Showing posts with label Jukwaa la Tafiti(Research). Show all posts
Showing posts with label Jukwaa la Tafiti(Research). Show all posts

Vifo vya Wajawazito vyapungua kwa Asilimia 78 Mkoani ArushaAfyaclass Forum •


KATIKA kipindi cha miaka minne ya uongozi wa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, mkoa wa Arusha umefanikiwa kupunguza vifo vya wajawazito kwa asilimia 78, kutoka vifo 50 mwaka 2021 hadi vifo 11 mwaka 2025.



Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi, amesema hayo Julai 20 jijini Dodoma, wakati akieleza mafaniko ya mkoa huo katika kipindi cha uongozi wa serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari.

“Uboreshaji wa huduma za afya umerahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha na kuwezesha kupunguza vifo vya wajawazito kwa asilimia 78, kutoka vifo 50 (2021) hadi vifo 11 mwaka (2025).

Miongoni mwa wanahabari kwenye mkutano huo“Lakini vifo vya watoto chini ya miaka mitano vimepungua kutoka 859 mwaka 2021 hadi vifo 117 mwaka 2025 sawa na asilimia 86.4,”amesema Kihongosi

Amesema, pia kuanzishwa kwa Mfumo wa Rufaa wa M-Mama, kumesaidia jumla ya akina mama wajawazito 1,332 kujifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, amesema mkoa umetekeleza programu ya elimu bila malipo kwa gharama ya Sh. bilioni 168.2 wanafunzi walionufaika imeongezeka kutoka wanafunzi 390,910 (2021) hadi 430,511 (2025).

0 Comment

Utafiti mpya Unywaji wa pombe na kuongezeka kwa hatari ya saratani ya kongoshoAfyaclass Forum •

Utafiti mpya Unywaji wa pombe na kuongezeka kwa hatari ya saratani ya kongosho



Muungano mkubwa wa kimataifa wa tafiti unaoongozwa na watafiti kutoka Shirika la Kimataifa la Utafiti juu ya Saratani (IARC) ambalo ni shirika tanzu la Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO na taasisi wadau, wamechunguza uhusiano kati ya unywaji wa pombe na hatari ya kupata saratani ya kongosho.

Taarifa iliyochapishwa leo Mei 26 jijini Lyon, France inafafanua kwa matokeo, yaliyochapishwa katika jarida la PLOS Medicine, yanaonesha uhusiano mdogo lakini muhimu kati ya matumizi ya pombe na hatari ya saratani ya kongosho, bila kuathiriwa na jinsia au hali ya uvutaji sigara.

Tathmini hiyo ilikusanya data kutoka kwa vikundi 30 vya watu waliokusanywa kutoka mabara manne (Asia, Australia, Ulaya, na Amerika Kaskazini). Vikundi hivyo vilihusisha takriban watu milioni 2.5 ambao hawakuwa na saratani mwanzoni mwa utafiti, waliosajiliwa kati ya mwaka 1980 na 2013 wakiwa na wastani wa umri wa miaka 57. Katika kipindi cha wastani cha ufuatiliaji wa miaka 16, kesi 10,067 za saratani ya kongosho ziliripotiwa.

“Unywaji wa pombe unajulikana kuwa sababu ya kusababisha saratani, lakini hadi sasa ushahidi wa kuhusiana kwake moja kwa moja na saratani ya kongosho umekuwa haueleweki vyema,” anasema Dkt. Pietro Ferrari, Mkuu wa Kitengo cha Lishe na Kimetaboliki katika IARC na mwandishi mkuu wa utafiti huo. “Matokeo yetu yanatoa ushahidi mpya kuwa saratani ya kongosho huenda ikawa aina nyingine ya saratani inayohusiana na matumizi ya pombe, uhusiano ambao umeonekana kupuuzwa hadi sasa.”

Matokeo muhimu

Tafiti za awali za matarajio zimependekeza kuwa pombe inaweza kuwa na athari mbaya katika kusababisha saratani ya kongosho, hasa pale matumizi yanapozidi gramu 30 za ethanoli kwa siku (g/siku), sawa na karibu vinywaji viwili vya kawaida vya pombe kwa siku.

Katika utafiti huu mpya, ilibainika kuwa kila ongezeko la 10 g/siku katika matumizi ya pombe lilihusishwa na ongezeko la asilimia 3 ya hatari ya kupata saratani ya kongosho.

Kwa kina zaidi, kwa wanawake, ikilinganishwa na unywaji wa pombe wa 0.1–5 g/siku (matumizi madogo), matumizi ya 15–30 g/siku yanahusishwa na ongezeko la asilimia 12 ya hatari ya saratani ya kongosho. Kwa wanaume, ikilinganishwa na unywaji wa pombe wa 0.1–5 g/siku, matumizi ya 30–60 g/siku yanahusishwa na ongezeko la asilimia 15, huku matumizi ya zaidi ya 60 g/siku yakihusishwa na ongezeko la asilimia 36 ya hatari ya saratani hiyo.

“Pombe mara nyingi hutumiwa pamoja na tumbaku, jambo ambalo limezua maswali kuhusu ikiwa uvutaji sigara unaweza kuchanganya uhusiano huu,” anaongeza Dkt. Ferrari. “Hata hivyo, uchambuzi wetu ulionesha kuwa uhusiano kati ya pombe na hatari ya saratani ya kongosho uliendelea kuonekana hata kwa watu wasiovuta sigara, ikimaanisha kuwa unywaji wa pombe peke yake ni sababu huru ya hatari ya kupata saratani ya kongosho.”

Saratani ya Kongosho: Tatizo linalokua kiwango cha kimataifa

Saratani ya kongosho imeibuka kuwa changamoto kubwa ya afya ya umma katika miaka ya hivi karibuni. Ingawa ni aina ya 12 ya saratani kwa uwingi duniani, mwaka 2022 ilichangia karibu asilimia 5 ya vifo vyote vinavyohusiana na saratani duniani, kutokana na kugunduliwa kwa kuchelewa na kiwango kikubwa cha vifo.

Viwango vya kuugua na kufariki kutokana na saratani ya kongosho barani Ulaya, Amerika Kaskazini, Australia na New Zealand, na Asia ya Mashariki ni mara 4–5 zaidi ya maeneo mengine. Licha ya maendeleo katika matibabu ya saratani, bado kuna mafanikio machache katika kuokoa maisha ya waathiriwa wa saratani ya kongosho.

“Ingawa kuna sababu kadhaa zinazojulikana kama vile matumizi ya tumbaku, unene wa kupindukia, uvimbe sugu wa kongosho, na kisukari, sababu za saratani ya kongosho bado hazieleweki vyema. Utafiti huu unatoa uelewa mpya kuhusu nafasi ya unywaji wa pombe katika mwanzo wa saratani ya kongosho,” anasema Dkt. Ferrari. “Utafiti zaidi unahitajika ili kuelewa vyema nafasi ya matumizi ya pombe katika maisha yote, kwa mfano wakati wa ujana, na athari za mifumo mahususi ya matumizi kama vile unywaji wa pombe kupita kiasi kwa mara moja (binge drinking).”

0 Comment

Viwango vya kemikali zenye sumu katika mchele kuongezekaAfyaclass Forum •

Viwango vya kemikali zenye sumu katika mchele kuongezeka



Mchele ni chakula kikuu kwa zaidi ya nusu ya Idadi ya watu duniani. Hutumiwa kila siku na watu wengi zaidi kuliko ngano au mahindi.

Na tafiti za hivi karibuni zinaonyesha,kadiri uzalishaji wa kaboni unavyoongezeka, na joto kuongezeka duniani, viwango vya kemikali zenye sumu katika mchele huongezeka.

Uwepo wa kemikali hizi katika mchele umejulikana kwa muda mrefu kuwa tatizo.

Karibu mchele wote una kemikali yenye sumu. Kemikali hii inayotokea kiasili inaweza kujilimbikiza kwenye udongo wa mashamba ya mpunga, na kuchafua nafaka za mpunga zinazolimwa.

Lakini kiasi kinachopatikana katika nafaka za mchele kinaweza kutofautiana kwa kiasi kikubwa, kutoka chini ya mipaka inayopendekezwa na mashirika ya udhibiti hadi viwango vya juu zaidi.

Nchini Brazil,kwa kawaida uwepo wa kemikali za sumu katika mchele si tatizo.

Kemikali yenye sumu katika mchele husababisha hatari kiafya, hasa kwa sababu ya mabadiliko ya tabianchi.

Mamlaka ya Kitaifa ya Usimamizi wa Afya ya Umma ya Brazil (Anvisa) inaeleza kuwa kwa kuwa kemikali hizi hupatikana kwa asili katika ardhi, inaweza pia kuwepo kwenye maji na vyakula.

Kwa sababu hiyo, kuna kikomo cha juu kilichowekwa kisheria kuhusu kiasi cha sumu hiyo kinachokubalika kwenye chakula.

Kiwango cha juu cha kemikali hiyo kinachoruhusiwa nchini Brazil ni:

0.20 mg kwa kila kilo ya mchele mweupe

0.35 mg kwa kila kilo ya mchele wa brown (mchele wa maganda)

Bruno Lemos Batista, profesa wa kemia katika Chuo Kikuu cha Shirikisho cha ABC (UFABC), mmoja wa watafiti wa kwanza kuchunguza kuhusu kemikali hii katika vyakula nchini Brazil, anasema kuwa tafiti zake za hivi karibuni zinaonyesha kuwa viwango vya arseniki viko ndani ya mipaka ya kimataifa na ya sheria ya Brazil.

Tathmini ya mwisho ya Anvisa ilifanyika mwaka 2023, na pia ilibaini kuwa hali ilikuwa ya kawaida.

Hata hivyo, Lemos anaonya kwamba hata kiasi kidogo cha kemikali yenye sumu isiyo ya kikaboni kinachopatikana kupitia chakula au maji ya kunywa kinaweza kusababisha; Saratani,Magonjwa ya moyo na hata Kisukari.

Anasema pia kuwa, "kama tungeweka kiwango sifuri cha arseniki katika vyakula, huenda tusingekuwa na chakula kabisa cha kutufaa kula." Kwa sasa, viwango vilivyowekwa kwa mchele vinahusishwa na matukio machache sana ya magonjwa yanayosababishwa na kemikali hiyo.

"Hii hupunguza hatari na kuruhusu matumizi ya mchele, lakini hatari bado ipo," anaongeza Lemos.

Watafiti duniani kote wanaendelea kutafuta mbinu za kupunguza kemikali yenye sumu kwenye mchele.

Wakati huo huo, kuna njia za kupika mchele zinazoweza kusaidia kuondoa sehemu ya kemikali hiyo hatari kwenye nafaka.

Lakini tafiti mpya kuhusu mkusanyiko wa arseniki isiyo ya kikaboni zimeonesha kuwa tatizo linaweza kuongezeka kutokana na mabadiliko ya tabianchi.

Watafiti walipanda aina 28 tofauti za mchele katika maeneo manne tofauti nchini China, chini ya hali ya majaribio kwa kipindi cha miaka 10.

Waligundua kuwa viwango viliongezeka kadri viwango vya hewa ya kaboni (CO₂) kwenye anga na joto la dunia vilivyoongezeka.

Baadaye, wataalamu wa magonjwa walichunguza mwenendo wa kisayansi kuonesha jinsi viwango hivyo vya kemikali yenye sumu vinavyoweza kuathiri afya ya watu kwa kuzingatia matumizi ya sasa ya mchele.

Walibaini kuwa ongezeko hilo la viwango vya kemikali yenye sumu linaweza kusababisha hadi kiasi cha watu milioni 19.3 kupata ugonjwa wa saratani nchini China pekee.

0 Comment

Sababu za kuosha Miguu kila Siku,Fahamu hapaAfyaclass Forum •

Sababu za kuosha Miguu kila Siku,Fahamu hapa

Baadhi ya watu husugua miguu yao kila siku, huku wengine wanapendelea kumwagia maji miguu inatosha.



Lakini, je, unatunza miguu yako vya kutosha?

Unapoingia bafuni kuoga, ni kawaida kuna sehemu ambazo huziangazia zaidi na hata kuna baadhi ya viungo havipati maji ya kutosha au hupendelei kuosha.

Hata hivyo, wataalamu wanasisitiza kuwa miguu inahitaji umakini wa kutosha.

Huduma ya Afya ya Kitaifa ya Uingereza (NHS) na Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Marekani (CDC) wanashauri kuosha miguu kila siku kwa sabuni na maji.

Sababu moja ya kufanya hivyo ni kuzuia harufu mbaya. Nyayo za miguu zina tezi nyingi za jasho, zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote ya mwili.

Ingawa jasho lenyewe halina harufu, lina mchanganyiko wa virutubishi vinavyoweza kuleta bakteria kwenye ngozi yako.

"Mguu, hasa katikati ya vidole, ni mazingira ya unyevu, joto na giza, ambayo hufanya kuwa sehemu bora kwa vijidudu kuishi," anasema Holly Wilkinson, mhadhiri wa uponyaji wa majeraha katika Chuo Kikuu cha Hull. 

Zaidi ya hayo, wengi wetu huvaa viatu na soksi, hivyo hufungia unyevu ndani.

Hii ikiwa mojawapo ya sababu kwanini unapaswa kuosha miguu yako.

Kwa mujibu wa wataalamu, miguu yetu inajumuisha aina nyingi za bakteria na fangasi.

Walakini kwa sababu nyayo za miguu yako zimejaa vijidudu, hiyo haimaanishi kwamba lazima iwe na harufu au kwamba kuna chochote cha kuwa na wasiwasi.

Kama kawaida, sio idadi tu, lakini pia kuna aina ya bakteria ambayo ni muhimu.

Wakati mwingine, bakteria aina ya Staphylococcus ndiyo husababisha harufu ya miguu kwa kutengeneza kemikali zinazozalisha harufu mbaya.

Katika utafiti mmoja, watafiti waligundua kuwa kuosha miguu mara mbili kwa siku hupunguza sana idadi ya bakteria, wakati wale wanaoosha mara moja kwa siku au baada ya siku mbili, wanakutana na bakteria wengi zaidi.

Katika utafiti mmoja wa 2014, watafiti walichunguza miguu ya watu 16 na kugundua kuwa asilimia 98.6% ya bakteria waliopo kwenye nyayo walikuwa Staphylococci.

Hata hivyo, si kila bakteria kwenye miguu husababisha matatizo.Baadhi yao ni muhimu kwa afya ya ngozi yetu.

Bakteria kama Staphylococcus huunda asidi zinazohusika na harufu ya miguu.

Hata hivyo, kusafisha miguu mara kwa mara husaidia kuzuia magonjwa ya ngozi kama vile maambukizo ya fangasi, ambao husababishwa na fangasi zinazokua kwenye mazingira zenye unyevu unyevu.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD