Showing posts with label Cameroon People’s Democratic Movement (CPDM). Show all posts
Showing posts with label Cameroon People’s Democratic Movement (CPDM). Show all posts

Rais Paul Biya wa Cameroon ametangaza rasmi kuwa atawania tena kiti cha UraisAfyaclass Forum •

Rais Paul Biya wa Cameroon ametangaza rasmi kuwa atawania tena kiti cha Urais wa Nchi hiyo kwa muhula wa nane (8) katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.



Tangazo la uamuzi huo amelitoa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X akisema atakuwa Mgombea katika uchaguzi wa Oktoba 12 kupitia Chama chake cha Cameroon People’s Democratic Movement (CPDM) ambacho yeye ndiye Mwenyekiti wake.

Biya ambaye kwa sasa ana umri miaka 92, ameitawala Cameroon kwa miaka 43 ambapo hata hivyo kwenye miaka ya hivi karibuni hali dhaifu ya afya yake imekuwa chanzo cha mjadala Nchini humo.

Washirika wake wawili wa zamani wamejitenga naye na sasa wanawania pia kiti cha Urais ikiwemo Waziri Mkuu wa zamani Bello Bouba Maigari atakayekuwa Mgombea wa Chama cha NUDP.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD