Showing posts with label afya ya uzazi. Show all posts
Showing posts with label afya ya uzazi. Show all posts

Mambo 5 yanayopunguza Ubora wa Mbegu za KiumeAfyaclass Forum •

Mambo 5 yanayopunguza Ubora wa Mbegu za Kiume

Katika Makala hii tumechambua baadhi ya Mambo makubwa ambayo huweza kuathiri ubora wa Mbegu za Kiume(Sperm quality),Soma Makala hii Mpaka mwisho kufahamu.

MAMBO 5 YANAYOPUNGUZA UBORA WA MBEGU ZA KIUME

Ubora wa mbegu za kiume ni muhimu kwa afya ya uzazi. Hata hivyo, mtindo wa maisha na mazingira yanaweza kuathiri uzalishaji na ubora wake. 

Hapa ni mambo 5 yanayoweza kupunguza ubora wa mbegu za kiume:

1. Msongo wa Mawazo (Stress)

Msongo wa mawazo huathiri uzalishaji wa homoni muhimu kwa uzazi, kama vile homoni ya testosterone, na kusababisha kupungua kwa idadi na kasi ya mbegu za kiume.

2. Lishe Duni

Upungufu wa virutubisho kama vile zinki, vitamini C, na antioxidants unaweza kupunguza uzalishaji wa mbegu zenye afya. Epuka vyakula vyenye mafuta mengi na sukari kupita kiasi.

3. Uvutaji wa Sigara na Matumizi ya Pombe Kupita Kiasi

Nikotini na kemikali nyingine kwenye sigara huathiri moja kwa moja uzalishaji wa mbegu za kiume. Pombe pia hupunguza viwango vya testosterone, hivyo huweza kuathiri uzazi.

4. Joto Kali Sehemu za Siri

Kuvaa nguo za kubana, matumizi ya laptop kwenye mapaja, au kukaa muda mrefu kwenye viti vyenye joto (kama vile kwenye gari) huongeza joto kwenye korodani na kupunguza uzalishaji wa mbegu.

5. Kutopata Usingizi wa Kutosha

Usingizi duni huathiri usawa wa homoni mwilini, na hivyo kupunguza uzalishaji wa mbegu za kiume. Hakikisha unapata saa 7-8 za usingizi bora kila usiku.

♻️ Badilisha mtindo wa maisha ili kuboresha afya ya uzazi!

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

#AfyaYaUzazi #MbeguZaKiume #AfyaBora

0 Comment

Maumivu Ya Chini Ya Kitovu,Mgongo Na Matiti Baada Ya Kujifungua/KuzaaAfyaclass Forum •

MAUMIVU YA CHINI YA KITOVU,MGONGO NA MATITI BAADA YA KUJIFUNGUA/KUZAA

Maumivu ya tumbo hasa chini ya kitovu,
mgongo na matiti mara baada ya
kujifungua/kuzaa na ambayo huongezeka
wakati wa kunyonyesha kitaalamu yanaitwa "afterpains"

Mara kadhaa watu wamekuwa wakiamini kuwa maumivu yanayoambatana na zoezi zima la kujifungua hupotea mara baada ya kujifungua. Kitu ambacho inawezekana si sahihi kwa wote.

Nyakati za awali mara baada ya kujifungua inaaminika kunakuwa na mabafiliko katika baadhi ya maeneo ya ubongo ambayo kwa namna moja ama nyingine hupelekea fikira na mitazamo ambayo hupelekea kuhisi maumivu makali isivyo kawaida.

Kuzaa kwa upasuaji au kuzaa kwa njia ya kawaida lakini kwa kusaidiwa na vifaa kunaambatana na maumivu makali baada ya kujifungua ukilinganisha na unapozaa kawaida. Kwa kawaida maumivu haya hutegemea hisia, mawazo na mtazamo.

Maumivu ya tumbo hutokea ikiwa ni matokeo ya mji wa mimba kunywea au kupungua kwa mji wa mimba katika hatua ya kurudi katika umbo la awali kabla ya kubeba ujauzito.

Namba ya nzao inahusishwa na kiwango cha maumivu haya. Katika mimba ya kwanza maumivu haya huweza kuwa sio makali sana n uweza kuisha ndani ya muda mfupi, lakini baada ya mimba mbili na kuendelea inaaminika maumivu huongezeka kutokana ukweli kuwa misuli ya mji wa mimba inakuwa imepunguza nguvu ya mvutano hivyo hupitia katika kipindi cha kunywea na kujilegeza hivyo kupelekea maumivu kuwa endelevu kwa muda.

Mimba zenye mapacha, watoto wakubwa, kiwango kikubwa cha maji katika mfuko wa mtoto, maambukizi nk zinaaminika kuambatana na maumivu haya mara baada ya kujifungua.

Kunyonyesha huweza kuleta au kuongeza kiwango cha maumivu kwasababu kitendo cha kunyonyesha hupelekea kutolewa kwa homoni ya oxytocin ambayo huchochea kunywea kwa mji wa mimba na hivyo maumivu.

Maumivu haya huweza kuwa chini ya kitovu, mgongoni au kwenye matiti.

Asilimia 64 ya kinamama hufananisha maumivu haya na maumivu ya hedhi. Baadhi hufananisha na maumivu au hisia mtoto akicheza awapo tumboni, wengine hufananisha na maumivu ya njaa na wengine huyafananisha na kitu kigumu kinachotembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

NAMNA YA KUZIA AU KUPUNGUZA
kukojoa mara kwa mara, kulalia tumbo (kulala kifudi fudi) AU kujikanda na maji ya vuguvugu inaweza kusaidia.

Matumizi ya dawa , za kutuliza maumivu, hupelekea kukata au kutulia kwa maumivu haya

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

Ni mara ngapi unaweza kuhitaji kubadilisha pedi yako kila siku?Afyaclass Forum •

 Ni mara ngapi unaweza kuhitaji kubadilisha pedi yako kila siku?

Kukaa na Pedi kwa Muda Mrefu huweza kuongeza hatari ya Mwanamke kupata magonjwa mbali mbali ikiwemo Fangasi.

Ni mara ngapi unaweza kuhitaji kubadilisha pedi yako kila siku?

Hii inaweza kutegemea kiwango chako cha Hedhi unachopata, jinsi mtiririko wako ulivyo mzito, na aina ya pedi unayotumia. Lakini unapaswa kuibadilisha kabla haijajaa.

Kwa Mujibu wa "The American College of Obstetricians and Gynecologists (ACOG)" wanapendekeza ubadilishe pedi yako angalau kila baada ya saa 4 hadi 8, lakini hayo ni masaa ya jumla tu.

Ni mara ngapi unabadilisha pedi yako inategemea na sababu mbali mbali ikiwemo; mtiririko wako, aina ya pedi unayotumia n.k.

0 Comment

AFYA YA UZAZI KWA WANAUMEAfyaclass Forum •

 AFYA YA UZAZI KWA WANAUME

Hapa tunazungumzia mfumo mzima wa uzazi ikiwemo,

via vya uzazi vya Mwanaume pamoja na mbegu za kiume.

Uwezo wa kufanya tendo la ndoa vizuri bila shida yoyote,

Pamoja na uzalishaji wa mbegu za kiume zenye ubora na kiwango kinachotakiwa.

ZINGATIA HAYA KWENYE AFYA YA UZAZI KWA MWANAUME

• Hakikisha unakula mlo kamili na kuepuka kula vyakula vyenye virutubisho vya aina moja kwa kiwango kikubwa

kama vile kula wanga mwingi,mafuta mengi n.k

• Epuka matumizi ya Pombe kama unataka kuboresha afya ya uzazi

• Epuka matumizi ya Sigara pamoja na dawa zingine za kulevyia

• Epuka matumizi ya dawa hovio pasipo maelekezo kutokwa kwa wataalam wa afya

• Zingatia matumizi ya maji ya kutosha kila siku,angalau lita 2.5 mpaka 3

• Fanya mazoezi mbalimbali ya mwili

• Epuka kuwa na uzito mkubwa au unene obesity/overweght

• Jilinge au jikinge na magonjwa yote ya zinaa, na pata tiba mara moja kama una ugonjwa wowote ambao unashambulia sehemu zako za siri.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584



0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD