Showing posts with label afya kwa watoto. Show all posts
Showing posts with label afya kwa watoto. Show all posts

Screen chanzo cha magonjwa ya Moyo kwa WatotoAfyaclass Forum •

Utafiti mpya umebaini kuwa kutumia muda mwingi kwenye vifaa vya kielektroniki kama Simu, Televisheni, Kompyuta na Michezo ya video kunaweza kuathiri si tu afya ya akili ya Watoto na vijana, bali pia afya ya mwili hususan afya ya moyo na mfumo wa Metaboli.



Utafiti huo, uliochapishwa leo katika Jarida la Chama cha Moyo cha Marekani (Journal of the American Heart Association), uliochunguza data kutoka zaidi ya washiriki 1,000 waliokuwa sehemu ya tafiti mbili zilizofanyika Denmark. 

Ripoti hiyo imesema kuwa Watoto wa umri wa miaka 10 na vijana wa miaka 18 waliotumia muda mwingi kwenye vifaa hivyo walionekana kuwa katika hatari kubwa ya kupata magonjwa ya moyo na metaboli kama shinikizo la juu la damu, kolesteroli nyingi na upungufu wa uwezo wa insulini kudhibiti sukari mwilini.

Watafiti walipima hatari ya kila mshiriki kwa kutumia alama maalum kulingana na wastani wa kundi zima, ambapo alama ya 0 ilimaanisha hatari ya wastani na 1 ilimaanisha kiwango cha juu cha hatari kwa kipimo cha standard deviation, ilibainika kuwa kila saa ya ziada ya matumizi ya skrini iliongeza hatari ya ugonjwa kwa asilimia 0.08 kwa watoto wa miaka 10, na asilimia 0.13 kwa vijana wa miaka 18.

Mwandishi Mkuu wa Utafiti huo, David Horner kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen, Denmark amesema kuwa ingawa ongezeko la hatari kwa kila saa ni dogo, linapojumlishwa hadi saa tatu, tano au hata sita kwa siku.

Kwa wastani, vijana wa miaka 18 walikuwa wanatumia takribani saa 6 kwa siku kwenye vifaa hivyo, huku watoto wa miaka 10 wakitumia saa 3 kwa siku, Utafiti pia uligundua kuwa usingizi uliathiri uhusiano huo kulala muda mfupi au kulala kwa kuchelewa kuliongeza hatari ya matatizo ya moyo kwa watoto wanaotumia muda mwingi kwenye skrini. 

0 Comment

Chanjo huzuia Vifo million 3.5 ila Zaidi ya watoto milioni 14 hawakuchanjwa 2024Afyaclass Forum •

Chanjo huzuia Vifo million 3.5 ila Zaidi ya watoto milioni 14 hawakuchanjwa 2024



Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya watoto milioni 14 hawakupata chanjo kabisa mwaka 2024.

Kulingana na makadirio ya Umoja wa Mataifa, chanjo huzuia vifo milioni 3.5 hadi 5 kwa mwaka.

Taarifa ya pamoja ya Shirika la Afya Duniani, WHO, na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto, UNICEF, iliyotolewa Jumanne, imeeleza kuwa barani Ulaya na Asia ya Kati, viwango vya wastani vya chanjo ya watoto vilishuka kwa asilimia 1.

Maafisa wameonya kwamba kuenea kwa habari potofu na kupunguzwa kwa misaada ya kimataifa kunaongeza pengo la chanjo na kuwaweka malioni ya watoto hatarini.

Nchi tisa ndiyo zimechangia zaidi ya nusu ya watoto wasiokuwa na chanjo duniani.

Nchi hizo ni pamoja na Nigeria, India, Sudan, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Ethiopia, Indonesia, Yemen, Afghanistan, na Angola.

Mkurugenzi Mkuu wa UNICEF, Catherine Russell, amesema mamilioni ya watoto bado hawajapata chanzo za kuwaepusha na magonjwa yanayoweza kuzuilika, na kwamba jambo hilo linatia wasiwasi.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD