Showing posts with label njia za uzazi wa mpango. Show all posts
Showing posts with label njia za uzazi wa mpango. Show all posts

Vidonge sio njia nzuri ya kuzuia mimba kwa Muda mrefuAfyaclass Forum •

Hata Kama Vinazuia Mimba,Vidonge sio njia nzuri ya kuzuia mimba kwa Muda mrefu.

Mfano;Ikiwa unataka kuzuia mimba kwa muda wa miaka 2 au 3, kama unatumia vidonge vya uzazi wa mpango,itakulazimu umeze kila siku kidonge1 kwa Muda wa miaka 3.

Kumbuka,tafiti mbali mbali zinaonyesha matumizi ya Muda Mrefu sana na njia hii huweza kuongeza hatari ya Mtu kupata Saratani ikiwemo Saratani ya Mlango wa kizazi(Cervical cancer).

Unashauriwa hata kama Unatumia vidonge vya Uzazi wa Mpango basi isiwe ndyo njia yako ya Muda mrefu kwa ajili ya kupanga Uzazi,

Usitumie njia hii ya vidonge kwa muda mrefu zaidi Mfano kwa Miaka 3, Miaka 5 n.k

Kadiri mwanamke anavyotumia vidonge vya kupanga Uzazi(Oral contraceptive piils) kwa muda mrefu, ndivyo hatari ya kupata saratani ya Mlango wa kizazi inavyoongezeka. 

Utafiti mmoja uligundua hatari ya Mwanamke kupata Saratani ya Mlango wa Kizazi(Cervical Cancer) iliyoongezeka kwa asilimia 10% kwa wanawake waliotumia Vidonge kwa muda wa chini ya miaka 5,

Lakini hatari iliyoongezeka zaidi kwa asilimia 60% kwa wanawake waliotumia Vidonge kwa Muda wa miaka 5 mpaka 9, 

na kuongezeka maradufu kwa hatari dhidi ya wanawake waliotumia Vidonge vya Uzazi kwa Muda wa miaka 10 au zaidi.

Mwanamke aliyetumia Vidonge vya Kupanga Uzazi kwa Muda wa Miaka 5  au Zaidi,yupo kwenye hatari zaidi ya Kupata Saratani ya Mlango wa Kizazi(Cervical cancer) kuliko Mwanamke ambaye hajawahi kabsa kutumia Vidonge.

Ingawa pia,hatari ya saratani ya Mlango wa kizazi imeonekana kupungua baada ya muda kwa wanawake ambao waliacha kutumia vidonge vya Uzazi wa mpango kwa muda wa miaka 10 mpaka 12.

0 Comment

Hii ni mikoa 10 inayoongoza kwa uzazi wa mpango TanzaniaAfyaclass Forum •

Hii ni mikoa 10 inayoongoza kwa uzazi wa mpango Tanzania

Miongoni mwa masuala yanayogusa zaidi vijana wengi waliopo kwenye ndoa na wasio kwenye ndoa kwa sasa ni suala la kuwa na watoto.

Miongoni mwa maswali makubwa huwa ni lini wapate watoto, idadi ya watoto lakini ni njia gani sahihi itakayomfanya wanawake vijana wasipate ujauzito bila kutarajia. Wataalamu wanasisitiza kuwa ni vema wazazi vijana wakapanga mipango yao vema ya kijamii na kiuchumi kabla ya kupata watoto.

Hata hivyo, si watu wote wanapanga ipasavyo juu ya kupata watoto. Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa mwaka 2022 unabainisha kuwa nchini Tanzania takriban wanawake wanne kati ya 10 au asilimia 38 ya waliolewa wenye umri wa miaka 15 hadi 49 wanatumia njia ya aina yeyote ya uzazi wa mpango.

Ripoti ya utafiti huo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa ushirikiano na taasisi nyingine iwepo Wizara ya Afya inabainisha ipo baadhi ya mikoa yenye kiwango kikubwa cha wanawake wenye wanaotumia ipasavyo njia za uzazi wa mpango ikiongozwa na Njombe huku mingine ikitumia kwa kiwango kidogo sana kama Simiyu.

Je, waifahamu mikoa inayoongoza kwa matumizi ya njia za uzazi wa mpango Tanzania?

Rejea Source Links;

Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa mwaka 2022

Ripoti ya utafiti huo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

Wizara ya Afya

• Nukta Page

>>Soma pia kuhusu Njia Mpya ya Uzazi wa mpango inayojulikana kama SAYANA PRESS

Hii ni mikoa 10 inayoongoza kwa uzazi wa mpango Tanzania
0 Comment

jinsi ya kuzuia mimba siku za hatariAfyaclass Forum •

jinsi ya kuzuia mimba siku za hatari

Kuna njia kadhaa za kuzuia mimba siku za hatari, ikiwa ni pamoja na kutumia kondomu, vidonge vya uzazi, kalenda ya hedhi, na njia nyingine za uzazi wa mpango.

Ni muhimu kuzungumza na mtaalamu wa afya ili kupata ushauri unaofaa na kuchagua njia inayofaa kwa mahitaji yako na mwenza wako.

Njia nzuri ya jinsi ya kuzuia mimba siku za hatari ni ile ambayo hutumika kwa muda mrefu na huhusisha mzunguko mzima wa hedhi, kwa kitaalam tunaita long-acting form of contraception.

Njia ya kuzuia mimba ambayo unaitumia Siku za hatari pekee inaweza isiwe njia bora inayofanya kazi kwa asilimia 100%,

Kwani Mzunguko wako wa hedhi unaweza kubadilika muda wowote, kitu ambacho kitakuweka kwenye hatari Zaidi ya kupata Mimba, Ikiwa unazuia mimba kwa kuangalia Siku za hatari pekee.

Njia za Uzazi wa mpango zimegawanyika kwenye Makundi mbali mbali yakiwemo;

(1) Njia za kiasili(traditional methods)

Mfano; matumizi ya kalenda, Withdrawal method n.k

(2) Njia za kisasa(modern methods)

Mfano: Kitanzi, Vipandikizi, Sindano,Vidonge n.k

Pia tunaweza kuzigawanya kwenye makundi Zaidi kama vile;

  • Njia za muda mfupi
  • Njia za Muda Mrefu
  • Njia za kudumu

Soma Zaidi hapa Njia hizi za Uzazi wa mpango

jinsi ya kuzuia mimba siku za hatari

Zipo njia mbali mbali za Kuzuia Mimba ambazo unaweza kuzitumia ikiwemo;

1. Matumizi ya kitanzi au Lupu(IUD)

Soma Zaidi hapa kuhusu njia hii ya kutumia kitanzi(Intrauterine device)

#PICHA: Huu ndyo mfano wa kitanzi katika picha hii hapa chini;

2. Matumizi ya Kipandikizi au Kijiti

Njia jii huweza kuzuia mimba Siku za hatari na muda wake wa kuzuia mimba ni miaka 3 mpaka 5

  • Kuna kijiti cha miaka 3
  • Kuna vijiti vya miaka 5

Soma Zaidi hapa kuhusu njia ya vijiti au implants

3. Matumizi ya Sindano

Njia nyingine ya Kuzuia Mimba siku za hatari ni Sindano, Soma hapa faida na hasara za kutumia Sindano kama njia ya Uzazi wa mpango.

4. Njia nyingine za Kuzuia mimba Siku za hatari ni pamoja na;

Njia hizi za kuzuia mimba siku za hatari, kama vile kondomu, pia ni chaguo. Ingawa njia hizi hazina ufanisi zaidi kuliko hizo za juu. Bila shaka, utahitaji kutumia hizi kabla ya kujamiiana ikiwa hakuna namna.

Kumbuka: Ni muhimu sana kupata Maelekezo kwa kina kutoka kwa Wataalam wa afya Juu ya njia Sahihi ya kutumia ili kuzuia Mimba kulingana na mwili wako,

Hii itakusaidia kuzuia madhara ambayo huweza kujitokeza baada ya kuamua kutumia njia flani ya Uzazi wa mpango, au;

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

jinsi ya kuzuia mimba siku za hatari
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD