Ingawa Wanaume hawawezi kupata PID lakini wanaweza kuwa carriers wa bacteria wanaosababisha Ugonjwa wa PID,

Hii inaweza kusababisha Mwanamke kuwa na maambukizi ya PID ambayo hujirudia rudia endapo mwanaume ambaye hushiriki naye tendo hakupata msaada wowote wa Matibabu.

Hivo basi kama Mwanamke ana PID ni vizuri yeye na mwenza wake kupata Tiba ili kuepuka tatizo hili kujirudia mara kwa mara.

SOMA Zaidi hapa,LINK IN HERE

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD