Showing posts with label Ugonjwa wa Mpox. Show all posts
Showing posts with label Ugonjwa wa Mpox. Show all posts

Ugonjwa wa mpox na dalili zake,Fahamu hapa ugonjwa huu wa homa ya nyaniAfyaclass Forum •

Ugonjwa wa mpox na dalili zake,Fahamu hapa ugonjwa huu wa homa ya nyani


 

Ugonjwa Wa Mpox,chanzo,dalili Na Tiba yake

Ugonjwa wa homa ya nyani au Mpox ni ugonjwa ambalo unasababishwa na virusi, Ugonjwa huu unasababishwa na virusi ambao hujulikana kwa jina la Mpox ambapo hapo awali vilijulikana kama MonkeyPox. Mpox Virus wapo kwenye kundi la Orthopoxvirus genus ndani ya familia ya Poxviridae.

Ugonjwa wa homa ya nyani kwa binadamu(Human Mpox),Mara ya kwanza kabsa uliripotiwa Mwaka 1970 nchini DRC(Democratic Republic of the Congo) kwa kijana mmoja wa Miaka 9 aliyekuwepo kwenye eneo ambalo ugonjwa wa Smallpox ulishaondolewa tangu mwaka 1968. Ndipo visa vingine vikaanza kuripotiwa na maeneo mengine, (Disease history Source:WHO)

Dalili za Ugonjwa wa Mpox

DALILI ZA UGONJWA HUU WA Homa ya Nyani NI PAMOJA NA;

– Mtu kuwa na homa pamoja na mwili kutetemeka

– Kupata maumivu makali ya kichwa

– Mwili kuchoka kupita kawaida

– Mwili kukosa nguvu na kuwa dhaifu sana

– Lymph nodes kuanza kuvimba ambapo kwa lugha nyingine hujulikana kama lymphadenopathy

– Kupata maumivu ya viungo,joints pamoja na misuli ya mwili

– Kupata maumivu ya mgongo(back ache)

– Kutokewa na UPELE kwenye maeneo mbali mbali ya mwili wako kama vile; Usoni, kwenye mikono pamoja na viganja vya mikono,
miguuni,machoni,,mdomoni,sehemu za siri n.k

Upele huu unaweza kuwasha sana, na hata baadae huweza kutumbuka kabsa,

Mwili huweza kubaki na makovu au alama alama.

UGONJWA HUU WA HOMA YA NYANI(MPOX) husambaa kutokana na ukaribu(Close contact) kwa mtu,wanyama au vitu ambavyo tayari vina virusi hawa wa Mpox.

Unaweza kuupata kwa njia ya ya mgusano sehemu zenye majeraha, kupitia body fluids zote kama vile damu,mate,jasho n.k, kutoka kwa Mtu au wanyama wenye Virusi hawa(Mpox virus).

Virusi vya MPox vinaweza kuingia mwilini kupitia kwenye ngozi iliyo na jeraha au michubuko yoyote, au kwa njia nyingine kama vile njia ya upumuaji au kupitia macho, pua pamoja na mdomo.

Pia Uenezwaji wake unaweza kuwa  kwa kugusana na wanyama walioambukizwa kama vile nyani, panya na kindi ,kupitia vitu kama vile matandiko au nguo za mgonjwa mwenye virusi hawa.

- Ugonjwa wa Homa ya Nyani unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine kwa njia zifuatazo; kupitia maji maji ya mwili ikiwemo mate, matapishi, jasho, mkojo, matone ya mfumo wa njia ya hewa na ngozi kupitia kugusana na kujamiana na mtu mwenye maambukizi ama kutumia vifaa, matandiko au kugusa sehemu zilizo na vimelea vya ugonjwa huu. Aidha, ugonjwa huu unaweza pia kuenezwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

- Dalili kuu ya Homa ya Nyani ni upele, malengelenge au vidonda kwenye mwili hasa, mikono na miguu, kifuani, usoni na wakati mwingine sehemu za siri. Dalili nyingine ni homa, uchovu, maumivu ya kichwa, misuli, mgongo, uchovu na kuvimba mitoki.

- Ugonjwa huu wa homa ya nyani haujaingia nchini, hivyo, ni vyema tukashirikiana kuhakikisha nchi yetu inabaki kuwa salama. Wizara inatoa tahadhari kwa Wananchi wote kuchukua hatua za kujikinga na ugonjwa wa huu kwa kutekeleza yafuatayo;-

i. Kutoa taarifa kupitia namba 199 bila malipo endapo utamuona mtu mwenye dalili za Homa ya Nyani(Mpox).

ii. Kuepuka kugusa majimaji ya mwili au ngozi ya mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Homa ya nyani(Mpox).

iii. Kuepuka kusalimiana kwa kupeana mikono, kukumbatiana na kubusiana mtu mwenye dalili za Ugonjwa wa homa ya nyani(Mpox).

iv. Kuepuka kugusana na mtu yeyote mwenye dalili za ugonjwa wa Homa ya Nyani(Mpox).

v. Kunawa mikono kila mara kwa maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono.

vi. Epuka kula au kugusa mizoga au wanyama mfano nyani au swala wa msituni.

vii. Safisha na kutakasa vyombo vilivyotumika na mhisiwa au mgonjwa pamoja na maeneo yote yanayoguswa mara kwa mara.

viii. Kuvaa barakoa iwapo itabidi kukaa na kuongea kwa karibu na mtu mwenye dalili za Ugonjwa wa Homa ya Nyani(Mpox).

ix. Kuwahi katika vituo vya huduma za afya unapoona dalili za ugonjwa wa Homa ya Nyani(Mpox).

x. Watoa huduma za afya kuzingatia miongozo ya kuzuia kusambaa kwa maambukizi (IPC) wakati wote wanapowahudumia wagonjwa.

Via:WizaraafyaTz.

MATIBABU YA UGONJWA WA HOMA YA NYANI(Mpox)

Ugonjwa huu wa Homa ya Nyani hauna tiba(no cure),bali watalaam wa afya hudhibiti dalili zinazotokana na ugonjwa huu wa homa ya nyani.

Kwa Sasa Shirika la Afya Duniani(WHO) limeidhinisha Chanjo za Kutumika Kuzuia Ugonjwa huu wa Homa ya Nyani. #SOMA Zaidi hapa Kuhusu WHO na Chanjo hii ya Mpox

Hata hivo ugonjwa huu huisha wenyewe kwa kipindi flani baada ya kumpata mtu.

Fahamu pia,Maambukizi haya ya ugonjwa wa homa ya nyani(Mpox) huisha yenyewe na hudumu kati ya siku 14 na 21.


Mpox ni nini? Mpox/Homa ya Nyani

Kumekua na mlipuko barani Africa, nchi za jirani pia zimetangaza kua na wagonjwa wa mpox. Hivi karibuni hata mabara mengine yameanza kutangaza uwepo wa ugonjwa huu kwa kasi, hiii imepelekea WHO kuutangaza ugonjwa wa homa ya nyani kama janga la kimataifa. Hata hivyo nchini Tanzania bado hakujatangazwa kupatikana kesi ya ugonjwa huu.

Homa ya nyani ni ugonjwa unaosababishwa na virusi.virusi hivi ni familia moja na virusi vinavyosababisha smallpox au ndui kwa kiswahili.

Tuone historia ya Homa ya nyani kifupi.

Homa ya nyani sio ugonjwa mpya, umegundulika mwaka 1958 katika nyani waliokua wakifanyiwa tafiti. Kesi ya kwanza ya homa ya nyani kwa binadamu iligundulika mwaka 1970 nchini  DRC.

Tangu wakati huo kumekua na kesi chache barani africa hasa  africa ya kati na afrika ya magharibi. Lakini mwaka 2022 tumeanza kuona ugonjwa huu ukienea kwa kasi maeneo ambayo sio endemic na hata nje ya bara la Africa.

Ugonjwa wa Homa ya Nyani Unaambukizwaje

  1. Mji maji au mate yanatotoka kinywani wakati wa Kuongea, kukohoa au kuoiga chafya. (Droplets)
  2. Aina zote za ngono zinaweza kuambukiza, hii inajuimuisha kumbusu mtu mwenye mpox(All forms of sexual contact including kissing)
  3. Kukutana au kugusana ngozi na mtu mwenye homa ya nyani (Skin to skin contact)
  4. Kuvaa nguo au kutumia mashuka na foronya za mtu mwenye homa ya nyani. (Sharing clothes and/or bedding)
  5. KUgusa au kula wanya walioathirika au mizoga.

Dalili za Ugonjwa wa Homa ya Nyani

  1. Upele (una wezakutokea kwenye ngozi, mdomoni, ukeni, au ndani ya njia ya haja kubwa)
  2. Homa
  3. KUskia maumivu kwenye koo. (Sore throat)
  4. Maumivu Kichwa
  5. Maumivu ya Misuli
  6. Maumivu ya mgongo
  7. Uchovu wa kupitiliza usio elezeka
  8. Kuvimba tezi

Tiba na chanjo ya Ugonjwa wa homa ya Nyani

  1. Homa ya nyani isiokua na dalili kali (severe) hupona yenyewe ndani ya wiki 2-4 ( self limiting)
  2. Nenda kituo cha afya kuhakiki kama ni mpox na sio kitu kingine.
  3. Matibabu ya upele na kutibu dalili zingine kama homa kali na maumivu ya misuli yanaweza kupatikana

Chanjo ya homa nyani ipo lakini bado haipatikani nchi nyingi za Africa.


Watu walio katika hatari Ya kupata Homa ya nyani yenye Dalili Kali (severe).

  1. Watoto chini ya mwaka mmoja
  2. Wajawazito
  3. Watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

Watu walio katika hatari ya kupata homa ya nyani

  1. Watoa huduma ya afya
  2. Wanaofanya kazi katika mkusanyiko/msongamano  wa watu wengi
  3. Watu wenye wenza wengi ( multiple sexual partners)
  4. Watu wenye kujihusisha na biashara ya ngono
  5. Wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja pia wametajwa kuwa na hatari ya kupata.

Jinsi ya kujikinga na Ugonjwa wa Homa ya Nyani

  1. Epuka sehemu zenye msongamano  ambazo utagusana na watu
  2. Nawa mikono kabla ya kujigusa, kula, au unapotoka kwenye mizunguko
  3. Tumia kinga wakati wa kujamiiana
  4. Epuka kugusa wanyama wanaumwa au mizoga bila kujua ugonjwa au sababu ya kifo.

Jinsi ya kuwalinda wengine endapo wewe umeathirika na Ugonjwa wa Homa ya Nyani.

  1. Kaa nyumbani au katika chumba chako mwenyewe kama inawezekana.
  2. Osha mikono mara nyingi kwa sabuni na maji au na vitakasa mikono, hasa kabla au baada ya kugusa vidonda.
  3. Vaa barakoa na funika vidonda unapokuwa karibu na watu wengine hadi upele wako upone.
  4. Weka ngozi yako kavu na bila kufunikwa (isipokuwa unapokuwa chumbani na mtu mwingine).
  5. Epuka kugusa vitu katika maeneo ya pamoja na safisha maeneo ya pamoja mara kwa mara.
  6. Fuata maelekezo ya daktari katika kutibu vipele/vidonda.
  7. Tumia dawa za kupunguza maumivu zinazopatikana bila agizo la daktari kama vile paracetamol au ibuprofen.

 Nini cha kuepuka kuhusu Ugonjwa wa Homa ya Nyani

Kupasua au kukuna vipele/malengelenge. Hii inaweza kuweka vijidudu kwenye vidonda na kusababisha vishambuliwe na bakteria au kuchelewa kupona kwa vidoonda. Au kusambaza zaidi mwilili.

Credits|Article By;

Dr Ladina Msigwa

0 Comment

Sarah aeleza jinsi ambavyo alianza kuona dalili za Ugonjwa wa MpoxAfyaclass Forum •

Sarah aeleza jinsi ambavyo alianza kuona dalili za Ugonjwa wa Mpox

Ni Sarah huyu, mmoja wa waathiriwa wa ugonjwa huo  katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya. Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox yalizikumba nchi nyingi barani Afrika. Sara anaeleza dalili  za MPOX   alipoanza kuugua, anasema,

"Mimi nilianza tu kusikia  muwasho baada ya siku mbili nikaona vidonda vimetoka vinatoa maji. Vilianza kutoka  kichwani halafu vikafura  kwenye  shingo, nisingeweza kugeuza  shingo, hivyo  nikaona vidonda vinazidi kuongezeka. Ndipo nikachukua hatua ya kwenda hospitalini, nikaangaliwe  shida nini na baada ya hapo walipata kuwa  ni MPOX  na hapo nikapewa  matibabu."

Na ndipo safari ya Sara kuelekea hospitalini. Alipofika hospitali, alilazwa katika wodi moja iliyoko katika kitua cha kutenga kwa ajili ya wagonjwa wa MPOX, anasema..

“Baada ya kufikishwa pale hospitalini. Tuliwekwa kwa  wodi ya wagonjwa wenye MPOX  kwa ajili ya matibabu. Nilikaa kwa muda wa wiki mbili nikifuata masharti ya daktari na kusafisha na maji ya moto na chumvi. Halafu unapaka dawa  uliyopewa ya maji y, na baada ya hapo unameza vidonge vya maumivu. Madaktari wenyewe walikuwa wanakuja wanatuongelesha wakituambia tusiwe na wasiwasi hapa tumekuja mahali sawa.”

UNICEF  na huduma za Umoja wa Mataifa za maji na usafi wa mazingira, WASH imewasaidia  kuunga mkono Idara ya Afya ya Kaunti ya Mombasa na kwa kushirikiana na Serikali ya Kenya waliweza kujenga uwezo wa wahudumu wa afya na wahamasishaji wa afya ya jamii, wakiwafundisha kuhusu ugonjwa wa MPOX.  Dkt. Mohammed Halif ambaye ni  Mkurugenzi wa Kaunti  ya Mombasa,Huduma za Kliniki za Afya, anasema

“Tangu kulipomgundua mgonjwa wa kwanza, tulianzisha mara moja vituo vya uendeshaji wa dharura za afya ya umma kuhusu usafi wa mazingira na kujisafi, na ninaona imekuwa ni jambo la ukarimu sana kwa UNICEF kuja na kutoa vifaa vya kunawia mikono ambavyo tumevigawa katika wanajamii.”

Sarah baada ya kutibiwa, akapatiwa ushauri ya jinsi ya kutangamana na wengine.

“Tuliambiwa kwamba ukishatoka nje mwepukane na mambo  ya ngono sana na pili mambo ya kushikana shikana. Vile nilitoka hospitalini, nilipewa mtungi wa maji na sabuni mche mzima nikaambiwa Mtungi utakuwa  wakuchotea  maji toka mtoni   na kuoga mzuri, usafi uendelee.”

UNICEF imeendelea kuunga mkono hospitali na pia kufanya uhamasishaji ndani ya jamii ili kuhakikisha kwamba visa vitakavyotokea siku za usoni vitashughulikiwa kwa wakati.

Sarah anatamatisha na furaha akisema familia yake pia wamejawa na furaha baada ya kupona, anasema…

“Niliporudi nyumbani watoto walifurahi sana kuniona. Saa hii nafurahia sana, nashukuru napata usingizi, nalala na najihisi niko sawa zaidi sina yale maumivu nilikuwa nayo.”

0 Comment

Maambukizi ya ugonjwa wa Mpox yaongezeka KenyaAfyaclass Forum •

Mamlaka za afya nchini Kenya zimeripoti kuongezeka kwa kasi kwa maambukizi ya ugonjwa wa Mpox katika kaunti ya pwani ya Mombasa, kusini mashariki mwa Kenya



Mombasa ni miongoni mwa majimbo 21 yaliyoathiriwa na mlipuko huo, ambapo maambukizi ya kwanza eneo hilo yalithibitishwa Septemba mwaka jana.

‘’Kuna maambukizi mengi eneo la Mombasa kwa sababu jamii haijakubali kuwa ugonjwa huu upo,’’ Dk Mohamed Hanif, mkurugenzi wa huduma za matibabu wa kaunti, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa.

Kufikia mwisho wa wiki, tangu mwaka jana, Mombasa ilikuwa imerekodi maambukizi 98 yaliothibitishwa na vifo viwili. Wakaazi wengi wamechanganya vipele vya Mpox kuwa hali nyingine kama vile ugonjwa wa ndui au vipele vya joto.

“Wagonjwa wengi wana umri wa kati ya miaka 24 na 45. Mtoto mdogo zaidi ana umri wa miaka 12. Sote tuko hatarini,” alisema Dk Hanif.

Tangu Kenya kutangaza mlipuko wa Mpox tarehe 31 Julai 2024, Wizara ya Afya imethibitisha maambukizi 226 na vifo vinne nchini kote.

Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Afrika CDC) vinasema visa vingi vya magonjwa ya MPOX vinashuhudiwa katika nchi zenye kiwango cha juu cha magonjwa kama VVU au kifua kikuu mfano Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Sierra Leone, lakini kwa sasa Mpox inaongezeka nchini Kenya na Guinea huku Uganda na Burundi pia wakishuhudia kuibuka tena kwa ugonjwa huo.

Hivi karibuni Kenya ilirekodi kiwango cha juu cha visa vya ugonjwa huo kwa kila wiki, ikiashiria kuwa huenda awali, visa vingi havikuwa vinatambuliwa, shirika hilo lilisema.

Nchini Kenya, maambukizi ya kwanza ya ugonjwa wa Mpox yalitambuliwa katika ukanda wa usafiri wa kaskazini kati ya madereva wa malori, wanaojihusisha na biashara ya ngono na wafanyabiashara. Sasa maambukizi yanaenea kwenye jamii, ambayo inatoa changamoto mpya", alisema Dk Yap Boum II, naibu mkuu wa timu ya msaada ya usimamizi wa matukio ya CDC ya Afrika, wakati wa kikao cha kila wiki siku ya Alhamisi.

"Tunahitaji kusaidia Kenya na uchunguzi. Dozi 10,000 za chanjo zinapatikana lazima zisambazwe kwa njia mahususi ili kudhibiti mlipuko huo kabla ya kuenea zaidi," ameongeza.

MPOX inasalia kuwa dharura ya afya ya umma ugonjwa uliosababisha wasiwasi kimataifa.

0 Comment

Ugonjwa wa Mpox waendelea kuisumbua DRCAfyaclass Forum •

Ugonjwa wa Mpox waendelea kuisumbua DRC, WHO yasaidia.

Mpox ugonjwa nadra lakini hatari yake ni sawa na virusi vya ndui ambavyo sasa vimetokomezwa.

Kuanzia Januari 1 hadi katikati ya Novemba mwaka huu 2023, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imerekodi zaidi ya wagonjwa 13,000 wanaoshukiwa kuwa na virusi vya Mpox na zaidi ya vifo 600 vimehusishwa na ugonjwa huo.

Hii ndiyo idadi kubwa zaidi ya maambukizi ya kila mwaka yaliyoripotiwa ikilinganishwa na kilele cha awali cha zaidi ya wagonjwa 6,000 walioripotiwa mwaka wa 2020.

“Mlipuko huo unaenea kijiografia, ikiwa ni pamoja na mikoa ambayo haikuwahi kuwa na Mpox. Maambukizi ya Mpox yameripotiwa katika kanda za afya 156 kutoka mikoa 22 kati ya 26 (85%).” Ameeleza leo Dkt Rosamund Lewis, Kiongozi wa wataalamu wa Mpox katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO alipozungumza na wanahabari hii leo mjini Geneva, Uswisi.

WHO hivi majuzi ilikamilisha kazi nchini DRC kutathmini hali na kuunga mkono mwitikio wa kitaifa. Hii ni hali tata sana, ikizingatiwa kwamba DRC inakabiliwa na masuala mengine ya dharura ikiwa ni pamoja na kipindupindu na migogoro ya kibinadamu.

Wataalamu wa afya wa mashinani na kitaifa wanajitahidi kukabiliana na janga ambalo linaenea kijiografia, na kuongeza kasi ya maambukizi kupitia ngono kwa mtu mmoja hadi mwingine.

Maambukizi ya ngono ya mpox yamerekodiwa kwa muda, ikiwa ni pamoja na mlipuko wa Nigeria unaoendelea tangu 2017. Ilikuwa njia kuu ya maambukizi katika nchi ambazo zilikumbwa na milipuko endelevu kwa mara ya kwanza mnamo 2022 – na nyingi za nchi hizi zinaendelea kushuhudia maambukizi hadi leo.

Afisa huyo wa WHO ameeleza kuwa kuna haja ya haraka ya kuwekeza katika uwezo wa kutambua, kuthibitisha na kughughulikia. WHO inafanya kazi na Wizara ya Afya ya DRC kusaidia usambazaji wa vufaa vya kukusanya sampuli na kusafirisha, na kuchunguza sampuli kutoka kwa watu wanaoshukiwa huko Kinshasa, Kivu Kusini na maeneo mengine yaliyoathirika. Kwa sasa, ni asilimia tisa tu ya maambukizi ya Mpoksi yamethibitishwa kimaabara.

Dkt. Rosamund Lewis amesisitiza akisema, “Mlipuko wa ugonjwa wa Mpox nchini DRC ni ukumbusho wa haja ya kuendelea kwa ushirikiano na uratibu wa kimataifa ili kudhibiti na hatimaye kukomesha maambukizi ya Mpox kutoka kwa binadamu hadi kwa binadamu. Mapema mwezi huu, WHO iliarifiwa kuhusu mlipuko unaoshukiwa kuwa kwenye meli ya kitalii yenye ratiba kusini-mashariki mwa Asia.

Tunawahimiza watu binafsi, mamlaka za afya za mitaa na waandaaji wa safari za baharini na mikusanyiko mingine mingi kuendelea kushirikishana taarifa, kuongeza ufahamu na kuchukua hatua zote ili kupunguza hatari ya milipuko ya Mpox.”

Ugonjwa wa Mpox waendelea kuisumbua DRC
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD