Wanafunzi wa FORM 3 waliwasha moto GODORO,Moto ukawaka,Shule Ikaungua
Waziri wa Elimu Julius Ogamba ametoa taarifa mpya kuhusu moto wa kusikitisha uliotokea Utumishi Girls Academy huko Gilgil, Nakuru County
Wanafunzi 16 wamepoteza maisha huku wengine 79 wakijeruhiwa na saba kati yao bado wamelazwa hospitalini
Moto huo sasa umethibitishwa kuwa wa makusudi na wanafunzi wanane kwa sasa wako chini ya uchunguzi
Inadaiwa walimu wawili walikuwa wamepewa taarifa na baadhi ya wanafunzi wa Form 3 kuhusu mipango ya vurugu lakini hawakuchukua hatua stahiki kuzuia shambulizi hilo la moto
Hatua zilizochukuliwa hadi sasa na Wizara ya Elimu:
1.Bodi ya Usimamizi wa shule imevunjwa rasmi
Mkuu wa shule pamoja na walimu walioshindwa kuchukua hatua watachukuliwa hatua za kinidhamu na TSC
2.Uchunguzi zaidi bado unaendelea huku maafisa wa DCI wakirekodi taarifa na kuchunguza ushahidi
3.Maafisa wa DCI wamewakamata wasichana wanane wa Utumishi Girls Senior Secondary School kufuatia mkasa wa moto ulioua wanafunzi 16 siku ya Alhamisi, tarehe 28 Mei 2026
Timu za forensic zinaendelea kuchunguza namna moto ulivyoenea , kemikali zilizotumika, mifumo ya umeme pamoja na picha za CCTV
Walionusurika wanadai baadhi ya wanafunzi wa kidato cha tatu waliwasha godoro moto kwa makusudi ndani ya bweni la Meline Waithera huku mlango mkuu na emergency exit zikidaiwa kufungwa kutoka ndani, jambo lililowanasa waathiriwa. Post Via kwa Mdau wetu....



Post a Comment