Showing posts with label afya ya watoto. Show all posts
Showing posts with label afya ya watoto. Show all posts

Cheti cha kuzaliwa cha mtoto,Maombi ya CHETI cha KuzaliwaAfyaclass Forum •

Cheti cha kuzaliwa cha mtoto,Maombi ya CHETI cha Kuzaliwa

Maelezo ya RITA juu ya Cheti cha Kuzaliwa na Upatikanaji wake.

Maombi ya Cheti cha Kuzaliwa

Usajili wa kuzaliwa unaweza kufanywa katika:

i.Katika kituo cha tiba au ngazi ya kitongoji kwa watoto wachanga (ndani ya siku 90)

ii.Katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya (usajili wa kuchelewa)

iii.Kwa mtandao (usajili wa kuchelewa, kubadilisha cheti cha zamani kuwa kipya)

Mtoto anasajiliwa mara tu baada ya kuzaliwa katika kituo cha tiba ambapo tukio la kizazi limetokea au katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata kwa vizazi vya nyumbani. Ikiwa kwa sababu fulani mtu anakosa kusajili mahali hapo, mtoto anaweza kusajiliwa wakati wa chanjo ndani ya siku 90. Aidha, tukio la kuzaliwa linaweza kusajiliwa kama usajili wa kuchelewa katika Ofisi ya Katibu wa Wilaya kwa kupitia mtandao.

Mahitaji ya jumla kwa maombi ya cheti cha kuzaliwa:

Mwombaji lazima aambatishe baadhi ya hati mbili kati ya zifuatazo:

  • Kadi ya Kliniki ya Mama
  • Kadi ya Kliniki ya Mtoto
  • Tangazo la kuzaliwa
  • Cheti cha Ubatizo cha Mtoto (kwa wale walio batizwa wakiwa na umri mdogo)
  • Cheti cha Kumaliza elimu (Shule za Msingi au Sekondari - O Level)
  • Pasi ya kusafiria
  • Kadi ya mpiga kura
  • Cheti cha ubatizo

Pamoja na mojawapo ya haya:

  • Kitambulisho cha Kitaifa cha mzazi/mlezi
  • Hati ya kusafiria ya mzazi
  • Utambulisho kutoka Mtendaji wa Kata

N.B: Uhitaji wa kuweka vitambulisho vya wazazi vitatumika ikiwa wazazi wapo hai.

USAJILI UNAVYOFANYIKA KWA WATOTO WACHANGA
Mwombaji (Mzazi/mlezi) atasajili tukio hili kwenye dawati la Usajili katika Kituo cha tiba kizazi kilipotokea wakati mtoto anapozaliwa au wakati wa kupata chanjo. Pia Usajili unaweza kufanyika katika ofisi ya kata kwa vizazi vya nyumbani.

Soma Zaidi kwenye Ukurasa Wao: https://www.rita.go.tz/page.php?p=9

0 Comment

Chuchu Za Watoto(Vifaa Vya Kumlishia Mtoto)Afyaclass Forum •

 CHUCHU ZA WATOTO(Vifaa vya kumlishia Mtoto)

Hapa nazungumzia chuchu za watoto,yaani vifaa vile vya kuweka maziwa na kumpa mtoto wako, kama kwenye picha hapo.

Kwanini mada hii? Wakina mama wengi wanajisahau kwenye usafi wakati wa unyonyeshaji.

Chuchu hizi hazisafishwi vizuri, hali ambayo hupelekea mtoto kunyonya maziwa pamoja na uchafu uliopo kwenye chuchu,

na matokeo yake mtoto anaanza kulia tu, tumbo linauma, anaharisha n.k

ZINGATIA HAYA WAKATI WA UNYONYESHAJI

- Mama unayenyonyesha hakikisha mwenyewe unakuwa safi kuanzia matiti yako mpaka mwili mzima, hivo oga au nawisha matiti yako kabla ya kuanza kumnyonyesha mtoto

- Hakikisha vifaa au vyombo vyote unavyotumia kumnyonyeshea mtoto wako ni safi kabsa, kuanzia chuchu za watoto n.k

- Mnyonyeshe mtoto kwa muda unayotakiwa,sio unamnyonyesha mtoto dakika mbili halafu unakimbia,

Wengine wanasema maziwa yanatoka mepesi,

Kumbuka; maziwa ya mama yamegawanyika kwenye sehemu kuu tatu,

(i) Sehemu ya kwanza ni mepesi sana kama maji, lengo ni ili kukata kiu ya mtoto, kwani mtoto hatakiwi kunywa maji

(ii) Sehemu ya pili yanaanza kubadilika kidogo tofauti na ya mwanzo

(iii) Na sehemu ya tatu ndyo maziwa mazito, haya ndyo mtoto akiyafikia na kunyonya hushiba sasa vizuri kama chakula, ukimnyonyesha mtoto dakika mbili huwezi kuyakuta haya maziwa mazito, ambayo ndyo chakula cha kumshibisha mtoto wako.

- Unyonyeshaji wa maziwa ya mama peke yake bila mtoto kuchanganyiwa na vitu vingine vyovyote unaenda mpaka miezi sita, hii kwa kitaalam hujulikana kama EXCLUSIVE BREASTFEEDING.

- Baada ya mtoto kunyonya maziwa ya mama peke yake ndani ya miezi sita ya kwanza ndyo unaanza kumchanganyia na vitu vingine,

ila usiache kumnyonyesha mpaka afikishe miaka 2 au wengine hadi 3 kama unaweza

KUMBUKA;

• Maziwa ya mama ni kinga bora kwa mtoto wako dhidi ya magonjwa mbali mbali, hasa katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza ambapo kinga ya mtoto ni ndogo saana

• Usafi wa vyombo vya kumlishia mtoto pamoja na wewe mwenye ni muhimu sana.

• Hakikisha mtoto anapata chanjo zote ikiwemo chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kifua kikuu maarufu kama BCG, chanjo ya POLIO n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

Dawa Ya Mafua Kwa Watoto WadogoAfyaclass Forum •

DAWA YA MAFUA KWA WATOTO WADOGO

Moja ya vitu ambavyo huwasumbua sana watoto wadogo ni pamoja na mafua,kuharisha,kutapika,maumivu ya tumbo na homa.

Na ndyo maana kuna chanjo kabsa inajulikana kama ROTAX kwa lengo la kumzuia mtoto na shida ya kuharisha.

Mtoto mwenye shida ya mafua huweza kuambatana na shida zingine mfano;

• Mtoto kupiga chafya sana au kwa kitaalam hujulikana kama Sneezing

• Mtoto kukohoa mara kwa mara

• Macho ya mtoto kuwa mekundu kuliko kawaida

• Mtoto kukosa kabsa hamu ya kunyonya au kula chochote

• Mtoto kulia sana mara kwa mara

• Mtoto kukosa kabsa usingizi na kuhangaika tu muda wote

• Na wakati mwingine mtoto kuwa na homa au joto la mwili kuwa juu

Je mtoto mwenye mafua anasaidiwaje?

MATIBABU YA MAFUA KWA MTOTO MDOGO,

Kwanza kabsa,kabla ya kwenda kwenye matibabu unashauriwa kupambana na kuzuia vitu vyote ambavyo huweza kuwa chanzo cha mafua kwa mtoto wako kama vile;

- Kuzuia mtoto kukaa sehemu zenye vumbi sana

- Kuwasha Feni muda wote kwa watoto

- Kutumia mafuta au perfumes zenye harufu kali sana

- Kukaa na mtoto sehemu ambazo kuna shughuli zozote ambavyo huhusisha vumbi,uchanganyaji wa kemikali,dawa n.k

- Kukaa na mtoto mdogo sehemu ambavyo kuna moshi sana

- Mtoto kuchezea maji au kuwa katika hali ya unyevu unyevu muda wote ikiwa ni pamoja na kuvaa nguo ambazo hazijakauka vizuri. n.k

TIBA AU DAWA YA MAFUA KWA WATOTO WADOGO

Kwa upande wa Tiba, Baada ya wataalam wa afya kumchunguza mtoto,huweza kumpatia dawa mbali mbali kama vile Sodium chloride nasal drops n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD