Dalili za Tatizo la Acid reflux,chanzo na Tiba
Tatizo hili hutokea pale ambapo Acid kutoka Tumboni hupanda juu kwenye mrija unaounganisha tumbo na Mdomo yaani esophagus,
Hali hii ya acid kupanda juu kutoka tumboni ndyo huanza kuleta shida mbali mbali.
Dalili za acid reflux
DALILI ZA TATIZO HILI NI PAMOJA NA;
– Mtu kuhisi Kiungulia(heartburn) mara kwa mara, hasa baada ya Kula, ambapo huzidi sana wakati wa Usiku au wakati wowote ukiwa umelala
– Mtu kupata shida ya chakula alichomeza au kinywaji alichokunywa kupanda juu au kurudi mdomoni yaani regurgitation
– Mtu Kupata maumivu ya tumbo juu ya kitovu karibu na mbavu au kupata maumivu ya Kifua(kichomi)
– Mtu kupata shida ya Kumeza Kitu yaani dysphagia
– Mtu kuhisi kama kuna kitu kimebakia Kooni
– Wakati mwingine unaweza kupata kikohozi ambacho hakiishi,hasa kama shida hii ya Acid Reflux hutokea wakati wa Usku
- Kama una tatizo la Pumu,Hali inaweza kuwa mbaya Zaidi.
JE,UNA TATIZO HILI NA HUJAPATA TIBA?
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE +255758286584.
Karibu kwenye Afyaclass WhatsApp Channel
Jiunge nasi leo na upate elimu ya afya kwa lugha nyepesi, kila siku moja kwa moja kwenye WhatsApp yako.
- 🩺 Ushauri wa kitaalamu wa afya
- 🍲 Lishe bora kwa familia
- 🤰 Elimu ya afya ya mama na mtoto
- 🌿 Tiba rahisi na ushauri wa kiafya
Elimu hii ni Muhimu sana. Boresha afya.
Tafuta msaada wa matibabu mara moja ikiwa una maumivu ya kifua, hasa ikiwa pia unabanwa na pumzi, au unapata maumivu ya taya au mkono. Hizi zinaweza kuwa dalili za matatizo mengine kama vile mshtuko wa moyo.
VITU HIVI HUONGEZA HATARI YA MTU KUPATA TATIZO LA ACID REFLUX
1. Mtu kuwa na Uzito mkubwa kupita kiasi(Overweight/Obesity)
2. Mwanamke Kuwa Mjamzito
3. Mtu kuwa na tatizo la tumbo kuchelewa kutoa vitu ikiwemo chakula kwenda sehemu zingine yaani Delayed stomach emptying
4. Uvutaji wa Sigara
5. Mtu kula chakula kingi sana kwa wakati mmoja
6. Mtu kuchelewa sana kula chakula wakati wa Usku
7. Kula aina ya vyakula kwa kiwango kikubwa sana,mfano vyakula vya mafuta mengi n.k
8. Mtu kunywa Pombe au Kahawa mara kwa mara
9. Kuwa na matatizo ya Connective tissues kama vile scleroderma
10. Matumizi ya baadhi ya Dawa mara kwa mara,mfano Asprin n.k
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





.jpeg)




image quote pre code