Showing posts with label dawa ya macho mekundu. Show all posts
Showing posts with label dawa ya macho mekundu. Show all posts

Fahamu Aina ya dawa za macho na matumizi YakeAfyaclass Forum •

Fahamu Aina ya dawa za macho pamoja na Matumizi yake

Dawa katika sehemu hii ni pamoja na zile ambazo hufanya kazi kwenye macho, na kawaida hutolewa kama matone ya macho(eye-drops) au mafuta(ointments).

Kuna aina nyingi tofauti – tofauti za dawa ambapo hutumika kwenye matibabu ya maambukizi kwenye macho, kwa mfano;

  • chloramphenicol,
  • fusidic acid,
  • Pamoja na ciprofloxacin.

Shida ya Macho makavu inaweza kutibiwa kwa urahisi kwenye duka la dawa kwa kutumia dawa kama vile hypromellose na carbomer, muulize mfamasia au daktari kwa ushauri Zaidi, au tuwasiliane hapa @afyaclass.

Aina ya dawa za macho

Tuchambue hapa Baadhi ya Aina ya dawa za Macho;

1. Timolol Maleate Ophthalmic Solution

Dawa hii ni Nzuri sana kwa Watu wenye tatizo la Presha ya macho au kwa kitaalam hufahamika kama Ugonjwa wa glaucoma.

Glaucoma husababishwa na shinikizo la damu kuongezeka ndani ya jicho na matibabu kama vile latanoprost na timolol huweza kutumika.

2. Dawa ya Acetazolamide (Diamox)

Acetazolamide ni dawa kwa ajili ya glaucoma Pia.

3. Acetylcysteine(Ilube)

Dawa hii ni kwa ajili ya tatizo la macho kuwa makavu yaani “dry eyes”

4. Aciclovir eye ointment

Dawa hii hutumika kwenye macho kwa ajili ya maambukizi yanayosababishwa na herpes simplex virus.

5.Hypromellose Eye drops

Dawa hii ya macho hutumika kwa mtu mwenye tatizo la macho kuwa makavu au Usumbufu wowote wa macho unaotokana na kupungua kwa mtiririko wa machozi(tear flow),

Pia inaweza kusaidia kuzuia uharibifu wa macho kutokana na baadhi ya magonjwa.

6. Antazoline pamoja na xylometazoline eye drops (Otrivine-Antistin)

Hapa ni mchanganyiko wa dawa mbili Antazoline na Xylometazoline ambapo kwa pamoja tunaita Otrivine-Antistin.

Dawa hii huweza kuwa kama vasoconstrictor ambapo husaidia kupunguza shida ya macho kuwa mekundu(reduces eye redness).

Kumbuka: Usitumie dawa hizi pasipo maelekezo ya kina kutoka kwa Wataalam wa afya. Au kwa ushauri Zaidi, tuwasiliane hapa @afyaclass.

7. Apraclonidine eye drops (Iopidine)

Dawa hii hutumika kusaidia kushusha shinikizo la damu kwenye macho, hivo inafaa kwa mtu mwenye ugonjwa wa presha ya macho(glaucoma).

8. Atropine eye drops (Minims Atropine)

Dawa hii mara nyingi hutumiwa na Wataalam wa macho wakati wanafanya uchunguzi wa macho(eye examination),

Hii ni kutokana na sifa yake ya kuweza kutanua(dilate/enlarge) pupil kwenye jicho na kuifanya Lensi kufa ganzi kwa muda

(It is used to dilate (enlarge) the pupil of the eye and to temporarily paralyse the lens so that your doctor can examine your eye(s)).

9. Azelastine eye drops (Optilast)

Dawa hii ya Azelastine eye drops hutumika kwa mtu mwenye mzio au allergies mbali mbali za macho.

10.Azithromycin eye drops (Azyter)

Dawa hii ya macho huweza kutumika kutibu maambukizi mbali mbali ya bacteria kwenye macho ikiwemo maambukizi ya bacteria kwa Wazee pamoja na watoto toka wanazaliwa mpaka wenye umri wa miaka 17.

Maambukizi mbali mbali ya bacteria ni pamoja na;

  • Purulent bacterial conjunctivitis;
  • trachoma conjunctivitis ( haya ni maambukizi kwenye macho kutokana na bacteria wanaojulikana kama Chlamydia trachomatis)

11. Betamethasone eye drops (Betnesol, Vistamethasone)

Dawa hii ya macho huweza kutumika kutibu hali Zozote zinazosababisha uvimbe wa macho(short-term inflammatory eye conditions).

Kwa sababu dawa hii ina corticosteroid(steroid’) huweza kutumika kupunguza hali ya Uvimbe kwenye macho pamoja na wekundu kwenye macho(It helps relieve inflammation, redness and irritation).

12. Betaxolol eye drops(Betoptic)

Dawa hii ya macho hutumika kwa watu wenye ugonjwa wa Presha ya macho(glaucoma).

Dawa Zingine za Ugonjwa wa Presha ya macho ni pamoja na dawa kama vile;

  • Brimonidine eye drops (Alphagan, Brymont).
  • Brinzolamide eye drops (Azopt)
  • Dorzolamide eye drops(Eydelto, Trusopt, Vizidor)
  • Carteolol eye drops (Ocupress)
  • Pilocarpine eye drops for acute glaucoma (Minims Pilocarpine) n.k

13. Chloramphenicol eye drops (Brolene, Golden Eye)

Dawa hii hutumika kutibu maambukizi mbali mbali ikiwemo ya bacteria kwenye macho

14. Ciprofloxacin eye preparations (Ciloxan)

Hii pia ni dawa ya macho ambayo hutibu baadhi ya maambukizi ya bacteria.

15. Dexamethasone eye drops (Maxidex, Dexafree, Dropodex)

Hii ni dawa ya macho ambayo hutumika kutibu kuvimba kwa macho(Inflammation), kutokana na mzio au allergies mbali mbali pamoja na hali kama vile;

Kuunguzwa na kemikali au joto(chemical and thermal burns).

Hivo kama una hali kama vile za allergies mbali mbali kwenye macho, hii pia ni nzuri.

16.Diclofenac eye drops (Voltarol Ophtha)

Diclofenac eye drops ni dawa ya macho ambayo hutumika kuondoa maumivu pamoja na hali ya kuvimba ambako huweza kutokana na sababu kama vile upasuaji wa jicho/macho,

mfano dawa hii ya Diclofenac eye drops huweza kutumika kuondoa maumivu na hali ya uvimbe baada ya mtu kufanyiwa upasuaji wa kutibu Mtoto wa jicho(cataract surgery).

17. Gentamicin eye drops

Dawa hii ya macho hutumika kutibu maambukizi ya bacteria kwenye jicho pamoja na ngozi kuzunguka macho, maambukizi hayo ya bacteria ni kama vile; blepharitis, conjunctivitis.

Pia hutumika kuzuia maambukizi kwenye jicho au macho baada ya mtu kuumia jichoni/macho au baada ya kufanyiwa Upasuaji wa macho.

18.Loteprednol eye drops (Lotemax)

Hii ni dawa ya macho kwa watu wenye shida ya kuvimba(Inflammation)

19. Moxifloxacin (Moxivig)

Hii ni kwa ajili ya maambukizi mbali mbali machoni.

20. Prednisolone eye drops

Hii ni dawa ya Macho ambayo hutumika kutibu hali mbali mbali za macho ikiwemo kuvimba inflammation  au kuumia,

Pia dawa hii huweza kutumika kuondoa dalili za magonjwa mbali mbali,Ikiwemo dalili kama vile;

  • Macho kuwa Mekundu
  • Kuvimba
  • Kuwasha n.k

Dawa hii ipo kwenye kundi la dawa jamii ya corticosteroids.

Zingitia haya Kabla ya kutumia dawa ya Macho?

– Hakikisha ni Dawa Sahihi kwa ajili ya tatizo lako,

Hivo pata maelekezo ya kina kutoka kwa Wataalam wa afya kwanza kabla ya matumizi

– Angalia muda wa matumizi kwenye dawa yako(Expire date)

– Hakikisha umenawa mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya kushika macho na kutumia dawa

– Hakikisha macho,Uso na mwili kwa ujumla ni Safi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Fahamu Aina ya dawa za macho na matumizi Yake
0 Comment

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyesAfyaclass Forum •

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyes’

Wataalamu wasema zinachangia kuongeza maumivu, waonya zaweza kusababisha uoni hafifu na upofu.

Wataalamu wa afya na madaktari bingwa wa macho wamesema wanapokea idadi kubwa ya wagonjwa wakiwa katika hali ya ugonjwa mkali, kutokana na matumizi ya njia mbadala kutibu macho, ikiwamo matumizi ya mkojo na chumvi.

Hali hiyo imebainika siku 15 tangu kutangazwa kuibuka ugonjwa huo ujulikanao viral keratoconjunctivitis (red eyes) Januari 13, 2024 mkoani Dar es Salaam.

Wataalamu waliozungumza na Mwananchi Digital jana Januari 28, 2024 wameeleza wagonjwa wanaotumia chumvi, mkojo, chai ya rangi na kitunguu saumu kama tiba, macho yao huvimba na kuuma zaidi pamoja na kupatwa homa. Athari hasi zaidi zinazotajwa ni kusababisha vidonda kwenye kioo cha jicho.

Tiba hizo mbadala zinaelezwa zinaweza kusababisha kovu kwenye jicho litakalomfanya mgonjwa apate uoni hafifu au kupoteze uwezo wa kuona kabisa.

Daktari bingwa na mkuu wa kitengo cha macho kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Sarah Mrema ameisema idadi ya wagonjwa wanaohudhuria hospitalini hapo kutibiwa macho imekuwa ikiongezeka na kupungua.

Amesema wamekuwa wakipokea wagonjwa wakiwa tayari walianza kutumia tiba za majani ya chai, vitunguu saumu na chai ya rangi.

“Si kwamba wanapona wakitumia tiba mbadala, maumivu yanazidi, wakija hapa wanakuwa na maumivu makali. Ukihoji anakwambia alitumia mkojo, chumvi na njia nyingine nyingi. Unampa dawa anatumia, kisha anapona,” amesema Dk Sarah.

Kwa mujibu wa Dk Sarah, takwimu za hospitali hiyo zinaonyesha tangu Desemba 22, 2023 wagonjwa 105 walifika kutibiwa na kuna siku orodha ya wagonjwa inapanda na siku nyingine inapungua.

Daktari bingwa wa macho katika Hospitali ya Muhimbili-Upanga, Neema Moshi amesema unapotumia vitu vikali kutibu macho, ni rahisi kuharibu kioo cha mbele cha jicho na maumivu yanayotokea huwa makali.

Amesema wakati mwingine unaweza kupoteza uoni kwa sababu ya kuharibu kioo hicho.

“Tunapokea wagonjwa wengine wana hali mbaya, lakini hawezi kuwa mkweli, unajua mgonjwa hawezi kuja kusema alitumia kitu fulani, mara nyingi wanafichaficha labda tatizo liwe kubwa zaidi ndipo wanasema ukweli,” amesema.

Dk Neema amesema kama mgonjwa ametumia vitu hivyo na hajapata athari hawezi kupata athari baadaye.

“Si kwamba athari hizo zinakuwa za taratibu, kama amepona na haikuonekana kupata shida yoyote haiwezi kutokea tena baadaye,” amesema.

Meneja Mpango wa Taifa wa huduma za macho kutoka Wizara ya Afya, Dk Bernadetha Shilio amesema wapo wagonjwa wanaopata athari, lakini hawana takwimu, akisisitiza ni muhimu wagonjwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu.

“Taarifa hizi zinatolewa na wataalamu wa afya, yaani madaktari kwenye vituo husika, labda mimi kuna mtu amekuja amefanya hivi na vile lakini kutoa hali ilivyo kwa sasa wangapi wamethirika kwa sasa bado.

“Hata leo nimepewa taarifa kuna mtu anatumia sijui vitu gani, lakini pia kuna taarifa za uvumi kuna mtu katoka huko anashauri wagonjwa wanywe Azuma inatibu, huo ni uongo,” amesema.

Dk Shilio amewataka wagonjwa waepuke kutibu macho kwa kutumia kitunguu saumu kwa kuwa kunaweza kusababisha michubuko kwenye ngozi ya jicho na kioo cha mbele ya jicho, hivyo kuathiri uwezo wa jicho kuona.

“Maji ya chumvi yanaweza kusababisha michubuko au kidonda kwenye kioo cha mbele cha jicho, hivyo kutengeneza kovu litakalopunguza uwezo wa jicho kuona au ulemavu wa kutoona wa kudumu,” amesema.

“Matumizi ya chai ya rangi katika kutibu macho yanaweza kusababisha vidonda kwenye kioo cha jicho na kusababisha kovu kwenye jicho litakalokufanya upate uoni hafifu au upoteze uwezo wa kuona kabisa,” amesema.

Dk Shilio amewataka wagonjwa pia kuepuka kutibu macho kwa mkojo, kwani ni hatari kwa usalama wa macho kwa kuwa mkojo hubeba uchafu na vijidudu vinavyoweza kusababisha maambukizi mengine na kupoteza uwezo wa kuona kabisa.

Amewataka kuzingatia kunawa mikono mara kwa mara na wapatapo ugonjwa huo kuwahi kituo cha afya kwa uchunguzi na matibabu sahihi na kwa wakati.

Via Mwananchi.

Soma Zaidi hapa Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa macho mekundu(Red Eyes)

Mkojo,Chumvi, kitunguu saumu sio dawa ya kutibu ‘red eyes
0 Comment

Dawa ya red eyes,Ifahamu dawa ya macho mekundu hapaAfyaclass Forum •

Dawa ya red eyes,Ifahamu dawa ya macho mekundu hapa

Je unahitaji kutumia Dawa ya red eyes? na kama ni hivo ni ipi Dawa ya red eyes?

Ingawa ugonjwa wa red eyes huiisha au kuondoka wenyewe, kuna wakati unahitaji matibabu maalumu kutoka kwa wataalam wa afya ikiwa umekusababishia madhara Zaidi.

Hakikisha unaongea na wataalam wa afya Ili kupata Dawa ya red eyes haraka Zaidi ikiwa unapata hali hizi hapa;

– Unahisi maumivu makali sana kwenye Macho

– Uwezo wako wa kuona umeathiriwa na ugonjwa wa Red Eyes

– Macho yako yanaogopa mwanga

– Macho yanazidi kuwa mekundu siku hadi siku badala ya kupungua wekundu

– Unapatwa na Homa

– Macho kutoa Usaha badala ya tongotongo n.k

Dawa ya red eyes

Hizi hapa ni jamii ya Dawa ambazo huweza kutumika kutibu Ugonjwa wa Red Eyes Duniani, si dawa Zote utazipata hapa Tanzania,

Hivo ni muhimu kuwasaliana kwanza na wataalam wa afya au tuwasiliane hapa afyaclass ili kupata Dawa ya red eyes sahihi na inayopatikana hapa kwetu Tanzania.

Kumbuka; Matibabu ya ugonjwa wa red eyes huhusika na chanzo husika.

Dawa ya red eyes ni pamoja na;

✓ Naphazoline, ambayo hupatikana kwenye dawa jamii ya Clear Eyes Itchy Eye Relief.

Naphazoline ni dawa jamii ya decongestant ambayo hutibu macho mekundu(red eyes) ikiwa chanzo chake ni mzio au allergic reactions.

✓ Tetrahydrozoline, ambayo hupatikana mfumo wa matone kama vile Visine. Tetrahydrozoline ni dawa jamii ya decongestant kama vile naphazoline,

Hivo huondoa wekundu kwenye macho ambao hutokana na Mzio(allergy, exhaustion, and irritation).

✓ Eye lubricant drops. Pia zipo dawa za macho ambazo kazi yake kubwa ni kuwa kama vilainishi machoni, hizi pia huweza kutumika kama Dawa ya red eyes.

✓ Dawa ya red eyes, Haya ni matibabu mengine ya Ugonjwa wa red eyes;

Ikiwa umepata shida ya red eyes kwa sababu kama hizi allergies, conjunctivitis, au blepharitis, unaweza kufanya matibabu haya rahisi kwako;

SOMA ZAIDI HAPA: Kuhusu Dawa Za Ugonjwa wa macho

(1) Kutumia vitu vya baridi(Apply a cool compress). kuweka kitu cha baridi juu ya macho ukiwa umefunika macho yako huweza kusaidia kupunguza dalili za wekundu na kuvimba kwa macho.

(2) Tumia baadhi ya dawa(Take over-the-counter (OTC) medications).

Kama nilivyokwisha kueleza,dawa jamii ya antihistamines au decongestants huweza kutumika kama dawa ya Red eyes, ambapo husaidia kupunguza na kuondoa  dalili za wekundu wa macho.

Pia dawa kama vile ibuprofen pamoja na acetaminophen huweza kutumika kupunguza maumivu na Uvimbe.

(3) Epuka vitu vyote vinavyoweza kuingia machoni(Avoid irritants).

Hapa tunazungumzia vitu kama vile Vumbi, Moshi, pollens, chemical fumes n.k.

(4) Hakikisha unanawa mikono(Wash your hands).

Hakikisha unanawa mikono yako mara kwa mara kwa kutumia maji safi tiririka na Sabuni.

Epuka kabsa kugusa macho yako au eneo la karibu na macho yako hasa ukiwa hujanawa mikono yako.

(5) Epuka makeup au kuvaa miwani.

Epuka kutumia makeup au kuvaa miwani kam ikiwezekana mpaka dalili za ugonjwa wa red eyes ziondoke.

(6) Epuka kutazama vitu kama Simu,TV, au computer kwa muda mrefu.

Kutumia muda mwingi mbele ya kompyuta, TV au skrini ya simu kunaweza kusababisha macho kuwa na mkazo zaidi(eyestrain) na kuwa makavu, kwa hivyo jaribu kupunguza muda wako wa kutumia kifaa kama hivi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Ugonjwa wa Macho Mekundu(RED EYES),chanzo,dalili na Matibabu

Dawa ya red eyes,Ifahamu dawa ya macho mekundu hapa
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD