Showing posts with label MOI. Show all posts
Showing posts with label MOI. Show all posts

WATOTO 25 wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi wafanyiwa UPASUAJIAfyaclass Forum •

WATOTO 25 WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI WAFANYIWA UPASUAJI AWAMU YA KWANZA YA KAMBI YA MATIBABU MOI

Na Abdallah Nassoro-MOI

Watoto 25 wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi wamefanyiwa upasuaji katika awamu ya kwanza ya kambi ya upasuaji inayoendelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), iliyoratibiwa na MOI kwa ushirkiano na chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi Tanzania (ASBATH) chini ya ufadhili wa taasisi ya MO Dewji Foundation.

Daktari bingwa wa Mbobezi wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu MOI Dkt. Hamisi Shabani amesema watoto hao ni kati ya 50 wanaotarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya matatibu.

“Jumla ya watoto wote katika mpango huu ni 50, katika awamu hii ya kwanza ya upasuaji watoto 25 wamefanyiwa upasuaji na Mei, 4, 2024 watoto 25 waliobakia watafanyiwa upasuaji ili kukamilisha malengo ya kambi hii” amesema Dkt. Shabani ambaye pia ni mratibu wa kambi hiyo na kuongeza kuwa

“Watoto hawa wanafanyiwa upasuaji kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu ya upasuaji wa kutumia matundu, ETV, upasuaji ambao humfanya mgonjwa kuruhusiwa kurudi nyumbani ndani ya siku chache tangu kufanyiwa upasuaji”

Amesema bado tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi ni kubwa hapa nchini ambapo takwimu zinaonesha kuwa watoto 7500 wanazaliwa na tatizo hilo ila mwaka.

“Sisi MOI kwa mwaka jana tuliweza kuwafanyia upasuaji watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi 800 hii inaonesha bado kuna wimbi kubwa la watoto ambao hawajapata matibabu”

Kwa upande wake Mratibu wa Miradi wa MO Dewji Foundation Amina Ramadhani amesema lengo la msaada huo ni kuwawezesha watoto hao kupata matibabu ili waweze kurejea katika hali zao za kawaida.

“Maisha ya kila mtu ni muhimu, iwapo kutakuwa na ongezeko la watoto zaidi ya 50 tutaangalia namna ya kuwasaidia ingawa lengo la mwaka huu lilikuwa watoto 50, tunawashukuru MOI na chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi (ASBATH)”

Merina Damon na Mohamed Hamisi ni wazazi wa watoto wenye vichwa vikubwa waliofanyiwa upasuaji wameishukuru MOI, chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi (ASBATH) MO Dewji Foundation kwa msaada wa matibabu hayo.

WATOTO 25 wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi wafanyiwa UPASUAJI
0 Comment

Wagonjwa 40 kubadilishwa nyonga MOIAfyaclass Forum •

Wagonjwa 40 kubadilishwa nyonga MOI

Na Radhia Balozi-MOI

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Prof. Abel Makubi amewapokea madaktari bingwa wabobezi wa upasuaji wa nyonga Watatu kutoka nchi ya Pakistan watakaoendesha kambi ya siku tano ya upasuaji wa nyonga kwa wagonjwa 40 kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa MOI.

Katika kambi hiyo iliyoanza jana Februari, 26, 2024 jumla ya wagonjwa 40 wanatarajia kufanyiwa upasuaji wa kubadilisha nyonga ambapo pia itatumika kama sehemu ya kuwajengea uwezo wa umahiri madaktari wazawa.

“Nashukuru kwa kuja kwenu, mjisikie mko nyumbani na iwapo mtapata changamoto yeyote msisite kuwasiliana nasi, uwepo wenu hapa ni wa umuhimu kwetu, tunaahidi kuendeleza ushirikiano huu muhimu kwa ustawi wa maendeleo ya tiba hapa MOI” amesema Prof. Makubi

Kwa upande wake kiongozi wa wataalam hao kutoka Pakistan Abdullah Amjad ameushukuru uongozi wa MOI kwa mapokezi mazuri, ukarimu na ushirikiano walioupata.

“Tunashukuru kwa mapokezi mazuri, na tunaahidi kuendeleza ushirikiano huu mzuri” amesema Amjad

Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Mifupa, Nyonga na Magoti Dkt. Athony Assey amesema kambi hiyo imeanza kwa upasuaji wa wagongwa wawili na baadae kuendelea na wengine hadi Machi, 01, 2024 kambi hiyo itakapomalizika.

Kambi hii ni matokeo ya jitihada za Serikali ya awamu ya sita baada ya kuiwezesha MOI kuwa na vipandikizi vyakutosha (Implants) ambapo hapo awali wagonjwa walisubiri huduma hii muda mrefu kutokana na uhaba wa vifaa.

Wagonjwa 40 kubadilishwa nyonga MOI
0 Comment

Wengine 9 kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Uvimbe kwenye UbongoAfyaclass Forum •

Wengine 9 kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Uvimbe kwenye Ubongo.

WAGONJWA 9 KUFANYIWA UPASUAJI MPYA WA KUONDOA UVIMBE KWENYE UBONGO.

Na Abdallah Nassoro-MOI

Madaktari bingwa wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na madaktari bingwa wabobezi kutoka Chuo Kikuu cha Colorado cha nchini Marekani wanatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa Tisa wenye matatizo ya uvimbe kwenye Ubongo kwa njia ya kisasa ya kutoboa tundu ndogo bila ya kufungua fuvu katika kambi ya mafunzo ya wiki moja inayoendelea MOI jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo wa tatu wa kimataifa wa mafunzo ya matibabu ya kisasa upasuaji wa uvimbe kwenye ubongo yanalenga kubadilishana uzoefu na kuwajengea uwezo madaktari bingwa wazawa, wauguzi wabobezi na wataalam wengine umefunguliwa leo Februari, 19, 2024 na na muwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Lemeri Mchome.

“Mwaka 2017 tulianza upasuaji wa uvimbe vya chini ya ubongo(Pituitary tumors) bila kupasua fuvu kwa mara ya kwanza. Madaktari wa MOI baada ya mafunzo na mashirikiano hayo wameendelea na upasuaji huo mpaka sasa kwa ufanisi mkubwa…

Kwa sasa hapa MOI takribani wagonjwa 572 tunawafanyia upasuaji wa vivimbe kwenye ubongo na karibia asilimia nne ya wagonjwa hawa bado wanaenda nje ya nchi kupata matibabu kwa vivimbe vilivyo ndani kabisa ya ubongo ambapo upasuaji wa kawaida unaweza kuleta madhara zaidi.

Hivyo mafunzo haya yatasadia uanzishwaji wa huduma hii mpya ya upasuaji wa uvimbe ndani ya ubongo (Stereotactic procedures).

Wengine 9 kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Uvimbe kwenye Ubongo
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD