Showing posts with label Mafuriko kutokana na mvua kubwa. Show all posts
Showing posts with label Mafuriko kutokana na mvua kubwa. Show all posts

Idadi ya waliokufa kutokana na mafuriko ya Texas yafikia 50Afyaclass Forum •

Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na mafuriko makubwa yaliyoyakumba 



Taarifa hiyo imetolewa na maafisa wa jimbo hilo wakati juhudi za uokoaji zikiendelea, huku makumi ya wasichana wakiwa bado hawajulikani walipo.Kwa mujibu wa takwimu zilizokusanywa na Shirika la Habari la AFP kutoka kwa maafisa wa maeneo husika, kaunti ya Kerr ndiyo iliyoathirika zaidi, ikiripoti vifo 43. 

Kaunti ya Travis imethibitisha vifo vinne, Burnet watu wawili, na mtu mmoja amefariki katika kaunti ya Tom Green. Kufuatia hali hiyo, Gavana wa Texas Greg Abbott ametangaza rasmi hali ya maafa, akilitaja tukio hilo kuwa "janga lisilo la kawaida.” 

Rais wa Marekani Donald Trump naye, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, amesema yeye na mkewe Melania wamekuwa wakiwaombea familia zote zilizoathirika na mkasa huo mkubwa.

0 Comment

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA Afyaclass Forum •

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA 

Kama unaishi mikoa ya Morogoro, Lindi, Iringa, Mtwara, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma, basi kaa mguu sawa kwani Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo kuhusu uwepo wa hali mbaya ya hewa kwa siku tano.

Utabiri huo unakuja siku chache tangu baadhi ya mikoa kama Dar es Salaam na Morogoro kushuhudia mvua kubwa iliyoathiri miundombinu na kusababisha vifo.

Utabiri huo wa TMA uliotolewa leo Januari 29,2024 utaanza kesho Januari 30 na utadumu hadi Februari 2 mwaka huu.

“Angalizo la mvua kubwa limetolewa katika maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Lindi, Mtwara, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma,”imeandikwa kwenye taarifa hiyo.

Wakazi katika mikoa hiyo watashuhudia athari ya makazi yao kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi.

Mkoani Morogoro hivi karibuni waliripotiwa watu watano kufariki dunia na wengine 246 kuokolewa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mjini Morogoro na kusababisha mafuriko yaliyoharibu makazi na barabara.

Kwa Mkoa wa Dar es Salaam mvua hizo zilisababisha barabara kutopitika, nyumba kuzingirwa maji na wananchi kupita  adha ya usafiri.

Mara kadhaa Serikali imekuwa ikisisitiza wananchi wote waliojenga bondeni kuhama mara moja kuepuka athari za mvua.

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA
0 Comment

Mvua imesababisha vifo vya watu 4 huko DRCAfyaclass Forum •

Mvua imesababisha vifo vya watu 4 huko DRC.

Watu watano waliokolewa na wengine 20 walisombwa na maji. Juhudi za kuwatafuta na kuwaokoa wengine zinaendelea katika eneo.

Mvua kubwa ilisababisha maporomoko ya ardhi mashariki mwa Congo usiku wa kuamkia Jumatatu na kusababisha vifo vya watu wasiopungua wanne na kuwaacha wengine 20 wakiwa hawajulikani waliko, afisa mmoja wa eneo hilo amesema.

Maporomoko hayo yalitokea Jumapili jioni karibu na mji wa Kamituga katika mkoa wa Kivu Kusini kulingana na Naibu Meya Alexandre Ngandu Kamundala. Kiasi cha watu 25 wengi wao wakiwa wachimba migodi walipata hifadhi kutokana na mvua zilizonyesha kwenye mabanda wakati maporomoko ya ardhi yalipochukua makazi yao na kuyapeleka katika mto uliofurika, Kamundala alisema.

Watu watano waliokolewa kwa urahisi na wengine 20 walisombwa na maji. Miili minne ilipatikana ikiwa imekufa, alisema Kamundala. Juhudi za kuwatafuta na kuwaokoa zinaendelea ili kuwapata wale ambao bado hawajulikani waliko. Mwaka 2020 watu wasiopungua 50 katika mji huo huo wa Kamituga walifariki dunia katika maporomoko ya ardhi yaliyopiga eneo la mgodi wa dhahabu katika eneo hilo.

Ajali zinazopelekea vifo ni za kawaida katika migodi mingi ambayo haijadhibitiwa nchini Kongo huku idadi kubwa ya vifo haviripotiwi kutokana na maeneo yao madogo kuwepo katika milima na misitu.

Chanzo: Voa

Mvua imesababisha vifo vya watu 4 huko DRC
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD