Showing posts with label bbcswahili. Show all posts
Showing posts with label bbcswahili. Show all posts

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya BBC kufuatia jinsi hotuba yake ilivyohaririwaAfyaclass Bongo Social •

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya BBC kufuatia jinsi hotuba yake ilivyohaririwa na kipindi cha Panorama, baada ya shirika hilo kuomba msamaha lakini kukataa kumlipa fidia.

Akizungumza na waandishi wa habari ndani ya Air Force One Ijumaa jioni, Trump alisema: “Tutawashtaki kwa chochote kati ya dola bilioni 1 hadi 5, pengine wiki ijayo.”

BBC imesema uhariri wa hotuba ya tarehe 6 Januari 2021 ulipelekea “taswira isiyo sahihi kwamba Rais Trump alitoa wito wa moja kwa moja wa kuchochea vurugu.” Ingawa shirika hilo liliomba msamaha, limesisitiza halitalipa fidia ya kifedha.

Sakata hilo limesababisha kujiuzulu kwa Mkurugenzi Mkuu wa BBC Tim Davie na Mkuu wa Habari Deborah Turness.

Trump aliwaambia waandishi kuwa anaamini hana budi kuwashtaki: “Walidanganya. Walibadilisha maneno yaliyotoka mdomoni mwangu.”

Alisema hakuzungumzia suala hilo na Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer, lakini Starmer ameomba kuzungumza naye, na atampigia simu mwishoni mwa wiki.

Mapema wiki hii, mawakili wa Trump walitishia kuishtaki BBC kwa fidia ya dola bilioni 1 iwapo haitatoa ufafanuzi wa wazi, kuomba msamaha rasmi na kumlipa fidia.

0 Comment

Kupatwa kamili kwa jua kutashuhudiwa leo katika bara la Amerika KaskaziniAfyaclass Bongo Social •

Kupatwa kamili kwa jua kutashuhudiwa leo katika bara la Amerika Kaskazini.

Mwezi utapita mbele ya Jua na kupunguza mwanga wa Jua hadi kutoonekana kwa muda na kuwa giza.

Mamilioni ya watu katika eneo kubwa la Amerika ya Kaskazini watashuhudia kupatwa kwa jua, wakati ambapo mwezi utalifunika kabisa jua kwa zaidi ya dakika nne katika baadhi ya maeneo.

Tukio hilo litashuhudiwa ikiwa hali ya hewa itaruhusu na linatarajiwa kuanzia Mexico, kupitia Marekani hadi Canada. Tukio hili la dakika 4 na sekunde 28 litadumu kwa muda mrefu zaidi ya la mwaka 2017 lililodumu kwa dakika 2 na sekunde 42.

https://www.instagram.com/p/C5f9p2pNV1Y/?igsh=MXNrbHB2eGVodjl1OQ==

Kupatwa kamili kwa jua kutashuhudiwa leo katika bara la Amerika
Kaskazini
0 Comment

Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini MarekaniAfyaclass Bongo Social •

Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani.

Miami, Florida:

Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti tukio la kusikitisha la kifo cha Mtanzania aliyekuwa akifanya kazi Google.

Mwili wa Mtanzania aliyeanguka kutoka kwenye boti iliyokodishwa aliyokuwa amepanda katika Mto Miami nchini Marekani mwishoni mwa juma umepatikana ukielea majini.

Abraham Mgowano, 35, ambaye alifanya kazi kama mhandisi wa programu za Google, alipatikana Jumanne baada ya kupotea tangu aanguke kutoka kwenye boti ya urefu wa futi 44 ya Sea Ray cabin cruiser siku ya Jumamosi.

Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD