Uchovu bila sababu ya moja kwa moja,Fanya haya

Uchovu bila sababu ya moja kwa moja,Fanya haya

#1

Uchovu bila sababu ya moja kwa moja unaweza kutokana na mambo mengi — kimwili, kiakili au hata kihisia. Hata kama haujaumwa, mwili unaweza kuwa unahitaji marekebisho madogo ya mtindo wa maisha. Haya ni mambo muhimu ya kufanya:

 1. Kunywa maji ya kutosha

Upungufu wa maji mwilini husababisha uchovu, kizunguzungu n.k.

Kunywa glass 6–8 za maji kwa siku, au zaidi ikiwa unafanya kazi ngumu au unaishi kwenye joto.

2. Pata usingizi wa kutosha

Jitahidi upate muda kulala angalau saa 7–9 za usingizi wa usiku kila siku.

Epuka simu au TV dakika 30 kabla ya kulala.

Lala na uamke saa zilezile kila siku.

3. Kula lishe bora

Epuka vyakula vyenye sukari nyingi na mafuta mengi.

Ongeza matunda, mboga, nafaka kamili, samaki, na protini safi.

Usiruke milo – hasa kiamsha kinywa.

 4. Fanya mazoezi mepesi

Tembea dakika 20–30 kila siku.

Mazoezi husaidia kuongeza nguvu na kuboresha mzunguko wa damu.

Hata kunyoosha (stretching) husaidia.

5. Punguza msongo wa mawazo (stress)

Tumia muda kupumzika, kusali, kutafakari, au kusikiliza muziki unaotuliza.

Ongea na mtu unayemwamini kuhusu hisia zako.

6. Kagua afya yako

Ikiwa uchovu unaendelea kwa zaidi ya wiki kadhaa, tafuta daktari.

Sababu za kiafya zinazoweza kusababisha uchovu ni pamoja na:

  • Upungufu wa damu (anemia)
  • Thyroid kushindwa kufanya kazi vizuri
  • Kisukari
  • Shida ya usingizi (sleep apnea)
  • Magonjwa kama Malaria,UTI n.k.
  • Stress,depression,anxiety n.k.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code