Afyaclass Bongo Social Ndugulile achaguliwa Mkurugezi Mkuu WHO Afrika

Ndugulile achaguliwa Mkurugezi Mkuu WHO Afrika

CONGO, Brazzaville – Mbunge wa Kigamboni na Naibu Waziri wa Afya wa zamani Dk Faustine Ndugulile ameshinda uchaguzi wa kiti cha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Dunia Kanda ya Afrika.

Katika Uchaguzi uliofanyika leo jijini Brazzaville nchini Congo, wajumbe 25 kati ya 46 wa Mkutano Mkuu wa 74 wa WHO uliofanyika leo wamemchagua Ndugulile na hivyo kuwashinda wagombea wengine kutoka Niger na Senegali.

Tayari Ndugulile ameweka wazi kuwa vipaumbele vyake ni kuhakikisha Watu wanapata haki ya kupata huduma bora za afya, Kuboresha utayari wa nchi za Afrika katika kukabiliana na majanga ya magonjwa ya mlipuko, Kuimarisha uwajibikaji ndani ya WHO kanda ya Afrika pamoja kuimarisha mawasiliano baina ya nchi wanachama katika masuala ya Afya.



You, Mehreen and others
Hashtag:

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD