TATIZO LA BANDAMA KUVIMBA AU KUJAA MAJI,CHANZO,DALILI NA TIBAAfyaclass Bongo Social •

 TATIZO LA BANDAMA KUVIMBA AU KUJAA MAJI,CHANZO,DALILI NA TIBA

Watu wengi kwa hivi sasa hupatwa na tatizo hili la bandama kuvimba huku wengine wakiambiwa bandama zimejaa maji baada ya kufanyiwa vipimo mbali mbali, tatizo la bandama kuvimba kwa kitaalam hujulikana kama Splenomegaly, je chanzo cha matatizo ya bandama kuvimba au kujaa maji ni nini?

CHANZO CHA TATIZO LA BANDAMA KUVIMBA NI PAMOJA NA;

- Maambukizi mbali mbali ya vimelea vya magonjwa kama vile;

1. Maambukizi ya bacteria mfano bacteria wanaosababisha ugonjwa wa kaswende au syphilis,maambukizi ya bacteria kwenye kuta za ndani ya moyo na kusababisha matatizo kama endocarditis n.k

2. Maambukizi ya virusi kama vile mononucleosis n.k

3. Maambukizi ya Parasites kama vile kwenye ugonjwa wa Malaria

4. Magonjwa ya ini kama Cirrhosis pamoja na magonjwa mengine yanayoshambulia Ini

5. Aina mbali mbali za anemia(upungufu wa damu mwilini), hasa anemia inayohusu uvunjaji wa seli nyekundu za damu yaani RED BLOOD CELLS(RBCs) kwenye hatua ya mwanzo kabsa kabla ya kukomaa

6. Uwepo wa tatizo la kansa kwenye damu kama vile: shida ya Leukemia,Lmyphomas,myeloproliferative neoplasms n.k

7. Magonjwa au matatizo mbali mbali kwenye mfumo wa uvunjaji chakula kwenye seli yaani metabolic disorders kama vile tatizo la Gaucher,Niemann n.k

8. Tatizo la presha kwenye mishipa ya Veins ndani ya Bandama au Ini au mtu kupatwa na shida ya damu kuganda au kutengeneza clots kwenye mishipa hii ya veins

9. Magonjwa kwenye mfumo wa kinga ya mwili yaani autoimmune conditions kama vile shida ya Lupus,Sarcoidosis n.k

DALILI ZA MTU MWENYE MATATIZO HAYA YA BANDAMA NI PAMOJA NA;

- Mtu kupata maumivu makali upande wa kushoto karibu na mbavu

- Mtu kuhisi uzito kwenye eneo la karibu na mbavu kushoto juu kidogo ya kitovu

- Hali ya mtu kuhisi kushiba hata kama umekula kidogo sana au hujala kitu,hii ni kwasababu bandama hugandamiza tumbo la chakula hivo kufanya chakula kiingie kidogo sana au mtu kuhisi kushiba muda wote

- Mtu kuanza kuonyesha dalili mbali mbali za upungufu wa damu yaani anemia kwenye mwili wake

- Mtu kupata shida ya kuvuja damu kwa urahisi zaidi,kushambuliwa na magonjwa mbali mbali mara kwa mara n.k

VIPIMO MBALI MBALI KUFANYIKA KAMA VILE

• Vipimo vya kuchukua Sample ya damu yaani blood tests

• Kufanya physical examination

• Kufanya ultrasound,Ct Scan au MRI n.k

MATIBABU YA TATIZO HILI LA BANDAMA

Tiba ya matatizo ya bandama kama vile bandama kuvimba au bandama kujaa maji hutegemea na chanzo chake,hivo kama chanzo ni maambukizi ya bacteria basi mgonjwa atapewa antibiotics mbali mbali kutibu shida hii n.k

Kama matibabu ya dawa yameshindikana huduma ya upasuaji huweza kufanyika kwa mgonjwa

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO HILI TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

Sababu za mwanaume kukosa hamu ya TENDO LA NDOAAfyaclass Bongo Social •

Sababu ya mwanaume kukosa hamu ya tendo la ndoa

Leo tutatazama tatizo lingine linalohusiana na ufanisi wa tendo la ndoa kwa Wanaume. Kwa kuwa neno upungufu wa nguvu za kiume limekwishazoeleka mapema kutumika na watanzania walio wengi,niseme tunatazama aina nyingine ya tatizo lenye uhusiano wa karibu sana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tafiti zinaonesha kuwa wanaume wengi hawapendi kuishi na tatizo la kukosa hamu au hisia ya kufanya tendo la ndoa,wakati hadi 46% ya Wanawake huonesha kuridhika kuishi na tatizo hili.

Katika mada hii tutatazama nini husababisha MWANAMUME kukosa hamu au hisia ya kufanya tendo la ndoa. Ingawa wakati mwingine huweza kuwa kawaida kupoteza hisia ya tendo la ndoa kwa vipindi tofauti tofauti.

Hisia ya kufanya tendo la ndoa hupungua pia kwa kadri umri unavyoongezeka japo siyo hivyo kwa wote,maana kuna Wanaume wengi hufikia uzeeni huku wakiwa na uwezo na hamu ya kushirikiana na wenzi wao kimapenzi.

Kupungua kwa hisia au hamu ya kufanya tendo la ndoa ni tatizo kubwa kwa jamii kwa sasa,takribani mwanamume 1 kati ya 5 huwa na tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Mara nyingi limekuwa likisababishwa na matatizo ya kisaikolojia na kimaisha pia. Fuatana nami sasa ndugu mpendwa tunapoangalia sababu hizi na inawezekana ukapata msaada kupitia mada hii ikiwa una tatizo hili.

CHANZO CHA MWANAMUME KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA NI NINI?

1. Upungufu wa homoni ya Testesterone-

Hii Ni homoni ya kiume ambayo huimarisha misuli,huboresha uzito wa mifupa na huchochea utengenezwaji wa mbegu za kiume (sperms). Pia homoni hii huongeza hamu ya tendo la ndoa. Kupungua kwa homoni hii inayozalishwa na korodani,husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa na uzalishaji wa mbegu za kiume huwa kwa kiwango kidogo.

2. Matumizi ya baadhi ya Dawa

Kutumia baadhi ya dawa huweza kupunguza uwezo wako wa kushiriki tendo la ndoa na Mke wako. Matumizi ya dawa kama za high blood pressure kama vile ACE na BLOCKER huweza kusababisha uwezo wa kufanya mapenzi kupungua na hamu ya tendo la ndoa kupotea kabisa.

3. Mfadhaiko

Mfadhaiko huathiri utendaji kazi wa mwili wako wote. Mfadhaiko na msongo wa mawazo humfanya mtu apoteze kuvutiwa na kazi alizozoea kuzifanya hapo kabla ikiwa ni pamoja na tendo la ndoa. Imethibitika kuwa dawa za kupunguza mfadhaiko pia hupunguza hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mtumiaji.

4. Magonjwa ya muda mrefu

Kama unajisikia vibaya kutokana na ugonjwa wa muda mrefu,kufanya tendo la ndoa haitakuwa hitaji lako la kwanza. Magonjwa kama Saratani n.k huweza kupunguza kiwango cha mbegu zako pamoja na hamu ya tendo la ndoa kupungua.

5. Kukosa usingizi

Imebainika kuwa tatizo la kukosa usingizi husababisha kupungua kwa kiwango cha homoni ya testesterone. Kupungua kwa homoni ya testesterone husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya mapenzi pia.

6. Msongo wa mawazo

kwa mtu mwenye msongo uwezo wake wa kufanya tendo la ndoa hupungua. Hii ni kwa sababu msongo husababisha hitilafu kwenye mfumo wa homoni. Na hii huweza kupelekea mishipa ya ATERI kubana na kuzuia damu kufikia sehemu muhimu zinazohusika na ufanyaji wa tendo la ndoa.

7. Kutojiamini

Haitawezekana kufanya tendo la ndoa vizuri kama wewe mwenyewe hujiamini. Kutojiamini hupelekea wasiwasi ambayo husababisha mvurugiko wa homoni zinazohusika kuongeza hamu na ufanyaji wa tendo la ndoa.

8. Pombe na dawa za kulevya

Matumizi ya pombe husababisha kupungua kwa uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Matumizi ya dawa za kulevya kama marijuana huharibu utendaji kazi wa tezi ya PITUITARIES inayoratibu utengenezwaji wa homoni ya TESTOSTERONE.

9. Uume kushindwa kusimama

Kukosa hamu ya tendo la ndoa huweza kuwa matokeo ya Uume kushindwa kusimama. Kama ulipatwa na tatizo la Uume kushindwa kusimama husababisha wasiwasi na kutojiamini. Hii ni kwa sababu ya kufikiri kwamba huenda ikatokea tena. Hata hivyo uume kushindwa kusimama ni dalili ya uwepo wa matatizo mengine ya kiafya kama vile magonjwa ya moyo.n.k.

10. Unene uliopitiliza-Na kitambii

Unene husababisha kupungua kwa homoni ya testesterone na kusababisha hamu ya tendo la ndoa kupungua. Pia unene huweza kusababisha magonjwa ya moyo na high blood pressure,ambayo kwa pamoja husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa.

11. Mahusiano baina ya Wanandoa

Kama kuna magomvi,matukano na kupigana kati ya Wanandoa hamu ya kushiriki pamoja tendo la ndoa pia hupungua kama sio kutoweka kabisa.

12. Umri mkubwa

Utengenezwaji wa homoni ya testesterone inayohusika na kuongeza hamu ya tendo la ndoa hupungua kwa kadri umri unavyoongezeka. Wanaume mara nyingi huanza kuhisi tatizo hili kuanzia miaka 60 hadi 65. Kupungua kwa homoni hii husababisha kupoteza hisia za tendo la ndoa na kuchelewa kufika kileleni

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

kuwashwa ukeni kabla ya hedhi,chanzo chake na TibaAfyaclass Bongo Social •

Kuwashwa ukeni kabla ya hedhi au Period,chanzo chake na Tiba

Mwanamke anaweza kupatwa na tatizo hili la kuwashwa Ukeni kabla ya hedhi kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo;

  • Mabadiliko ya vichocheo ambayo hutokea kipindi hiki,
  • maambukizi ya magonjwa n.k

Katika Makala hii tutachambua Zaidi kuhusu kuwashwa ukeni kabla ya hedhi,chanzo chake na Tiba yake.

CHANZO CHA KUWASHWA UKENI KABLA YA HEDHI

Zipo sababu mbali mbali zinazopelekea tatizo la Mwanamke kuwashwa ukeni kabla ya hedhi, na Sababu hizo ni Pamoja na;

- Tatizo la ukavu ukeni yaani Vaginal dryness

Kiwango cha Vichocheo aina ya Estrogen huongezeka sana kipindi cha ovulation,kisha hushuka kwa haraka sana kwenye siku karibia na Hedhi,

Hii huweza kusababisha ukavu ukeni Hali hii ya Vaginal dryness huweza kusababisha uke kuwa na maumivu na kuwashwa hasa wakati wa kufanya mapenzi au kuwashwa ukeni kabla ya hedhi.

Pia hali hii ya ukavu ukeni huweza kutokea kwa Mwanamke anayekaribia ukomo wa hedhi(menopause), na kwa baadhi ya wanawake ambao wametoka kujifungua muda mfupi, au ambao wananyonyesha.

- Kuvimba yaani inflammation

Kuna ushahidi unaonyesha kuwa hedhi huongeza unyeti wa ngozi(skin sensitivity),

Utafiti wa mwaka wa 1991 uligundua kuwa wanawake katika siku ya kwanza ya mzunguko wao wa hedhi walikuwa na uwezekano mkubwa wa kupata mwasho wa ngozi kuliko ilivyokuwa siku za baadaye katika mzunguko wao,

Na hii ilitokana na kuvimba kwenye ngozi,hali ambayo hupelekea pia  kuwashwa ukeni kabla ya hedhi.

- Period products, hapa tunazungumzia vitu ambavyo unavyovitumia ukiwa karibu na hedhi au ukiwa kwenye hedhi kama vile nguo za ndani, pedi au taulo za kike n.k

Vitu hivi pia huweza kuchangia uwepo wa tatizo la kuwashwa ukeni kabla ya hedhi.

Matumizi ya baadhi ya Visodo(Tampons) huweza kufyoza vilainishi asilia ukeni(natural vaginal lubrication) na kusababisha hali ya Ukavu ukeni kisha kuongeza hatari ya kupata tatizo la kuwashwa ukeni kabla ya hedhi,

Hivo hivo kwa baadhi ya nguo za ndani,matumizi ya baadhi ya sabuni n.k huweza kusababisha hali hii ya kuwashwa ukeni kabla ya hedhi,

na wakati mwingine kuleta allergic reaction ya ngozi kwa baadhi ya Wanawake,kisha kupelekea miwasho ukeni.

- Maambukizi ya magonjwa kama vile Fangasi sehemu za Siri(Yeast infection),

Hii pia huweza kupelekea Mwanamke kupata tatizo la kuwashwa ukeni kabla ya hedhi.

- Tatizo la Cyclic vulvovaginitis, ambalo huhusisha maambukizi ya muda mrefu ambayo hutokea tena kabla au wakati wa kipindi cha Hedhi.

Mwanamke mwenye tatizo la Cyclic vulvovaginitis huweza kupatwa na dalili kama hizi;

  • Kuhisi hali ya kuungua ukeni,kuuma,
  • kupatwa na miwasho ukeni au kuhisi hali ya kuchomwa chomwa kabla ya kuanza hedhi
  • Au kuwashwa ukeni kabla ya hedhi

- Tatizo la Bacterial Vaginosis, ambapo huhusisha maambukizi ya bacteria Ukeni,

Haya ni maambukizi ambayo hutokea sana kwa Wanawake wenye umri kuanzia miaka 15-44,

Wanawake wenye tatizo hili hupatwa na hali ya kutoa harufu kama shombo la samaki ukeni(strong fishy odor), hasa baada ya kufanya mapenzi,

Lakini pia huweza kupata dalili zingine kama vile;

  • kutokwa na uchafu mwembamba wenye rangi nyeupe au Kijivu,
  • kupata maumivu wakati wa tendo,
  • kuhisi hali ya kuungua
  • pamoja na kuwashwa ukeni.

- Magonjwa ya Zinaa(Sexually transmitted infections) kama vile kisonono(gonorrhea) huweza kusababisha pia hali hii ya kuwashwa ukeni,pamoja na kutokwa na uchafu wenye harufu.

Maambukizi haya huwa hayazidi kuwa mabaya kabla au wakati wa kipindi cha hedhi. Walakini, watu wengine wanaweza kugundua dalili kwa mara ya kwanza kabla ya kipindi cha hedhi kuanza.

MATIBABU YA TATIZO HILI La kuwashwa ukeni kabla ya hedhi

Kama nilivyokwisha kueleza baadhi ya Sababu za tatizo hili la kuwashwa Ukeni kabla ya hedhi, hata Matibabu yake yatategemea chanzo husika cha tatizo hili, hivo hakuna Tiba moja maalumu(specific treatment) kwa tatizo hili.

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je, kuwashwa ukeni kabla ya hedhi husababishwa na nini?

Zipo sababu mbali mbali zinazopelekea tatizo la Mwanamke kuwashwa ukeni kabla ya hedhi, na Sababu hizo ni Pamoja na;

Tatizo la ukavu ukeni yaani Vaginal dryness,Kuvimba yaani inflammation,Maambukizi ya magonjwa kama vile Fangasi sehemu za Siri(Yeast infection) n.k

Hitimisho

Tatizo la kuwashwa ukeni kabla ya hedhi ni tatizo ambalo huweza kumpata mwanamke yoyote,

Na Zipo sababu mbali mbali zinazopelekea tatizo la Mwanamke kuwashwa ukeni kabla ya hedhi, na Sababu hizo ni Pamoja na;

Tatizo la ukavu ukeni yaani Vaginal dryness,Kuvimba yaani inflammation,Maambukizi ya magonjwa kama vile Fangasi sehemu za Siri(Yeast infection) n.k

Kama una tatizo hili la kuwashwa ukeni kabla ya hedhi,hakikisha unaongea na wataalam wa afya ili kupata Msaada Zaidi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

JINSI YA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME(JINSI YA KUONGEZA MANII)Afyaclass Bongo Social •

 JINSI YA KUONGEZA MBEGU ZA KIUME(JINSI YA KUONGEZA MANII)


Hizi hapa ni baadhi ya tips za kuwasaidia wanaume wenye tatizo la Mbegu chache au kwa kitaalam hujulikana kama Low sperm count. Tips hizi zitakusaidia kuongeza mbegu za kiume au manii


1. Kupunguza uzito wa mwili, Watu wengi hawajui kwamba, kama una tatizo la uzito kuwa mkubwa(overweight/obesity) huweza kuathiri mpaka mfumo wako wa uzazi,


Baadhi ya tafiti zinaonyesha mtu mwenye shida ya uzito mkubwa akipunguza uzito wake husaidia sana kuboresha afya ya mbegu za kiume(overall sperm health) ikiwemo kuongeza Semen Volume,concentration pamoja na mobility,


Hivo hakikisha unapunguza uzito wako wa mwili kama una shida hii ya uzito mkubwa(Overweight).


2. Fanya mazoezi mbali mbali ya mwili, mbali na faida lukuki za mazoezi ikiwemo kuimarisha mzunguko wa damu mwilini, pia mazoezi husaidia sana kwenye afya ya uzazi ikiwemo swala la mbegu za kiume,


Hivo hakikisha unafanya mazoezi ya mwili angalau kwa dakika 30 au nusu saa kila siku kwa ajili ya afya ya mwili pamoja na afya ya uzazi.


3. Hakikisha unapata Vitamins D,C,E Pamoja na madini ya Calcium vyote hivi ni muhimu kwenye afya ya uzazi,


Baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba kwa mwanaume ambaye anapata 1,000mg za Vitamin C kila siku husaidia sana kuongeza sperm concentration pamoja na mobility hivo huongeza uwezo wa mwanaume kutungisha mimba,


Na utafiti huo unazidi kuonyesha kwamba, wanaume ambao hupata kiwango kidogo cha Vitamin D wanakuwa na uwezo mdogo sana wa kutungisha mimba.


4. Epuka matumizi ya Pombe kupita kiasi, Miongoni mwa vitu ambavyo huchangia uwepo wa tatizo la mbegu chache kwa wanaume au Low sperm count ni pamoja na matumizi ya Pombe kupita kiasi


5. Epuka uvutaji wa sigara ikiwemo tumbaku,ugoro, au vilevyi vingine kama vile Coccaine n.k


6. Jikinge ukiwa kwenye mazingira ya kemikali, heavy metals,solvents,Au dawa za kuua wadudu(pesticides) kwani vyote hivi huweza kuathiri sperms.


7. Vaa nguo za ndani ambazo hazibani sana na zenye material ya pamba(cotton boxers) ili kuruhusu hewa kupita na kuepuka joto zaidi,


Kumbuka moja ya vitu muhimu kwenye utengenezaji wa mbegu za kiume ni pamoja na joto(temperature),


Hivo uwepo wa korodani nje ni mahususi kabsa ili kuwa na joto kiasi(moderared temperature) ambalo litasaidia katika utengenezaji wa mbegu za kiume.


8. Pata muda wa kutosha wa kupumzika na kulala, hakikisha unaondoa Stress au msongo wa mawazo,maana vyote hivi huweza kuathiri mpaka uzalishwaji wa Mbegu za kiume


9. Epuka matumizi ya dawa hovio,Tumia dawa hizi kwa uangalifu na maelekezo ya kina kutoka kwa wataalam wa afya;


- Baadhi ya antibiotics,Anti-Inflammatories,Antipyschotics,Antidepressants,Anabolic steroids,methadone n.k


10. Epuka matumizi ya madawa kama Vumbi la Congo n.k na tumia dawa kama Viagra kwa maelekezo maalumu kutoka kwa wataalam wa afya.


Pia tafiti zinaonyesha Dawa za asili ambazo hujulikana kama ashwagandha au Indian Ginsey,zimekuwa zikitumika kwa muda mrefu na kusaidia sana wanaume wengi wenye shida hii. Japo faida na hasara za matumizi yake huhitaji utafiti zaidi(Research).


11. Hakikisha unakula vyakula ambazo vitakupa health fat kama vile;Polyunsaturated fats ambayo ni muhimu sana kwa afya ya mbegu za kiume hasa kwenye utengenezaji wa sperm membrane,


aina hii ya Fats ina omega-3 and omega-6.


Epuka matumizi ya chakula ambayo yatakupa unhealthful fat,


Utafiti huu ambao ulifanyika Mwaka 2014 Nchini Spanish kwa wanaume 209 wenye umri wa miaka 18–23 ulionyesha kwamba,

Wanaume hao walikuwa wanatumia kiwango kikubwa cha trans fatty acids na wakati huo huo tatizo la Low sperm count lilionekana kwao.


12. Hakikisha unapata madini ya ZINC pamoja na FOLATE, Bila shaka umekuwa ukisikia sana habari za Zinc kwenye swala la mbegu za kiume, yeah ni kweli Zinc ni muhimu sana kwenye mbegu za kiume ikiwemo faida ya kuongezea mwendo mbegu za kiume yaani mobility.


Baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba ukipata Zinc pamoja na Folate kwa kiwango kinachotakiwa mwilini hata afya ya mbegu za kiume(Overall sperm health) ikiwemo concentration pamoja na Count huongezeka sana.


KUMBUKA; Ni salama na Unaweza kutumia supplements ambazo zina virutubisho vinavyotakiwa kama vile Vitamins,Madini(Minerals),antioxidants n.k, ila Mwili hauwezi kufanya ufyonzwaji kwa urahisi zaidi kama mtu ambaye anakula vyakula vyenye virutubisho hivi.


Hivo badala ya kukimbilia Supplements, kula vyakula vyenye virutubisho hivi itasaidia mwili kufanya ufyonzwaji kwa urahisi zaidi na kwa haraka,


"The best way to increase sperm count naturally may be to increase the consumption of foods high in sperm-friendly nutrients, such as vitamin C, antioxidants, and polyunsaturated fats.Than taking Supplements directly".


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

TATIZO LA MISULI YA UKE KUBANA AU KUKAZA(VAGINISMUS),CHANZO,DALILI NA TIBA YAKEAfyaclass Bongo Social •

 TATIZO LA MISULI YA UKE KUBANA AU KUKAZA(VAGINISMUS),CHANZO,DALILI NA TIBA YAKE

Vaginismus,hili ni tatizo la misuli ya uke kubana au kukaza yenyewe pasipo kupanga au bila hiari ya mwanamke mwenyewe,na tatizo hili la misuli ya uke kubana hutokea pale ambapo kuna kitu chochote kinatakiwa kupitishwa ukeni kama vile uume wakati wa tendo la ndoa n.k,

Hali hii husababisha mwanamke kutokufurahia kabsa tendo la ndoa,uume kushindwa kupita au kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa au wakati akiguswa maeneo yaliyo karibu na uke,

Kumbuka; Kuna watu wengi huchanganya maumivu wakati wa tendo la ndoa yaani Dyspareunia pamoja na tatizo hili la misuli ya uke kubana yaani vaginismus, fahamu kwamba vitu hivi ni tofauti,japo mtu mwenye tatizo la misuli ya uke kubana huweza kupata tatizo la maumivu makali wakati wa tendo la ndoa

CHANZO CHA TATIZO HILI LA MISULI YA UKE KUBANA

Mpaka sasa hakuna sababu ya moja kwa moja ambayo husababisha tatizo hili,ila tafiti zinaonyesha kuna baadhi ya sababu mbali mbali ambazo huongeza uwezekano wa mtu kupatwa na tatizo hili la misuli ya uke kubana,na sababu hizo ni kama vile;

- Mwanamke kuwa na historia ya kufanyiwa vitendo vya kikatili hapo nyuma kama vile kubakwa au kuingiliwa kinyume na maumbile bila ridhaa yake

- Mwanamke kuwa na historia ya kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa

- Mwanamke kupata majeraha sehemu za siri

- Tatizo la hofu na wasiwasi mkubwa wa kufanya tendo la ndoa n.k

DALILI ZA TATIZO HILI LA MISULI YA UKE KUBANA NI PAMOJA NA;

• Misuli ya uke kukakamaa na kubana yenyewe pale unapojaribu kuingiza kitu chochote ukeni

• Maumivu makali sana wakati wa tendo la ndoa,kumbuka sio kila maumivu makali wakati wa tendo la ndoa basi chanzo chake ni tatizo la misuli ya uke kubana

• Mwanamke kuingiwa na hofu ya kuingiza kitu chochote ukeni

• Mwanamke kukosa kabsa hamu ya tendo la ndoa hasa pale anapofikiria uume utakavyopita ukeni

• Mwanamke kuhisi hali ya kuungua ukeni au kuchoma wakati kitu chochote kikiwekwa ukeni au kuguswa maeneo ya kuzunguka uke

MATIBABU YA TATIZO LA MISULI YA UKE KUBANA

Zipo njia mbali mbali za kumsaidia mwanamke mwenye tatizo hili la misuli ya uke kubana na njia hizo ni kama vile;

✓ Mwanamke kufundishwa jinsi ya kufanya mazoezi ya kubana misuli ya uke au mazoezi ya kudhibiti utendaji kazi wa misuli ya ukeni ambapo yote kwa kitaalam hujulikana kama Kegel exercise

✓ Mazoezi hayo pia huhisisha zoezi ya kupitisha kitu ukeni ili kusaidia misuli ya ukeni kufanya kazi vizuri,kumbuka unatakiwa kufanya mazoezi haya kwa maelekezo kamili kutoka kwa wataalam wa afya

✓ Pia kuna matumizi ya dawa mbali mbali za kusaidia utendaji kazi wa misuli ya ukeni na kuondoa hali ya misuli ya ukeni kukakamaa pamoja na kubana.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

je unaweza kupata ukimwi bila kuchubukaAfyaclass Bongo Social •

 je unaweza kupata ukimwi bila kuchubuka

HIV ni nini?
ni ufupisho wa Human Immunodefeciency Virus yaani virusi vinavyoua kinga ya mwili.HIV ni kirusi kinachoharibu uwezo wa mwili wako wa kujihami dhidi ya maambukizi.

AIDS ni ufupisho wa Acquired Immunodefeciency Syndrome, Tatizo la Upungufu wa Kinga Mwilini.

Watu wengi hufikiria kwamba watu ambao wana virusi hivyo, wana Ukimwi, ukweli ni kwamba virusi vya HIV ndivyo vinavyosababisha Ukimwi, yaani yawezekana mtu akawa na virusi vya ukimwi kwa muda mrefu bila ya kuugua ukimwi.

Hii inamaanisha Mtu anaweza kuwa na HIV bila kujua, wala kuona dalili zozote – Wakati huo iwapo tahadhari hazitachukuliwa anaweza kumwambukiza mtu mwengine .

Ukimwi ni nini?
Neno Ukimwi lina maana ya Ukosefu wa Kinga Mwilini. Hapa virusi vya HIV huwa vimeshambulia kinga ya aliyeambukizwa kiasi kuwa, mwili wake hauwezi tena kujipa ulinzi dhidi ya maambukizi.

Hivyo huonyesha dalili za magonjwa tofauti tofauti na hata saratani, hapo ndipo inasemekana kwamba wana ukimwi. Wakati huo ndipo kinga yao ya mwili huwa ni dhaifu sana,

na magonjwa nayo yanawashambulia kwa urahisi zaidi na yanakuwa vigumu kuyatibu,ndipo hapo ukimwi unasababisha kifo.

Fahamu kuwa kila mtu hukumbana na viini ambavyo husababisha magonjwa, lakini kama kinga yako ni imara si rahisi kupata maambukizo na hata ukipata ni rahisi kuyatibu lakini kwa wale waishio na virusi vya ukimwi kinga yao huwa imedhoofishwa sana kiasi kuwa akikumbana na viini ni rahisi kwake kupata maradhi na hata akitibiwa inachukua mda kupona.

JE UNAWEZA KUPATA UKIMWI BILA KUCHUBUKA?

Unaweza kupata VVU tu kwa kugusana moja kwa moja na majimaji/viowevu(fluids) fulani vya mwili kutoka kwa mtu aliye na VVU ambaye ana kiwango cha virusi kinachotambulika. Viowevu hivi ni pamoja na;

✓ Damu(Blood)

✓ Shahawa (cum) na maji kabla ya mbegu za kiume (pre-cum)

✓ Majimaji ya rectum(Rectal fluids)

✓ Majimaji ya ukeni(Vaginal Fluids)

✓ Maziwa ya mama

KUMBUKA: Ili maambukizi haya yatokee, Virusi vya UKIMWI katika viowevu hivi nilivyovitaja, lazima viingie kwenye mkondo wa damu wa mtu asiye na VVU kupitia utando wa mucous (unaopatikana kwenye puru, uke, mdomo, au ncha ya uume),

kwa kupitia njia mbali mbali kama vile kwenye vidonda, baada ya kuchomwa na vitu vya ncha kali kama sindano,nyembe n.k

HIVO UNAWEZA KUWA KWENYE HATARI ZAIDI YA KUPATA UKIMWI KWA NJIA HIZI

Hizi ndyo baadhi ya njia ambazo mtu huweza kuwa kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi ya UKIMWI;

- Kwa Kufanya ngono zembe au bila kinga kama Condom

- Kuwa na Wapenzi wengi,Multiple Sexual partners

- Kwa Kuchangia vitu vya ncha kali kama sindano,wembe,pini n.k na mtu aliyeathirika

- Mama aliyeambukizwa anaweza kumwambukiza mwanawe wakati wa uja uzito, kuzaa au kunyonyesha.

- Kuchangamana kwa damu au majimaji mengine ya mwili – mfano damu iliyo na virusi ikipenya kwenye jeraha au mchubuko.

- Kuongezewa damu iliyo na virusi N.k

HUWEZI KUAMBUKIZWA VIRUSI KUPITIA:

- kuamkiana kwa kushikana mikono.

- Kutumia kwa pamoja vifaa vya kulia chakula kama sahani,vijiko n.k

- Kukohoa au kwenda chafya.

- Kuumwa na wadudu kama kunguni au mbu au wanyama.

- Kula chakula kilichotayarishwa na mtu aliye na virusi vya ukimwi.N.k



0 Comment

MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO(KAMA HUKUPATA TIBA)Afyaclass Bongo Social •

 MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO(KAMA HUKUPATA TIBA)

Tatizo la msongo wa mawazo huwapata watu wengi sana kwa hivi sasa kutokana na sababu mbali mbali,

Katika Dunia ya Sasa mambo yamekuwa mengi sana ambayo huweza kumfanya binadamu kupitia vipindi vigumu sana kwenye maisha yake,

Hali ambayo huchangia watu wengi kuwa na huzuni sana,wasi wasi,hofu,hasira,msongo wa mawazo,Sonona n.k

BAADHI YA SABABU AMBAZO HUWEZA KUSABABISHA MTU KUWA NA MSONGO WA MAWAZO NI PAMOJA NA;

- Kupoteza pesa nyingi,kukosa hela,anguko la kiuchumi

- Majanga kama vile ya mafuriko,Moto,Vitu kuungua,nyumba,biashara n.k

- Kufukuzwa kazini,

- Mtu kuibiwa vitu vyake,

- Migogoro mbali mbali kama vile migogoro ya kwenye mahusiano,ndoa,Familia au Ukoo

- Mwanafunzi kufeli mitihani yake

- Kufiwa na mtu au watu wako wa karibu sana ambao unawategemea kwa namna moja au nyingine, kama vile wazazi,ndugu na hata marafiki. N.K

DALILI ZA MTU MWENYE SHIDA YA MSONGO WA MAWAZO AMBAPO WAKATI MWINGINE HUFIKA HADI KWENYE SONONA

Mtu mwenye shida ya msongo mkali wa mawazo huweza kuonyesha dalili mbali mbali kama vile;

✓ Kuanza kujitenga sana na watu na kuanza kukaa peke yake

✓ Kukasirika haraka sana kwa vitu vidogo na vyakawaida sana

✓ Kuonekana mwenye huzuni au kukosa raha muda wote

✓ Kufanya kazi ndogo kwa muda mrefu sana, mfano mtu anaweza kufagia kaeneo kadogo tu lakini akatumia masaa anafanya kazi hyo tu

✓ Mtu kuanza kuongea mwenyewe

✓ Mtu kulia kila mara

✓ Mtu kuanza kuongea vitu ambavyo vinaashiria kujidhuru au kudhuru wengine, pamoja na kuonyesha kukosa kabsa tumaini la maisha N.K

MADHARA YA MSONGO WA MAWAZO(KAMA HUKUPATA TIBA)

Je wajua tatizo la msongo wa mawazo huweza kusababisha madhara makubwa kama halikupata Tiba?

haya hapa ni baadhi tu ya madhara ambayo huweza kusababishwa na shida ya msongo mkali wa mawazo;

• Mtu kupoteza uwezo au ufanisi wake kwenye kazi yoyote aliyokuwa anafanya

• Mtu kufukuzwa kazi kwa kushindwa kufanya kazi

• Mtu kupoteza uwezo wake wa kufanya maamuzi sahihi juu ya mambo mbali mbali anayokutana nayo

• Mtu kukosa kabsa hisia za kufanya tendo la ndoa

• Mtu kushindwa kabsa kufanya tendo la ndoa au uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume kupungua sana

• Mwanafunzi kuwa na msongo wa mawazo hadi kupelekea kufeli mitihani yake

• Maumivu makali ya kichwa

• Mtu kuanza kujiingiza kwenye vitendo vibaya kama vile; matumizi ya madawa ya kulevyia,uvutaji wa sigara,kunywa pombe kupita kiasi n.k

• Mtu kujidhuru mwenyewe au kudhuru wengine, na wakati mwingine mtu kupoteza kabsa maisha. N.K

KUMBUKA; Ukiona mtu mwenye dalili kama hizi ongea na wataalam wa afya ili mtu huyu asaidiwe haraka kabla madhara zaidi kujitokeza.



0 Comment

Kuwashwa Kwenye Mrija wa Mkojo: Sababu, Dalili na MatibabuAfyaclass Bongo Social •

 

Kuwashwa Kwenye Mrija wa Mkojo: Sababu, Dalili na Matibabu

Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni tatizo la kawaida ambalo linaweza kumtokea mtu yeyote. Hii ni hali inayosababisha mwasho kwenye njia ya mkojo, ambayo ni mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na nje ya mwili.

Mwili wa binadamu una njia ya mkojo yenye urefu wa sentimita 15-20, ambayo inajumuisha figo, ureta, kibofu cha mkojo, na urethra,

Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni dalili ya magonjwa kadhaa, na inaweza kusababisha usumbufu mkubwa. Katika makala hii, tutajadili sababu za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo, dalili, na matibabu.

Sababu za Kuwashwa Kwenye Mrija wa Mkojo:

Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo inaweza kusababishwa na sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na:

1. Maambukizi ya njia ya mkojo(UTI): Hii ni sababu ya kawaida ya kuwashwa kwenye mrija wa mkojo.

Maambukizi haya husababishwa na bakteria ambazo zinaweza kusababisha maumivu na kuwashwa.

2. Kupungua kwa homoni ya estrogeni: Kupungua kwa homoni ya estrogeni kwa wanawake baada ya kufikia umri wa kubalehe, ujauzito au kumaliza hedhi (menopause) kunaweza kusababisha kuwashwa kwenye mrija wa mkojo.

3. Matumizi ya dawa: Matumizi ya baadhi ya dawa kama vile antibiotiki, antihistamini, au dawa za chemotherapy zinaweza kusababisha kuwashwa kwenye mrija wa mkojo.

4. Maambukizi ya virusi: Virusi kama vile virusi vya ukimwi (HIV) na virusi vya Human papiloma (HPV) vinaweza kusababisha kuwashwa kwenye mrija wa mkojo.

Dalili za Kuwashwa Kwenye Mrija wa Mkojo:

Dalili za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo zinaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu, lakini dalili za kawaida ni pamoja na:

  • Kuwashwa kwenye njia ya mkojo
  • Kuhisi kiu kali ya kunywa maji
  • Kupata shida wakati wa kukojoa
  • Maumivu au usumbufu wakati wa kukojoa n.k

Matibabu ya Kuwashwa Kwenye Mrija wa Mkojo:

Matibabu ya kuwashwa kwenye mrija wa mkojo hutegemea sababu za msingi za tatizo.

Kwa mfano, ikiwa tatizo ni maambukizi ya njia ya mkojo, daktari atampa mgonjwa antibiotics,

Ikiwa kuwashwa kwenye mrija wa mkojo husababishwa na kupungua kwa homoni ya estrogeni, mgonjwa anaweza kupewa dawa za homoni. n.k

Baadhi ya njia zinazoweza kusaidia kupunguza dalili za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni pamoja na:

✓ Kunywa maji mengi: Kunywa maji mengi husaidia kupunguza dalili za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo kwa kusafisha njia ya mkojo.

✓ Kuzuia maambukizi: Unaweza kuzuia maambukizi ya njia ya mkojo kwa kunywa maji mengi, kukojoa wakati wa kuhisi haja ndogo(epuka tabia ya kubana mkojo), na kuosha eneo la karibu na njia ya mkojo kwa maji safi mara kwa mara.

✓ Epuka vyakula na vinywaji vyenye kusababisha usumbufu: Vyakula vyenye viungo na vinywaji kama vile kahawa, chai, na vinywaji vyenye kileo vinaweza kusababisha kuwashwa kwenye mrija wa mkojo.

FAQs;

[sc_fs_multi_faq headline-0="h3" question-0="Je! Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni dalili ya nini?" answer-0="Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni dalili ya magonjwa kadhaa ikiwa ni pamoja na maambukizi ya njia ya mkojo(UTI), kupungua kwa homoni ya estrogeni, matumizi ya dawa na maambukizi ya virusi. " image-0="" headline-1="h3" question-1="Je! Ni njia gani nzuri za kuzuia kuwashwa kwenye mrija wa mkojo?" answer-1="Njia nzuri za kuzuia kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni pamoja na kunywa maji mengi, kuzuia maambukizi, na kuepuka vyakula na vinywaji vyenye kusababisha usumbufu." image-1="" count="2" html="true" css_class=""]

Hitimisho:

Kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni tatizo linalowaathiri wengi, lakini ni jambo linaloweza kutibiwa.

Sababu za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo ni nyingi, lakini matibabu hutegemea sababu za msingi za tatizo,

Ni muhimu kutambua dalili za kuwashwa kwenye mrija wa mkojo na kutafuta ushauri wa kitaalamu ikiwa dalili hizo zinaendelea kwa muda mrefu au zinazidi kuwa kali. Kwa kufuata njia za kuzuia na matibabu sahihi, tatizo hili linaweza kuisha kabsa.

kuwashwa kwenye mrija wa mkojo,chanzo na Tiba

muwasho kwenye njia ya mkojo husababishwa na nini?

Watu wengi hupatwa na shida hii ya muwasho kwenye njia ya Mkojo,na katika makala hii tumechambua baadhi ya vyanzo vya tatizo hili,

Mrija wa mkojo kuwasha kwa wanaume huweza kuwa ni dalili kadhaa zinazohusiana na tatizo la urethritis, au kuvimba kwa urethra,

Tatizo hili la urethritis huweza kusababishwa na vitu mbali mbali ikiwemo magonjwa ya Zinaa(STIs) kama vile Kisonono au chlamydia n.k

Na Dalili zake kufanana kabsa na dalili za UTI, kama vile;

  •  Kuhisi muwasho au hali ya kuchoma choma kwenye uume au njia ya mkojo
  •  kupata maumivu au kuhisi hali ya Kuungua wakati wa Kukojoa(dysuria)
  • Uume kuuma na Kuvimba
  • Kupata Maumivu wakati wa tendo
  • Kukojoa mkojo wa rangi kama Pink n.k

CHANZO CHA MUWASHO KWENYE MRIJA WA MKOJO

Kuna Sababu mbali mbali ambazo huweza kusababisha Muwasho kwenye Njia ya Mkojo ikiwemo;

1. Maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa,

Na magonjwa haya huonekana zaidi kusababisha shida hii ya muwasho kwenye Mrija wa Mkojo;

  • Ugonjwa wa Kisonono(gonorrhea)
  • Ugonjwa wa chlamydia

Kwa Mujibu wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa yaani Centers for Disease Control and Prevention (CDC), bacteria hawa huhusika zaidi na tatizo la Urethritis:

(i) Neisseria gonorrhoeae

(ii) Chlamydia trachomatis

(iii) Mycoplasma genitalium

Chanzo cha mtu kupata Muwasho kwenye Mrija wa Mkojo ni pamoja na magonjwa ya zinaa, kama kisonono na chlamydia, na pia sababu zingine ni kama vile matumizi ya baadhi ya sabuni n.k(-)

2. Maambukizi ya fangasi,Candidiasis au yeast infection

Pia mashambulizi ya Fangasi sehemu za Siri huweza kuwa chanzo cha tatizo hili

3. Tatizo la UTI,

Maambukizi ya bacteria kwenye Njia ya Mkojo yaani urinary tract infection (UTI).

Maambukizi haya huweza kutokea kwenye maeneo kama vile Figo,Kwenye kibofu cha Mkojo, au kwenye mrija wa Mkojo, ureters au urethra.

4. Tatizo la Ngozi(Contact dermatitis),

ambapo huhusisha muwasho kwenye ngozi baada ya ngozi yako kugusana na vitu ambavyo ni allergen kwako, vivyo hivo huweza kutokea kwenye ngozi laini sana sehemu za siri kama kwenye kitundu cha Mkojo pamoja na mrija wa Mkojo.

5. Matumizi ya baadhi ya Vitu vyenye Kemikali, Kama vile baadhi ya Sabuni n.k

6. Mwanamke kuwa na tatizo la Bacterial Vaginosis. n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

UGONJWA WA MASUNDO SUNDO-warts KWA UJUMLA WAKE(soma hapa)Afyaclass Bongo Social •

 UGONJWA WA MASUNDO SUNDO-warts KWA UJUMLA WAKE(soma hapa)

UGONJWA WA MASUNDO SUNDO (WARTS)

Huu ni ugonjwa wa Ngozi ambao unasababishwa na virusi waitwao Human papillomaviruses (HPVs).

Virusi hawa wapo wa aina nyingi sana na wanasababisha madhara au ugonjwa katika sehemu husika katika mwili na Mpaka sasa kuna aina Zaidi ya 220 ya virusi hawa wa HPV. Mfano masundosundo yatokeayo maeneo ya haya kubwa na maeneo ya via vya uzazi husababishwa na HPV aina ya 6 na 11, masundosundo ya kwenye kanyagio na kisigino ni HPV aina ya 1.

Masundo sundo ya Ngozi inawapata sana Watoto na vijana,kwa watu wa makamo,wazee wnapata masundosundo kama hayo lakini masundosundo ya maeneo ya njia ya haja kubwa na maeneo ya uzazi wa mwanamke na mwanaume.

Masundosundo kwa Watoto na vijana hua yanaweza kuisha menyewe hata bila dawa na ikumbukwe kwamba kuisha kwa masundosundo hutegemea na uimara wa kinga ya mwili wa muhusika na umri wa mtu husika;hata kwa kwa upande wa kutokea kwa dalili Watoto na vijana wenye kinga nzuri hua inachukua takribani wiki 2 hadi 6 kwa dalili za awali kuonekana;

lakini kwa wazee na watu wenye upungufu wa kinga mwilini kutokana na sababu yeyote inaweza kuchukua miezi kadhaa hata miaka kadhaa kwa dalili kuanza kuonekana.

Maambukizi ya virusi wa HPV ni kutoka mtu kwa mt una inasadikika kwamba ni kwa njia ya migusano au ngono baina ya mgonjwa na mtu asie mgonjwa na virusi hao humuingia mtu kupitia mikatiko midogo midogo ambayo itakuwepo kwa Ngozi au maeneo ya uzazi.

DALILI ZA UGONJWA WA MASUNDOSUNDO

Ugonjwa huu hupelekea mtu kupata vipele au vinundu vigumu vingumu katika Ngozi.masundo sundo haya hutegemea na sehemu yaliyipo na yamepewa na majina kutokana na sehemu vilivyotokea. Kuwepo kwa majina tofauti tofauti hakubadilishi dalili,makali au matibabu yake bali ni katika kuvielezea tu. Matibabu ya aina zote yanafanana kabisa.

Kuna aina kadhaa ya masundosudo kutokana na mionekano yao na sehemu yaliyopo mfano kuna masundosundo ya kawaida ambayo hutokea mikonon,kifuani,tumboni,usoni nk (verruca vulgaris),masundo sundo yatokeayo kwenye viiganja vya miguu na mikono (verruca plantaris),masundosundo yasokua na vinundu au vipele (verruca plana) na masundosundo ya maeneo ya haja kubwa na maeneo ya uzazi (condylomata acuminata).masundosundo tofauti na vinundu au vipele pele vinauaga vinawasha washa mwingine

MATIBABU YA MASUNDOSUNDO

Ugonjwa huu kama yalivyo magonjwa mengine hutibika vizuri sana ,aidha masundo sundo sio lazima yatibiwe kwa dawa kwani mengine yanaweza kuisha menyewe bila hata dawa. Matibabu ya masundosundo kabla ya kufanyika mambo kadhaa hutizamwa kwani madawa au tiba zingine hua ni za gharama na kuna madhara yake pia.

Matibabu ya masundo sundo yapo ya aina mbalimbali kama vile kwa kutumia dawa za kupaka na za kuchoma,kufanya operesheni ya kuvikata,kuviunguza kwa baridi au kuvikata kwa umeme.

Ikumbukwe kwamba tunatoa matibabu ya masundo sundo kama mgonjwa ana mojawapo ya mambo yafuatayo.

1)Kama yamekaa kwa muda mrefu sana (Persistent warts)

2)Kama mgonjwa anataka kuyaondoa kwa sababu za muonekano au kuogopa kusemwa au kunyanyapaliwa (Patient concern for cosmesis or social stigma)

3)Kama  mtu ana upungufu wa kinga mwilini (Immunosuppression)

4)Kama yanamletea maumivu  mgonjwa (Associated pain)

5) Kama yanamkera kera mtu au kumzuia mtu kufanya majukumu yake (Associated with discomfort/functional impairment)

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Mapigo ya moyo kwenda mbio, chanzo, dalili, na Matibabu ya TachycardiaAfyaclass Bongo Social •

 Mapigo ya moyo kwenda mbio, chanzo, dalili, na Matibabu ya Tachycardia

Tachycardia ni tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio ambapo huhusisha kiwango cha mapigo ya moyo kuwa zaidi ya mapigo 100 kwa dakika.

Tatizo hili la Mapigo ya moyo kwenda mbio linaweza kutokuwa na dalili au matatizo yoyote. Lakini likiachwa bila matibabu, baadhi ya aina za tachycardia zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya, ikiwa ni pamoja na tatizo la kushindwa kwa moyo kufanya kazi(heart failure), kiharusi au kifo cha ghafla.

Matibabu ya tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio yanaweza kujumuisha matumizi ya mbinu maalum, dawa, cardioversion, au upasuaji ili kudhibiti mapigo ya moyo yanayokwenda kwa kasi.

Dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Moyo ukienda kwa kasi sana, huenda usisikume damu ya kutosha kwenda kwenye sehemu nyingine za mwili. Kama matokeo, viungo na tishu zinaweza kutopata kiasi cha kutosha cha oksijeni.

Kwa ujumla, tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio linaweza kusababisha dalili na ishara zifuatazo:

  1. Kuhisi moyo kwenda kasi sana
  2. Kupata Maumivu ya kifua
  3. Kuzirai (syncope)
  4. Kupata Kizunguzungu
  5. Moyo kupiga kwa kasi sana
  6. Kupumua kwa shida n.k

Baadhi ya watu wenye tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) hawana dalili zozote. Hali hii inaweza kugundulika wakati wa uchunguzi wa mwili au vipimo vya moyo vinapofanywa kwa sababu ya tatizo lingine.

Chanzo cha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Tachycardia ni ongezeko la kasi ya mapigo ya moyo kwa sababu yoyote. Inaweza kuwa ongezeko la kawaida la mapigo ya moyo kutokana na mazoezi au majibu ya mkazo kwa kitaalam (sinus tachycardia). Sinus tachycardia inachukuliwa kuwa ni dalili, si ugonjwa.

Mambo yanayoweza kusababisha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio ni pamoja na:

  • Homa
  • Matumizi makubwa ya pombe au kuacha kutumia pombe ghafla
  • Kiwango kikubwa cha kafeini
  • Shinikizo la damu la juu au chini
  • Kutofanana kwa viowevu mwilini vinavyoitwa electrolytes - kama vile potasiamu, sodiamu, kalsiamu na magnesiamu
  • Madhara ya dawa
  • Tezi la Koo Kufanya kazi kwa kasi (hyperthyroidism)
  • Kupungua kwa kiasi cha chembe chembe nyekundu za damu (anemia), mara nyingi husababishwa na kutokwa na damu
  • Uvutaji wa sigara
  • Matumizi ya dawa za kulevyia/haramu, ikiwa ni pamoja na dawa zenye vichocheo kama vile kokaini au methamphetamine n.k

Jinsi ya Kuzuia tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio

Chukua hatua zifuatazo:

✓ Kula lishe bora. kitu unachokula huweza kuleta faida au madhara mwilini,hivo chagua mlo kamili wenye virutubisho vyote muhimu,

kula nafaka nzima, nyama isiyo na mafuta mengi, maziwa yasiyo na mafuta mengi, matunda, na mboga mboga za Majani. Punguza matumizi ya chumvi, sukari, pombe, mafuta mengi, na mafuta yenye utomvu(saturated fat and trans fats).

✓Fanya mazoezi mara kwa mara. Jaribu kufanya mazoezi angalau dakika 30 kila siku.

✓ Dhibiti Uzito wako wa Mwili. Kuwa na uzito uliozidi kunaweza kuongeza hatari ya kupata  magonjwa ya moyo pamoja na matatizo mengine kama vile tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio.

✓ Dhibiti shinikizo la damu na viwango vya cholesterol. Fanya mabadiliko ya mtindo wa maisha na tumia dawa kama ilivyopendekezwa ili kudhibiti shinikizo la juu la damu (hypertension) au viwango vya cholesterol vilivyopanda.

✓Acha kuvuta sigara. Ikiwa unavuta sigara na huwezi kuacha peke yako, ongea na mtoa huduma wako wa afya kuhusu mikakati au programu za kukusaidia kuacha tabia ya kuvuta sigara.

✓ Acha kabsa matumizi ya Pombe au Kunywa kwa kiasi. Ikiwa unachagua kunywa pombe, fanya hivyo kwa kiasi. Kwa watu wazima wenye afya, hiyo inamaanisha kunywa chupa moja ya pombe kwa siku kwa wanawake na chupa mbili kwa siku kwa wanaume.

Kwa baadhi ya hali za Kiafya, inashauriwa kabisa kuacha pombe. Uliza ushauri kutoka kwa mtoa huduma wako wa afya kuhusu hali yako maalum.

✓ Usitumie dawa za kulevyia au kichocheo, kama vile kokaini. Ongea na mtoa huduma wako wa afya kuhusu programu inayofaa kwako ikiwa unahitaji msaada wa kuacha matumizi ya dawa za kulevyia.

✓ Tumia dawa kwa uangalifu. Baadhi ya dawa za kukabili homa na kikohozi zina viyeyusho ambavyo vinaweza kusababisha mapigo ya moyo kwenda kwa kasi. Uliza mtoa huduma wako wa afya ni dawa gani unahitaji kuepuka.

✓ Punguza matumizi ya kafeini. Ikiwa unakunywa vinywaji vyenye kafeini, fanya hivyo kwa kiasi.

✓ Dhibiti msongo wa mawazo. Tafuta njia za kupunguza msongo wa Mawazo, Kufanya mazoezi zaidi ikiwemo kufanya mazoezi yanayohusisha utulivu wa akili n.k ni baadhi ya njia za kupunguza msongo wa mawazo.

✓ Fanya chekups mara kwa mara. Pata uchunguzi wa mwili mara kwa mara na ripoti mabadiliko yoyote katika mapigo yako ya moyo kwa mtoa huduma wako wa afya. Ikiwa dalili zako zinabadilika au kuwa mbaya au unapata dalili mpya, mwambie mtoa huduma wako wa afya mara moja.

✓ Usijaribu kujitibu mwenyewe. Ikiwa una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) au wasiwasi kuhusu afya yako ya moyo, usijaribu kujitibu mwenyewe. Ni muhimu kumuona mtoa huduma wa afya kwa uchunguzi na ushauri sahihi.

✓ Tafuta matibabu mapema. Ikiwa una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) au dalili zingine ambazo huzielewi tafuta matibabu mapema. Kupata utambuzi na matibabu sahihi kwa wakati kunaweza kusaidia kuzuia matatizo makubwa zaidi ya kiafya.

✓ Elewa historia yako ya Kiafya. Jifunze kuhusu historia yako ya Kiafya na historia ya magonjwa ya moyo katika familia yako. Hii itasaidia daktari wako kutambua hatari kwako ya kuwa na  tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia) pamoja na matatizo mengine ya moyo.

✓ Epuka sababu zinazoweza kusababisha tachycardia. Kama ilivyoelezwa hapo juu, kuna sababu kadhaa zinazoweza kusababisha tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio. Kwa kuzingatia mtindo bora wa maisha na kufuata miongozo ya kuzuia magonjwa inaweza kupunguza hatari kwako ya kuwa na tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio(tachycardia).

Kumbuka, Ikiwa una wasiwasi kuhusu afya yako au una dalili za tatizo la Mapigo ya moyo kwenda mbio, tafadhali wasiliana na mtoa huduma wako wa afya kwa ushauri na matibabu sahihi. Kujali afya yako ni muhimu ili kuishi maisha yenye afya na furaha.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapaAfyaclass Bongo Social •

Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapa

Katika Makala hii tumechambua zaidi kuhusu Dalili za malaria sugu na Tiba yake,Fahamu zaidi hapa.

malaria sugu

Malaria Sugu au Chronic malaria ni pale ambapo ugonjwa wa Malaria umekuwa wa muda mrefu ambapo kwa kitaalam tunasema ni "long-term malarial infection" 

Kumbuka: Tofauti ya Malaria Sugu(chronic Malaria) na malaria ya muda mfupi(acute Malaria) ni kwenye Swala la muda tu wa mashambulizi,madhara yake pamoja na matibabu yake,

ambapo Malaria Sugu ni tatizo la muda mrefu,lakini acute malaria;mgonjwa huugua malaria baada ya muda mfupi hupona kabsa na kurudi kwenye hali yake ya kawaida pasipo maambukizi tena.

Hivo basi,Malaria Sugu na Malaria yakawaida ya muda mfupi,vyote husababishwa na vilemelea sawa,dalili sawa n.k

CHANZO CHA UGONJWA WA MALARIA SUGU

Malaria Sugu ni ugonjwa ambao husababishwa na vimelea vya magonjwa viitwavyo Plasmodium, vimelea ambavyo huendelea kufanya mashambulizi kwa muda mrefu ndani ya mwili wako.

Vimelea hivi vya Plasmodium vinavyosababisha Malaria Sugu(chronic Malaria) vipo vya aina mbali mbali kama vile;

  • Plasmodium vivax,
  • plasmodium malariae,
  • plasmodium falciparum,
  • plasmodium ovale

Vimelea hivi huenezwa na mbu jike aina ya anofelesi (anopheles). Lakini watu wengi huelewa kwamba malaria husababishwa na mbu. Mbu huyu husaidia katika usambazaji tuu wa vimelea husika.

Dalili za Malaria Sugu

DALILI ZA MALARIA SUGU NI PAMOJA NA KUPATA DALILI HIZI MARA KWA MARA NDANI YA MUDA MREFU;

1. Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa

2. Mgonjwa kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika

3. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kichwa

4. Mgonjwa kuhisi hali ya kizunguzungu kikali

5. Hamu ya kula au appetite ya chakula kupotea

6. Wakati mwingine mgonjwa kutoa jasho sana

7. Mgonjwa kuwa na dalili zote za kuchanganyikiwa au kuweweseka sana wakati malaria ikiwa kali

•Soma zaidi hapa,Kuhusu dalili za ugonjwa wa Malaria

VIPIMO VYA MALARIA SUGU

Moja ya vipimo ambavyo hutumika kupima ugonjwa wa Malaria Sugu ni pamoja na kipimo cha Damu kwa kutumia kifaa kinachoitwa MRDT,hadubini n.k.

Malaria Sugu,endapo Ugonjwa wa Malaria haujatibiwa huweza kusababisha madhara zaidi mwilini ikiwemo;

  • Kusababisha tatizo la kuvimba kwa bandama,kwa kitaalam hujulikana kama hyper-reactive malarial splenomegaly (HMS),
  • Matatizo kama vile; Kuchanganyikiwa,
  • Na hata Mtu kupoteza Maisha kabsa.

MATIBABU YA UGONJWA WA MALARIA

Mgonjwa wa malaria hutibiwa baada ya kufanyiwa vipimo kwa kutumia dawa mbali mbali kama vile; ALU au mseto, Malaffin, Quinine N.K

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je, Malaria Sugu husababishwa na nini?

Malaria Sugu ni ugonjwa ambao husababishwa na vimelea vya magonjwa viitwavyo Plasmodium, vimelea ambavyo huendelea kufanya mashambulizi kwa muda mrefu ndani ya mwili wako.

Vimelea hivi vya Plasmodium vinavyosababisha Malaria Sugu(chronic Malaria) vipo vya aina mbali mbali kama vile;

  • Plasmodium vivax,
  • plasmodium malariae,
  • plasmodium falciparum,
  • plasmodium ovale

Vimelea hivi huenezwa na mbu jike aina ya anofelesi (anopheles). Lakini watu wengi huelewa kwamba malaria husababishwa na mbu. Mbu huyu husaidia katika usambazaji tuu wa vimelea husika.

Hitimisho

Ni muhimu sana kufahamu kuhusu dalili za Ugonjwa wa Malaria ikiwemo Malaria Sugu,ili kuhakikisha unafanya vipimo na kupata tiba mapema zaidi kabla ya kupata madhara zaidi,

DALILI ZA MALARIA SUGU NI PAMOJA NA KUPATA DALILI HIZI MARA KWA MARA NDANI YA MUDA MREFU;

1. Joto la mwili la mgonjwa kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa

2. Mgonjwa kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika

3. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kichwa

4. Mgonjwa kuhisi hali ya kizunguzungu kikali

5. Hamu ya kula au appetite ya chakula kupotea

6. Wakati mwingine mgonjwa kutoa jasho sana

7. Mgonjwa kuwa na dalili zote za kuchanganyikiwa au kuweweseka sana wakati malaria ikiwa kali

Ukiona dalili kama hizi,hakikisha unawahi hospitalini kwa ajili ya Vipimo pamoja na Matibabu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

VYAKULA VYA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO(Je mgonjwa wa vidonda vya tumbo aleje?)Afyaclass Bongo Social •

 VIDONDA VYA TUMBO

• • • • •
VYAKULA VYA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO(Je mgonjwa wa vidonda vya tumbo aleje?)
 

Ugonjwa wa vidonda vya tumbo ni ugonjwa ambao husababishwa na bacteria aitwaye Helicobacteria pylori, Huku ukichangiwa na sababu mbali mbali kama vile; Msongo wa mawazo,kukaa na njaa kwa muda mrefu pasipo kula chakula  mara kwa mara N.K
 
 
VYAKULA VYA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO NI PAMOJA NA;
 
 
1. Pendelea kula vyakula jamii ya nyuzi nyuzi au fiber,Mfano mboga za majani pamoja na matunda mbali mbali kama vile machungwa, Maembe N.K
 
 
2. Pendelea kunywa juice ya kabegi, tafiti mbali mbali zinaonyesha kwamba juice ya kabegi ina alkaline ya kutosha ambayo itakusaidia kupunguza makali na maumivu yatokanayo na acid inayozalishwa tumboni, lakini pia juice hii ya kabegi ina kiwango kikubwa cha Vitamin C ambayo pia nimuhimu sana mwilini.
 
 
3. Epuka kula vyakula ambavyo vina viungo vingi ndani yake mfano wa sambusa zenye pilipili N.K
 
 
4. Epuka matumizi ya pombe kama una vidonda vya tumbo
 
 
5. Majani ya Alovera ni mazuri pia kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
 
 
6. Epuka kukaa na Njaa kwa muda mrefu. Pendelea kula mara kwa mara.
 
 
-
 
 
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
 



0 Comment

MTOTO MCHANGA KUKOJOA DAMU,CHANZO NA TIBA YAKEAfyaclass Bongo Social •

 MTOTO MCHANGA KUKOJOA DAMU,CHANZO NA TIBA YAKE

Kwenye wiki ya kwanza baada ya mtoto kuzaliwa,

Mama huweza kuona vidamu damu kwenye diapers wakati anamsafisha mtoto,

Lakini mara nyingi sio kwamba mtoto kakojoa damu ila ni mkojo ambao ni High concentrated ambao unaweza kusema ni damu.

Kwa watoto wakike unaweza kuona kama mtoto mdogo ila kaanza Blid, hii hutokana na mtoto kuwepo kwenye mazingira ya vichocheo au hormones kwenye tumbo la uzazi la mama yake kwa muda mrefu,

hali ambayo hupelekea mtoto kuanza kupata blid, ila baada ya kukaa kwenye mazingira ya Nje, hali hii hupotea yenyewe.

ANGALIZO: Endapo mtoto wako anakojoa damu na kupata dalili zingine kama vile;

- Maumivu makali ya tumbo

- Kutonyonya kabsa au uwezo mdogo sana wa kunyonya

- Mtoto kulegea

- Mtoto kutapika,kuharisha n.k

- Mtoto kupata homa au joto la mwili kuwa juu sana.

Mkimbize mtoto hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi na matibabu ya haraka.

BAADHI YA VITU VINGINE AMBAVYO HUWEZA KUSABABISHA HALI YA KUKOJOA DAMU NI PAMOJA NA;

• Maambukizi kwenye kibofu cha mkojo

• Maambukizi kwenye Figo

• Kiwango kikubwa sana cha Calcium na madini mengine kwenye mkojo

• Maambukizi kwenye mfumo wa mkojo au UTI

• Kupata majeraha kwenye njia ya mkojo,figo au kibofu cha mkojo n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Chanzo cha Miguu kufa ganzi pamoja na Matibabu yakeAfyaclass Bongo Social •

 Chanzo cha Miguu kufa ganzi pamoja na Matibabu yake

Watu wengi wamekuwa wakichanganya ganzi na hisia nyingine kama miguu kuwaka moto, kutekenywa na hata kuhisi kukanyaga kitu chenye ncha kali.

Kufa ganzi ni kitendo cha kupoteza hisia katika sehemu husika. Tatizo/ kitendo hiki kinaweza kuwa ni cha muda mfupi au muda mrefu na kinaweza kuwa baadhi ya sehemu au sehemu mbalimbali.

Hali hii inaweza kuwa ni dalili ya shida katika mfumo wa fahamu.

Mtu anapogusa kitu hisia au taarifa hupokelewa na vipokeo vilivyo katika ngozi kisha husafirishwa na mishipa ya neva mpaka kwenye uti wa mgongo na kisha kwenye ubongo kwaajili ya kutafasiriwa. Na baada ya ubongo kuchakata taarifa hizi hurudisha taarifa kupitia mishipa ya neva mpaka eneo husika.

Kufa ganzi hupelekea kupoteza uwezo wa kuhisi kuguswa, joto, kuhisi maumivu na mitetemo na baadhi ya watu hupelekea kushindwa kutambua zilipo sehemu husika za mwili wao.

Kufa ganzi hupelekea kukosekana kwa hisia/taarifa na kunaweza pelekea mtu kupata maambukizi, vidonda na majeraha yanayoweza kupelekea majanga ya kukatwa mguu au sehemu husika.

SABABU ZA MIGUU KUFA GANZI

Kufa ganzi hutokea iwapo kuna changamoto katika njia ya usafirishaji wa hisia/ taarifa. Shida hii inaweza tokeo kwenye vipokeo(receptors), mishipa ya neva, uti wa mgongo au ubongo.

Miongoni mwa mambo yanayoweza haribu njia hii ya usafirishwaji wa taarifa/hisia ni

1. Kupungua au kuzuiwa kwa usafirishwaji wa damu kwenda kwenye mishipa ya neva mfano kwenye kiharusi (stroke)

2. Ajari au magonjwa ambayo yanashambulia mishipa ya neva

3. Kukandamizwa kwa neva (mfano watu wenye tatizo za pingili za mgongo, uvimbe, usaha au mabonge ya damu yatokanayo na ajari)

4. Upungufu wa vitamin hasa vitamin B12

5. Sumu, madawa na kemikali kali

6. Magonjwa kama kisukari na magonjwa ya figo

7. Magonjwa yatokanayo na kinga mwili kushambulia mishipa ya neva.

>> Soma pia tatizo la Mikono kufa ganzi na chanzo chake

DALILI AMBAZO HUWEZA KUAMBATANA NA KUFA GANZI.

Chanzo/sababu ya kufa ganzi inaweza kugundulika kutokana na dalili ambazo zimeambatana kwamfano

1. Maumivu ya mgongo na shingo, kichwa na viungo

2. Homa na mabakamabaka mwilini kwa baadhi ya wagonjwa

3. Miguu kukakamaa sana hasa pale unapohitaji kutembea

4. Kushindwa kunyoosha miguu au mguu n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Ugonjwa wa Gumboro ( Infectious Bursal Diseases) katika ufugaji wa kukuAfyaclass Bongo Social •

 Ugonjwa wa Gumboro ( Infectious Bursal Diseases) katika ufugaji wa kuku

Ufahamu ugonjwa wa Gumboro ( Infectious Bursal Diseases) katika ufugaji wa kuku.

Ni ugonjwa utokanao na virusi  viitwavyo ”BIRNAVIRUS" . Ugonjwa huu huwashambulia kuku na ndege wengine wafugwao.

Kuenea/kusambaa kwa ugonjwa;

Kuenea au kusambaa kwa ugonjwa huu wa Gumboro Kutoka banda moja kwenda linginge asilimia kubwa ni Kupitia kinyesi cha kuku anayeumwa.

Dalili za Ugonjwa wa Gumboro

Dalili za Ugonjwa wa Gumboro kwa Kuku ni pamoja na;

  1. Kuku kutapika na kuharisha majimaji.
  2. Manyoya husimama.
  3. Kuku kusinzia na kukosa hamu ya kula.
  4. Kuku kufa sana,Vifo hufikia hadi asilimia thelathini (30%).
  5. Kuku kujidokoadokoa sehemu ya haja kubwa.
  6. Cloaca kuvimba.
  7. Kutokea Vidonda, Chini ya ngozi hasa mapajani vidonda hutokea hasa kwa vifaranga.

Namna ya kukinga na kuzuia ugonjwa wa Gumboro

✓ Safisha banda kwa dawa za kuua vijidudu (Disinfectants).

✓ Wapatie chanjo ya Gumboro vifaranga wakiwa na umri wa wiki 2 na rudia tena wakiwa na umri wa wiki 3 (yaan siku ya 14 na 21)

Tiba za ugonjwa wa Gumboro

Hakuna matibabu ya ugonjwa huu, ila kwa msaada zaidi wasiliana na mtaalam au daktari wa mifugo. Asante.!!!



0 Comment

KUCHUTAMA/KUCHUCHUMAA(SQUATTING TOILETS):NJIA SALAMA YA KWENDA HAJA KUBWAAfyaclass Bongo Social •

 KUCHUTAMA/KUCHUCHUMAA(SQUATTING TOILETS):NJIA SALAMA YA KWENDA HAJA KUBWA

Kabla ya kuanza kuelezea baadhi ya tafiti mbali mbali ambazo zimefanyika kuhusu faida za kujisaidia ukiwa umechuchumaa yaani Squatting position, nitoe ufafanuzi kuhusu aina za vyoo,

Kuna vile vyoo vya kukaa kabsa ambavyo mara nyingi hutumika hospitalini kwa ajili ya wagonjwa ambao hawawezi kujisaidia wakiwa wamechuchumaa, ila kwa hapa tunazungumzia squatting toilets kama hapo kwenye picha,

Aina hii ya vyoo itakulazimu ujisaidie haja kubwa ukiwa umechuchumaa yaani squatting position, na wataalam wa afya husema kujisaidia kwa staili hii kuna faida zaidi kuliko kujisaidia ukiwa umekaa kabsa(vyoo vya kukaa).

FAIDA ZA KUJISAIDIA HAJA KUBWA UKIWA UMECHUCHUMAA(SQUATTING) KULIKO UKIWA UMEKAA KABSA NI PAMOJA NA;

- Kusaidia haja kubwa itoke haraka,kwa urahisi zaidi, na ujisaidie kinyesi chote mpaka kiishe, hali hii husaidia kuzuia tatizo la kinyesi kukwama wakati wa kujisaidia, na kukuepusha na matatizo mengine mbali mbali kama vile; kuvimba kwa njia ya haja kubwa,michubuko,kuvimba kwa kidole tumbo(appendicitis) n.k

- Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia pia katika kulinda Nerves za tezi dume(prostate),kibofu cha mkojo, pamoja na tumbo la uzazi yaani uterus ambavyo huweza kuharibiwa kabsa

- Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia kulinda valve yaani Ileocecal valve, kati ya utumbo mkubwa na utumbo mdogo, tofauti na mtu ambaye hujisaidia akiwa amekaa, valve hizi hukosa kabsa support na mara nyingi huweza kutengeneza uwazi au Kuleaks hali ambayo huweza kupelekea uchafu kuingia kwenye utumbo mdogo

- Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia kurelax misuli mbali mbali kama vile Puborectalis muscle na kusaidia mtu kujisaidia  kwa urahisi zaidi

- Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia kusupport utumbo mkubwa yaani colon na kukukinga na matatizo mbali mbali kama vile; hernia,Diverticulosis,Pelvic organ prolapse n.k

- Kutokana na tafiti mbali mbali za afya, Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia kupunguza tatizo la bawasiri au hemorrhoids kama ilivyoripotiwa na "Clinical health Research"

- Kwa Mama Mjamzito, Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia kuepuka mgandamizo mkubwa wa Uterus na pia huweza kuwa ni mojawapo ya mazoezi ambayo huweza kumsaidia mama mjamzito kujifungua kwa urahisi zaidi

- Kujisaidia haja kubwa kwa staili hii husaidia hata mkojo kutoka vizuri na kusaidia misuli ya kwenye kibofu cha mkojo kufanya kazi vizuri zaidi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Tatizo La Usonji,Chanzo,Dalili Na TibaAfyaclass Bongo Social •

TATIZO LA USONJI(AUTISM),CHANZO,DALILI NA TIBA YAKE

Tatizo la usonji(autism) ni tatizo ambalo huhusisha hitilafu kwenye maendeleo ya ubongo wa mtoto ambayo huleta shida zingine kama vile; tatizo la mtoto kutokuongea,kujitenga n.k,na tatizo hili huanzia utotoni na kusababisha matatizo makubwa mpaka utu uzima.

Tatizo hili la Usonji ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Autism hutokea kwa baadhi ya watoto na tafiti zinaonyesha kwa wazazi wengi huchelewa kugundua kama watoto wao wana shida hiyo mpaka watoto wakiwa na umri wa miaka 2-3 na kuendelea.

Mtoto mwenye tatizo la Usonji hupatwa na tatizo la kutokuongea,hupenda kujitenga sana na wenzake au watu wengine, na pia tafiti zinaonyesha kwamba tatizo hili la Usonji huwapata watoto wa jinsia ya KIUME zaidi kuliko ya KIKE.

CHANZO CHA TATIZO LA USONJI

- Mpaka sasa hakuna sababu ya moja kwa moja ya kutokea kwa tatizo la Usonji au Autism,japo kuna baadhi ya sababu ambazo zimeonekana kuweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa tatizo hili la Usonji,na sababu hizo ni kama vile;

1. Tatizo la vinasaba(genetics) ambapo hujulikana kwa kitaalam kama vile neurodevelopmental disorders, hapa tunazungumzia matatizo mbali mbali kama vile Rett syndrome,Fragile X syndrome n.k

2. Sababu za kimazingira kama vile; Kupatwa na maambukizi ya (Virusi) ugonjwa wa RUBELLA n.k

3. Matumizi ya baadhi ya dawa kipindi cha ujauzito

4. Complications mbali mbali ambazo huweza kumpata mama wakati wa ujauzito

5. Mama mjamzito kutumia vilevyi mbali mbali kama vile pombe,madawa ya kulevyia kama Coccaine n.k

6. Uchafuzi wa hewa hivo kusababisha watu kuvuta hewa chafu n.k

7. Kuwa na mtoto mwenye tatizo hili la usonji kwenye familia au koo flani huweza kuongeza uwezekano wa watoto wengine kuzaliwa na tatizo hili

8. Mtoto kuzaliwa kabla ya wakati hasa kama imetokea kabla ya wiki 26 za ujauzito, na kwa hapa kwetu Tanzania ni ngumu sana kwa mtoto huyu kuishi,angalau kuanzia wiki 28 na kuendelea uwezekano wa kuishi ni mkubwa.

9. Wazazi kujifungua watoto wakiwa na umri mkubwa sana,japo tafiti zinaendelea kufanyika juu ya hili,ila baadhi ya tafiti zinasema mwanamke kuchelewa kuzaa au kuzaa akiwa na umri mkubwa sana huweza kuchangia uwepo wa tatizo hili la Usonji

NJIA ZA UTAMBUZI WA TATIZO HILI KWA MTOTO

• Wataalam wa afya watataka kujua kuhusu hatua za ukuaji wa mtoto,uwezo wake wa akili pamoja na kufanya vipimo mbali mbali kama vile genetic testing n.k

DALILI ZA TATIZO LA USONJI NI PAMOJA NA;

- Mtoto kushindwa kuitika baada ya kuitwa jina lake au mtoto kuonekana kutokusikia kabsa wakati akiitwa jina lake

- Mtoto kushindwa kutazama watu usoni(eye contacts), kutokucheka,n.k

- Mtoto kutokuongea kabsa au kuchelewa sana kuongea kuliko kawaida

- Kupoteza uwezo wa kutamka maneno au sentensi ambazo mwanzoni alikuwa anaweza kutamka

- Mtoto kushindwa kabsa kuanzisha mazungumzo

- Mtoto kuongea huku akitoa sauti zisizozakawaida

- Mtoto kushindwa kuelewa maswali rahisi akiulizwa na watu

- Mtoto kufanya vitu vya kujidhuru mwenyewe kama vile; kujipiga mwenyewe,kujibamiza kichwa n.k

- Mtoto kutokutaka mwanga,kushtuka sana akiguswa au kusikia sauti yoyote

- Mtoto kutokutamka maneno ya kitoto mpaka afikishe umri wa mwaka mmoja na kuendelea

- Mtoto kutokuongea neno lolote mpaka afikishe kipindi cha umri wa miezi kumi na sita

- Mtoto kupoteza kabsa uwezo wake wa kuongea

- Mtoto kushindwa kufanya vitu mbali mbali kama kupunga mkono kwa wazazi au mtu yoyote kama ishara ya kumsalimia au kumuaga mpaka anapofikisha kipindi cha umri wa miezi kumi na mbili

- Mtoto kushindwa kuongea maneno zaidi ya mawili au sentensi ya maneno mpaka anapofikisha umri wa miezi 24

- Mtoto kuwa na tabia ya kukaa peke yake pamoja na kujitenga na watu N.k

MADHARA YA TATIZO LA USONJI KWA WATOTO NI PAMOJA NA;

• Mtoto kushindwa kuongea kabsa,kuchelewa sana kuongea au kuongea maneno ambayo hayaeleweki

• Mtoto kushindwa kuchangamana na watu wengine(kujitenga muda wote)

• Mtoto kuwa na matatizo ya kutokuelewa akiwa shuleni

• Tatizo la kupewa ajira au kuajiriwa

• Kusababisha msongo wa mawazo na hali ya huzuni katika familia N.k

MATIBABU YA TATIZO LA USONJI

Tatizo hili halitibiki au hakuna tiba ya kuondoa kabsa tatizo hili,ila kuna tiba ya kudhibiti dalili mbali mbali ambazo husababishwa na tatizo hili la Usonji, na kwa ujumla wake zipo tiba mbali mbali kama vile;

✓ Matumizi ya dawa za kudhibiti dalili za tatizo la Usonji

✓ Huduma ya kimawasiliano pamoja na ufundishwaji wa tabia mbali mbali kwa mtoto yaani Behavior and Communication therapy

✓ Huduma ya uelimishwaji yaani educational therapy n.k



0 Comment

kuwashwa sehemu ya haja kubwa,chanzo na Tiba yakeAfyaclass Bongo Social •

 kuwashwa sehemu ya haja kubwa,chanzo na Tiba yake

Tatizo la kuwashwa sehemu ya haja kubwa huweza kuambatana na;

• Mtu kuhisi hali ya kuungua

• Kubadilika rangi ya ngozi na kuwa nyekundu eneo hili la haja kubwa

• Uwepo wa michubuko au vidonda

• Kuvimba Sehemu ya haja kubwa

• Kutokea Vipele au Rashes sehemu ya haja kubwa n.k

ONANA NA DAKTARI AU WATAALAM WA AFYA KAMA;

- Miwasho sehemu ya haja kubwa ni mikali sana na haiishi au niendelevu

- Unajisaidia choo kimechanganyika na damu

- Unatokwa na haja kubwa bila kujizuia

- Unakosa usingizi kwa sababu ya miwasho

- Umepatwa na vipele,michubuko au vidonda ambavyo haviponi n.k

CHANZO CHA TATIZO HILI LA KUWASHWA SANA SEHEMU YA HAJA KUBWA

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu ambazo huweza kuchangia uwepo wa Tatizo hili;

1. Maambukizi ya magonjwa mbali mbali ikiwemo; Magonjwa ya Zinaa, Tatizo la Minyoo(pinworms), au Maambukizi ya Fangasi

2. Uwepo wa magonjwa mbali mbali ya ngozi kama vile; psoriasis,contact dermatitis au atopic dermatitis/eczema(Ukurutu/Pumu ya Ngozi) n.k

3. Msuguano mkali sehemu ya haja kubwa kutokana na kutumia vitu ambavyo hukwaruza wakati wa kujisafisha baada ya haja kubwa, mfano; kutumia karatasi ngumu,magunzi n.k

4. Tatizo la kutokwa na kinyesi bila kujizuia au tatizo la kuharisha kwa muda mrefu, hivi huweza kuchangia pia ngozi ya sehemu ya haja kubwa kuwasha

5. Swala zima la usafi pamoja na utunzaji wa ngozi ikiwemo; matumizi ya products zenye kemikali kali kama baadhi ya Sabuni wakati wa kujisafisha,

Kutumia Toilet paper au nguo za ndani zenye chembe chembe kali zilizowekwa kwenye manukato au rangi zilizotumika kutengenezea vitu hivo.

kujisafisha kwa fujo sana(washing too aggressively) n.k, vyote hivi huweza kuwa chanzo cha wewe kuanza kuwashwa sehemu ya haja kubwa

6. Sababu zingine ni pamoja na; tatizo la bawasiri au hemorrhoids, Uvimbe sehemu ya haja kubwa(anal tumors) N.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Faida za Mafuta ya Mawese(Palm Oil),Soma hapaAfyaclass Bongo Social •

 Faida za Mafuta ya Mawese(Palm Oil),Soma hapa

Leo nmekuchambulia baadhi ya faida za Mafuta ya Mawese yaani Palm Oil, na Hizi ni baadhi ya Faida hizo;

1. Kusaidia kuboresha uwezo wa macho kuona,

Hii ni kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha Beta Carotene ndani ya mafuta ya Mawese, ambacho hubadilishwa na kuwa vitamin A,

Vitamin A ni msaada mkubwa katika kuboresha afya ya macho.

2.Kusaidia Kulainisha Ngozi yako,

Hii ni kutokana na uwepo wa agents maarufu kama Re-fattening agents ambazo husaidia kurudisha mafuta asilia ya ngozi pamoja na unyevu unyevu kwenye ngozi.

3. Kusaidia Kupunguza hatari ya Saratani za aina mbali mbali,

Kuwa na kiwango kikubwa cha Antioxidants

4. Kuboresha afya na ukuaji wa nywele

5. Pia Mafuta ya Mawese hayana Trans-Fat zozote yaani ni Zero Trans-Fat,

ila Yana Unsaturated fats

6. Husaidia kuzuia hatari ya mtu kupata magonjwa mbali mbali ya Moyo

7. Mafuta ta Mawese yana kiwango kikubwa cha Vitamins mbali mbali, kama vile; Vitamin K, Vitamin D, Vitamin A, na Vitamin E

8. Mafuta ya Mawese ni msaada pia kwa mama Mjamzito,

Kutokana na wingi wa Virutubisho kama vile Vitamin D,A na E,

ambavyo ni muhimu sana kwenye afya na Ukuaji wa Mtoto tumboni.

9. Kusaidia kuupa Mwili nguvu(Energy)

10. Na Kusaidia katika urekebishaji wa vichocheo mbali mbali mwilini.

NB: Ingawa ni mara chache sana huweza kuleta madhara ila matumizi ya kiwango kikubwa zaidi kuliko kawaida cha Mafuta ya Mawese huweza kuleta madhara mbali mbali kama vile;

Kubadilisha rangi ya ngozi na kuwa ya yanjano(yellowish) na hii ni kutokana na uwepo wa kiwango kikubwa cha Carotenes.



0 Comment

LINI MAMA MJAMZITO(MAMA KIJACHO) AANZE KLINIKI?Afyaclass Bongo Social •

 LINI MAMA MJAMZITO(MAMA KIJACHO) AANZE KLINIKI?

KABLA hata mwanamke HAJABEMBA MIMBA,kama ana plan ya Kubeba MIMBA,Inashauriwa mwanamke na Mwenzi wake Wafike hospitali kwa ajili ya USHAURI na baadhi ya Uchunguzi,

lakini pia mama huyu mara moja anaanzishiwa madini kwajili ya maandalizi ya mtoto,hapa hasa ni FOLIC ACID kuzuia mtoto asije zaliwa na Magonjwa ya viungo kama Mguu kifundo,mgongo wazi,kichwa kikubwa n.k,

lakini pia kwa wenye magonjwa kama Ukimwi,presha,Homa ya ini yaani Hepatitis unaangaliwa, mfano kama Viral load Ipo chini sio risk kwa kumuambukiza mtoto na mengineyo kama ushauri wa kijumla juu ya lifestyle.

lakin sasa Kuna ile Haujajipanga,mara IMEINGIA,???

MAMA MJAMZITO ANATAKIWA AANZE CLINIC MARA TU ANAVYOGUNDUA AMEPATA UJAUZITO (umegundua una MIMBA,Plan ndani ya Wiki moja Uwe umefika Hospitali kuanza clinic na Kuonana na Dr wako)

na unatakiwa kwenda na mwenzi wako hasa kwa vipimo vya Ukimwi,hepatitis,group za damu kama Hazipo tofauti.

mfano: Unakuta mwanamke HANA MAAMBUKIZI ya VVU,mwanaume ANAYO(Discordant couple),Tukipima na kujua hili,Mnazingatia ushauri ili Kumlinda mtoto (ndio FAIDA za kuja mapema).

lakin Pia kama WOTE wanamaambukizi Pia kuna ushauri Tunatoa,Lengo ni kumlinda mtoto asizaliwe na MAAMBUKIZI.

kuna FAIDA nyingi sana za kuja kapata Uchunguzi mapema.

UMUHIMU WA MAHUDHURIO YA KLINIKI KWA MAMA MJAMZITO

➡️ Ombeni Mkumbwa

?SUMMARY
 
Kwa Ujumla wake safari ya kupata Mtoto huanza pale tu mwanamke anapokuwa Mjamzito mpaka atakapofikisha mda wa Kujifungua. Ambapo inaweza kuwa kutoka wiki 0-42 za Ujauzito.

VITU VYA MUHIMU KATIKA MAHUDHURIO YOTE KWA UJUMLA WAKE

➖ Kupata Elimu ya kutosha katika maswala mbali mbali ya afya kama vile; lishe,Usafi,Maandalizi ya Kujifungua,Dalili zahatari kipindi cha Ujauzito na mara tu baada ya kujifungua.
➖ Upimaji wa magonjwa kama Shinikizo la damu,Sukari,protein kwenye Mkojo,Malaria,Uti,Kasendwe,Ukimwi n.k
➖ Vipimo juu ya Group la damu la mama na wingi wake wa Damu
➖ Utoaji wa dawa za Kuzuia malaria maarufu kama SP,Dawa za minyoo maarufu kama Mebendazole,na vidonge vyekundu kwa ajili ya kuongeza damu,kuzuia watoto kuzaliwa na matatizo kama mgongo wazi na Vichwa vikubwa.
➖ Kuendelea kuchunguzwa maendelo ya mtoto tumboni ikiwemo,kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto,mlalo wake n.k
➖ Tarehe za matarijio ya kujifungua kujulikana pamoja na maandalizi kamili ya kujifungua
➖ Kuendelea kupata Elimu juu ya Njia sahihi za Kupanga Uzazi
➖ Uchomaji wa Chanjo zote muhimu kwa mama Mfano chanjo muhim ya kuzuia Ugonjwa wa PEPOPUNDA maarufu kama TETENUS
 
Karibu sana kusoma Makala hii na Kupata Elimu ya kutosha Juu ya Umuhimu wa Kliniki kwa Mama mjamzito

SOMO KAMILI ➡️

Mahudhurio ya Kliniki yamegawanyika katika makundi manne kulingana na Umri wa Ujauzito japo yanaweza kuzidi manne kulingana na Hali ya Ujauzito.
 
(1)Hudhurio la kwanza  ni Ujauzito kabla ya kufika wiki 16
 
(2)Hudhurio la Pili ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 20-24
 
(3)Hudhurio la Tatu ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 28-32
 
(4)Na hudhurio la Nne ni Ujauzito ukiwa na umri wa wiki 36-40
 
Nb; Mahudhurio haya yanaweza kuzidi manne kulingana na Hali ya Ujauzito,mfano mama akiwa na magonjwa mengine kama presha n.k

UMUHIMU WA MAHUDHURIO YA KLINIKI KWA MAMA MJAMZITO

(1) Mama atapewa Elimu juu ya maandalizi ya kujifungua yaani INDIVIDUAL BIRTH PREPAREDNESS (IBP),Lishe wakati wa Ujauzito,Usafi wa mwili,Kujua dalili za Hatari kwa Mjamzito,n.k
 
  ?MAANDALIZI YA KUJIFUNGUA
*Mama kujua vitu vya kuandaa mfano Pesa ya kutosha,Usafiri wa kwenda hosptal,Mtu atakayebaki na Familia pindi mama akiwa hospital, Kuweka vitu vyako pamoja kama kadi la Kliniki,nguo n.k, Kuwa na mtu atakayekupeleka hospital,Kuandaa vifaa kama gloves,makintosh,Chupi,pamba n.k  kama vitahitajika
 
?BAADHI YA DALILI ZA HATARI KWA MJAMZITO
*kutokwa na Damu ukiwa Mjamzito
*Kutokwa na uchafu wenye harufu kali ukeni hii ni dalili ya maambukizi kama Fangasi
*Miguu kuvimba kupita kiasi,mikono pamoja na Uso
*kuona Maruerue wakati wa Ujauzito
*kutokumsikia mtoto anacheza tumboni zaidi ya masaa 24 kwa mama ambaye umri wa mtoto kucheza tumboni umefika mfano kuanzia wiki 20-24. endelea kutufwatilia kujua zaidi...
*Presha kupanda na kuwa na Protein kwenye mkojo,hiki ni kiashiria kikubwa cha Ugonjwa wa Kifafa cha Mimba
 
(2) Mama mjamzito atapimwa magonjwa mbali mbali kama Ukimwi,UTI,Fangasi,PID,Kaswende,Malaria,Wingi wa Damu,Group lake la Damu, Presha, na Magonjwa mengine ya zinaa
 
(3) Mama mjamzito atasaidiwa Kujua Tarehe yake ya Matarijio kwa ajili ya kujifungua ili awe tayari.
 
(4) Mama mjamzito atachomwa chanjo ya kuzuia Tetenus kama hakuchoma
 
(5) Mama mjamzito atapewa dawa muhim sana kipindi cha Ujauzito kama Fefol au Vidonge vyekundu vya kuongeza damu kwa ajili ya kuongeza damu,kuzuia watoto kuzaliwa na vichwa vikubwa pamoja na Mgongo wazi,
 Dawa za Minyoo,Pamoja na Dawa za kuzuia ugonjwa wa Malaria
 
KUMBUKA; Baada ya kuwa Mjamzito mambo mengi hubadilika ikiwemo swala la lishe,na uvaaji- hasa kutokuvaa nguo zinazobana,au viatu virefu, na mabadiliko mbali mbali ya mwili hutokea kipindi hiki.
* Kama una tatizo lolote au kuna kitu hujakielewa usisite tuwasiliane kupitia namba +255758286584 Piga au Tuma Ujumbe utajibiwa kwa haraka.

 VIDONGE VYA KUONGEZA DAMU

Vidonge hivi ni maarufu kama vidonge vyekundu au FEFOL ikiwa kirefu chake ni Ferous and Folic acid. Vidonge hivi hutakiwa kutolewa kwa mwanamke akiwa mjamzito hadi wiki 6 au siku 42 baada ya kujifungua, japo wengine huacha tu baada ya kujifungua au wengine hata wakiwa na mimba wakipewa hawamezi wanatupa, Leo nikufungue macho juu ya Umuhimu mkubwa wa Vidonge hivi vya kuongeza damu.
Umuhimu wa Kuhudhuria Kliniki kwa Mjamzito,endelea kutufwatilia kujua zaidi.
 
UMUHIMU WA VIDONGE VYA KUONGEZA DAMU MAARUFU KAMA FEFOL AU VIDONGE VYEKUNDU
 
(1) Huongeza damu kwa mama,kwani Damu nyingi hupotea kipindi mjamzito anajifungua.
 
(2) Hupunguza Idadi kubwa ya watoto kuzaliwa na Tatizo la Mgongo wazi
 
(3) Hupunguza idadi kubwa ya watoto kuzaliwa na Tatizo la vichwa vikubwa
 
NB; VIDONGE HIVI HUSAIDIA SANA WAKATI WA UUMBAJI WA MTOTO,NA KUREKEBISHA MATATIZO MBALI MBALI AMBAYO YANAWEZA KUTOKEA KIPINDI CHA UUMBAJI WA MTOTO TUMBONI.

Soma: Chanjo Zote za Mtoto toka anazaliwa mpaka umri wa miaka Mitano

KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584






0 Comment

Ugonjwa wa fistula kwa wanaume,chanzo,dalili na TibaAfyaclass Bongo Social •

 Ugonjwa wa fistula kwa wanaume,chanzo,dalili na Tiba

Watu wengi hawajui kwamba Ugonjwa wa Fistula sio kwa Wanawake pekee, hata wanaume wanaweza kupata Ugonjwa wa Fistula,

Ugonjwa wa fistula ni nini?

Ugonjwa wa Fistula huhusisha kuwepo kwa tundu au uhusiano usio wa kawaida kati ya sehemu mbili za mwili, kama vile kiungo kimoja na kingine,mishipa ya damu,tishu na tishu n.k.

Zipo aina mbali mbali za fistula kama vile;

  • Vesicovaginal fistula(kwa wanawake)
  • Uterovaginal fistula(kwa wanawake)
  • Anal fistula(Kwa wote) n.k

Fahamu kwamba,Hata Wanaume huweza kupata Fistula, na Leo tunachambua zaidi kuhusu Ugonjwa wa fistula kwa wanaume,chanzo,dalili na Tiba yake.

Anorectal fistula ni aina ya fistula ambayo hutokea zaidi kwa wanaume kuliko kwa wanawake, Ingawa fistula aina ya anorectal inaweza kutokea kwa watu wa umri wowote na jinsia yeyote.

Chanzo cha Ugonjwa wa fistula kwa wanaume

Kama tulivyokisha kueleza wanaume hupatwa Zaidi na fistula aina ya Anorectal fistula,

na kwa asilimia kubwa aina hii ya anal fistula husababishwa na maambukizi ya vimelea vya magonjwa ambayo huanza ndani ya tezi linalojulikana kama anal gland,

Maambukizi haya husababisha jipu ambalo hutoka lenyewe au kutolewa kwa upasuaji kupitia ngozi karibu na njia ya haja kubwa.

Sababu zinazoongeza hatari ya Mtu kupata anal fistula

Sababu zinazoongeza hatari ya Mtu kupata fistula aina ya anal fistula ni pamoja na;

1. Kuwa na Jipu eneo la haja kubwa lililotolewa hapo awali

2. Kuwa na magonjwa kama vile;

  • Crohn's disease
  • Au inflammatory bowel disease n.k

3. Kuumia eneo la haja Kubwa

4. Kupata maambukizi ya vimelea vya magonjwa sehemu ya haja kubwa

5. Kufanyiwa upasuaji eneo la haja kubwa

6. Upasuaji au mionzi kwa ajili ya matibabu ya saratani ya eneo la haja kubwa(anal cancer) n.k

Dalili za anal fistula

Dalili za anal fistula ni pamoja na ;

- Kupata muwasho kuzunguka eneo la haja kubwa

- kupata maumivu eneo la haja kubwa ambayo ni endelevu na yanayozidi wakati wa;

  • kukaa,
  • kutembea,
  • kujisaidia haja kubwa
  • au kukohoa

- Kutokwa na uchafu wenye harufu mbaya eneo karibu na njia ya haja kubwa

- Kutokwa na damu au Usaha wakati wa kujisaidia haja kubwa

- Kupata Homa hasa pale ukiwa na jipu n.k

-  Eneo la kuzunguka njia ya haja kubwa kuvimba na kubadilika rangi na kuwa jekundu n.k

- Kushindwa kudhibiti haja kubwa, na kutoka pasipo kujizuia wewe mwenyewe.n.k

Matibabu ya Ugonjwa wa Fistula kwa Wanaume

Matibabu ya Ugonjwa wa Fistula hutegemea na chanzo chake, ila kwa ujumla mgonjwa huweza kupata matibabu ya;

  • Upasuaji
  • Pamoja na Dawa mbali mbali

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

Mtoto Kunywa Maji Wakati Wa KujifunguaAfyaclass Bongo Social •

 MTOTO KUNYWA MAJI WAKATI WA KUJIFUNGUA

MADHARA YA MTOTO KUNYWA MAJI YA UCHUNGU AU UZAZI

Moja ya ishara ya tatizo hili ni mtoto kutokulia baada ya kuzaliwa

Baada ya mtoto kunywa maji ya uchungu au uzazi wakati wa kuzaliwa huweza kupata madhara mbali mbali kama vile;

1. Kuziba kwa njia ya hewa ambayo huweza kusababisha tatizo la upungufu wa oxygen kwenye ubongo

2. Kuwa na matatizo ya ubongo

3. Kuwa na tatizo la upumuaji

4. Kuwa na tatizo la mapafu

5. Maambukizi ya magonjwa mbali mbali hasa baada ya mtoto kunywa maji ya uzazi ambayo yamechanganyika na kinyesi kwa kitaalam hujulikana kama meconium

6. Kupatwa na tatizo la kukakamaa mwili

7. Kulegea viungo mbali mbali vya mwili

8. Kuwa na tatizo la kuharisha

9. Kuwa na tatizo la kutapika

10. Mtoto kupatwa na tatizo la Pneumonia

N.k

Soma zaidi hapa.!!

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



 
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD