Showing posts with label Makosa ya P Diddy. Show all posts
Showing posts with label Makosa ya P Diddy. Show all posts

P Diddy awalisha Chakula wafungwa wote kama shukrani kwa wafungwa wenzake huko Fort DixAfyaclass Forum •

P Diddy apanga na kufadhili Chakula kama shukrani kwa wafungwa wenzake huko Fort Dix

Wafungwa wenzake na Sean Combs huko FCI Fort Dix walipokea Ofa,baada ya Combs kupanga na kufadhili kutoa milo katika kituo chote. Kulingana na mwakilishi wa Combs, tajiri huyo wa muziki alifanya kazi na kikundi cha ndani kinachojulikana kama Bankroll Bosses, wakinunua chakula kutoka kwa kamishna, wakikiandaa kwa siku mbili, na kukisambaza kwa kila kitengo cha makazi katika gereza la New Jersey.

Combs aliiambia TMZ, "Shukrani, kwangu mimi, ni kuhusu kuhakikisha watu wengine wanakula. Kila mtu anaikosa familia yake. Watu hukata tamaa wakati kama huu. Tulitaka tu kukusanyika pamoja kama familia na kufanya mambo yetu wenyewe." Magereza kwa kawaida hutoa mlo wakawaida tu, lakini Combs na kikundi hicho walitaka kuunda kitu chenye maana zaidi kwa wafungwa.

0 Comment

P Diddy akutwa na hatia dhidi ya Makosa mawiliAfyaclass Forum •

Jopo la majaji limefikia uamuzi wa makosa yote matano ya Sean "Diddy" Combs.



Wakiwa katika chumba cha mahakama majaji walitaja mashtaka na hukumu zake.

Kwa muhtasari wa kile tulichosikia mahakamani, ni mchanganyiko wa hukumu za hatia na zisizo na hatia:

Kosa la njama za ulaghai: hana hatia

Ulanguzi wa ngono wa Cassie Ventura: hana hatia

Usafirishaji wa ukahaba wa Ventura na wengine: ana hatia

Ulanguzi wa ngono wa mwanamke anayejulikana kama "Jane": hana hatia

Usafirishaji kwa ajili ya ukahaba wa "Jane" na wengine: ana hatia

Majaji walichukua saa 13 kufikia uamuzi

Kwa jumla, majaji walijadili kwa saa 13 kwa siku tatu ili kufikia uamuzi wa pamoja juu ya mashtaka dhidi ya Combs.

Kesi hiyo imekuwa ikifanyika huko New York tangu mwezi Mei. Muda mwingi wa mahakama hiyo ulilenga kesi ya mwendesha mashtaka.

Upande wa utetezi unataka Combs aachiliwe kwa dhamana

Timu ya wanasheria na wakili wa Combs, Marc Agnifilo ameomba mteja wake aachiliwe kutoka kizuizini.

Amekuwa gerezani tangu alipokamatwa Septemba mwaka jana.

Agnifilo anapendekeza dhamanai ya $1m.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD