Showing posts with label Kitovu cha Mtoto. Show all posts
Showing posts with label Kitovu cha Mtoto. Show all posts

Kitovu cha mtoto kuchelewa kukauka Afyaclass Forum •

Kitovu cha mtoto kuchelewa kukauka 

KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,Damu,Sababu ni nini?

Dalili za hatari kwa Kitovu cha Mtoto

Zipo dalili mbali mbali huweza kujitokeza kwenye Kitovu cha Mtoto wako,Ukiona Dalili hizi,hakikisha Mtoto anapata Msaada, Dalili hizi ni hatarishi sio nzuri wake:

  • Kitovu kinatoa usaha wenye harufu mbaya
  • Damu inatoka mara kwa mara
  • Ngozi kuzunguka kitovu kuwa nyekundu au kuvimba
  • Mtoto ana homa au analia sana
  • Kitovu hakikauki hata baada ya siku 7–14

Sababu zinazoweza kusababisha

1.Maambukizi ya bakteria (kutokana na uchafu au utunzaji mbaya)

2.Kitovu kubaki na unyevunyevu muda mrefu

3.Kitovu Kuguswa na vitu vichafu (mfano majivu, mafuta, dawa za asili zisizo salama) n.k

Nini cha kufanya

Hii ni hali ya muhimu—usichelewe:

Mpeleke mtoto hospitali au kituo cha afya mara moja Au Ongea na Mtaalam wa Afya au Kwa Ushauri Zaidi na Tiba tuwasiliane hapa hapa afyaclass,kupitia namba +255758286584(Call,Sms,Whatsapp).

-Usitumie dawa za kienyeji au kubonyeza kitovu bila Ushauri Sahihi.

-Acha kitovu kiwe kikavu (dry cord care) usiweke maji au Vitu vitakavyoongeza unyevu unyevu

-Epuka kukifunika kwa diaper

-Usikigusie mara kwa mara

Kwa mtoto mchanga, maambukizi ya kitovu yanaweza kuenea haraka mwilini, hivyo ni muhimu kuchukua hatua mapema.

YAPO BAADHI YA MAMBO MUHIMU SANA YA KUZINGATIA KUHUSU KITOVU CHA MTOTO

1-Mama hakikisha kitovu cha mtoto hakivuji damu baada ya kukatwa na kufungwa na mtaalam wa afya.

2-Kitovu hudondoka chenyewe,ambapo kwa asilimia kubwa kwa watoto wengi ndani ya wiki moja,kitovu huwa tayari kimeshadondoka.

3-Hakikisha kitovu cha mtoto hakitoi usaha,au kubalika rangi hasa ya manjano na kutoa harufu mbaya,hii sio dalili nzuri.

4-Usiweke kitu chochote kwenye kitovu cha mtoto mpka kidondoke chenyewe.

5-Epuka imani potofu kama zile za kuweka mavi ya Ng'ombe n.k,kwenye kitovu cha mtoto.

KWA USHAURI,ELIMU AU MSAADA WA KIAFYA MAWASILIANO NI +255758286584.

0 Comment

Kitovu Cha Mtoto kikidondokea sehemu za siri – kinaathiri nguvu za kiume?Afyaclass Forum •

Kitovu Cha Mtoto kikidondokea sehemu za siri – kinaathiri nguvu za kiume?

Hii si kweli kabisa (ni imani tu).

Kitaalamu:

  • Kitovu ni mabaki ya kamba ya uzazi (umbilical cord)
  • Hakihusiani kwa namna yoyote na ukuaji wa uume, korodani au homoni za kiume
  • Nguvu za kiume zinategemea:
    • Homoni kama testosterone
    • Afya ya mishipa ya damu
    • Mfumo wa uzazi

Hivyo, kitovu kuangukia sehemu yoyote hakina uwezo wa kumfanya mtoto awe hanithi au apungukiwe nguvu za kiume.

Kitovu kinatakiwa kidondokee wapi?

Kitaalamu:

  • Hakuna sehemu maalum kinatakiwa kudondokea
  • Kinaweza kuanguka:
    • kwenye nguo
    • kitandani
    • ardhini
    • hata karibu na mwili wa mtoto

Muhimu si mahali kinapoangukia, bali:

  • Kianguke chenyewe (bila kung’olewa)
  • Hakina maambukizi
  • Eneo libaki safi na kavu

Kwa nini imani hizi zipo?

Katika jamii nyingi:

  • Kitovu huonekana kama sehemu muhimu ya uhai wa mtoto akiwa tumboni
  • Hivyo watu walihusisha na mambo ya nguvu au hatima ya mtoto
    Lakini hizi ni tafsiri za kitamaduni, si za kitabibu.

Hitimisho la kitaalamu

Kitovu hakina athari yoyote kwa nguvu za kiume, Hakina sehemu maalum ya kudondokea,Hakina uhusiano na uchawi kwa mtazamo wa sayansi ya tiba.

Rejea: Kitovu cha Mtoto hakikauki,Kinatoa damu,Usaha,Sababu zake>>>
0 Comment

Tatizo la KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,DamuAfyaclass Forum •

KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,Damu,Sababu ni nini?

Zipo dalili mbali mbali huweza kujitokeza kwenye Kitovu cha Mtoto wako,Ukiona Dalili hizi,hakikisha Mtoto anapata Msaada, Dalili hizi ni hatarishi sio nzuri wake:

  • Kitovu kinatoa usaha wenye harufu mbaya
  • Damu inatoka mara kwa mara
  • Ngozi kuzunguka kitovu kuwa nyekundu au kuvimba
  • Mtoto ana homa au analia sana
  • Kitovu hakikauki hata baada ya siku 7–14

Sababu zinazoweza kusababisha

1.Maambukizi ya bakteria (kutokana na uchafu au utunzaji mbaya)

2.Kitovu kubaki na unyevunyevu muda mrefu

3.Kitovu Kuguswa na vitu vichafu (mfano majivu, mafuta, dawa za asili zisizo salama) n.k

Nini cha kufanya

Hii ni hali ya muhimu—usichelewe:

Mpeleke mtoto hospitali au kituo cha afya mara moja Au Ongea na Mtaalam wa Afya au Kwa Ushauri Zaidi na Tiba tuwasiliane hapa hapa afyaclass,kupitia namba +255758286584(Call,Sms,Whatsapp).

-Usitumie dawa za kienyeji au kubonyeza kitovu bila Ushauri Sahihi.

-Acha kitovu kiwe kikavu (dry cord care) usiweke maji au Vitu vitakavyoongeza unyevu unyevu

-Epuka kukifunika kwa diaper

-Usikigusie mara kwa mara

Kwa mtoto mchanga, maambukizi ya kitovu yanaweza kuenea haraka mwilini, hivyo ni muhimu kuchukua hatua mapema.

YAPO BAADHI YA MAMBO MUHIMU SANA YA KUZINGATIA KUHUSU KITOVU CHA MTOTO

1-Mama hakikisha kitovu cha mtoto hakivuji damu baada ya kukatwa na kufungwa na mtaalam wa afya.

2-Kitovu hudondoka chenyewe,ambapo kwa asilimia kubwa kwa watoto wengi ndani ya wiki moja,kitovu huwa tayari kimeshadondoka.

3-Hakikisha kitovu cha mtoto hakitoi usaha,au kubalika rangi hasa ya manjano na kutoa harufu mbaya,hii sio dalili nzuri.

4-Usiweke kitu chochote kwenye kitovu cha mtoto mpka kidondoke chenyewe.

5-Epuka imani potofu kama zile za kuweka mavi ya Ng'ombe n.k,kwenye kitovu cha mtoto.

KWA USHAURI,ELIMU AU MSAADA WA KIAFYA MAWASILIANO NI +255758286584.

2 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD