Bibi arusi aliye na Saratani afariki wiki kadhaa baada ya kufunga Harusi ya ndoto yake

#1

Bibi arusi aliye na Saratani afariki wiki kadhaa baada ya kufunga Harusi ya ndoto yake.

“Kwa kweli alikuwa mwanga chanya unaoangaza”

Katelen Green na mumewe Billy walifunga ndoa yao kwa “muujiza” mnamo Novemba – baada ya ukumbi wao na wasambazaji zaidi ya 30 kuchangia kila kitu bila malipo.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 24, kutoka Shropshire nchini Uingereza, alikuwa na hatua ya nne ya Hodgkin lymphoma- saratani isiyo ya kawaida ambayo hujitokeza katika mfumo wa lymphatic.

Saratani ilirejea kwa mara ya tatu mwaka jana na madaktari walikuwa wamemwambia hakuna kitu zaidi wangeweza kufanya.

Katelen alitarajia kuchangisha pesa kwa ajili ya majaribio ya kimatibabu ili aweze kuwa na muda zaidi na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka mitatu, lakini alifariki wiki iliyopita.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code