Super Eagles ya Nigeria iliishinda Tunisia 3-2 na kufuzu kwa Raundi ya 16 ya AFCON
Super Eagles ya Nigeria imefuzu kwa raundi ya 16 ya Kombe la Mataifa ya Afrika linaloendelea nchini Morocco.
Nyota hao wa Nigeria waliishinda Tunisia 3-2 Jumamosi usiku katika Uwanja wa Fez kwa mabao kutoka kwa Victor Osimhen, Wilfried Ndidi, na Ademola Lookman, na kuhakikisha timu hiyo inafuzu kutoka kundi lao.
Victor Osimhen alifungua bao dakika ya 44 kupitia krosi kutoka kwa Ademola Lookman kabla ya mapumziko. Katika dakika ya 50, nahodha wa timu hiyo, Widfred Ndidi alifunga bao la pili dakika ya 50, akisaidiwa tena na Lookman.
Lookman aliongeza bao la tatu dakika ya 70, kufuatia pasi ya Osimhen.
Wakati huo huo, Tunisia ilifanikiwa kupata bao moja kupitia Montassar Talbi, kabla ya penalti ya dakika za mwisho kufungwa na Ali Al-Abdi.
Matokeo hayo yanamaanisha kuwa Nigeria ina pointi sita kutokana na mechi mbili, huku Tunisia ikibaki ya pili ikiwa na pointi tatu.









image quote pre code