Showing posts with label Ugonjwa wa red eyes. Show all posts
Showing posts with label Ugonjwa wa red eyes. Show all posts

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho MekunduAfyaclass Forum •

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu

Baada ya Ugonjwa huu wa macho kusumbua watu wengi kwa kipindi cha Hivi Karibuni, ndani ya Afyaclass tulitoa elimu mbali mbali kuhusu Ugonjwa huu,

Na leo Katika Makala hii tunazidi kukuelimisha Uujue Vizuri Ugonjwa huu wa macho Mekundu Maarufu kama RED EYES.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu

Ugonjwa wa macho mekundu ni ugonjwa ambao hujulikana kama Red Eyes,

Ugonjwa wa red eyes ni ugonjwa ambao huhusisha macho kuwa mekundu kama dalili kubwa.

Katika Makala hii tumechambua chanzo cha Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes), dalili Zake kuu, jinsi ya kuzuia usipate Pamoja na Matibabu yake.

CHANZO CHA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

Ugonjwa wa Macho mekundu(Red Eyes) hutokana na mashambulizi ya vimelea vya magonjwa kama vile Virusi ambavyo husababisha vishipa vidogo ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

Maambukizi ya kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalam “Viral Keratoconjunctivitis” ni Maambukizi yanayosambaa kwa kasi kubwa .Hakuna tiba maalum kwa ugonjwa huu na hata bila tiba, dalili huisha zenyewe ndani ya wiki mbili . Usafi ni jambo muhimu katika kuzuia maambukizi haya kusambaa kwa wengine.

Mlipuko huu husababishwa na Kirusi kijulikanacho kwa jina la “Adenovirus”kwa zaidi ya asilimia 80%.

Dalili za Ugonjwa wa Macho Mekundu

DALILI ZA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NI PAMOJA NA;

• Macho kubadilika rangi na kuwa mekundu,

hii ni ishara ya Vishipa vidogo vya damu ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

• Kuwashwa na macho

• Kuhisi kitu kama mchanga ndani ya jicho lako

• Kuvimba macho yako

• Kuhisi hali ya kuungua ndani ya macho,

Hii ni ishara ya kutengeneza hali ya vidonda ndani ya jicho(Conjunctivitis Sore),

• Macho kuwasha au kutoa maji/nachozi yenyewe n.k

Ni nini cha Kufanya Kama Una Ugonjwa wa Macho Mekundu(Red Eyes)?

Ikiwa jicho lako haliumi na kuona kwako hakujaathiriwa, labda sio jambo kubwa. Ugonjwa huu wa macho mekundu(Red Eyes) unaweza kupona wenyewe ndani ya siku chache.

Mpaka Unapona Unashauriwa;

  • Kutokugusa au kusugua macho yako
  • Usivae miwani inayogusa macho, na kama kuna ulazima wa kuvaa,Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa
  • Zingatia Usafi

JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

– Watoto wadogo Wagonjwa wanaoenda shule wanashauriwa wakae nyumbani hadi dalili zinapoisha kwa kuwa ni ngumu kuzuia maambukizi yasisambae kwenye mazingira ya shule.

– Watu wazima wanaweza kwenda kazini ila wanapaswa kuzingatia kanuni za kuzuia kutokuambukizwa au kuambukiza wengine kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

– Watumishi wa Afya wazingatie kutopeleka Maambukizi hayo nyumbani kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

Zingatia Zaidi Mambo Haya Muhimu;

1. Usisugue au kupikicha macho yako,

Uchafu pamoja na Viini vya magonjwa(germs) kwenye mikono yako pamoja na Vidole vinaweza kusababisha hali Zaidi ya Wekundu na Muwasho ndani ya macho.

2. Kama unavaa miwani, Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa

3. Zingatia Usafi kwa Ujumla, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mikono yako unanawa kwa maji safi tiririka na Sabuni

4. Kwa Wale wanaopaka MakeUp, Hakikisha unaondoa MakeUp yako Vizuri na kuacha macho yako yakiwa Safi(Remove your eye makeup properly, and keep your eyes clean).

5. Pata Mapumziko ya mara kwa mara, ikiwa unafanya kazi zinazohusisha kuangalia computer screen kwa Muda Mrefu.

6. Epuka vitu ambavyo huweza kuleta usumbufu(irritation) wowote machoni kama vile; vumbi,moshi n.k

7. Hakikisha unaenda kuchunguzwa macho au kufanya Vipimo vya macho(Eye exam) ikiwa una shida ya macho kuwa mekundu mara kwa mara au Ikiwa hali ya macho kuwa mekundu haiishi.

MATIBABU YA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU(RED EYES)

– Ugonjwa huu wa Macho mekundu(red eyes) hupona wenyewe ndani ya siku 3 mpaka 5, ndani ya wiki 2 n.k kulingana na uwezo au uimara wa kinga yako ya mwili Wala huhitaji matumizi ya dawa yoyote ile.

Japo lazima kwanza kuchuguzwa na wataalam wa afya baada ya kujihakikishia kuwa ni shida ya red eyes watakupa maelekezo kwa kina ikiwa ni pamoja na jinsi ya kutunza jicho lako.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Mlipuko wa ugonjwa wa macho,Macho Mekundu
0 Comment

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyesAfyaclass Forum •

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyes’

Wataalamu wasema zinachangia kuongeza maumivu, waonya zaweza kusababisha uoni hafifu na upofu.

Wataalamu wa afya na madaktari bingwa wa macho wamesema wanapokea idadi kubwa ya wagonjwa wakiwa katika hali ya ugonjwa mkali, kutokana na matumizi ya njia mbadala kutibu macho, ikiwamo matumizi ya mkojo na chumvi.

Hali hiyo imebainika siku 15 tangu kutangazwa kuibuka ugonjwa huo ujulikanao viral keratoconjunctivitis (red eyes) Januari 13, 2024 mkoani Dar es Salaam.

Wataalamu waliozungumza na Mwananchi Digital jana Januari 28, 2024 wameeleza wagonjwa wanaotumia chumvi, mkojo, chai ya rangi na kitunguu saumu kama tiba, macho yao huvimba na kuuma zaidi pamoja na kupatwa homa. Athari hasi zaidi zinazotajwa ni kusababisha vidonda kwenye kioo cha jicho.

Tiba hizo mbadala zinaelezwa zinaweza kusababisha kovu kwenye jicho litakalomfanya mgonjwa apate uoni hafifu au kupoteze uwezo wa kuona kabisa.

Daktari bingwa na mkuu wa kitengo cha macho kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Sarah Mrema ameisema idadi ya wagonjwa wanaohudhuria hospitalini hapo kutibiwa macho imekuwa ikiongezeka na kupungua.

Amesema wamekuwa wakipokea wagonjwa wakiwa tayari walianza kutumia tiba za majani ya chai, vitunguu saumu na chai ya rangi.

“Si kwamba wanapona wakitumia tiba mbadala, maumivu yanazidi, wakija hapa wanakuwa na maumivu makali. Ukihoji anakwambia alitumia mkojo, chumvi na njia nyingine nyingi. Unampa dawa anatumia, kisha anapona,” amesema Dk Sarah.

Kwa mujibu wa Dk Sarah, takwimu za hospitali hiyo zinaonyesha tangu Desemba 22, 2023 wagonjwa 105 walifika kutibiwa na kuna siku orodha ya wagonjwa inapanda na siku nyingine inapungua.

Daktari bingwa wa macho katika Hospitali ya Muhimbili-Upanga, Neema Moshi amesema unapotumia vitu vikali kutibu macho, ni rahisi kuharibu kioo cha mbele cha jicho na maumivu yanayotokea huwa makali.

Amesema wakati mwingine unaweza kupoteza uoni kwa sababu ya kuharibu kioo hicho.

“Tunapokea wagonjwa wengine wana hali mbaya, lakini hawezi kuwa mkweli, unajua mgonjwa hawezi kuja kusema alitumia kitu fulani, mara nyingi wanafichaficha labda tatizo liwe kubwa zaidi ndipo wanasema ukweli,” amesema.

Dk Neema amesema kama mgonjwa ametumia vitu hivyo na hajapata athari hawezi kupata athari baadaye.

“Si kwamba athari hizo zinakuwa za taratibu, kama amepona na haikuonekana kupata shida yoyote haiwezi kutokea tena baadaye,” amesema.

Meneja Mpango wa Taifa wa huduma za macho kutoka Wizara ya Afya, Dk Bernadetha Shilio amesema wapo wagonjwa wanaopata athari, lakini hawana takwimu, akisisitiza ni muhimu wagonjwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu.

“Taarifa hizi zinatolewa na wataalamu wa afya, yaani madaktari kwenye vituo husika, labda mimi kuna mtu amekuja amefanya hivi na vile lakini kutoa hali ilivyo kwa sasa wangapi wamethirika kwa sasa bado.

“Hata leo nimepewa taarifa kuna mtu anatumia sijui vitu gani, lakini pia kuna taarifa za uvumi kuna mtu katoka huko anashauri wagonjwa wanywe Azuma inatibu, huo ni uongo,” amesema.

Dk Shilio amewataka wagonjwa waepuke kutibu macho kwa kutumia kitunguu saumu kwa kuwa kunaweza kusababisha michubuko kwenye ngozi ya jicho na kioo cha mbele ya jicho, hivyo kuathiri uwezo wa jicho kuona.

“Maji ya chumvi yanaweza kusababisha michubuko au kidonda kwenye kioo cha mbele cha jicho, hivyo kutengeneza kovu litakalopunguza uwezo wa jicho kuona au ulemavu wa kutoona wa kudumu,” amesema.

“Matumizi ya chai ya rangi katika kutibu macho yanaweza kusababisha vidonda kwenye kioo cha jicho na kusababisha kovu kwenye jicho litakalokufanya upate uoni hafifu au upoteze uwezo wa kuona kabisa,” amesema.

Dk Shilio amewataka wagonjwa pia kuepuka kutibu macho kwa mkojo, kwani ni hatari kwa usalama wa macho kwa kuwa mkojo hubeba uchafu na vijidudu vinavyoweza kusababisha maambukizi mengine na kupoteza uwezo wa kuona kabisa.

Amewataka kuzingatia kunawa mikono mara kwa mara na wapatapo ugonjwa huo kuwahi kituo cha afya kwa uchunguzi na matibabu sahihi na kwa wakati.

Via Mwananchi.

Soma Zaidi hapa Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes)

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyes
0 Comment

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na MatibabuAfyaclass Forum •

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu

Ugonjwa wa macho mekundu ni ugonjwa ambao hujulikana kama Red Eyes,

Ugonjwa wa red eyes ni ugonjwa ambao huhusisha macho kuwa mekundu kama dalili kubwa.

Katika Makala hii tumechambua chanzo cha Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes), dalili Zake kuu, jinsi ya kuzuia usipate Pamoja na Matibabu yake.

CHANZO CHA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

Ugonjwa wa Macho mekundu(Red Eyes) hutokana na mashambulizi ya vimelea vya magonjwa kama vile Virusi ambavyo husababisha vishipa vidogo ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

Maambukizi ya kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalam “Viral Keratoconjunctivitis” ni Maambukizi yanayosambaa kwa kasi kubwa .Hakuna tiba maalum kwa ugonjwa huu na hata bila tiba, dalili huisha zenyewe ndani ya wiki mbili . Usafi ni jambo muhimu katika kuzuia maambukizi haya kusambaa kwa wengine.

Mlipuko huu husababishwa na Kirusi kijulikanacho kwa jina la “Adenovirus”kwa zaidi ya asilimia 80%.

Dalili za Ugonjwa wa Macho Mekundu

DALILI ZA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU NI PAMOJA NA;

• Macho kubadilika rangi na kuwa mekundu,

hii ni ishara ya Vishipa vidogo vya damu ndani ya macho kuvimba na kupasuka, kisha damu kuvilia ndani ya jicho.

• Kuwashwa na macho

• Kuhisi kitu kama mchanga ndani ya jicho lako

• Kuvimba macho yako

• Kuhisi hali ya kuungua ndani ya macho,

Hii ni ishara ya kutengeneza hali ya vidonda ndani ya jicho(Conjunctivitis Sore),

• Macho kuwasha au kutoa maji/nachozi yenyewe n.k

Ni nini cha Kufanya Kama Una Ugonjwa wa Macho Mekundu(Red Eyes)?

Ikiwa jicho lako haliumi na kuona kwako hakujaathiriwa, labda sio jambo kubwa. Ugonjwa huu wa macho mekundu(Red Eyes) unaweza kupona wenyewe ndani ya siku chache.

Mpaka Unapona Unashauriwa;

  • Kutokugusa au kusugua macho yako
  • Usivae miwani inayogusa macho, na kama kuna ulazima wa kuvaa,Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa
  • Zingatia Usafi

JINSI YA KUZUIA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU

– Watoto wadogo Wagonjwa wanaoenda shule wanashauriwa wakae nyumbani hadi dalili zinapoisha kwa kuwa ni ngumu kuzuia maambukizi yasisambae kwenye mazingira ya shule.

– Watu wazima wanaweza kwenda kazini ila wanapaswa kuzingatia kanuni za kuzuia kutokuambukizwa au kuambukiza wengine kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

– Watumishi wa Afya wazingatie kutopeleka Maambukizi hayo nyumbani kwa kufuata kanuni za kuzuia maambukizi.

Zingatia Zaidi Mambo Haya Muhimu;

1. Usisugue au kupikicha macho yako,

Uchafu pamoja na Viini vya magonjwa(germs) kwenye mikono yako pamoja na Vidole vinaweza kusababisha hali Zaidi ya Wekundu na Muwasho ndani ya macho.

2. Kama unavaa miwani, Hakikisha miwani yako(contact Lenses) inakuwa Safi, na Usiivae kwa muda mrefu Zaidi ya inavyoshauriwa

3. Zingatia Usafi kwa Ujumla, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mikono yako unanawa kwa maji safi tiririka na Sabuni

4. Kwa Wale wanaopaka MakeUp, Hakikisha unaondoa MakeUp yako Vizuri na kuacha macho yako yakiwa Safi(Remove your eye makeup properly, and keep your eyes clean).

5. Pata Mapumziko ya mara kwa mara, ikiwa unafanya kazi zinazohusisha kuangalia computer screen kwa Muda Mrefu.

6. Epuka vitu ambavyo huweza kuleta usumbufu(irritation) wowote machoni kama vile; vumbi,moshi n.k

7. Hakikisha unaenda kuchunguzwa macho au kufanya Vipimo vya macho(Eye exam) ikiwa una shida ya macho kuwa mekundu mara kwa mara au Ikiwa hali ya macho kuwa mekundu haiishi.

MATIBABU YA UGONJWA WA MACHO MEKUNDU(RED EYES)

– Ugonjwa huu wa Macho mekundu(red eyes) hupona wenyewe ndani ya siku 3 mpaka 5, ndani ya wiki 2 n.k kulingana na uwezo au uimara wa kinga yako ya mwili Wala huhitaji matumizi ya dawa yoyote ile.

Japo lazima kwanza kuchuguzwa na wataalam wa afya baada ya kujihakikishia kuwa ni shida ya red eyes watakupa maelekezo kwa kina ikiwa ni pamoja na jinsi ya kutunza jicho lako.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE LILE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD