Showing posts with label Elon Musk. Show all posts
Showing posts with label Elon Musk. Show all posts

Elon Musk afikia Utajiri wa dola za Marekani bilioni 600 sawa na Quadrilion 1.4Afyaclass Forum •

Mjasiriamali na bilionea wa teknolojia Elon Musk ameandika historia mpya baada ya kuwa mtu wa kwanza duniani kufikia utajiri wa dola za Marekani bilioni 600 sawa na Quadrilion 1.4, kulingana na takwimu za Forbes.

Hatua hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni yake ya anga, SpaceX, ambayo imezindua mpango wa kuuza hisa unaothamini kampuni hiyo kufikia dola bilioni 800  ongezeko kubwa kutoka dola bilioni 400 zilizokuwepo mwezi Agosti.

Musk, ambaye anamiliki takriban asilimia 42 ya SpaceX, amenufaika moja kwa moja na ongezeko hilo la thamani. Utajiri wake umeongezeka kwa dola bilioni 168, na kufikia takriban dola bilioni 677 kufikia siku ya jana Jumatatu.

Kwa mafanikio haya, Musk anakuwa mtu wa kwanza katika historia ya dunia kufikia kiwango hicho cha utajiri. Kulingana na rekodi za Forbes, hakuna mtu mwingine aliyewahi kufikia hata dola bilioni 500 hapo awali.

0 Comment

Elon Musk anaweza kuwa trillionaire wa kwanza duniani Afyaclass Forum •

Elon Musk anaweza kuwa trillionaire wa kwanza duniani huku wanahisa wa Tesla wakiidhinisha kifurushi chake cha malipo cha dola trilioni 1 ili kuboresha chapa hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla na mtu tajiri zaidi duniani alishinda kura ya wanahisa Alhamisi, na kumhakikishia hisa zenye thamani ya dola trilioni 1 ikiwa atafikia malengo fulani ya utendaji katika muongo mmoja ujao, kulingana na Mail Online.

Kura hiyo ilifuatia wiki kadhaa za mjadala kuhusu rekodi yake ya usimamizi katika kampuni ya kutengeneza magari ya umeme na kama kuna mtu yeyote aliyestahili malipo hayo ambayo hayajawahi kutokea.

Mwishowe, zaidi ya asilimia 75 ya wanahisa waliokuwepo katika makao makuu ya kampuni hiyo huko Austin, Texas walipiga kura kuunga mkono mpango huo.

0 Comment

Elon Musk kujiuzulu Ukurugenzi wa Tesla ikiwa kifurushi cha dola trilioni 1 hakitaidhinishwaAfyaclass Forum •

Elon Musk anaweza kujiuzulu kama Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla ikiwa kifurushi chake cha malipo cha dola trilioni 1 hakitaidhinishwa, kulingana na onyo la hivi karibuni kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tesla Robyn Denholm.


Rufaa ya dharura ilitumwa katika barua kwa wanahisa wa kampuni kubwa ya magari ya umeme Jumatatu, Oktoba 27, kabla ya mkutano wa kila mwaka wa Novemba 6 ambapo wawekezaji wamepangwa kupiga kura kuhusu pendekezo kubwa la malipo ambalo halijawahi kutokea.

Onyo hilo linakuja huku kampuni mbili kuu za ushauri wa wakala, Glass Lewis na Institutional Shareholder Services, zikiwahimiza sana wanahisa kupiga kura dhidi ya fidia iliyopendekezwa.

Washauri wa wakala wana ushawishi mkubwa, haswa kwa wawekezaji wakubwa wa taasisi na wa mfuko ambao wanamiliki hisa kubwa katika Tesla.

Mpango wa malipo wenye utata umeundwa ili kumhifadhi na kumtia moyo Musk, ukimtia moyo kuongoza Tesla kwa angalau miaka mingine saba na nusu, Denholm alisema katika barua yake. Alisisitiza kwamba uongozi wa Musk ni "muhimu" kwa mafanikio ya kampuni, akionya kwamba bila motisha zinazofaa,
0 Comment

Utajiri wa Elon Musk Washuka kwa kiasi cha dolla billion 15Afyaclass Forum •

Utajiri wa Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla na SpaceX, Elon Musk, umepungua kwa kiasi cha dola bilioni 15 kwa siku ya leo pekee baada ya hisa za kampuni ya Tesla kuporomoka kwa karibu asilimia 7 na kushuka kwa takriban dola 21.



Kulingana na Bloomberg Billionaires Index, imesema licha ya kupungua kwa kiwango hicho cha fedha Musk bado anaongoza kwa utajiri duniani.

Tukio hili linajiri baada ya Musk kuzindua chama chake kipya cha kisiasa hatua ambayo inaongeza moto kwenye mgogoro wake wa hadharani na Rais wa Marekani, Donald Trump, ambaye Musk alimuunga mkono kwa kiasi kisichopungua dola milioni 277 katika kampeni za uchaguzi wa urais wa mwaka 2024.

Hali ya hisa za Tesla imekuwa mbaya tangu kuapishwa kwa Trump Januari 2025, ambapo thamani ya kampuni hiyo imeshuka kwa asilimia 31, wakati S&P 500 ikiongezeka kwa karibu asilimia 4 katika kipindi hicho hicho.

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni, Tesla pia imekumbwa na kushuka kwa mfululizo kwa utoaji wa magari katika robo mbili za mwanzo wa mwaka 2025, hali ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu mwaka 2022.

0 Comment

Elon Musk atangaza kuanzisha chama chake kipya cha Kisiasa,America PartyAfyaclass Forum •

Bilionea na mkurugenzi wa kampuni ya Tesla na X (zamani Twitter), Elon Musk, ametangaza kuanzisha chama kipya cha siasa kinachoitwa America Party  akisema lengo lake ni kurudisha uhuru kwa wananchi wa Marekani ambapo hatua hii ikiwa ni ya kujibu hali ya kisiasa ambayo kwa maoni yake inafanya kazi kama mfumo wa chama kimoja.



Tangazo hilo limekuja baada ya kufanya kura mtandaoni kupitia jukwaa lake la X ambapo zaidi ya Watu milioni moja walipiga kura na asilimia 65 wakaunga mkono kuanzishwa kwa chama hicho na Musk ameeleza kuwa chama hicho hakitalenga kugombea urais bali kitawania viti vichache katika Bunge la Marekani ili kuleta ushawishi wa kweli kwenye mchakato wa kutunga sheria.

Elon Musk pia amedokeza kuwa chama hicho kitaweka mkazo katika kupunguza matumizi ya serikali, kupambana na urasimu na kulinda uhuru wa Raia, ingawa hajaeleza kwa undani sera rasmi za chama hicho kwa sasa ila Watu wengi wameona hatua hii kama muendelezo wa tofauti zake za wazi na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Hata hivyo inaonekana chama kipya kitaingia kwenye changamoto kubwa hasa kutokana na mfumo wa Marekani wa vyama viwili vikuu (Democrat na Republican) ambapo ni vigumu kwa chama kipya kupata nafasi ya kujiimarisha kitaifa na hadi sasa haijajulikana ni wanasiasa gani au Watu mashuhuri watakaojiunga naye.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD