Showing posts with label Rais wa Marekani. Show all posts
Showing posts with label Rais wa Marekani. Show all posts

Rais Donald Trump asema kama angejua Uzito na hatari ya Urais asingegombeaAfyaclass Bongo Social •

Trump Aeleza Uzito na Hatari ya Kazi ya Urais Baada ya Tukio la Usalama

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa angejua mapema uzito na hatari ya kazi ya urais, huenda asingegombea nafasi hiyo.

Kauli hiyo ameitoa kufuatia tukio la kiusalama lililotokea wakati wa hafla ya White House Correspondents’ Dinner, ambapo milio ya risasi ilisikika na kusababisha taharuki miongoni mwa wageni waliohudhuria.

Trump alimrejelea Marco Rubio akisema kama angepewa picha halisi ya changamoto za kazi hiyo mapema, huenda angefanya uamuzi tofauti kuhusu kugombea urais.

Katika maelezo yake kwa waandishi wa habari, Trump alisema kazi ya urais ni yenye changamoto kubwa na hatari, lakini ameendelea kusisitiza kuwa anajivunia kulitumikia taifa lake na yupo tayari kutekeleza wajibu wake.

Baada ya tukio hilo, maafisa wa usalama walichukua hatua za haraka kwa kuwaondoa Trump pamoja na viongozi wengine waliokuwepo ukumbini, huku wakihakikisha eneo hilo linawekwa salama.

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, mshukiwa ametambulika kama Cole Tomas Allen, mwenye umri wa miaka 31 kutoka California. Inadaiwa alikamatwa na kupelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi, wakati maafisa wa FBI wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo. Afisa mmoja wa usalama anaripotiwa kujeruhiwa lakini anaendelea kupatiwa matibabu.


0 Comment

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema amepata wa kuinunua kampuni ya TikTokAfyaclass Bongo Social •

NEWS: Kwenye Jukwaa la Teknolojia leo hii tuna habari kuhusu kampuni ya Tiktok.



Rais wa Marekani, Donald Trump amesema amepata wa kuinunua kampuni ya TikTok.

Kauli hiyo inakuja wakati ambapo kampuni ya ByteDance ya China inakabiliwa na shinikizo la kuiuza TikTok kwa Marekani, vinginevyo itazuiwa kutumika nchini humo.

1 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD