Jaji Masaju ateuliwa kuwa Jaji Mkuu kuchukua nafasi ya Profesa Ibrahim

Jaji Masaju ateuliwa kuwa Jaji Mkuu kuchukua nafasi ya Profesa Ibrahim

#1

Jaji Masaju ateuliwa kuwa Jaji Mkuu kuchukua nafasi ya Profesa Ibrahim



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani, George Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Jaji Masaju anachukua nafasi ya Jaji Profesa Ibrahim Juma ambaye amestaafu rasmi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari leo Ijumaa, Juni 13, 2025, Jaji Masaju ataapishwa Juni 15, 2025 katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Kabla ya uteuzi huo, Jaji Masaju amewahi kushika nafasi mbalimbali ikiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Pia, aliwahi kuwa mshauri wa masuala ya kisheria wa Rais mstaafu wa awamu wa nne, Jakaya Kikwete.

REPLY HAPA


image quote pre code