Showing posts with label chanzo cha komwe. Show all posts
Showing posts with label chanzo cha komwe. Show all posts

komwe ni nini? na chanzo chake kikubwa ni kipi?Afyaclass Forum •

komwe ni nini? na chanzo chake kikubwa ni kipi?

Huko mtaani kwa sasa ni kitu cha kawaida kusikia Watu wakitaniana kuhusu komwe ‘varanda ya uso’ au kukuta utani na comments kuhusu komwe mitandaoni,

lakini je umewahi kukutanishwa na Mtaalamu akalielezea komwe lenyewe na sababu zinazolisababisha ?

Sababu za kuwa na Komwe

Daktari Bingwa wa ubongo, mgongo, uti wa mgongo na mishipa Doctor Max Gama Ndosi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) anasema zipo sababu nyingi za kitaalamu ambazo zinasababisha Binadamu awe na komwe ambapo kuna sababu za kawaida na kuna nyingine ni kubwa au zinazotokana na magonjwa.

“Sababu za kuwa na komwe ni nyingi lakini kubwa zaidi ni maumbile,

tunatofautiana tulivyoumbwa kwahiyo unakuta wengine ni jinsi tu Familia zao zilivyo wana vichwa vikubwa na wana uwanda mpana wa uso wao kwahiyo wanaonekana kama wanakomwe lakini kuna sababu nyingi za kitaalamu zinazosababisha komwe’ ——— Dr. Gama.

“Moja ya sababu ni kuwa unaweza kuwa na homoni… katika zile ogani ambazo zinatengeneza homoni kwenye mwili wako mojawapo inaweza kutengeneza homoni ya ukuaji ikawa kubwa kuliko kawaida,

hiyo itafanya mifupa yako ikue kwa haraka na pia sehemu nyingine zifunge kwa haraka kwahiyo utakuta hawa Watu wanamifupa mikubwa sana ya uso, viganja vikubwa, pua kubwa, nyayo kubwa… hii ni kutokana na hii homoni ambayo ni kichocheo” – Dr. Gama.

komwe ni nini? na chanzo chake kikubwa ni kipi?
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD