Afyaclass Bongo Social Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani

Mtanzania mfanyakazi wa Google afa maji nchini Marekani.

Miami, Florida:

Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti tukio la kusikitisha la kifo cha Mtanzania aliyekuwa akifanya kazi Google.

Mwili wa Mtanzania aliyeanguka kutoka kwenye boti iliyokodishwa aliyokuwa amepanda katika Mto Miami nchini Marekani mwishoni mwa juma umepatikana ukielea majini.

Abraham Mgowano, 35, ambaye alifanya kazi kama mhandisi wa programu za Google, alipatikana Jumanne baada ya kupotea tangu aanguke kutoka kwenye boti ya urefu wa futi 44 ya Sea Ray cabin cruiser siku ya Jumamosi.

You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD