Afyaclass Bongo Social Takribani watu 63 wamethibitishwa kufariki dunia kwa ajali ya Basi Uganda

Takribani watu 63 wamethibitishwa kufariki dunia na wengine kujeruhiwa kwa ajali iliyohususha magari manne katika Barabara ya Kampala na mji wa Gulu.

Ajali hiyo iliyotokea Jumatano asubuhi,katika Kijiji cha Kitaleba, ilihusisha mabasi mawili, Lori na Gari ndogo aina ya Toyota Land Cruiser, kwa mujibu wa ripoti ya awali ya polisi.

Idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka kutokana na baadhi ya abiria kujeruhiwa vibaya.

“Inaelezwa kuwa basi lililokuwa likitoka Kampala lilikuwa likilipita lori na basi jingine lililokuwa likielekea Kampala lilikuwa likiipita gari ndogo ya Toyota Land Cruiser, lakini lilishindwa kufanya hivyo kwani tayari basi lililokuwa likitoka Kampala lilikuwa limekaribia’’. Taarifa ya polisi imeeleza.

You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD