Showing posts with label Uzazi wa mpango. Show all posts
Showing posts with label Uzazi wa mpango. Show all posts

Mtoto azaliwa akiwa ameshika KitanziAfyaclass Forum •

Mtoto azaliwa akiwa ameshika Kitanzi ambacho kilishindwa kuzuia ujauzito kwa mama yake

Mtoto mchanga aligonga vichwa vya habari baada ya kuzaliwa akiwa ameshika kifaa cha ndani ya uterasi (IUD) au Kitanzi au Lupu ambacho kilikusudiwa kuzuia ujauzito.

Madaktari waliripotiwa kushangazwa kuona kifaa hicho bado kipo mahali pake wakati wa kuzaliwa, na kuifanya kuwa tukio la nadra na lisilo la kawaida kimatibabu.

Ingawa IUD ni miongoni mwa aina bora za njia ya uzazi wa mpango—ujauzito bado unaweza kutokea ikiwa kifaa kitabadilika au kushindwa kufanya kazi kama ilivyokusudiwa. Ingawa ni nadra sana, kesi hii inaonyesha uwezekano mdogo wa IUD kushindwa kufanya kazi na imezua mjadala mkubwa katika duru za kimatibabu na kijamii.

#IUD #Udhibiti wa Kuzaliwa #Kesi ya Kimatibabu nadra #Ukweli wa Mtoto Mchanga #Uzazi wa Mpango.....

0 Comment

Njia ya Vipandikizi yatumika zaidi miongoni mwa wanawakeAfyaclass Forum •

Njia ya Vipandikizi yatumika zaidi miongoni mwa wanawake.

Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria Tanzania (TDHS) ya mwaka 2022 unaonyesha asilimia 45 ya wanawake wenye uwezo wa kufanya tendo la ndoa wanaotumia njia za uzazi wa mpango, asilimia 36 wanatumia njia za kisasa na asilimia nane wanatumia za asili.

Hata hivyo, njia ya vipandikizi ndiyo inayotajwa kutumika zaidi miongoni mwa wanawake kwa asilimia 14 ikifuatiwa na njia ya sindano kwa asilimia tisa.

Hayo yamebainishwa na Mhariri wa Afya wa Mwananchi, Herieth Makwetta Siku ya Jumatano, Septemba 25, 2024 wakati akichokoza mada kwenye mjadala wa Mwananchi Space, ulioandaliwa na Mwananchi Communications Limited (MCL) kwa kushirikiana na Marie Stopes Tanzania @mariestopestz isemayo ‘Uhuru wa Kuamua: Namna upatikanaji wa haki muhimu za afya ya uzazi unavyochangia maendeleo Tanzania’. 

Amesema takwimu zinaonyesha mwaka 2022 vifo vitokanavyo na uzazi vilikuwa 104 kwa kila vizazi hai 100,000. Hata hivyo, lengo la Serikali ni kupunguza vifo kutoka 104 katika kila vizazi hai 100,000 hadi 70 kufikia mwaka 2025.

“Uzazi wa mpango ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania, kwani huokoa maisha kwa kusaidia kupunguza magonjwa ya kina mama na vifo, na kuongeza viwango vya kuishi kwa watoto wachanga,” amesema. 

Amefafanua kuwa uzazi wa mpango ni sehemu ya kuboresha afya ya mama na mtoto lakini pia kujenga uchumi wa familia na Taifa kwa ujumla. 

Amesema kwamba upatikanaji wa uzazi wa mpango wa hiari na huduma ya afya ya uzazi kwa wanandoa na watu binafsi ni muhimu katika kuhakikisha uzazi salama, familia zenye afya na jamii zinazostawi.

(Imeandikwa na Sute Kamwelwe)

Via; mwananchiupdates

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD