Rais wa Marekani Donald Trump amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya BBC kufuatia jinsi hotuba yake ilivyohaririwa

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya BBC kufuatia jinsi hotuba yake ilivyohaririwa

#1

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya BBC kufuatia jinsi hotuba yake ilivyohaririwa na kipindi cha Panorama, baada ya shirika hilo kuomba msamaha lakini kukataa kumlipa fidia.

Akizungumza na waandishi wa habari ndani ya Air Force One Ijumaa jioni, Trump alisema: “Tutawashtaki kwa chochote kati ya dola bilioni 1 hadi 5, pengine wiki ijayo.”

BBC imesema uhariri wa hotuba ya tarehe 6 Januari 2021 ulipelekea “taswira isiyo sahihi kwamba Rais Trump alitoa wito wa moja kwa moja wa kuchochea vurugu.” Ingawa shirika hilo liliomba msamaha, limesisitiza halitalipa fidia ya kifedha.

Sakata hilo limesababisha kujiuzulu kwa Mkurugenzi Mkuu wa BBC Tim Davie na Mkuu wa Habari Deborah Turness.

Trump aliwaambia waandishi kuwa anaamini hana budi kuwashtaki: “Walidanganya. Walibadilisha maneno yaliyotoka mdomoni mwangu.”

Alisema hakuzungumzia suala hilo na Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer, lakini Starmer ameomba kuzungumza naye, na atampigia simu mwishoni mwa wiki.

Mapema wiki hii, mawakili wa Trump walitishia kuishtaki BBC kwa fidia ya dola bilioni 1 iwapo haitatoa ufafanuzi wa wazi, kuomba msamaha rasmi na kumlipa fidia.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code