Showing posts with label Kombe la Dunia. Show all posts
Showing posts with label Kombe la Dunia. Show all posts

Italia haiwezi kuchukua Nafasi ya Iran kwenye kombe la DuniaAfyaclass Forum •

Italia haiwezi kuchukua Nafasi ya Iran kwenye kombe la Dunia

Vuta nikuvute katika kutafuta Nafasi kwenye Kombe la Dunia,Pendekezo la Italia kuchukua nafasi ya Iran kwenye Kombe la Dunia la mwaka 2026 lakataliwa,

Mjumbe mmoja wa Marekani anayefahamika kwa jina la Paolo Zampolli alitoa pendekezo kwamba Italia ipewe nafasi ya Iran kutokana na mzozo unaoendelea kati ya Iran, Marekani na Israel,

Hata hivo Shirikisho la Soka Duniani, FIFA limekataa Pendezo hilo,Waziri wa michezo wa Italia, Andrea Abodi na Waziri wa Uchumi, Giancarlo Giorgetti pia wamekataa pendekezo hilo wakisisitiza kwamba kama ni Italia kushiriki Kombe la Dunia lazima ishinde uwanjani na sio kwa njia za aina nyingine kama hii.

0 Comment

Nigeria yadai DR Congo walitumia wachezaji wasiostahikiAfyaclass Forum •

Nigeria yadai DR Congo walitumia wachezaji wasiostahiki kwenye mechi ya kufuzu Kombe la Dunia

Nigeria inataka Fifa kuangalia ustahiki wa baadhi ya wachezaji waliochezeshwa na DR Congo katika fainali ya kombe la dunia la Afrika 2026.Chanzo cha picha,Getty Images

Maelezo ya picha,Nigeria inataka Fifa kuangalia ustahiki wa baadhi ya wachezaji waliochezeshwa na DR Congo katika fainali ya kombe la dunia la Afrika 2026.

Nigeria inatarajia kuongeza nafasi yake ya kufuzu Kombe la Dunia mwaka ujao baada ya kuwasilisha malalamiko FIFA, ikidai kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo) ilitumia wachezaji wasiostahiki kwenye fainali ya kufuzu ya Afrika mwezi uliopita.

DR Congo ilishinda dhidi ya Super Eagles kwa penalti na kupata nafasi ya kucheza mechi ya kufuzu mashindano ya kimataifa Machi, ambayo itatenga nafasi mbili za mwisho za Kombe la Dunia katika Canada, Mexico na Marekani.

Madai ya Nigeria kuhusu “udanganyifu” yanahusu wachezaji waliobadilisha taifa lao la kimataifa hivi karibuni na kujiunga na timu pinzani.

Shirikisho la Soka la Nigeria (NFF) linaamini wachezaji kama Aaron Wan-Bissaka na Axel Tuanzebe, ambao walicheza mchezo huo Morocco, hawakuwa na sifa za kucheza kwani sheria za Kongo haziruhusu uraia pacha.

Shirikisho la Soka la Kongo (Fecofa) limekataa malalamiko hayo. “Suala letu ni kwamba FIFA ilidanganywa na kuwaruhusu kucheza,” alisema katibu mkuu wa NFF, Mohammed Sanusi. “Sheria za Kongo haziwaruhusu kuwa na uraia wa pacha, lakini baadhi ya wachezaji wao wana pasipoti za Ulaya na Ufaransa. Hii ni kinyume cha kanuni za FIFA. Tunadai ilikuwa ni udanganyifu.”

NFF imesema tayari imewasilisha nyaraka na hoja za kisheria kwa FIFA.

BBC imewasiliana na FIFA kwa maoni na inasubiri majibu.

Fecofa, kwa upande wake, imedai malalamiko hayo ni jaribio la “kushinda mlango wa nyuma.” “Kombe la Dunia lazima lichezwe kwa heshima na kujiamini, si kwa ujanja wa mawakili,” ilisema chapisho kwenye mitandao rasmi ya Leopards.

Ujumbe huo pia uliwataja Wana-Nigeria kama “washindwa mbaya” na kutupilia mbali malalamiko hayo kama mwenendo mbaya wa michezo.

0 Comment

Cristiano Ronaldo ‘arudishwa nyumbani’ baada ya kadi nyekunduAfyaclass Forum •

Cristiano Ronaldo ameripotiwa kurudishwa nyumbani kutoka kambi ya timu ya taifa ya Ureno baada ya kupata kadi nyekundu ya kwanza kimataifa.

Mshindi huyo mara tano wa Ballon d'Or alipewa kadi kwa kumpiga kiwiko Dara O'Shea baada ya saa moja ya kushindwa kwa timu yake 2-0 dhidi ya Ireland siku ya Alhamisi.

Kadi nyekundu za moja kwa moja katika soka ya kimataifa kwa kawaida hubeba marufuku ya mechi mbili, ikimaanisha kuwa Ronaldo anaweza kukosa mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Dunia la mwisho kwake kucheza.

Hata hivyo, vijana wa Roberto Martinez bado hawajafanikiwa kufuzu kwa mashindano ya msimu ujao wa joto - na watahitaji ushindi dhidi ya Armenia Jumapili ili kufanikiwa.

Lakini kulingana na chombo cha habari cha Ureno A Bola, Ronaldo hatakaa nje kuwashangilia wachezaji wenzake kwa ajili ya mchezo mgumu katika Uwanja wa Estádio do Dragão kwa sababu ‘ameachiliwa kutoka timu ya taifa’.

 Nahodha huyo wa Ureno sasa anatarajiwa kurejea Saudi Arabia, ambapo atatumainia utendaji bora kutoka kwa klabu yake ya Al-Nassr watakapokabiliana na Al-Khaleej mnamo Novemba 23.

0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD