Tatizo la mimba kuharibika,Sababu kubwa ni hizi hapa

Tatizo la mimba kuharibika,Sababu kubwa ni hizi hapa

#1

Tatizo la mimba kuharibika,Sababu kubwa ni hizi hapa



Zifuatazo ni Baadhi ya Sababu Zinazochangia Kutokea kwa Tatizo hili la Mimba kuharibika au kutoka Zenyewe;

1. Matatizo yanayotokana na Mfumo mzima wa Kijenetiki ambapo kitaalam hujulikana kama-Genetics Abnormalities,tatizo hili huchangia mimba kuharibika hasa hasa katika kipindi cha Miezi mitatu(3) ya Mwanzoni.

2. Matatizo katika Via vya Uzazi vya Mwanamke kama Vile;

  • Kulegea kwa shingo ya kizazi hivo kushindwa kuhimili kushikilia ujauzito hatimaye ujauzito kutoka wenyewe, 
  • Matizo kama Vile Uvimbe kwenye kizazi n.k

3. Tatizo la Mvurugiko wa Vichocheo vyako vya Mwili ambapo kitaalam hujulikana kama Hormone Imbalance

4. Uwepo wa Magonjwa mbali mbali kipindi cha Ujauzito kama vile; 

  • Ugonjwa wa kisukari, 
  • Kifafa cha Mimba,
  • Shinikizo la Damu,
  • Ugonjwa wa Goita
  • Pamoja na maambukizi mengine kama vile ya Rubella.

5. Matumizi ya baadhi ya dawa ambazo ni hatari kipindi cha Ujauzito kama vile,

  • matumizi ya dawa za Msongo wa mawazo mfano; paroxetine au venlafaxine

TABIA HATARISHI ZA KUPATA TATIZO LA MIMBA KUTOKA ZENYEWE

- Matumizi ya vilevi kama vile Pombe

- Uvutaji wa Sigara

- Matumizi ya vinywaji venywe Caffeine Nyingi

- Matumizi ya Dawa kiholela au Ovio bila kupewa maelekezo na wataalam wa afya n.k.

KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

REPLY HAPA


image quote pre code