P Diddy akutwa na hatia dhidi ya Makosa mawili

P Diddy akutwa na hatia dhidi ya Makosa mawili

#1

Jopo la majaji limefikia uamuzi wa makosa yote matano ya Sean "Diddy" Combs.



Wakiwa katika chumba cha mahakama majaji walitaja mashtaka na hukumu zake.

Kwa muhtasari wa kile tulichosikia mahakamani, ni mchanganyiko wa hukumu za hatia na zisizo na hatia:

Kosa la njama za ulaghai: hana hatia

Ulanguzi wa ngono wa Cassie Ventura: hana hatia

Usafirishaji wa ukahaba wa Ventura na wengine: ana hatia

Ulanguzi wa ngono wa mwanamke anayejulikana kama "Jane": hana hatia

Usafirishaji kwa ajili ya ukahaba wa "Jane" na wengine: ana hatia

Majaji walichukua saa 13 kufikia uamuzi

Kwa jumla, majaji walijadili kwa saa 13 kwa siku tatu ili kufikia uamuzi wa pamoja juu ya mashtaka dhidi ya Combs.

Kesi hiyo imekuwa ikifanyika huko New York tangu mwezi Mei. Muda mwingi wa mahakama hiyo ulilenga kesi ya mwendesha mashtaka.

Upande wa utetezi unataka Combs aachiliwe kwa dhamana

Timu ya wanasheria na wakili wa Combs, Marc Agnifilo ameomba mteja wake aachiliwe kutoka kizuizini.

Amekuwa gerezani tangu alipokamatwa Septemba mwaka jana.

Agnifilo anapendekeza dhamanai ya $1m.

Related Discussions

REPLY HAPA


image quote pre code