Showing posts with label Mwongozo wa WHO. Show all posts
Showing posts with label Mwongozo wa WHO. Show all posts

WHO yatoa mwongozo wa kwanza wa kimataifa kuhusu UTASAAfyaclass Forum •

Shirika la Afya Duniani linachukulia utasa kuwa suala la afya ya umma duniani.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo tarehe 28 Novemba,  limezitaka nchi duniani kuongeza usalama, usawa na upatikanaji wa huduma za uzazi kwa wote, kupitia mwongozo wake wa kwanza kabisa wa kimataifa kuhusu kuzuia, kugundua na kutibu tatizo la utasa.

Inakadiriwa kuwa mtu 1 kati ya 6 mwenye uwezo wa kuzaa hukumbana na changamoto ya utasa katika kipindi fulani cha maisha yao ya uzazi. Hata hivyo, licha ya ongezeko la mahitaji ya huduma hizo, upatikanaji wake bado ni mdogo katika maeneo mengi duniani.

Katika nchi nyingi, vipimo na matibabu ya utasa hugharamiwa na watu binafsi, hali inayosababisha mzigo mkubwa wa kifedha kwa familia. Kwa baadhi ya maeneo, mzunguko mmoja wa utungishaji mimba kwa njia ya maabara (IVF) unaweza kugharimu zaidi ya mara mbili ya kipato cha wastani cha kaya kwa mwaka.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mwongozo huo, mjini Geneva, Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema, “utasa ni moja ya changamoto zinazopuuzwa zaidi katika afya ya umma na ni suala kubwa la usawa duniani. Mamilioni ya watu hujikuta wakikabiliana na safari hii peke yao wakishindwa kumudu gharama za matibabu, wakilazimika kutumia njia zisizo na ushahidi wa kisayansi, au kuchagua kati ya matarajio ya kupata watoto na usalama wao wa kifedha.”

Ameongeza kuwa WHO inahimiza nchi kutekeleza mwongozo huo ili kuzifanya huduma hizi kuwa za bei nafuu, zenye heshima na zinazoendana na ushahidi wa kisayansi.

Mapendekezo muhimu ya mwongozo mpya

Mwongozo huu mpya unajumuisha mapendekezo 40 yanayolenga kuimarisha hatua za kuzuia, kugundua na kutibu utasa, huku ukihimiza chaguo nafuu katika kila hatua ya huduma. Pia unasistiza umuhimu wa kujumuisha huduma za uzazi katika sera na mipango ya afya ya kitaifa, pamoja na mifumo ya ufadhili.

Huduma za uzazi shirikishi na inayolenga mahitaji ya watu

Utasa hufafanuliwa kama kushindwa kupata ujauzito baada ya zaidi ya miezi 12 ya kushiriki tendo la ndoa bila kutumia njia ya uzazi wa mpango. Hali hii husababisha msongo wa mawazo, unyanyapaa na mzigo wa kifedha, hivyo kuathiri ustawi wa kimwili, kiakili na kijamii.

Katika mwongozo huu mpya, WHO imeelekeza hatua muhimu za usimamizi wa kimatibabu wa utasa, sambamba na kuhimiza uwekezaji katika elimu na uelewa wa masuala ya uzazi, hasa kuhusu athari za umri, katika shule na katika vituo vya afya.

Mwongozo unasisitiza pia umuhimu wa kukabiliana na vihatarishi vinavyochangia utasa, ikiwemo maambukizi ya magonjwa ya zinaa yasiyotibiwa na matumizi ya tumbaku. Mabadiliko ya mtindo wa maisha kama lishe bora, mazoezi ya mwili na kuacha kuvuta sigara yanapendekezwa kwa watu na wanandoa wanaotafuta kupata ujauzito.

Changamoto za kijamii, kisaikolojia na kiafya zinazohusiana na utasa

Mwongozo unaeleza njia mbalimbali za kitabibu zinazoweza kutumika kubaini chanzo cha utasa kwa wanaume na wanawake. Aidha, unaelekeza namna ya kuendeleza matibabu hatua kwa hatua kuanzia ushauri kuhusu nyakati sahihi za kushiriki tendo la ndoa hadi mbinu tata zaidi kama vile uingizaji wa mbegu ndani ya mfuko wa uzazi (IUI) na IVF.

Kutambua athari mbaya za kisaikolojia zinazotokana na utasa kama vile msongo, wasiwasi na hali ya kujitenga ni mojawapo ya maeneo ambayo yamepatiwa kipaumbele, ambapo mwongozo unasisitiza hitaji la huduma endelevu za msaada wa kisaikolojia.

Mwelekeo mpya wa mataifa katika kuboresha uzazi wa mpango na huduma za utasa

WHO imetoa wito kwa nchi kutafsiri na kutekeleza mapendekezo hayo kwa kuzingatia mazingira yao ya ndani na kufuatilia hatua za utekelezaji. Ufanisi wa mwongozo huo unahitaji ushirikiano mpana baina ya Wizara za Afya, mashirika ya kitaaluma ya afya, asasi za kiraia na wadau wa huduma za afya ya uzazi.

Utekelezaji huo lazima uendane na mbinu jumuishi na zinazozingatia haki za afya ya uzazi, ili kuwawezesha watu kufanya maamuzi sahihi na yenye taarifa kuhusu ikiwa na lini wanataka kupata watoto.

Dkt. Pascale Allotey, Mkurugenzi wa Idara ya Afya ya Uzazi, Mama, Mtoto na Vijana wa WHO na Mpango Maalum wa Umoja wa Mataifa wa Utafiti kuhusu Uzazi (HRP), amesema, “kuzuia na kutibu utasa kunapaswa kuzingatia usawa wa kijinsia na haki za uzazi. Kuwawezesha watu kufanya maamuzi yenye taarifa kuhusu maisha yao ya uzazi ni suala la msingi katika afya na haki ya kijamii.”

Hatua na utafiti unaotarajiwa katika toleo lijalo la mwongozo

Licha ya kuwa mwongozo huu ni mpana, WHO imekiri kuwepo kwa mapungufu katika ushahidi uliopo na maeneo yanayohitaji utafiti wa ziada. Toleo lijalo la mwongozo linatarajiwa kujumuisha masuala kama kudumisha uwezo wa kupata ujauzito, mbinu za uzazi unaohusisha mhusika wa ziada, na madhara ya magonjwa sugu katika uwezo wa kupata ujauzito.

0 Comment

WHO: Jinsi ya kusaidia afya ya akili katika nyakati za misukosukoAfyaclass Forum •

Mwongozo wa WHO: Jinsi ya kusaidia afya ya akili katika nyakati za misukosuko



Zaidi ya watu milioni 300 duniani wanahitaji msaada wa kibinadamu kutokana na migogoro, mabadiliko ya tabianchi, misukosuko ya kisiasa na majanga ya asili. Na hali hiyo imeongeza uhitaji mkubwa wa huduma za afya ya akili na msaada wa kisaikolojia limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO.

Ili kukabiliana na changamoto hiyo, WHO kwa kushirikiana na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa ambayo ni lile la masuala ya Watoto- UNICEF, linashughulikia masuala ya wakimbizi -UNHCR, la idadi ya watu na afya ya uzazi - UNFPA na wadau wengine, wameunda Mfumo wa Huduma za Msingi za Afya ya Akili na Msaada wa Kisaikolojia (MSP).

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa yasiyoambukiza na Afya ya Akili wa WHO Dévora Kestel amesema mfumo huu unatoa mwongozo wa haraka kuhusu nini kifanyike kwenye dharura ili kuhakikisha msaada unawafikia walioathirika kwa wakati. “Katika majanga, maamuzi yanapaswa kufanywa haraka na fedha kutengwa ili hatua za kipaumbele zichukuliwe. MSP inatoa mwongozo wa kuratibu shughuli muhimu na kuhakikisha msaada unafika kwa walengwa,” amesema,

Mfumo huu umeundwa kwa kuzingatia uzoefu wa kimataifa na unajumuisha nyenzo  kuu saba:

Mwongozo wa MSP wa huduma za msingi.

Mafunzo ya MSP.

Miongozo ya haraka ya sekta mbalimbali.

Viashiria vya kutumika wakati wa ufuatiliaji na tathmini (M&E)

Zana za tathmini ya mahitaji kwa sekta nyingi.

Hifadhidata ya ripoti za tathmini na ramani.

Hifadhidata ya mafunzo ya MHPSS.

Kwa mujibu wa WHO, mwongozo huu mpya unasaidia sekta tofauti kupanga na kushirikiana, kuhakikisha msaada wa afya ya akili na kisaikolojia unakuwa wa haraka, bora na unaojali mahitaji ya jamii zilizoathirika.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD