Afyaclass Mama ajifungua watoto watano kwa wakati mmoja

Mama ajifungua watoto watano kwa wakati mmoja

Mwanamke mmoja amebarikiwa na watoto watano warembo ambao alijifungua kwa wakati mmoja na ameshiriki ushuhuda wake kwenye mitandao ya kijamii.

Katika video ya kufurahisha iliyoshirikiwa kwenye TikTok, mwanamke huyo aliyejitambulisha kama @ebyfullmoon alifichua kuwa aliwakaribisha wasichana wawili warembo na wavulana watatu.

Alionekana hospitalini alipokuwa akitembeatembea tayari kukaribisha malaika wake wachanga.

Tumbo lake lililochomoza lilivutia watu mtandaoni, ambao walimsifu kwa kuweza kulibeba kwa miezi tisa.

Alisema: “Nina shukrani na taadhima kuu moyoni mwangu kwako wewe Mungu wangu. Matokeo yalikuwa watoto watano, wavulana watatu na wasichana wawili warembo.”

You, Mehreen and others
Hashtag:

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD