Mwenza wa Waziri Mkuu wa Israel Sara Netanyahu ameutumia ukurasa wake wa Instagram kuwasilisha ujumbe wa upendo na amani kwa raia wa Iran kufuatia mgogoro unao endelea baina ya nchi hizo mbili akiashiria kuwa nchi hizo mbili ni ndugu na hawapaswi kuvutana.
Ujumbe huo wa Sara Netanyahu ni wito wa nchi hizo mbili ambazo zimekuwa na mzozo kuzitaka kumaliza mzozo huo akiitaja Irani kama nchi yenye utamaduni wa kipekee na utajiri wa kihistoria ambapo Israel na Irani sio maadui huku mvutano kati ya Israel na Iran unazidi kuongezeka hasa baada ya mashambulizi ya hivi karibuni.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameweka picha ya simba wawili wakiwa za nchi hizo mbili akiambatanisha ujummbe usemao “Ninyi watu wa Iran ni warithi wa utamaduni mzuri Taifa lenye vipaji na historia nzuri. Sisi si maadui zenu. Vita vyetu ni na serikali ya kidikteta inayowadhulumu, si na ninyi.
Tunaamini katika mustakabali wa amani, uhuru, na urafiki kati yetu.”
Aidha picha hiyo ya Simba waliovikwa bendera ya Israel na Iran iliyotumiwa na Sara Netanyau Chaguo la simba katika picha hiyo linaonekana kuwasilisha marejeleo ya nembo ya Iran ya zama za Shah ambaye alikuwa mfalme aliyetawala Iran hadi 1979 wakati utawala wa ayatollah wenye msimamo mkali ulipoandaa Mapinduzi ya Kiislamu.
REPLY HAPA
image quote pre code